Mume wangu hapendi ndugu zangu

Mume wangu hapendi ndugu zangu

daah, pole sana

hapo imebaki hatua mbaya zaidi, endeleeni kuomba na ikiwezekana mdogo ako ahame hapo alipo

allivyoweka chumvi huoni ni Mungu tu angeweza kuweka sumu? maisha haya jamaniiiii
Ahsante sana .
Yani dada angu ana mtihani Sana.
Mdogo wetu kuondoka hawezi maana anamsaidia Dada kwenye uzazi maana kipindi Cha mwisho Cha ujauzito alikua na changamoto.
 
Mdogo wangu ana akili sana huwa tunakaa tunapiga sana story na tuna viakili flani vinafanana. Ni mtu ambae ukimuuliza swali straight forward anajua unataka kumaanisha nini. Na hata mimi ndo nilivyo. Ukija ukiniuliza swali flani, ntajua unataka information gani au unanishutumu. Naona bora nisali tu Mungu ali sort
Ubaya wa watu wazuri kama wewe dada huwa wanaweza kumuamini mtu kwa asilimia zote kirahisi maana wanahisi kila mtu ana moyo mzuri kama wao

Dunia hii kila mtu ana dark side ambayo wewe huijui, KAMWE usiusesemee moyo wa mtu, iwe mdogo au mume wako

Uaminifu uliokithiri huzaa uadui na chuki iliyokithiri. Kuwa makini isikukute
 
Namrudishaje nyumbani mtoto sasa nawaambiaje? Wakati mimi ndo nilishadadia aje akae huku karibu na chuo. Leo nasema arudi kwasababu gani.
Kama ni mwanafunzi wa chuo, mtafutie chumba ajitegemee mtaani, hapo kwako anaweza kuja weekends.
 
Never gaslight hasa katika hiki kizazi, utavuna mabua. Ubinafsi amekuja ujulia ndani ya ndoa, muulize sababu ni nini hasa maana mwanamke sikuzote hujitoa ndani ya picha mbaya. Aseme ni nini hasa lasivyo hata process za ndoa zisingeenda na mwanaume mbinafsi hutambulika mapema sana kuliko mwanamke.

Sent using Jamii Forums mobile app
Hiyo tabia ni ya muda mrefu ni vile watu huficha makucha kipindi Cha mahusiano na kujidhihirisha ndani ya ndoa. Hata mwanamke mbinafsi huonekana mapema pia all in all hii tabia sio kabisa Mimi najuaga wanaume watu wenye mioyo safi wasio na hekaheka kama hizi kulinganisha na wanawake
 
Story ya upande mmoja hii, hatujajua mapungufu ya mleta mada na mdogo wake. Nnavyowajua wanawake (hasa hawa waliolelewa na mzazi mmoja) huwa wana matatizo sana kwenye mahusiano so tutunze maneno yetu.
 
Na

ndo ushauri nliokua naomba kwamba mtoto namwambiaje sasa nenda nyumbani hapa basi. Naona watu wananihukumu. Hakuna anasema mwambie dogo sasa ondoka yani hilo neno la busara ndo nnalolitafuta.
Siku hizi sipendi kutoa ushauri lakini ngoja nijaribu.

Mwambie mdogo wako una tatizo la uzazi so unaomba arudi nyumbani kwa muda mbaki wenyewe , kuna kitu mlishauriwa. Hopefully anakuheshimu kama mkubwa wake so hatouliza maswali mengi. Kama mna utani sana iweke kirafiki I such a way asijifikirie yeye akufikirie wewe na tatizo lako
 
Ahsante sana .
Yani dada angu ana mtihani Sana.
Mdogo wetu kuondoka hawezi maana anamsaidia Dada kwenye uzazi maana kipindi Cha mwisho Cha ujauzito alikua na changamoto.
Mungu atamvusha, maombi yenu kwake Mwenyezi Mungu atayasikia
bora ameondoka

hivi jamani kwa nini watu tunakuwa wabinafsi kama tunajua sekunde ijayo ya maisha yetu? Mungu atuongoze
 
Mungu aniepushie hili🙏
Ubaya wa watu wazuri kama wewe dada huwa wanaweza kumuamini mtu kwa asilimia zote kirahisi maana wanahisi kila mtu ana moyo mzuri kama wao

Dunia hii kila mtu ana dark side ambayo wewe huijui, KAMWE usiusesemee moyo wa mtu, iwe mdogo au mume wako

Uaminifu uliokithiri huzaa uadui na chuki iliyokithiri. Kuwa makini isikukute
 
Nani kakwambia nimelelewa na single mom? Mama angu kavumilia hadi leo anavumilia vituko vya mmewe eh ya huko sitaki kuyaingilia hayanihusu. Yangu yenyewe napambana nayo. Mapungufu yangu ndo yakamfanye mtu amchukie mtu mwengine? How
Story ya upande mmoja hii, hatujajua mapungufu ya mleta mada na mdogo wake. Nnavyowajua wanawake (hasa hawa waliolelewa na mzazi mmoja) huwa wana matatizo sana kwenye mahusiano so tutunze maneno yetu.
 
Anajua sina tatizo la uzazi ila asante kwa ushauri. Ni wazo zuri sana naanza kupata mwanga wa design ya vitu vya kushauri
Siku hizi sipendi kutoa ushauri lakini ngoja nijaribu.

Mwambie mdogo wako una tatizo la uzazi so unaomba arudi nyumbani kwa muda mbaki wenyewe , kuna kitu mlishauriwa. Hopefully anakuheshimu kama mkubwa wake so hatouliza maswali mengi. Kama mna utani sana iweke kirafiki I such a way asijifikirie yeye akufikirie wewe na tatizo lako
 
Hakuna wetu wenye lawama kama ndugu!! Ndugu hutumika kuvunja ndoa ! Kwani wakati unamleta ndugu yako ulimshirikisha mumeo? Kama uliamua mwenyewe kumleta bila kumshirikisha mume wako hapo Kuna shida! Kwa maelezo yako unapenda sana kuleta ndugu nyumbani kwako ukishaolewa unahitaji nafasi ya kuishi na kujitawala namume. Ndugu wakishajaa kwenye nyumba Kuna freedom kubwa hupotea kwa wanandoa mfano itakuwa ngumu kumhag mume akiwa anatoka kazini wakati ndugu wamejazana sebuleni hata mapenzi mtaanza kuvizia usiku tu wakati ndugu wamelala nk
Kuna watu by nature hawapendi wageni pengine mume wako yupo katika hilo group kumbadili itakuwa ngumu itabidi umvumilie tu maana hakuna namna ! Nimeandika mengi lakini ndugu Wana changamoto sana sio wa upande wa mke Wala wa mume! Mke anaweza kuwa anatumia muda mwingi na ndugu zake kuongea mambo tu ya kwao akasahau kabisa kuwa kaolewa
 
Anajua sina tatizo la uzazi ila asante kwa ushauri. Ni wazo zuri sana naanza kupata mwanga wa design ya vitu vya kushauri
👌You killed it, kwa sentensi yako umefanya vizuri kukataa roho ya matatizo ya uzazi, akhuu mwenzio tafuta kitu kingine cha kudanganya na si hicho maana shetani yuko hapo pembeni ana nukuu na Mungu ananukuuu,,,isije kuwa fimbo ya kukushitakia kwa Mungu kuwa "alisema ana matatizo ya uzazi",,,NGUVU YA MANENO YA KINYWA CHAKO...huwezi kosa kitu cha kujitetea ila usichukue hicho,,,hahahahhahahahahaha
Anajua sina tatizo la uzazi ila asante kwa ushauri. Ni wazo zuri sana naanza kupata mwanga wa design ya vitu vya kushauri
 
Habari wakuu, nahitaji ushauri,

Mimi ni binti nimeolewa naishi na familia, mume wangu pamoja na mdogo wangu wa kike. Tatizo ni kwamba mume wangu amekuwa na kisirani sana juu ya huyu mdogo wangu wa kike. Kila anachofanya lazima mwanaume alalamike.

Na wala sijawahi kuwa na mawazo labda anamtaka, ndiyo maana anafanya hivi visirani vyote. Mazingira niliyomlea mdogo wangu namjua na ana tabia njema sana.

Mume wangu pia siwezi kumuhukumu kwa uhuni, hajanipa sababu ya kufanya hivyo. Kwahiyo kinachonichanganya ni kwanini ananipa wakati mgumu wa kumfanya mdogo wangu aishi kama yuko kwa mtu baki wakati mimi ni dada yake wa kuzaliwa naye kabisa?

Kila kitu ni lazima aseme kana kwamba huyu mtoto anamkwaza. Kinachoniuma mimi ni kwamba kila siku namuuliza hivi kama angekuwa anaishi hapa ndugu yako halafu mimi namfanyia hivi
Ungejiskiaje? Si ningeonekana mimi ndiyo mbaya sipendi ndugu wa mume?

Na kinachonishangaza, kuna kijana tunaishi naye hapa siyo ndugu wa damu wa mume wangu lakini anatusaidia kazi za hapa nyumbani, ametokea kijijini kwao. Sasa huyu hata akosee vipi mume wangu ukimwambia huyu kakosea hiki na hiki wala hutomuona akijigusa kwenda kumfokea wala kumsema.

Sana sana atajibaraguza tu ili uone ame 'react' na hii siyo mara ya kwanza. Chochote kinachomuhusu mtu wa kwao hutomuona mume wangu amekasirika, lakini ikiwa ni swala la kuhusu ndugu yangu atafoka haswa.

Inafika hatua anamnyima hadi vitu vya kutumia ndani ambavyo hata yeye anavitumia. Hiyo siyo shida, naumia kwasababu mimi huyu mtoto namchukulia kama mwanangu wa kumzaa, nimelichukua hilo jukumu kwa mama yangu tangu mdogo na kwa sasa mama haishi Dar na hatujawa na mahusiano mazuri sana na baba yetu kwa sababu ya mambo ambayo amekuwa akifanya kwetu sisi kama familia.

Kwahiyo najitahidi sana mdogo wangu asijihisi mpweke wala asione kuna pengo la kuumizwa kimalezi na baba yetu.

Na kuna siku ilikuwa sikukuu, nilimwambia mume ndugu zangu wanakuja kwasababu wazazi wetu hawaishi hapa Dar naomba sisi hapa tuwafanyie kitu kama kuwaalika wale hata chakula cha kawaida tu, akasema yeye hana hela.

Wala sikukasirika, nikajikokota nikanunua vyakula nikapika nioneshe kama mume wangu ndiyo amewaalika na wao waone wana kaka hapa mjini. Mume wangu wala hakuonesha ule ushirikiano ambao mimi huwa nautoa wakija ndugu zake, maana huwa napika haswa hadi kwenye kuni.

Nahangaika, napanga, naandaa, nikijua ndugu wa mume wangu wanakuja ila siku wamekuja wadogo zangu sikupata ushirikiano huo. Nilisema acha tu nivumilie kwasababu namheshimisha mume wangu mwenyewe.

Mara nyingine aliniliza na nikamwambia mimi huwa silii lakini unanitenda kama vile sisi kwetu ni masikini, yaani wadogo zangu walipita kutusalimia wakawa sebuleni akaniita chumbani akaniambia nataka kuja kukaa sebleni, naomba nikute siti ya kukaa. Kanakwamba wadogo zangu wamejaa pale maana walikuja kusalimia.

Kinachoniuma ni kwamba, sisi katika kukua kwetu hatujawahi kulelewa na ndugu, kama wadogo zangu wanakaa nje ya kwa baba na mama basi kwangu ndiyo pa kwanza, kwahiyo nikiona wanatendewa hivi naona kama ni mimi ndiyo napitia, sitamani wajione watu baki.

Na kuna muda huwa nawaza, ningekuwa na uwezo ningejenga nyumba yangu niwaweke wadogo zangu hadi watakapokuja kuolewa. Atakae tawanyika sawa, ila kwakuwa mzazi wetu ana uwezo ataona nampokonya wanae. Ila natamani sana wadogo zangu waishi maisha niliyotamani kuishi.


Ushauri unaohitajika;

1. Ni kosa mimi kumtetea mdogo wangu? Kwasababu ninapo jaribu kuuliza kwani tatizo lipo wapi hadi ufoke juu ya jambo dogo hivi, naonekana mkorofi au nataka kumpanda mume kichwani?!

2. Kiubinadamu, huyu mdogo wangu amekosea kuja kuishi kwangu? Nimemlea na hana tabia mbovu kwahiyo namjua, na kila siku namwambia mdogo wangu ikitokea leo dada yako nimedondoka, watoto wangu hutowaacha naamini.

Nampenda sana huyu mtoto, Mungu pekee ndiyo anajua. Kuna muda namwambia mume wangu basi nisamehe mimi naomba vumilia kidogo huyu mtoto akipata kazi ataondoka.

Kwasababu siyo kwamba kwetu tuna shida ya kifedha na wala mume wangu hamgharamii chochote zaidi ya chakula ninachokula mimi ndiyo anachokula huyu mtoto. Ni anakaa kwangu kwasababu ni karibu na chuoni anaposoma yeye.

Kwa upande wa nauli na gharama za kujikimu anatoa mzazi na mimi nikipata huwa nampa kidogo, nashindwa hata kusema namuhudumia maana biashara niliyokuwanayo ilishavurugika baada ya kumuomba mume tusimamie wote ili asiwe na wivu na wateja (stori ndefu haihusiki na mada).

Kwahiyo sina uwezo wa kumgharamia mdogo wangu kwa asilimia mia ila nikipataga 20, 30 nampa ajisogeze. Na mdogo wangu najua ananijali sana, kuna vitu ananifanyiaga huwa nahisi kama nina binti wa kike kabisa.

Yaani kiufupi sipo tayari ndoa yangu iingie doa kwasababu ya mimi kumtetea mdogo wangu na sipo tayari kugombana na mdogo wangu kwasababu yoyote, sijui kama nimeeleweka hapa?

3. Nifanyeje ili mume wangu awe na amani, mdogo wangu pia awe na amani na asijue kwamba shemeji yake huwa analalamika? Kwasababu kila ambacho mume huwa analalama mimi huwa natafuta namna ya kumuelekeza mdogo wangu kama vile mimi ndiyo nataka iwe hivyo, namwelekeza ili asije akafanya tena mume asione tunamdharau.

Na kibaya ni kwamba kuna siku mdogo wangu alisikia nikilalamika sana kwamba hii hali ya yeye mume wangu kukosa amani inaninyima raha, nataka anisaidie mawazo nifanyeje ili awe na furaha na nimuelewe ili niwe namrekebisha mdogo wangu na mimi niwe na amani, hakunijibu! Kesho yake mdogo wangu alikosa raha na sikutaka tena kuibua hiyo mada.

Kiukweli ndoa yetu haina miaka mingi lakini naumia, nilitamani sana mume wangu amlee mdogo wangu kama ambavyo mimi ningelea wa kwake. Lakini inanipa wakati mgumu sana kwamba isije ukatokea mtafaruku kati yao. Nitakae kuwa kwenye wakati mgumu ni mimi.

Uadui huwa hauishi ikiwa mmoja akijua mwengine anamchukia. Na kuna muda huwa namwambia mume, natamani hata na wewe aje ndugu yako hapa akae nikuoneshe jinsi inavyokua kuishi na familia, kuna vitu unavichukulia kama ni mwanao kafanya. Na mume kwangu ana upendo, anajitahidi sana kwakweli, kama kuna makosa ni madogo ya kiubinadamu, ndiyo maana nafukia mengine yoote.

Ninachotamani ni ushauri tu wa kumfanya mume wangu amuone mdogo wangu kama mdogo wake. Niwe na amani pia.

Naombeni ushauri.
Umeolewa ww au mdogo wako?.

Peleka dogo nyumbani huyo acheni maswala ya kiswahili, ww usingeolewa angeishi wapi?.

Kiukweli hili swala la ndugu kujazana kwa wana ndoa ni kero kubwa na ndio sababu mojawapo ya ndoa nying kuyumba na mwishowe kuvunjika.
 
Kumbe ulizoandika ni sifa njema?
Sasa unataka ushauriwe nini?.

Kaa pembeni uvue huo ujuaji then urudi jukwaani upokee ushauri labda utaelewa.

Mmeo atakuwa yuko sahihi lakini nina hisi kuna kitu hakiko sawa kwako.
Sio lazima unjibu...naishia hapa
Na kweli nimjuaji ,na ana maneno mengi hashauriki,walomshauri ampangie ndugu yake wametisha sana,hiyo ndo solution.. anaonekana anapenda misifa anataka mamaake amuone *HERO*kwamba anamsaidia majukumu huku kwny reality analeta mvurugano na mmewe anaependa privacy,ndoa bado changa "km alivyo sema mtoa post"mme anataka privacy a-enjoy na mkewe , awe huru na mji wake ,sema mkewe ndo much know wa viwango
 
Na wala sijawahi kuwa na mawazo labda anamtaka, ndiyo maana anafanya hivi visirani vyote. Mazingira niliyomlea mdogo wangu namjua na ana tabia njema sana.
ring... ring... ring... kengele hiyo inatakiwa ikuamshe kimawazo.

Rudisha huyo mdogo wako nyumbani haraka sana, inawezekana japo hakuambii kiukamilifu lakini kuna kitu kimejificha.
 
Back
Top Bottom