Mungu atawaadhibu kwa dhambi za wazazi wenu, hata kizazi cha tatu mpaka cha nne

Hauoni au unajifanya kutokuona ,
  1. Izo dhambi za waisrael zinakuhusu nini wewe mpaka nyama ioze mpaka leo?
Bado hiyo hadith haijadai kuwa mpaka leo nyama huoza sababu ya waIsrael, na wala haikutaja kuwa sababu ni DHAMBI za Waisrael kama unavyodai.

Vipi kama imetaja wakati ule mahususi ambapo WaIsrael walikuwa jangwani wakashushiwa chakula na wakaambiwa wasihifadhi bali wale kinachowatosha, badala yake wakahifadhi na matokeo yake kikaoza?
  1. na dhambi ya eva iinawahusu nini wanawake mpaka leo wanatoka nje ya ndoa?
Wapi pamesemwa ni kutokana na dhambi yake?
Suala la mama yetu Hawa hadithi haijasema kimahsusi kutokana na dhambi yake, imesema tu “Isingekuwa Hawa Wanawake wasingewasaliti waume zao”

Vipi kama inamaanisha asingeumbwa Hawa wanawake wasingekuwepo, kutokuwepo kwao kungemaanisha kusingekuwa na ndoa, ambapo ingemaanisha kutokuwepo kwa usaliti kwa waume zao?

NB: Na hiyo ni kutokana na kibailojia kwamba ili watu wazaliwe ni lazima awepo ME na KE.

Na vipi kama inamaanisha tendo la Hawa kula tunda kule Eden linamaanisha ushawishi alokuwa nao Hawa kwa mumewe Adam, ambapo umerithishwa kijenetiki na kimazingira kwa KE wote. Sio siri tunafahamu Wake zetu wana ushawishi mkubwa kwetu na wengine ni wanautumia kufanya ulaghai?.
Kuhifazi ❌
Kuhifadhi ✅

Frigi ❌
Friji ✅

Si jokofu tu, Binaadamu walizikausha nyama kwa moshi na kuzihifadhi miaka mingi jokofu halijagunduliwa na hazikuoza haraka mkuu.

Ninachojaribu kusema ni kuwa hadith iko ‘vague’ hivyo inavutia tafsiri za kila namna, ktk muktadha huu ni lazima tuwaulize wataalam wa somo hili la hadith kutupa ufafanuzi.
 
Ndio tatizo la Kanisa la sasa. Usomaji wa biblia wa namna hii ya kutumia nukuu za agano la kale bila utimilifu wake kwenye agano jipya si Ukristo! Ni dini ya kiyahudi.

Ukibatizwa ya kale yamepita yanakuwa mapya! Ubatizo unafuta hadi dhambi ya urithi ya Adamu na Eva achilia mbali za baba yako wa juzi. Ukisema unabaki na hizo laana ni ku undermine nguvu ya ubatizo ambao ndio sakramenti pekee inayokuingiza kwenye Ukristo.

Laana na mababa/mababu zinaweza kukupata kutokana na mwenendo wako kwa wewe mwenyewe kujirudisha utumwani. Mfano mbatizwa unaendelea na mambo ya matambiko! Hata watoto wadogo inaleta shida kupitia mzazi, ukihoji utajua shetani amepata wapi uhalali.

Sent from my SM-A315F using JamiiForums mobile app
 
Bado hiyo hadith haijadai kuwa mpaka leo nyama huoza sababu ya waIsrael, na wala haikutaja kuwa sababu ni DHAMBI za Waisrael kama unavyodai.
Unaandika insha hadith ipo wazi kabisa ,
  • Kama sio waisrael nyama isinge oza
  • Kama sio Eva wanawake wasingetoka nje ya ndoa
Muhammad said, "Were it not for Bani Israel, meat would not decay; and were it not for Eve, no woman would ever betray her husband."Sahih al-Bukhari 3399

  1. waisrael ndio sababu nyama zinaoza, sisi tunahusikaje mpaka nyama zioze , tutafute mbinu mbalimbali na kuingia gharama kumzui Allah ?
  2. Eva ndie sababu wanawake wanatoka nje ya ndoa ,wanawake wanahusikaje na aliyofanya Eva mpaka leo wanatoka nje ya ndoa , kwa nini lisiishie kwake ?
 
Vipi kama inamaanisha asingeumbwa Hawa wanawake wasingekuwepo, kutokuwepo kwao kungemaanisha kusingekuwa na ndoa, ambapo ingemaanisha kutokuwepo kwa usaliti kwa waume zao?
Huu ni ujinga umeandika nautupa kwenye 🚽
 
Wapi pamesemwa ni kutokana na dhambi yake?
Suala la mama yetu Hawa hadithi haijasema kimahsusi kutokana na dhambi yake, imesema tu “Isingekuwa Hawa Wanawake wasingewasaliti waume zao”
Hawa alifanya nini mpaka leo wanawake wanawasaliti waume zao?
Kwa nini hilo jambo lisiishie kwake tu?
 
Kwa hivyo laana ipo pale pale duuh ya kizazi chatatu mpaka channe! Watoto mpaka wajukuu

Makosa hasa hayo ambayo yapo hapo ambayo yanafanywa na wazazi na kuja kupelekea laana kwa watoto ni yapi? Haswa

Kosa lolote ambalo hautalilipia ukiwa hai lazima kizazi chako kilipie kama deni.

Baraka yoyote ambayo haujaitumia ukiwa hai lazima Watoto wako walipwe
 
Hapo sijaona kuwa Mungu anatuadhibu kwa kuozesha nyama kisa WaIsrael, sijaona ati Mungu anawafanya KE wasaliti waume zao kisa Hawa.

Au wewe umeona wapi bwana Mokiti
Ana maana kua dhambi Eden wamefanya wailing,lakini kipigo tunapata sisi,kwanini adhabu isingekoma palepale Eden??pia mtoa maada kaweka mstari nusu, mwisho unasema nami nawarehemu maelfu elfu wanipendao na kushika amri zangu
 
Nadhani hii alijiwekea kama principle yake. Na huenda hii inatokana na ukweli kuwa, Mungu akikujalia jambo fulani, hawezi kukunyang'anya, hata kama utakufuru kiasi gani; huu ni uadilifu wake kwetu sisi binadamu. Mungu sio kigeugeu kama tulivyo binadamu; sio ajabu kwetu kumpa mwenzetu kitu au msaada fulani, lakini tunabadili mawazo na kumnyang'anya tena; Mungu akikupa amekupa.

Sasa habari ya kupatilisha adhabu inakujaje? Hii inakuja ili kufuta Makosa aliyoyafanya ancestor wenu na kuanza mahusiano mazuri na Mwenyezi Mungu. Tukumbuke dhambi hudumu katika damu, vivyo hivyo ancestors wetu wanapomkosea Mungu na kufa katika dhambi, dhambi hiyo huiacha kwa damu zao ambao ndio sisi.

Dhambi hurithishwa, Adamu na Hawa walipotenda dhambi pale bustani ya Edeni, deni hilo mpaka leo tumebebeshwa na hatujuwi litaisha lini. Kumbe hata dhambi ya kurithi kwa mababu (ancestors) zetu zina afadhali, maana Mungu amesema anapatilisha mpaka kizazi cha nne, lakini hii ya kutoka kwa Adamu na Hawa haina kikomo. Labda huko mbele Mwenyezi Mungu anaweza kubadili mawazo na kuiondoa kabisa.

Tukumbuke Yesu Kristo alitolewa sadaka (kafara) kwa ajili yetu, hii yote ni mapenzi mema ya Mungu kwetu sisi binadamu. Dhambi zetu zilisababisha Yesu Kristo amwage damu yake kwa kusulibiwa msalabani ili kuondoa dhambi zetu na hatimaye kutupatanisha na Mwenyezi Mungu! Kumbe sisi kutumikia adhabu za mababu zetu ni njia ya kurudisha uhusiano mwema kwa Mungu wetu!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ukimchunguza huyu Mungu utagundua ana stress na matatizo mengi kuliko sisi wanadamu.

Ipo siku tutampoteza huyu Mungu sababu anaonekana anao msongo wa mawazo
 
Biblia ni Fiction stories, Hadithi za kusadikika.

Biblia ingekuwa kitabu cha Mungu kisingekuwa na "mkanganyiko" wa kutofautiana maudhui.

Sent from my Infinix X657B using JamiiForums mobile app
 
Biblia ni Fiction stories, Hadithi za kusadikika.

Biblia ingekuwa kitabu cha Mungu kisingekuwa na "mkanganyiko" wa kutofautiana maudhui.

Sent from my Infinix X657B using JamiiForums mobile app

Habari kwenye kitabu hicho zinapingana zenyewe sijui nan? Alikiandika hicho kitabu
 
Ukimchunguza huyu Mungu utagundua ana stress na matatizo mengi kuliko sisi wanadamu.

Ipo siku tutampoteza huyu Mungu sababu anaonekana anao msongo wa mawazo

Ah ah ah duuuh
 
Mambo mengi tu hushindwa kujibu ila Wana JF wanamkweza sana sababu ya vinukuu vyake mbali mbali vya vitabu vya Wanasayansi na dokezo kidogo za kiingereza basi naye anajiona kumbe katika ulimwengu wa rohoni ni mweupe kabisaaa [emoji1]

Sent from my CPH2387 using JamiiForums mobile app
 

Mjanja mjanja tu

Ameogopa kujibu kwa sababu swali lilikuwa lina mjaji ni kwa mujibu wa nan?

Akisema yeye nani? Anabidi ajibu kwa mujibu wa nan?

Na pia akisema yupo wapi? Ajibu pia Kwa mujibu wa nan?

Wanasoma soma wajinga wajinga kwenye mavitabu yao huko wametuandikia ujinga tu ili watutawale na sisi tumewaamini hatari, hapo sana sana akijaribu kujibu hilo swali atakuwa anachekesha tu maana hatoweza kujibu kuringana na kichwa chake atatoa ujinga ujinga alinakirishwa na wazembe ili wamtawale
 
Baba yako alikufa bila ya kutubu dhambi, tambua kipindi anafanya huenda ulikuwa bado upo kiunoni mwake hujazaliwa au ulishazaliwa.

Ni kweli kabisa huusiki, lakini wewe si version ya kizazi cha Baba yako?

Au kwanini uitwe jina lenye ubini wa Baba yako ikiwa huusiki na adhabu za dhambi zake?

Au wewe hupendi kuona uzao wako (Watoto/Wajukuu/Vitukuu) wakiishi vizuri ungali hai, kama unapendezwa na hilo halikadhalika ndivyo ilivyo katika adhabu ambazo Mababu/Mabibi/Baba/Mama zako walifanya kisha hawakutubu wakafa kwa dhambi hizo lakini damu zao bado zi hai kupitia uzao wao ambao ni wewe mwenyewe.

Sent from my CPH2387 using JamiiForums mobile app
 
Kizuri zaidi mwenye mamlaka na uhai wako hasemi neno kwa kuwa lina ukweli ndani yake la hasha! Bali akishasema ndiyo kashatenda, hivyo basi ni swala la muda tu kutimia alichokinena utake usitake maana Mungu huwa hapangiwi nini cha kufanya na Binadamu.

MATHAYO 24:35

Mbingu na nchi zitapita; lakini maneno yangu hayatapita kamwe.

Sent from my CPH2387 using JamiiForums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…