Mume wangu hapendi ndugu zangu

Mume wangu hapendi ndugu zangu

Ww unashida moja umekuja na majibu yako kichwani ukiwa na shauku ya kupata sapoti ya mawazo yako......kuna watu kibao huko juu washakushauri muondoe huyo dogo hapo home ila bado unakaza fuvu....unaendelea kuuliza umpeleke wapi???😬😬😬mumeo alikuoa ww sio familia yako so kaa ukijua nyumba yenu ni yako...jamaa na watoto wenu wa kuwazaaa.....hao watu wengine ni nyongeza tu usilazimishe maisha ya kiswahiliswahili jaribu kubeba mzigo wako bila kutafuta kichaka cha kuonewa huruma.
Swali langu jingine,, wakati unamleta hapo huyo mdogo wako ulimshirikisha mwamba na unauwakika alikubali au ulifosi????inabidi utambue mwenzako anapenda kujitawala akiwa nyumbani kwake so jaribu kucope ukishindwa omba talaka ukiolewe na waswahili wenzako wanaopenda extended familiies....na ukiendelea kukaza fuzu huyo dogo atakupindua kwenye hiyo ndoa🤝dogo aende hosteli au utegemee mwamba kuna siku itaikula tu hiyo pisi kali.
 
Aiseee pole sana kwa changamoto. Lkin ki ukweli ukishamjua mtu hawezi kukupa shida. Huwezi kumbadilisha mtu kama yeye mwenyewe hajaamua kubadilika. Ila unaweza kucheza kwenye tune yake.

Kuna watu ni wabinafsi hata uonyeshe upendo wa kutoa roho yako kwa ajili yao kamwe hawewezi kujifunza.
Jiridhishe kwanza kama hakuna sababu ya msingi ya mume wako kumchukia mdogo wako,,kaa chini na wako ongea naye amekuja hapo kwa ajili yako. Yeye ndo anayekufahamu huyo bwana mmekutana ukubwani. Chochote atachosema au kumfokea mdogo wako uwe na kauli moja tu samahani ,,,usibishane wala usitake kumdhihirishia kuwa nani mkosaji na nani si mkosaji. Na akilalamika kujaa kwenye sofa acha wadogo zako wakae chini. Trust me fanya hivyo miezi kadhaaa utakuja kunishukuru.

Hakuna njia bora ya kumbadilisha zaidi ya kumpuuza. Na usipambane kuwaonesha ndugu zako kuwa mume ni bora,,acha ajipambanie mwenyewe kwa kufanya matendo mema.
 
Mawazo yake ni kwamba amekuoa wewe tu! Na sio umlete NDUGU uishi nae, akakae na NDUGU zake.
 
Yani ndugu yangu acha tu. Kuna tuvisa tudogo dogo hadi unaona aibu hata mtu wa nje akiskia. Anaweza tu akaamka akaanza kusema hivi kule ana mashuka mangapi kayachukue si ulimuazima siku moja tu. Nyie nachanganyikiwa naona kama hii roho inamuandama. Akili iliyonijia hapa ni kupiga maombi. Naona aibu kwakweli. Sio kawaida
Hakuna cha maombi hapo...huyo kaomba K kanyimwa ndo maana kisirani

Unajisumbua bure ukweli ndo huo

Mhamishe mdogo ako hapo!
 
Habari wakuu, nahitaji ushauri,

Mimi ni binti nimeolewa naishi na familia, mume wangu pamoja na mdogo wangu wa kike. Tatizo ni kwamba mume wangu amekuwa na kisirani sana juu ya huyu mdogo wangu wa kike. Kila anachofanya lazima mwanaume alalamike.

Na wala sijawahi kuwa na mawazo labda anamtaka, ndiyo maana anafanya hivi visirani vyote. Mazingira niliyomlea mdogo wangu namjua na ana tabia njema sana.

Mume wangu pia siwezi kumuhukumu kwa uhuni, hajanipa sababu ya kufanya hivyo. Kwahiyo kinachonichanganya ni kwanini ananipa wakati mgumu wa kumfanya mdogo wangu aishi kama yuko kwa mtu baki wakati mimi ni dada yake wa kuzaliwa naye kabisa?

Kila kitu ni lazima aseme kana kwamba huyu mtoto anamkwaza. Kinachoniuma mimi ni kwamba kila siku namuuliza hivi kama angekuwa anaishi hapa ndugu yako halafu mimi namfanyia hivi
Ungejiskiaje? Si ningeonekana mimi ndiyo mbaya sipendi ndugu wa mume?

Na kinachonishangaza, kuna kijana tunaishi naye hapa siyo ndugu wa damu wa mume wangu lakini anatusaidia kazi za hapa nyumbani, ametokea kijijini kwao. Sasa huyu hata akosee vipi mume wangu ukimwambia huyu kakosea hiki na hiki wala hutomuona akijigusa kwenda kumfokea wala kumsema.

Sana sana atajibaraguza tu ili uone ame 'react' na hii siyo mara ya kwanza. Chochote kinachomuhusu mtu wa kwao hutomuona mume wangu amekasirika, lakini ikiwa ni swala la kuhusu ndugu yangu atafoka haswa.

Inafika hatua anamnyima hadi vitu vya kutumia ndani ambavyo hata yeye anavitumia. Hiyo siyo shida, naumia kwasababu mimi huyu mtoto namchukulia kama mwanangu wa kumzaa, nimelichukua hilo jukumu kwa mama yangu tangu mdogo na kwa sasa mama haishi Dar na hatujawa na mahusiano mazuri sana na baba yetu kwa sababu ya mambo ambayo amekuwa akifanya kwetu sisi kama familia.

Kwahiyo najitahidi sana mdogo wangu asijihisi mpweke wala asione kuna pengo la kuumizwa kimalezi na baba yetu.

Na kuna siku ilikuwa sikukuu, nilimwambia mume ndugu zangu wanakuja kwasababu wazazi wetu hawaishi hapa Dar naomba sisi hapa tuwafanyie kitu kama kuwaalika wale hata chakula cha kawaida tu, akasema yeye hana hela.

Wala sikukasirika, nikajikokota nikanunua vyakula nikapika nioneshe kama mume wangu ndiyo amewaalika na wao waone wana kaka hapa mjini. Mume wangu wala hakuonesha ule ushirikiano ambao mimi huwa nautoa wakija ndugu zake, maana huwa napika haswa hadi kwenye kuni.

Nahangaika, napanga, naandaa, nikijua ndugu wa mume wangu wanakuja ila siku wamekuja wadogo zangu sikupata ushirikiano huo. Nilisema acha tu nivumilie kwasababu namheshimisha mume wangu mwenyewe.

Mara nyingine aliniliza na nikamwambia mimi huwa silii lakini unanitenda kama vile sisi kwetu ni masikini, yaani wadogo zangu walipita kutusalimia wakawa sebuleni akaniita chumbani akaniambia nataka kuja kukaa sebleni, naomba nikute siti ya kukaa. Kanakwamba wadogo zangu wamejaa pale maana walikuja kusalimia.

Kinachoniuma ni kwamba, sisi katika kukua kwetu hatujawahi kulelewa na ndugu, kama wadogo zangu wanakaa nje ya kwa baba na mama basi kwangu ndiyo pa kwanza, kwahiyo nikiona wanatendewa hivi naona kama ni mimi ndiyo napitia, sitamani wajione watu baki.

Na kuna muda huwa nawaza, ningekuwa na uwezo ningejenga nyumba yangu niwaweke wadogo zangu hadi watakapokuja kuolewa. Atakae tawanyika sawa, ila kwakuwa mzazi wetu ana uwezo ataona nampokonya wanae. Ila natamani sana wadogo zangu waishi maisha niliyotamani kuishi.


Ushauri unaohitajika;

1. Ni kosa mimi kumtetea mdogo wangu? Kwasababu ninapo jaribu kuuliza kwani tatizo lipo wapi hadi ufoke juu ya jambo dogo hivi, naonekana mkorofi au nataka kumpanda mume kichwani?!

2. Kiubinadamu, huyu mdogo wangu amekosea kuja kuishi kwangu? Nimemlea na hana tabia mbovu kwahiyo namjua, na kila siku namwambia mdogo wangu ikitokea leo dada yako nimedondoka, watoto wangu hutowaacha naamini.

Nampenda sana huyu mtoto, Mungu pekee ndiyo anajua. Kuna muda namwambia mume wangu basi nisamehe mimi naomba vumilia kidogo huyu mtoto akipata kazi ataondoka.

Kwasababu siyo kwamba kwetu tuna shida ya kifedha na wala mume wangu hamgharamii chochote zaidi ya chakula ninachokula mimi ndiyo anachokula huyu mtoto. Ni anakaa kwangu kwasababu ni karibu na chuoni anaposoma yeye.

Kwa upande wa nauli na gharama za kujikimu anatoa mzazi na mimi nikipata huwa nampa kidogo, nashindwa hata kusema namuhudumia maana biashara niliyokuwanayo ilishavurugika baada ya kumuomba mume tusimamie wote ili asiwe na wivu na wateja (stori ndefu haihusiki na mada).

Kwahiyo sina uwezo wa kumgharamia mdogo wangu kwa asilimia mia ila nikipataga 20, 30 nampa ajisogeze. Na mdogo wangu najua ananijali sana, kuna vitu ananifanyiaga huwa nahisi kama nina binti wa kike kabisa.

Yaani kiufupi sipo tayari ndoa yangu iingie doa kwasababu ya mimi kumtetea mdogo wangu na sipo tayari kugombana na mdogo wangu kwasababu yoyote, sijui kama nimeeleweka hapa?

3. Nifanyeje ili mume wangu awe na amani, mdogo wangu pia awe na amani na asijue kwamba shemeji yake huwa analalamika? Kwasababu kila ambacho mume huwa analalama mimi huwa natafuta namna ya kumuelekeza mdogo wangu kama vile mimi ndiyo nataka iwe hivyo, namwelekeza ili asije akafanya tena mume asione tunamdharau.

Na kibaya ni kwamba kuna siku mdogo wangu alisikia nikilalamika sana kwamba hii hali ya yeye mume wangu kukosa amani inaninyima raha, nataka anisaidie mawazo nifanyeje ili awe na furaha na nimuelewe ili niwe namrekebisha mdogo wangu na mimi niwe na amani, hakunijibu! Kesho yake mdogo wangu alikosa raha na sikutaka tena kuibua hiyo mada.

Kiukweli ndoa yetu haina miaka mingi lakini naumia, nilitamani sana mume wangu amlee mdogo wangu kama ambavyo mimi ningelea wa kwake. Lakini inanipa wakati mgumu sana kwamba isije ukatokea mtafaruku kati yao. Nitakae kuwa kwenye wakati mgumu ni mimi.

Uadui huwa hauishi ikiwa mmoja akijua mwengine anamchukia. Na kuna muda huwa namwambia mume, natamani hata na wewe aje ndugu yako hapa akae nikuoneshe jinsi inavyokua kuishi na familia, kuna vitu unavichukulia kama ni mwanao kafanya. Na mume kwangu ana upendo, anajitahidi sana kwakweli, kama kuna makosa ni madogo ya kiubinadamu, ndiyo maana nafukia mengine yoote.

Ninachotamani ni ushauri tu wa kumfanya mume wangu amuone mdogo wangu kama mdogo wake. Niwe na amani pia.

Naombeni ushauri.
Maelezo mengi ila utambue jambo moja "UMEOLEWA WEWE NA SI NDUGU ZAKO"
 
😂😂😂😂
Mtani wangu ninatamani sana nikushauri kitu ambacho kamwe huwezi kukikwepa lkn ndio hivyo.

Najua hutaipenda post yangu lkn hutaiepuka kukupata siku za usoni.

1. Huwezi kumpenda mdogo wako akiwa
nje ya kwako na ahisi unampenda?

2. Unajua pia huwezi kupata vyote unavyovitaka viwe? Yaani kuwa na mdogo wako home kwako na furaha ya ndoa kwa pamoja?

3. Yes unaweza kufanikisha mdogo wako akae nawe lkn furaha ya mume hutaipata kwani sio utashi wake.

4. Jifunze kuchagua cha kwanza kwanza...kumbuka sheria ya ndoa ni kutengwa na ndg na jamaa zaki usijidanganye...ndg watakuja kusalimia na kuondoka.

5. Msikilize mmeo anachotaka eidha awe na roho mbaya au hata hujamwelewa kwanini afanya hivyo...nenda naye taratibu. Ukilazimisha utalia kwani anaweza kufanya maamuzi magumu yakakuumiza milele, mimi ni mwanaume na nina huruma kuliko unavyofikiri lkn ukienda kinyume na sheria yangu utalia.

6. Unaweza kuwapenda ndg sanaa lkn kuna siku watakusapraiz na utawachukia milele...ipo siku utamkuta kitandani kwako na mmeo na hutaamini macho yako na upendo unao wapa.

Katika hili nilikuwaga na gf wangu mrembo sana wadogo zake mapacha visu hatari.
Aliwapenda sana, kiasi kwamba tulikuwa tukisafiri pamoja nao na aliwaamini sana.
Huwezi amini walimgeuka na kuanza kutaka kutembea na shemeji yao na akagundua hilo...nisingekuwa na msimamo ningewachanganya....nahisi unalitaka hili hasa siku ujiona mmeo anampenda huyo binti ujue tayari.

Kuwa na kiasi katika kupenda ndg
Shukrani🤝🤝
 
dada anajiamini eti mume wake hawez omba Tunda[emoji23][emoji23].

mimi mwenyew hapa nilishawahi omba tunda la mama mdogo wa wife, mbna ishue ni simple kama ni mzuri basi unaomba.

ila tunda nilinyimwa na nkapewa onyo, baada ya hapo nilimchukia na sitaki kumuona kwangu,

wife akiuuliza kwanini namchukia mama ake mdogo?
huwa sina majibu zaidi ya kufoka tu[emoji23]
[emoji38][emoji38][emoji38][emoji38][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji23][emoji23]

Na kwanini unafoka foka?
 
Tabia zinatofautiana na kila binadamu ana mapungufu yake
Huyu wa kwako ni mbahili kupitiliza yaani anachukia hata hewa ya bure anayopumua hapo

Watu wa hivyo wapo ila usiumize roho ingawa wanawake mna roho ya huruma mda mwingi
Mwambie mdogo wako amchukulie kama alivyo ila jitahidi wewe kumsaidia zaidi mdogo wako kwa mambo madogo madogo

Asiwe mtu wa kukaa sitting room kila wakati hilo aepuke nalo pia amkwepe tu kila wakati
La kuachana kwa sababu hiyo sio uamuzi mzuri kwani sioni shida kubwa sana

Unajua madhaifu yake na ndugu waambie kama unavyotuambia sisi kuwa hawapendi na yeye mwambie kuwa ujumbe unaenda hivyo
Ikishindikana kabisa mdogo wako arudi kwenu tu
 
Swali la kujiuliza kama ilitokea mzazi na ndugu zenu Kuna baadhi hawakuwahi kuwapenda unafikir ni rahis mumeo ambae sio nduguyako kumpenda mdogowako??mtu kuwa na upendo Kwa watu wengine mara nying ni asili tu pia marachache mtu kuweza kubadilika,

kubali ndo tabia ya mumeo na kukwepa madhara ni kuongea na mumeo abadilike akishindwa mtoe mdogowako hapo..
 
Mimi nimeona watu wameshauri vitu Vingi lakin tayari una majibu yako kichwani ukitaka ushauri kubali kishauriwa japo wakat mwingine ushauri unaopewa unaweza kuwa mgumu kwako
Asante kwa kuniunga mkono
 
Haya ndio nionavyo Mimi

 Mosi, uwezo wa huyo mdogo wako kupanga chumba upo Ila unajisikia vibaya kwanini akapange na Hali wewe upo na anaweza kuishi kwako

Jibu ni rahisi mumeo hamtaki hapo kwake,Busara ni huyo kuhama hapo na mweleze ukweli mdogo wako kuwa inaonekana uwepo wako hapo mumeo hapendi na hujui sababu,hii itakusaidia mdogo wako kujua kuwa sio mapenzi yako yeye kuhama Ila Kero zimezidi toka Kwa mumeo.

 Pili, unapenda Sana mumeo aonekane ni mtu mzuri kwenu ndio maana unajitahidi kuficha upuuzi wake,Hilo ni Jambo zuri lakini wakati mwingine sio Sawa aonekane yeye ni Malaika,nahisi ndio maana unahisi mdogo wako alienda kupanga basi mumeo ataonekana sio mtu mzuri,Kwa mazingira hayo kuwa muwazi sema kweli kuwa mumeo hapendi uwepo wa mdogo wako pale.


Tatu, ambalo ndio kubwa na wanabodi wengi wamesema ni kuwa mumeo anataka kumla supu huyo mdogo wako,na hivyo mdogo wako amegoma kuliwa supu,hiyo ndio sababu kubwa Kwa sababu zifuatazo:

* Mumeo hamhudumii huyo binti Kwa nauli wala Karo ya chuo na mambo mengine,kwahiyo wala sio mzigo kwake hata kidogo useme labda Maisha magumu ndio maana hamtaki hapo

* Huyo binti Mda mwingi yupo chuoni sio kwamba anashinda hapo na kuwafanya msiwe huru na nyumba yenu .


* Kama unavyosema huyo binti ana Tabia njema hivyo naamini hajawahi kuvunja heshima ya nyumba yenu.


Kitu pekee ambacho kimebakia hapo ni kuliwa supu na huyo mumeo.

Raisi mstaafu aliwahi kutuambia akili za kuambiwa changanya na zako.
 
Ushauri wangu,tafuta siku utoke out na mumeo sehemu nzuri nzuri hivi I mean sehemu yenye mandhari nzuri lakini pia itakayowapa nafasi ya kufurahia as if mna update penzi vile mkipiga mastori ya hapa na pale huku mkikumbushana kipindi cha ujana wenu, halafu kwa upole na unyenyekevu huku ukiwa huna chembe za kuonesha kulaumu ongea na mwamba kuhusu mdogo wako(amvumilie kwa mapungufu madogo anayoyaona kwa muda mfupi atakaokua hapo) natumaini atakuelewa.
Ikishindikana hapo nashauri uongee na wazazi wako huyo dogo apangishiwe chumba jirani na chuo ili amani iwepo kwenye familia yako.
 
Ww unashida moja umekuja na majibu yako kichwani ukiwa na shauku ya kupata sapoti ya mawazo yako......kuna watu kibao huko juu washakushauri muondoe huyo dogo hapo home ila bado unakaza fuvu....unaendelea kuuliza umpeleke wapi???😬😬😬mumeo alikuoa ww sio familia yako so kaa ukijua nyumba yenu ni yako...jamaa na watoto wenu wa kuwazaaa.....hao watu wengine ni nyongeza tu usilazimishe maisha ya kiswahiliswahili jaribu kubeba mzigo wako bila kutafuta kichaka cha kuonewa huruma.
Swali langu jingine,, wakati unamleta hapo huyo mdogo wako ulimshirikisha mwamba na unauwakika alikubali au ulifosi????inabidi utambue mwenzako anapenda kujitawala akiwa nyumbani kwake so jaribu kucope ukishindwa omba talaka ukiolewe na waswahili wenzako wanaopenda extended familiies....na ukiendelea kukaza fuzu huyo dogo atakupindua kwenye hiyo ndoa🤝dogo aende hosteli au utegemee mwamba kuna siku itaikula tu hiyo pisi kali.
Kujazana ndg ni tabia za kinyamwezi, kinyiramba na kirangi zaidi
 
Pole sana dadangu, mke mwema na mme mwema hutoka kwa Mungu, na kwa namna ulivyojieleza nimeona hapo Kuna tatizo!!! Ushauri wangu fanya mambo yafuatayo
1: mme wako ndiye baba wa familia na ndiye mwaamuzi wa mwisho, kaa naye faragha mwambie juu ya udhaifu wake huo wa kutowapenda ndugu zako, pamoja na mdogo wako huyo, na mwambie labda Kama yeye hataki ukae naye Basi umuondoe nyumbani hapo!!
2: yawezekana kweli mdogo wako huyo anakosea kweli katika hali ya kuonywa wewe unaona anaonewa kwa sababu sio ndugu yake( wanawake wengi wapo hivyo), jaribu kujithathimini pia kwa Hilo
3: mme wako ndiye mwenye maamuzi, usimpelekee taarifa mbali mpelekee maombi!!! Usipange ndugu zako kuja nyumbani alafu wewe ndo uende kumpa taarifa huku tiyari ulishawaambia ndugu zako wake siku Fulani, Hilo ni kosa, mme wako unatakiwa umuombe Kwanza juu ya Hilo akikukubalia ndo uende kuwapanga ndugu zako! Vinginevyo mme akikataa utasema amewakataa ndugu zako

4: mme wako ndiye mwenye familia akisema Hana hela Wala usimhukumu, vinginevyo mna mfuko mmoja wa kutunza pesa, Mara nyingi wanaume wakiwa na hela au kutokuwa na hela hawasemi Kama Wanahela! Alafu Wana mipango mingi tofauti na wewe mwanamke, hilo ni vyema ulijue, maana yeye mda wote atawajibika lakutokea likitokea nyumbani hapo yeye ndiye atakaye ulizwa! Wala sio wewe mpendwa!

6: mwanamke automatically ukishaolewa unaingia kwenye familia ya mwanaume, maana nyingine ndugu wa mwanaume ndiyo ndugu zako, ndo maana mpaka na jina mwanamke unabadilisha, hii maanake ni kwamba, mmeo bado ataendelea kuwasaidia ndugu zake zaidi, kuliko ndugu zako, wazazi wake zaidi kuliko wazazi wako, marafiki zake zaidi kuliko marafiki zako, hii ni kwa sababu wewe umeletwa kwenye familia, lakini wao bado wapo pale pale, hivyo basi ukishalijua Hilo mpendwa, unachotakiwa kukifanya ni wewe kupambana aidha Kama una kazi, au biashara kuwasaidia ndugu zako, lakini usitegemee hela ya mme wako kuwasaidia ndugu zako, maana hela ya mme wako ni familia yenu!! Ambayo wewe umejumuishwa pia,

7: ndoa ni ya mme na mke!! Nyie mkae mkubaliane mweleze tu kuwa unampenda na haupo tiyari kumkwaza kwa sababu ya ndugu zako, kama hawataki akuambie tu!!! Mm ninaamini ukikaa naye vzr ukamweleza Kama ni mtu mwenye akili atajirudi tu mpendwa!!! Maana hiyo ni tabia ya asili, lakini inarekebishika

8: ndoa inalindwa na maombi, mpendwa, Bwana Yesu akitawala ndoa Yenu hayo mambo yataondoka outomaticallly
Wagalatia 5:22
Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu,

Wagalatia 5:23
upole, kiasi; juu ya mambo kama hayo hakuna sheria.

Wagalatia 5:24
Na hao walio wa Kristo Yesu wameusulibisha mwili pamoja na mawazo yake mabaya na tamaa zake.

Barikiwa
 
Back
Top Bottom