Mume wangu hapendi ndugu zangu

Mume wangu hapendi ndugu zangu

Watu wapole, unaoona wametulia ni noma sana.

Tuombe tu asije akakupiga sapraizi ukabaki mdomo wazi...
Sitoshangaa ndugu yangu. Kikubwa ntamshukuru Mungu kwa yote. Ila sitoishi na guilt kwamba nilimtendea mtu ubaya
 
Dada yangu angekua mtu wa mitandao ningesema ni wewe aisee
Ila nyie Kuna wanaume wana gubu na roho mbaya[emoji119]..majuzi nimepata taarifa mume wa Dada Katia chumvi juice za mdogo wangu[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]Jamani ..mwezi uliopita Katia simu kwenye ndoo ya maji...ngachokaaa
Kuuwa kunaanzia hapo hapo
Mungu awaepushe na balaa ila huyo ni zaidi ya mchawi
 
Watu wapole, unaoona wametulia ni noma sana.

Tuombe tu asije akakupiga sapraizi ukabaki mdomo wazi...
Sitoshangaa ndugu yangu. Kikubwa ntamshukuru Mungu kwa yote. Ila sitoishi na guilt kwamba nilimtendea mtu ubaya
 
Watu humu ndani mna ubinafsi, mnasema amfukuze mdogo wake, we wako ungefukuza? Siku akipata shida na mume akimkimbia ndugu hawatomsaidia hata kidogo mimi nna uzoefu na hilo tukio nna binamu yangu hadi leo anagalagala kwa marafiki. Mume alimwambia sitaki kuona ndugu zako hapa na yeye akatii ndoa, mume kamzalia nje na kahamia kwa hawara, wanae hawana hata ada na ndugu wote wanamuangalia tu. Na uwezo wa kumsaidia wanao.

Huyu mtoa mada namuelewa sana tu ila nyie mnaosema afanye maamuzi ndo mnafeli
 
Moyo wa mtu ni kichaka.
Usiamini unamjua.

Hawezi akaanza tu kumchukia mdogo wako bila sababu zilizojificha ndani ya uvungu wa moyo wake.
 
Shida ni mila zetu. Mwanaume kuwapenda ndugu zako ni bonasi. Wewe kuwapenda ndugu zake ni wajibu. Wewe umeolewa yeye ameoa. Upo kwenye mji wake. So usawa sahau. Inatarajiwa iwahudumie ndugu zake na sio kinyume chake ingawa ingekuwa bora zaidi. So chagua moja. Kilinda ndoa ama familia. Katika hali yako huwezi kulinda yote mawili. Kuhusu mdogo wako naamini kuna countless alternatives. Kuhusu ndoa ikiisha ndo kwaheri. Jua vipaumbele vyako
Kwa binadamu wa kawaida ni ngumu labda akufanyie unafki. Atawapenda ukiwepo lakini moyoni ataumia
 
Nikuulize kitu, mfano mkeo akijifungua utaweza kumhudumia uzazi peke yako? Bila msaada wa ndugu zake?
Ww unashida moja umekuja na majibu yako kichwani ukiwa na shauku ya kupata sapoti ya mawazo yako......kuna watu kibao huko juu washakushauri muondoe huyo dogo hapo home ila bado unakaza fuvu....unaendelea kuuliza umpeleke wapi???😬😬😬mumeo alikuoa ww sio familia yako so kaa ukijua nyumba yenu ni yako...jamaa na watoto wenu wa kuwazaaa.....hao watu wengine ni nyongeza tu usilazimishe maisha ya kiswahiliswahili jaribu kubeba mzigo wako bila kutafuta kichaka cha kuonewa huruma.
Swali langu jingine,, wakati unamleta hapo huyo mdogo wako ulimshirikisha mwamba na unauwakika alikubali au ulifosi????inabidi utambue mwenzako anapenda kujitawala akiwa nyumbani kwake so jaribu kucope ukishindwa omba talaka ukiolewe na waswahili wenzako wanaopenda extended familiies....na ukiendelea kukaza fuzu huyo dogo atakupindua kwenye hiyo ndoa🤝dogo aende hosteli au utegemee mwamba kuna siku itaikula tu hiyo pisi kali.
 
Dada yako amefanyaje sasa. Mi ndo nachotaka kujua.
Dada yangu angekua mtu wa mitandao ningesema ni wewe aisee
Ila nyie Kuna wanaume wana gubu na roho mbaya🙌..majuzi nimepata taarifa mume wa Dada Katia chumvi juice za mdogo wangu😂😂😂😂Jamani ..mwezi uliopita Katia simu kwenye ndoo ya maji...ngachokaaa
 
familia haijui haya yote na haina sababu ya kujua. Najaribu kuficha ila sasa malalamiko yamezidi ina maana ndugu zangu hawatakua wanakuja kunitembelea kwangu. Hata siku nikipata mtoto nani atanisaidia na uzazi sasa kama nikiwaondoa. Wanaume wanadhani ni rahisi kufukuza ndugu ila siku nikiumwa yeye ataweza kufanya yote bila msaada. Kuna incident ilitokea kwa ndugu yangu, mume aliwahi kufukuza ndugu wa mkewe na siku mkewe alifanyiwa operation wakamwambia dada yao tunaogopa kupigwa na shemeji tukija kwako. Yule dada aliuguzwa na watu baki
Kumbe mna tabia ya kujazana kwa ndugu
 
Tabia zinatofautiana na kila binadamu ana mapungufu yake
Huyu wa kwako ni mbahili kupitiliza yaani anachukia hata hewa ya bure anayopumua hapo

Watu wa hivyo wapo ila usiumize roho ingawa wanawake mna roho ya huruma mda mwingi
Mwambie mdogo wako amchukulie kama alivyo ila jitahidi wewe kumsaidia zaidi mdogo wako kwa mambo madogo madogo

Asiwe mtu wa kukaa sitting room kila wakati hilo aepuke nalo pia amkwepe tu kila wakati
La kuachana kwa sababu hiyo sio uamuzi mzuri kwani sioni shida kubwa sana

Unajua madhaifu yake na ndugu waambie kama unavyotuambia sisi kuwa hawapendi na yeye mwambie kuwa ujumbe unaenda hivyo
Ikishindikana kabisa mdogo wako arudi kwenu tu
Nashukuru sana. Mtoto akija anafanya vishughuli vidogo vya nyumbani then anaingia kulala. Kukaa sebleni ni hadi mimi ni lazimishe
 
Kumbe mna tabia ya kujazana kwa ndugu
Kujazana wapi? Mdogo mmoja ndo amejazana? Hivi nyie wenzangu mnaishi Afrika au marekani? Hivi afrika hapa utakaa nyumbani peke yako. Ukizaa mtoto unamuacha na nani na hawa mahousegirl wanaotoroka kutwa. Mume anashinda ofisini, unarudi nyumbani unakuta housegirl ametoroka kaacha mtoto ndani kafunga na mlango. Hivi situation kama hiyo napo utamwita nani aje kwako akusaidie? Mume atakubali mlee mtoto pamoja?

Ushauri nnaoomba ni maneno ya kumwambia huyu mtoto arudi kwao ili mume awe na amani anayotaka
 
Huu mjadala unathibitisha wanaosema wanawake huwa hawaongei kutafuta solution wanaogea kutoa nyongo tu basi (though mimi nakuwa outlier kwenye hili swala), mtu unapewa solution unatumia muda kuelezea nadharia, mara nampenda, ananipenda, sijui sisi waafrika, hukutaka solution ulitaka tu kuelezea hisia zako otherwise majibu yako yangejikita zaidi kwenye nini ufanye na ufanyeje, practical solutions, wewe umejikita zaidi kwenye hisia zako juu ya tatizo zima na mumeo na mdogo wako.

Samahani me sina suluhisho nilikuwa nasoma tu comments.

Pia I can't relate to your problem maana mimi nyumba yangu ni kama kituo cha mabasi yaendayo kasi ile sas 12 jioni, tukipika mchana utadhani msiba kumbe hata mgeni hamna siku hiyo, sitting room utafikiri kibanda cha kuonyeshea mechi, na vyumbani ndo usiseme utafikiri kambi ya wakimbizi hadi tumeamua kuongeza kitanda kingine chumbani kwetu mashemeji wapate pa kulala, juzi nikasikia wanatuteta eti hii mimba ya nane wameipataje mbona kila siku tunalala wote?
 
Haya ndio nionavyo Mimi

 Mosi, uwezo wa huyo mdogo wako kupanga chumba upo Ila unajisikia vibaya kwanini akapange na Hali wewe upo na anaweza kuishi kwako

Jibu ni rahisi mumeo hamtaki hapo kwake,Busara ni huyo kuhama hapo na mweleze ukweli mdogo wako kuwa inaonekana uwepo wako hapo mumeo hapendi na hujui sababu,hii itakusaidia mdogo wako kujua kuwa sio mapenzi yako yeye kuhama Ila Kero zimezidi toka Kwa mumeo.

 Pili, unapenda Sana mumeo aonekane ni mtu mzuri kwenu ndio maana unajitahidi kuficha upuuzi wake,Hilo ni Jambo zuri lakini wakati mwingine sio Sawa aonekane yeye ni Malaika,nahisi ndio maana unahisi mdogo wako alienda kupanga basi mumeo ataonekana sio mtu mzuri,Kwa mazingira hayo kuwa muwazi sema kweli kuwa mumeo hapendi uwepo wa mdogo wako pale.


Tatu, ambalo ndio kubwa na wanabodi wengi wamesema ni kuwa mumeo anataka kumla supu huyo mdogo wako,na hivyo mdogo wako amegoma kuliwa supu,hiyo ndio sababu kubwa Kwa sababu zifuatazo:

* Mumeo hamhudumii huyo binti Kwa nauli wala Karo ya chuo na mambo mengine,kwahiyo wala sio mzigo kwake hata kidogo useme labda Maisha magumu ndio maana hamtaki hapo

* Huyo binti Mda mwingi yupo chuoni sio kwamba anashinda hapo na kuwafanya msiwe huru na nyumba yenu .


* Kama unavyosema huyo binti ana Tabia njema hivyo naamini hajawahi kuvunja heshima ya nyumba yenu.


Kitu pekee ambacho kimebakia hapo ni kuliwa supu na huyo mumeo.

Raisi mstaafu aliwahi kutuambia akili za kuambiwa changanya na zako.
Asante🤝
 
Dada yangu angekua mtu wa mitandao ningesema ni wewe aisee
Ila nyie Kuna wanaume wana gubu na roho mbaya🙌..majuzi nimepata taarifa mume wa Dada Katia chumvi juice za mdogo wangu😂😂😂😂Jamani ..mwezi uliopita Katia simu kwenye ndoo ya maji...ngachokaaa
daah, pole sana

hapo imebaki hatua mbaya zaidi, endeleeni kuomba na ikiwezekana mdogo ako ahame hapo alipo

allivyoweka chumvi huoni ni Mungu tu angeweza kuweka sumu? maisha haya jamaniiiii
 
Huu mjadala unathibitisha wanaosema wanawake huwa hawaongei kutafuta solution wanaogea kutoa nyongo tu basi (though mimi nakuwa outlier kwenye hili swala), mtu unapewa solution unatumia muda kuelezea nadharia, mara nampenda, ananipenda, sijui sisi waafrika, hukutaka solution ulitaka tu kuelezea hisia zako otherwise majibu yako yangejikita zaidi kwenye nini ufanye na ufanyeje, practical solutions, wewe umejikita zaidi kwenye hisia zako juu ya tatizo zima na mumeo na mdogo wako.

Samahani me sina suluhisho nilikuwa nasoma tu comments.

Pia I can't relate to your problem maana mimi nyumba yangu ni kama kituo cha mabasi yaendayo kasi ile sas 12 jioni, tukipika mchana utadhani msiba kumbe hata mgeni hamna siku hiyo, sitting room utafikiri kibanda cha kuonyeshea mechi, na vyumbani ndo usiseme utafikiri kambi ya wakimbizi hadi tumeamua kuongeza kitanda kwingine chumbani kwetu mashemeji wapate pa kulala, juzi nikasikia wanatuteta eti hii mimba ya nane wameipataje mbona kila siku tunalala wote?
pole kwa kituo cha mabasi. Mimi anaishi mtu mmoja tu anaeshinda jioni tu akitoka chuo, weekend anashinda nyumbani kwa wazazi. Mda mwengine hata usiku hali chakula nyumbani anakula anapotoka.
 
Na
Huu mjadala unathibitisha wanaosema wanawake huwa hawaongei kutafuta solution wanaogea kutoa nyongo tu basi (though mimi nakuwa outlier kwenye hili swala), mtu unapewa solution unatumia muda kuelezea nadharia, mara nampenda, ananipenda, sijui sisi waafrika, hukutaka solution ulitaka tu kuelezea hisia zako otherwise majibu yako yangejikita zaidi kwenye nini ufanye na ufanyeje, practical solutions, wewe umejikita zaidi kwenye hisia zako juu ya tatizo zima na mumeo na mdogo wako.

Samahani me sina suluhisho nilikuwa nasoma tu comments.

Pia I can't relate to your problem maana mimi nyumba yangu ni kama kituo cha mabasi yaendayo kasi ile sas 12 jioni, tukipika mchana utadhani msiba kumbe hata mgeni hamna siku hiyo, sitting room utafikiri kibanda cha kuonyeshea mechi, na vyumbani ndo usiseme utafikiri kambi ya wakimbizi hadi tumeamua kuongeza kitanda kwingine chumbani kwetu mashemeji wapate pa kulala, juzi nikasikia wanatuteta eti hii mimba ya nane wameipataje mbona kila siku tunalala wote?
ndo ushauri nliokua naomba kwamba mtoto namwambiaje sasa nenda nyumbani hapa basi. Naona watu wananihukumu. Hakuna anasema mwambie dogo sasa ondoka yani hilo neno la busara ndo nnalolitafuta.
 
Back
Top Bottom