Mungu aweza kukutoa kwenye hiyo shida!

Mungu aweza kukutoa kwenye hiyo shida!

YEREMIA 1:12, Ndipo Bwana akaniambia, umeona vema, kwa maana ninaliangalia neno langu, ili nilitimize. (hii maana yake nini?, anatafuta wapi alisema kitu ili akitimize vilevile kama alivyosema, anaangalia alichokisema ili akitimize, analinda kile alichokisema hadi kitimizwe, yupo nyuma ya chochote alichokisema hadi kitimie).
 
Mtoa mada usichoshwe na wale team Kiranga.

Waebrania 11:6 Lakini pasipo imani haiwezekani kumpendeza; kwa maana mtu amwendeaye Mungu lazima aamini kwamba yeye yuko, na kwamba huwapa thawabu wale wamtafutao.
 
Nani kawafanya waumwe kama sio huyo mungu

Imani potofu hizi mimi nakuambia
🤣🤣🤣📌
Waebrania 11:1 Basi imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni bayana ya mambo yasiyoonekana.

Waebrania 11:3 Kwa imani twafahamu ya kuwa ulimwengu uliumbwa kwa neno la Mungu, hata vitu vinavyoonekana havikufanywa kwa vitu vilivyo dhahiri.
 
🤣🤣🤣📌
Waebrania 11:1 Basi imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni bayana ya mambo yasiyoonekana.

Waebrania 11:3 Kwa imani twafahamu ya kuwa ulimwengu uliumbwa kwa neno la Mungu, hata vitu vinavyoonekana havikufanywa kwa vitu vilivyo dhahiri.
Chai.
 
Yohane 14:6
Aliyekwisha niona mimi amemwona Baba.
….. Yohana 14:10 Husadiki ya kwamba mimi ni ndani ya Baba, na Baba yu ndani yangu? Hayo maneno niwaambiayo mimi siyasemi kwa shauri langu; lakini Baba akaaye ndani yangu huzifanya kazi zake.
 
Mtoa mada usichoshwe na wale team Kiranga.

Waebrania 11:6 Lakini pasipo imani haiwezekani kumpendeza; kwa maana mtu amwendeaye Mungu lazima aamini kwamba yeye yuko, na kwamba huwapa thawabu wale wamtafutao.
Amen!
 
Hizi kauli kuwa Mungu anaweza, kufunga na kuomba, ni katika dunia ya tatu kwa wingi, ni kwa nini? Usikute kale kausemi kuwa "religion is for low minded people ". Kanafanya kazi. Which comes first, reason or faith? For the third world countries is "faith ".
 
Hizi kauli kuwa Mungu anaweza, kufunga na kuomba, ni katika dunia ya tatu kwa wingi, ni kwa nini? Usikute kale kausemi kuwa "religion is for low minded people ". Kanafanya kazi. Which comes first, reason or faith? For the third world countries is "faith ".
nilishawahi kuishi kwenye dunia ya kwanza, nawafahamu watu wenye pesa nyingi sana, elimu kubwa sana, civilization kubwa, lakini wanapiga magoti, wanasujudu, wanafunga na kuomba mbele za Mungu. Hakuna aliye na hadhi ya kutokumhitaji Mungu hapa duniani, ingekuwa hivyo wazungu wasingeugua cancer, kwasababu anaweza kuwa na kila kitu materially, akawa hana dawa ya kuponya cancer, na icho tu kikamhumble down kiburi chote kikaisha hadi akamtafuta Mungu kwa machozi, kulia, na kufunga. anaacha kula wakati ana kila kitu hadi ampate Mungu.

cha kushangaza ni pale mwanadamu mwingine toka dunia ya tatu kama africa, kama wewe, anapokuja kuamini kuwa religion is for low minded people. wakati hata maisha yako tu ya kipesa yanatia huruma, achilia hayo mengine yanayowahumble hao wengine wa dunia ya kwanza.
 
kwasababu allah sio Mungu wa kweli, ni shetani mwenyewe yaani Ibilisi aliyekuja kupotosha Neno la Mungu wa kweli. pia hapa sipo kwa ajili ya malumbano ya dini, wewe kama allah wako alishawahi kukusaidia chochote utajua mwenyewe ila kwa upande wangu nimethibitisha kuwa Mungu wa Ibrahim Isaka na Yakobo aliyefanyika mwili kwa njia ya Yesu Kristo awe kafara la kutukomboa, huyo pekee ndiye Mungu. mababu zako pia walikuwa na miungu mashetani. mwamini Mungu wa kweli.
🤣🤣🤣🤣🤣Sawa mkuu.
 
Mtoa mada usichoshwe na wale team Kiranga.

Waebrania 11:6 Lakini pasipo imani haiwezekani kumpendeza; kwa maana mtu amwendeaye Mungu lazima aamini kwamba yeye yuko, na kwamba huwapa thawabu wale wamtafutao.
😁😁😁😁Kwa nini unapaswa kuuamini yupo?
 
Tatizo mwisho wa siku mnataka mpewe hela, acheni utapeli!
 
Mimi ndio maana sichelei kusema ulokole ni aina ya ugonjwa wa akili .
 
Mimi ndio maana sichelei kusema ulokole ni aina ya ugonjwa wa akili .
unaweza kuwa sahihi, kwasababu hata wale wagonjwa walioko hospitali ya mirembe, wamefungiwa wasitoke kabisa nje ya geti, huwa wanaamini sisi tulioko huku mtaani ni machizi wa kutupwa, wao ndio wenye akili.

Ndugu yangu, wewe sio wa kwanza kuona ulokole (wokovu) ni upuuzi, katika 1 Wakorintho 1:18 IMEANDIKWA, Kwa sababu neno la msalaba kwao wanaopotea ni upuuzi, bali kwetu sisi tunaookolewa ni Nguvu ya Mungu.

hii njia ya wokovu kwako ni upuuzi na uchizi, ila uhalisia, huku ndiko kwenye uzima na nguvu za Mungu. Mungu akusaidie. mnadhafau sana ulokole ila kuna siku itakuja mtatamani siku zirudi hata moja tu ili muokoke ila muda utakuwa umepita.
 
Wengi huwa wanamwendea Mungu kwa kutia huruma, yaani wanadeka yaani, wakihitaji kuonewa huruma, wakati Mungu anachohitaji kwako ili akutendee chochote ni Imani. unaweza kulia na kutia huruma bila imani ikawa kazi bure. Ni kweli Mungu ana huruma, lakini namna pekee anafanya kazi na sisi ni kwa njia ya imani, ukiwa na shida hutapona kwasababu unatia huruma mbele zake, unapiga magoti uombe badala ya kuomba unalia tuu kwa uchungu, badala ya kumwambia shida zako. Ongea shida yako, amini, nalo litatokea. Sema shida ni kwenye ufahamu wa Neno la Mungu, kuna watu wanamhitaji Mungu wakiwa na shida tu, ila wakati wakiwa wazima au hawana shida hawasomi hata Neno lake hivyo wanakuwa so ignorant of the word of God.

Faith never comes through discussing with people their, pains and aches, weaknesses and sicknesses. Faith is born when we hear the word of truth. Jesus said: You shall know the truth, and the truth shall make You free. He is the truth.

Imeandikwa, Ninyi mkikaa ndani yangu na Maneno yangu yakikaa ndani yenu ombeni lolote mtakalo nanyi mtatendewa. sasa mtu husomi Neno halipo moyoni mwako, utajua unaombaje? na imani yako itakujaje wakati Imani huja kwa kusikia, kusikia Neno la Mungu. muda wote watu wamekalia mitandao ya kijamii mara facebook, twitter, whatsapp, n.k ambavyo havijengi roho, ila wakipata shida hata kipiga magoti kuomba hawana Neno la Mungu moyoni walau la kuwatia imani wajue tu hata maeneo Mungu aliahidi kuwatatulia matatizo yao. mwisho wanaishia kutafuta waombeaji wawauzie mafuta maji na chumvi kama waganga wa kienyeji, na hakuna kinachotokea maishani mwako.

mtakuja kuishia kudondokea hadi kwa waombeaji wenye upako wa kishetani na wanaofanya kweli mazingaombwe, jueni kuwa hata shetani akikufanyia mazingaombwe yeyote ukaona kama kuna badiliko fulani, hakika imeandikwa "baraka za Mungu hutajirisha wala haichanganywi na huzuni (Baraka za BWana hazina majuto). Mungu anaponya na uponyaji wake ni wa kudumu na hauna garama, ni bure, ila mazingaombwe ya shetani hata ukiona kama amekuponya sio wa kudumu na lazima utegemee kulipa garama, waumini wote wa shetani wanajua kuwa hajawaku kukufanyia kitu bure, lazima kuna majuto yameambatana nacho icho kitu na kuna siku utajuta tu. Mithali 10:22.
 
naongea na watu ambao majibu ya madaktari yamewakatisha tamaa kabisa, solution iliyobaki ni kwa Mungu tu.

kuna siku nilishawahi kupitia katika hali kama hiyo, nikasikia sauti inaniambia moyoni "GEUZA MACHO YAKO MTAZAME YESU" turn your eyes unto Jesus. wakati akili za wanadamu zimefika mwisho, hapo ndipo Mungu huanzia. Madaktari hutibu, ila Mungu huponya.

1 YOHANA 5:14 INASEMA, na huu ndio ujasiri tulio nao kwake kwamba tukiomba kitu sawasawa na mapenzi yake atusikia. Na huu ndio ujasiri tulio nao kwake, ya kuwa, tukiomba kitu sawasawa na mapenzi yake, atusikia. 15 Na kama tukijua kwamba atusikia, tuombacho chote, twajua kwamba tunazo zile haja tulizomwomba. UPONYAJI ni mapenzi ya Mungu kwako, hivyo ukiomba uponyaji atakuponya. MARKO 11:24 Kwa sababu hiyo nawaambia, Yo yote myaombayo mkisali, aminini ya kwamba mnayapokea, nayo yatakuwa yenu.
 
Back
Top Bottom