Mungu aliyeumba Milkway(kilimia) galaxy na ulimwengu kwa ujumla ni mkuu sana

Mungu aliyeumba Milkway(kilimia) galaxy na ulimwengu kwa ujumla ni mkuu sana

Kuna watakaodai kwamba eti hayo yote ni kwa sababu ya Bing bang theory,,,ambayo Bado haijawa Bing bang law... Nadhani wanaendelea kujiridhisha na Bing bang kama inaweza kuwa law au ipigwe chini kama Darwin theory of evolution
In short bado haujui maana ya theory kwenye science...unaichanganya na maana ya Theory in Language.
Utakuwa ulisoma HKL
 
Nadhani nami pia nahitaji elimu zaidi juu ya malimwengu (galaxies)
1. Tofauti ya universe, galaxy, constellation, star, some sort of those nebula and star dusts ni kipi na kipi siyo kipi.
Universe ni kila kitu (Galaxies+Nebula+planets+blackholes+Everything).

Galaxy ni kundi la nyota zinazoorbit kwenye plane moja(galaxy nyingi zina nyota nyingi sana mabillioni kwa matrillioni).Mfano wa galaxy ni hii tunayoishi inaitwa milkyway.

Constellation ni nyota ambazo zinaunda shape fulani ukiziangalia kutokea duniani..Mfano kuna nyota zina shape ya nge wanaita scorpion constellation, Lakini kiuhalisia unaweza kukuta nyota ya kichwa cha nge na nyota ya mkia wake zimeachana umbali wa lightyear hata 1000(haziko pamoja)..Constellation zote tunazoziona zipo ndani ya galaxy yetu ya milky way.

Nyota ni body angani inayotoa mwanga kwa kuunguza gesi zake.

Nebula ni wingu kubwa la vumbi au gesi angani, mara nyingi huwa ni gesi au vumbi zinazopatikana baada ya nyota kufa.(stardust)
2. Ni kweli Milky way Galaxy (njia ya maziwa ndiyo seven sisters constellation (kilimia)?
Si kweli...constellation zipo ndani ya galaxy.
Ukielewa jibu la hapo juu hii inajieleza
3. Our universe ( Milky way Galaxy) with 9 planet (entirely solar system) including our home Earth is the same to kilimia (seven sisters constellation)
Ukielewa jibu la kwanza hili swali halimake sense.
4. Je hiyo Orion/Lion (Simba mwindaji) constellation iko hapa kwenye solar system au iko kwenye galaxy nyingine km vile spiral galaxy, au Andromeda ( our neighboring galaxy?
Ipo kwenye milky way, Constellation zote zipo milky way..Yaani nyota zote tunazoziona angani hazizidi 6000 tu. Lakini milky way ina nyota billioni 100-400
5. Je kuna ulimwengu/malimwengu/ universe ngapi? Na kila universe is it equal or same as galaxy or equal to constellation or star?
No one knows.
Lakini kuna kitu kinaitwa observable universe..Yani sehemu ya ulimwengu inayoonekana.
Hiyo sehemu ya ulimwengu inayoonekana ina galaxies kama milkyway zaidi ya trillioni 2
Na hapo bado kuna unobservable universe, yani ile sehemu ya ulimwengu ambayo mwanga wake haujafika duniani na hautakuja kufika kwasababu ulimwengu unapanuka fasta kuliko spidi ya mwanga.

Na inaaminika ulimwengu ambao hatuuoni ni mkubwa kuliko tunaouona wenye galaxies trillion 2.

Lakini swali la je, ulimwengu una mwisho? Upo mmoja? Hayana majibu..No one knows.
6. Vipi kuhusu makundi nyota hizi (constellation) dubu, nge, vigor, msalaba wa kusini, Orion vs Betelgeuse (the giant star in constellation) , kilimia nk?
Yote yapo katika hizi nyota 5000+ tunazoziona kwa naked eyes hapa duniani. Zote zipo milky way, tena huu upande tuliopo sisi, kasehemu kadogo sana.
7. Je Orion vs Betelgeuse deep hole concerp of heaven place ikoje boss?
Hizi ni story za kufikirika hazina ushahidi wowote. Ni changamsha genge la kanisa au kijiwe cha gahawa tu.
Mi sijakupata Mzee baba naomba ongeza nyama kwenye huu Uzi km bado upo kwenye hili jukwaa.

Ahsante sana
emoji120.png
emoji120.png
 
Isa 55:8-9

Maana mawazo yangu si mawazo yenu, wala njia zenu si njia zangu; asema BWANA. Kwa maana kama vile mbingu zilivyo juu sana kuliko nchi, kadhalika njia zangu zi juu sana kuliko njia zenu, na mawazo yangu kuliko mawazo yenu.
 
Hakika ni Mungu mwenye nguvu sana yeye ni Niko ambaye Niko[emoji3531][emoji3531]
 
Napenda sana mambo ya astronomy, jua linapozama tu kwanza nakaa sehemu ambayo Haina light pollution na Huwa naangalia sayari kama Venus, Jupiter Saturn na mars kwani huonekana vizuri sana.

After sometime natupia macho yangu na kuangalia constellation mbalimbali ambazo nishajifunza kama Orion, Gemini, canis major, canis minor, casiopia, na Andromeda.

Nilijifunza pia, kuwa ukiacha hii milkyway unaweza kuiona galaxy nyingine ambayo ni Andromeda, kweli nikafanya jitihada mpaka nimefanikiwa kuiona iyo galaxy ambayo ipo karibu na caseopia na Andromeda constellation.
 
Ukishamaliza kuimba pambio za sifa, Nenda kaulize tena kwa mungu wako

Kwanini kafanya tubanane kwenye kisayari hiki kidogo_Wakati kuna masayari ya kumwaga
Una uhakika gani kama hakuna viumbe kwenye sayari nyingine katika galaxies nyingine, hata hiyo Milky Way kuna uwezekano bado ni small part ya mfumo mzima lakini uwezo wa binadamu kwa sasa umeishia kufahamu hayo tu.
Kuhusu super natural power or rather super natural creator(Mungu) ya kwamba alitamka tu vyote hivyo vikatokea nobody can prove that.
 
Kwa hiyo kumbe macho yanaona hayo makilometa yote hayo ya mwanga?
Kama nyota zinaonekana kwann usione milkyway? Kikubwa uwe sehemu isio na taa nyingi miji mikubwa ni ngumu kuona kwakua anga linaakisi mwanga wa taa ila ukiwa kijijini unaiona vizuri tu
 
Ni kweli kabisa ndugu. Mm nakaaga na dogo nje toka nimemuonyesha hii kitu ananiuliza maswali hadi nabaki nastaajabu uumbaji wa mungu yaani nafurahi sana dogo anapozingatia hasa akiwa mwenyewe nimemnunulia darubini ya 1000× military anajitahidi sana kuangalia anga usiku kila akienda kwa bibi yake hawez acha kifaa chake
Mkuu darubin kama hiyo naweza Pata wapi na kwa gharama kias gani?

Sent from my TECNO-C8 using JamiiForums mobile app
 
"Na kwa hakika tumekuwekeni katika ardhi, na tumekufanyieni humo njia za kupatia maisha, ni kuchache mno kushukuru kwenu.."

Qur'an 7:10
Je ni kina nani hao waliotuweka wanadamu hapa, maana wanasema Kwa nafsi ya.kwanza wingi
 
Ni kweli kabisa ndugu. Mm nakaaga na dogo nje toka nimemuonyesha hii kitu ananiuliza maswali hadi nabaki nastaajabu uumbaji wa mungu yaani nafurahi sana dogo anapozingatia hasa akiwa mwenyewe nimemnunulia darubini ya 1000× military anajitahidi sana kuangalia anga usiku kila akienda kwa bibi yake hawez acha kifaa chake
Mkuu hiyo 1000× military unaweza kuona mambo mengi? ukirudi utanijulisha naona umekula ban ya kimataifa.
 
Napenda sana mambo ya astronomy, jua linapozama tu kwanza nakaa sehemu ambayo Haina light pollution na Huwa naangalia sayari kama Venus, Jupiter Saturn na mars kwani huonekana vizuri sana.

After sometime natupia macho yangu na kuangalia constellation mbalimbali ambazo nishajifunza kama Orion, Gemini, canis major, canis minor, casiopia, na Andromeda.

Nilisikia kuwa ukiacha hii milkyway pia unaweza kuiona galaxy nyingine ambayo ni Andromeda, kweli nikafanye jitahadi mpaka nimefanikiwa kuiona iyo galaxy ambayo ipo karibu na caseopia na Andromeda constellation.
Mkuu nikitaka kuiona andromeda nifanyaje?.
 
Mkuu nikitaka kuiona andromeda nifanyaje?.
Kuna njia nyingi,

Kwanza, unaweza kutumia bright stars za constellation ya caseopia kuweza kukuongoza Hadi kwenye iyo galaxy.

Pili unaweza kutumia stars za Andromeda constellation kuona Andromeda Galaxy.

So lazima ujifunze kwanza namna na kujua location ya hizo constellation mbili, then itakuwa rahisi kuiona.

Unaweza download application za star map na unaweza kujifunza YouTube kuhusu hizilo constellation na vitu vingine
 
Back
Top Bottom