Mume wangu hapendi ndugu zangu

Mume wangu hapendi ndugu zangu

Daah wewe dada una dhambi.
Ndoa bado changa unaanza kuleta ndg?

Mmeo anataka mjiachie kwanza.
Waisrael wana tabia kuwa watu wakioana wapewe zaidi ya mwaka wafurahie hata vitani mme hatakiwi kwenda.
Mapema mno kwa ninyi nyote kuanza kuleta ndg zaidi ya kusalimia na kuondoka.

Muendako utaiharibu ndoa yenu.
Kama mna uwezo kubalianeni mumpangishie huyo binti then baadae mnaweza kuanza kuishi na ndg daah
Hili nalo ne o yaani ndoa changa alafu unaleta mdogo wako kwa kweli mume ana haki ya kununa. Mtu alikuwa na expectations za kugegeduana garden sebuleni kitchen shower leo unaleta ndugu naakosa uhuru. Aise amefanya vibaya sana.
 
Mume wangu ana ndugu wengi kuliko mimi. Tatizo langu mimi ni mtu nnaependa sana wageni niwapikie tufurahi. Anaeishi hapa ni mdogo wangu mmoja tu na sio kwamba tunamuhudumia kifedha. Ni anahudumiwa na mzazi bado ila hapa anakua karibu na chuo tu, nilichokuelewa ni kwamba nilitakiwa nikae mimi kama mimi. Mungu anipe busara sasa ya kusema ndugu wasije kwangu
Kabisa...muishi mume na mke basi. Ndugu saidia kwa njia nyingine wakiwa huko mbali. Shauri yako mtashare de libolo wewe na mdogo wako 🤣🤣🤣🤣
 
Nikushauri dada, kwa mazingira hayo mpeleke mdogo wako kwa ndugu wengine, maana hapo ni shida mumeo hampendi
🤝 mdogo wangu ata opt kurudi nyumbani maana hata wenyewe wanasemaga mimi ndo nawaelewa kuliko mtu mwengine so akitoka hapa ni atarudi nyumbani tu. Bora awe ameamua yeye. Nikiamua mimi ni kama kumfukuza. Yaani acha tu ndugu yangu Mungu anipe busara haswa
 
Maandiko yanasema ."mwanamke ataachana na wazazi wake,na ndugu zake,ataambatana na mume wake na wao watakua mwili mmoja.ukitafakari maneno haya vizuri wote ntakua na makosa,kwanza Kama sasa mmekua ni mwili mmoja kwa nini mume wako afanye hivyo?la pili kiuhalisia hautakiwi kuishi na ndugu zako swala linakuja familia zetu za kiafrica umaskini bado ni tatizo kubwa.hauwezi kuishi bila kusaidia ndugu,kwani sio wote wanakua wamepiga hatua,ni jinsi gani ya kuangalia namna gani unamsaidia
 
Hili nalo ne o yaani ndoa changa alafu unaleta mdogo wako kwa kweli mume ana haki ya kununa. Mtu alikuwa na expectations za kugegeduana garden sebuleni kitchen shower leo unaleta ndugu naakosa uhuru. Aise amefanya vibaya sana.


Mkuu wanawaje wa kiafrika ndio wachawi wa mahusiano yao.
Huyu dada sisi ambao tunakoment tofauti na anavyotaka kusikia yeye anatuona wachawi na kututukana kimoyomoyi lkn ipo siku atakumbuka hizi koments.

Nakuhakikishia hilo lijamaa ipo siku litakula wadogo zake ajutie hili analolileta, atamchukia mune na atawachukia hao ndg zake anaowatetea hadi kijasho kinamshuka.

Wengine tumeona mengi.
Unaowapenda zaidi ndio watakuumiza zaidi...fanya mambo kwa kiasi na tahadhari
 
Akae hostel za ndani ya chuo haitakuwa changamoto sana
Sasa wewe ni mwanaume. Kumtupa mtoto huko si ntakua katili na kikubwa ntampa tu stress bi mkubwa maana stress za wanae zote huwa ananimwagia mimi nizisort so hawa ni wangu
 
Pole sana dear,nimekuelewa
Unakumbuka ulipoolewa uliambiwa ndoa ni uvumilivu?Basi maana yake ni hiyo sasa,uliambiwa unaishi na binadamu na si malaika basi binadamu mwenyewe ndo huyo sasa!
Kwanza kubali kuwa umeolewa na mwanaume mchoyo na mbinafsi na ndo mana wakija ndugu zako anasema hana ela ila wakija ndugu anatoa,hizo ni tabia za ubinafsi!
Kama mwanamke nilie kwenye ndoa nakushauri umtoe huyo mdogo wako hapo as umesema kwenu una uwezo wa kumlipia hostel,usitake kuforce kukaa nae though umesema unampenda mana utaumia tena sana tu huko mbele kadri siku zinavyozidi kwenda na hata huo upendo unaosema unauona kwa mumeo hutauona tena!
Kumbuka kuna kuchoka as wewe pia ni binadamu,na maudhi na maumivu ndo husababisha ndoa nyingi leo kuwa ndoa jina au kusambaratika kabisa!
Mwache aende alafu wewe endelea kumuombea kwa Mungu aguse moyo wake mana uchoyo ni dhambi!
Kuna vitu unaweza kuvumilia kirahisi kwenye ndoa ila sio kuona mwenzio hataki ndugu zako,yani unajiona hata wewe huna thamani kwake ndo mana nakwambia mtoe kwanza huyo hapo ili usijitengenezee maumivu yasiyo ya lazima!
Once again pole sana,
Uishi Maisha marefu madam

Nakazia hapo
 
🤝 mdogo wangu ata opt kurudi nyumbani maana hata wenyewe wanasemaga mimi ndo nawaelewa kuliko mtu mwengine so akitoka hapa ni atarudi nyumbani tu. Bora awe ameamua yeye. Nikiamua mimi ni kama kumfukuza. Yaani acha tu ndugu yangu Mungu anipe busara haswa
😂😂😂😂
Mtani wangu ninatamani sana nikushauri kitu ambacho kamwe huwezi kukikwepa lkn ndio hivyo.

Najua hutaipenda post yangu lkn hutaiepuka kukupata siku za usoni.

1. Huwezi kumpenda mdogo wako akiwa
nje ya kwako na ahisi unampenda?

2. Unajua pia huwezi kupata vyote unavyovitaka viwe? Yaani kuwa na mdogo wako home kwako na furaha ya ndoa kwa pamoja?

3. Yes unaweza kufanikisha mdogo wako akae nawe lkn furaha ya mume hutaipata kwani sio utashi wake.

4. Jifunze kuchagua cha kwanza kwanza...kumbuka sheria ya ndoa ni kutengwa na ndg na jamaa zako? usijidanganye...ndg watakuja kusalimia na kuondoka tu na sio kukaa.

5. Msikilize mmeo anachotaka eidha awe na roho mbaya au hata hujamwelewa kwanini afanya hivyo...nenda naye taratibu. Ukilazimisha utalia kwani anaweza kufanya maamuzi magumu yakakuumiza milele, mimi ni mwanaume na nina huruma kuliko unavyofikiri lkn ukienda kinyume na sheria yangu utalia.

6. Unaweza kuwapenda ndg sanaa lkn kuna siku watakusapraiz na utawachukia milele...ipo siku utamkuta kitandani kwako na mmeo na hutaamini macho yako na upendo unao wapa.

Katika hili nilikuwaga na gf wangu mrembo sana wadogo zake mapacha visu hatari.
Aliwapenda sana, kiasi kwamba tulikuwa tukisafiri pamoja nao na aliwaamini sana.
Huwezi amini walimgeuka na kuanza kutaka kutembea na shemeji yao na akagundua hilo...nisingekuwa na msimamo ningewachanganya....nahisi unalitaka hili hasa siku ukiona mmeo anampenda huyo binti ujue tayari.

Kuwa na kiasi katika kupenda ndg
 
Dah. Nimeusoma huu ujumbe kwa maumivu sana. Yani unawekwa katika wakati mgumu wa kuamua kati ya ndoa na ndugu yako wa damu mliopitia matatizo na kuyavuka pamoja. Hivi ikatokea siku mume amekuacha, kwa ndugu yako unarudije sasa kupata msaada na mnakua msha hitilafiana
Unatakiwa tu utafute njia ya hekima ya kuongea na ndugu yako ili asije akamchukia shemejie au akakufikiria vibaya wewe,
Mdanganye either kipato cha shemeji kimeshuka sasa kutulisha itakua ishu so nenda kwanza tuweke mambo sawa!
Maji ndo ushayavulia nguo mama na huwezi kuachana na mumeo kwa hiyo sababu so tumia akili zaidi kuliko moyo kutafuta suluhu!
 
Habari wakuu, nahitaji ushauri,

Mimi ni binti nimeolewa naishi na familia, mume wangu pamoja na mdogo wangu wa kike. Tatizo ni kwamba mume wangu amekuwa na kisirani sana juu ya huyu mdogo wangu wa kike. Kila anachofanya lazima mwanaume alalamike.

Na wala sijawahi kuwa na mawazo labda anamtaka, ndiyo maana anafanya hivi visirani vyote. Mazingira niliyomlea mdogo wangu namjua na ana tabia njema sana.

Mume wangu pia siwezi kumuhukumu kwa uhuni, hajanipa sababu ya kufanya hivyo. Kwahiyo kinachonichanganya ni kwanini ananipa wakati mgumu wa kumfanya mdogo wangu aishi kama yuko kwa mtu baki wakati mimi ni dada yake wa kuzaliwa naye kabisa?

Kila kitu ni lazima aseme kana kwamba huyu mtoto anamkwaza. Kinachoniuma mimi ni kwamba kila siku namuuliza hivi kama angekuwa anaishi hapa ndugu yako halafu mimi namfanyia hivi
Ungejiskiaje? Si ningeonekana mimi ndiyo mbaya sipendi ndugu wa mume?

Na kinachonishangaza, kuna kijana tunaishi naye hapa siyo ndugu wa damu wa mume wangu lakini anatusaidia kazi za hapa nyumbani, ametokea kijijini kwao. Sasa huyu hata akosee vipi mume wangu ukimwambia huyu kakosea hiki na hiki wala hutomuona akijigusa kwenda kumfokea wala kumsema.

Sana sana atajibaraguza tu ili uone ame 'react' na hii siyo mara ya kwanza. Chochote kinachomuhusu mtu wa kwao hutomuona mume wangu amekasirika, lakini ikiwa ni swala la kuhusu ndugu yangu atafoka haswa.

Inafika hatua anamnyima hadi vitu vya kutumia ndani ambavyo hata yeye anavitumia. Hiyo siyo shida, naumia kwasababu mimi huyu mtoto namchukulia kama mwanangu wa kumzaa, nimelichukua hilo jukumu kwa mama yangu tangu mdogo na kwa sasa mama haishi Dar na hatujawa na mahusiano mazuri sana na baba yetu kwa sababu ya mambo ambayo amekuwa akifanya kwetu sisi kama familia.

Kwahiyo najitahidi sana mdogo wangu asijihisi mpweke wala asione kuna pengo la kuumizwa kimalezi na baba yetu.

Na kuna siku ilikuwa sikukuu, nilimwambia mume ndugu zangu wanakuja kwasababu wazazi wetu hawaishi hapa Dar naomba sisi hapa tuwafanyie kitu kama kuwaalika wale hata chakula cha kawaida tu, akasema yeye hana hela.

Wala sikukasirika, nikajikokota nikanunua vyakula nikapika nioneshe kama mume wangu ndiyo amewaalika na wao waone wana kaka hapa mjini. Mume wangu wala hakuonesha ule ushirikiano ambao mimi huwa nautoa wakija ndugu zake, maana huwa napika haswa hadi kwenye kuni.

Nahangaika, napanga, naandaa, nikijua ndugu wa mume wangu wanakuja ila siku wamekuja wadogo zangu sikupata ushirikiano huo. Nilisema acha tu nivumilie kwasababu namheshimisha mume wangu mwenyewe.

Mara nyingine aliniliza na nikamwambia mimi huwa silii lakini unanitenda kama vile sisi kwetu ni masikini, yaani wadogo zangu walipita kutusalimia wakawa sebuleni akaniita chumbani akaniambia nataka kuja kukaa sebleni, naomba nikute siti ya kukaa. Kanakwamba wadogo zangu wamejaa pale maana walikuja kusalimia.

Kinachoniuma ni kwamba, sisi katika kukua kwetu hatujawahi kulelewa na ndugu, kama wadogo zangu wanakaa nje ya kwa baba na mama basi kwangu ndiyo pa kwanza, kwahiyo nikiona wanatendewa hivi naona kama ni mimi ndiyo napitia, sitamani wajione watu baki.

Na kuna muda huwa nawaza, ningekuwa na uwezo ningejenga nyumba yangu niwaweke wadogo zangu hadi watakapokuja kuolewa. Atakae tawanyika sawa, ila kwakuwa mzazi wetu ana uwezo ataona nampokonya wanae. Ila natamani sana wadogo zangu waishi maisha niliyotamani kuishi.


Ushauri unaohitajika;

1. Ni kosa mimi kumtetea mdogo wangu? Kwasababu ninapo jaribu kuuliza kwani tatizo lipo wapi hadi ufoke juu ya jambo dogo hivi, naonekana mkorofi au nataka kumpanda mume kichwani?!

2. Kiubinadamu, huyu mdogo wangu amekosea kuja kuishi kwangu? Nimemlea na hana tabia mbovu kwahiyo namjua, na kila siku namwambia mdogo wangu ikitokea leo dada yako nimedondoka, watoto wangu hutowaacha naamini.

Nampenda sana huyu mtoto, Mungu pekee ndiyo anajua. Kuna muda namwambia mume wangu basi nisamehe mimi naomba vumilia kidogo huyu mtoto akipata kazi ataondoka.

Kwasababu siyo kwamba kwetu tuna shida ya kifedha na wala mume wangu hamgharamii chochote zaidi ya chakula ninachokula mimi ndiyo anachokula huyu mtoto. Ni anakaa kwangu kwasababu ni karibu na chuoni anaposoma yeye.

Kwa upande wa nauli na gharama za kujikimu anatoa mzazi na mimi nikipata huwa nampa kidogo, nashindwa hata kusema namuhudumia maana biashara niliyokuwanayo ilishavurugika baada ya kumuomba mume tusimamie wote ili asiwe na wivu na wateja (stori ndefu haihusiki na mada).

Kwahiyo sina uwezo wa kumgharamia mdogo wangu kwa asilimia mia ila nikipataga 20, 30 nampa ajisogeze. Na mdogo wangu najua ananijali sana, kuna vitu ananifanyiaga huwa nahisi kama nina binti wa kike kabisa.

Yaani kiufupi sipo tayari ndoa yangu iingie doa kwasababu ya mimi kumtetea mdogo wangu na sipo tayari kugombana na mdogo wangu kwasababu yoyote, sijui kama nimeeleweka hapa?

3. Nifanyeje ili mume wangu awe na amani, mdogo wangu pia awe na amani na asijue kwamba shemeji yake huwa analalamika? Kwasababu kila ambacho mume huwa analalama mimi huwa natafuta namna ya kumuelekeza mdogo wangu kama vile mimi ndiyo nataka iwe hivyo, namwelekeza ili asije akafanya tena mume asione tunamdharau.

Na kibaya ni kwamba kuna siku mdogo wangu alisikia nikilalamika sana kwamba hii hali ya yeye mume wangu kukosa amani inaninyima raha, nataka anisaidie mawazo nifanyeje ili awe na furaha na nimuelewe ili niwe namrekebisha mdogo wangu na mimi niwe na amani, hakunijibu! Kesho yake mdogo wangu alikosa raha na sikutaka tena kuibua hiyo mada.

Kiukweli ndoa yetu haina miaka mingi lakini naumia, nilitamani sana mume wangu amlee mdogo wangu kama ambavyo mimi ningelea wa kwake. Lakini inanipa wakati mgumu sana kwamba isije ukatokea mtafaruku kati yao. Nitakae kuwa kwenye wakati mgumu ni mimi.

Uadui huwa hauishi ikiwa mmoja akijua mwengine anamchukia. Na kuna muda huwa namwambia mume, natamani hata na wewe aje ndugu yako hapa akae nikuoneshe jinsi inavyokua kuishi na familia, kuna vitu unavichukulia kama ni mwanao kafanya. Na mume kwangu ana upendo, anajitahidi sana kwakweli, kama kuna makosa ni madogo ya kiubinadamu, ndiyo maana nafukia mengine yoote.

Ninachotamani ni ushauri tu wa kumfanya mume wangu amuone mdogo wangu kama mdogo wake. Niwe na amani pia.

Naombeni ushauri.
Nikipata nafasi nitakagua simu ya mama Yoyoo kama yupo JF... maana na yeye ana hii mambo kaniletea mdogo wake half brother nimlee.... hiyo kitu sikuielewa.
 
Sio bure kuna sababu inayosababisha hayo. Nachokushauri mtoe huyu binti akakae hosteli ili kupunguza hiyo migogoro.
Hayo mambo ya ndugu yanategemea mtu anachukuliaje na inabidi uende nae taratibu Malezi ya familia yako na mumeo ni tofauti na the way mnavyo handle ndugu inatofautiana pia

Muombe MUNGU mambo yakae sawa hapo baadae ni muda tu
 
Pole sana dear,nimekuelewa
Unakumbuka ulipoolewa uliambiwa ndoa ni uvumilivu?Basi maana yake ni hiyo sasa,uliambiwa unaishi na binadamu na si malaika basi binadamu mwenyewe ndo huyo sasa!
Kwanza kubali kuwa umeolewa na mwanaume mchoyo na mbinafsi na ndo mana wakija ndugu zako anasema hana ela ila wakija ndugu anatoa,hizo ni tabia za ubinafsi!
Kama mwanamke nilie kwenye ndoa nakushauri umtoe huyo mdogo wako hapo as umesema kwenu una uwezo wa kumlipia hostel,usitake kuforce kukaa nae though umesema unampenda mana utaumia tena sana tu huko mbele kadri siku zinavyozidi kwenda na hata huo upendo unaosema unauona kwa mumeo hutauona tena!
Kumbuka kuna kuchoka as wewe pia ni binadamu,na maudhi na maumivu ndo husababisha ndoa nyingi leo kuwa ndoa jina au kusambaratika kabisa!
Mwache aende alafu wewe endelea kumuombea kwa Mungu aguse moyo wake mana uchoyo ni dhambi!
Kuna vitu unaweza kuvumilia kirahisi kwenye ndoa ila sio kuona mwenzio hataki ndugu zako,yani unajiona hata wewe huna thamani kwake ndo mana nakwambia mtoe kwanza huyo hapo ili usijitengenezee maumivu yasiyo ya lazima!
Once again pole sana,
Itoshe kusema kuwa unajielewa sana na u mke bora
 
Aiseee ila tupunguze ishi na watu, tujitahidi kuishi kila mtu kivyake
 
Mimi nimeona watu wameshauri vitu Vingi lakin tayari una majibu yako kichwani ukitaka ushauri kubali kishauriwa japo wakat mwingine ushauri unaopewa unaweza kuwa mgumu kwako
 
Huyo kamtongoza mdogo wako kachomoa!

Amini nakwambia, ndo maana kisirani

Kongole kwa mdogo wako ana tabia njema sana[emoji122][emoji122]
 
Kama uwezo wa kupangisha chumba mahali unao, Basi mpangishie chumba.

Amani ni nzuri sana.
 
Back
Top Bottom