Inawezekana, kwa upande mmoja vitabu vitakatifu na mapokeo kama msingi mkuu wa mafundisho ya dini vimeibua maswali mengi kwa baadhi ya watu kuhusu Mungu.
Na kwa upande mwingine, Ukana Mungu ambao msingi wake ni kutokuwa na uelewa wa kina wa mambo na elimu ya vitu umewavutia watu wengi katika mwelekeo huo kwa sababu ya kutokujua kama ambavyo ilivyo pia kwa wafuasi wengi wa dini.
Kile kinachoweza kuonekana kama kutoelewana - wengine wakikubali kuna Mungu na wengine wakikana hakuna Mungu, kimeendelea hata wakati ambao kuna ukuaji mkubwa wa maarifa ya sayansi na teknolojia. Na kwa kweli ni kama, kwa baadhi wasio na uelewa wa imani na sayansi, na walio na uelewa wa imani na sayansi, sayinsi imeimarisha mwelekeo wao.
Si kweli kwamba sayansi haibainishi kweli za akili, yaani kweli zilizotufikia kwa njia ya imani: mfano kuna Mungu na tokeo la uhai na ulimwengu, kwanini kuna ouvu duniani, nini hutokea baada ya kifo, nakadhalika.
Hatahivyo, pamoja na sayansi kuweka wazi mambo mengi ya imani (dini), ni dhahiri watu wengi bado hawajaelewa, na hivyo wanajiuliza:-
Je , ni kweli Mungu yupo au hayupo? Au Je, ni kweli Mungu yupo mahali pote (omnipresent)? Je, Mungu anauwezo wote (omnipotent)? Je, Mungu anajua yote, ana ujuzi wote; ana maarifa yote (omniscience)?
Na kama ni kweli! Kwa nini Mungu ambaye ni upendo, anauwezo wote, anajua yote, ana maarifa yote, ana nguvu na mamlaka yote, aumbe na aruhusu dunia ambayo inawezekana uovu kufanyika?
Kimsingi mjadala huu au maswali hayo hayawezi kuwa na maana au kujibika kama hatujui msingi wa neno Mungu, (au Hali hiyo) ambaye Ndiye mjadala wenyewe na ambaye Ndiye maswali yanaelekezwa kwake, umetokana na ni nini.
Ndugu zangu:-
Ni nini hutufanya tuseme Mungu? Yaani ni nini tunakirejelea tunapoita Mungu? Neno Mungu au wazo Mungu; au wazo kuna Mungu tumelitoa wapi? Sababu gani zimetusababisha kusema kuna Mungu; au wazo Mungu limesababishwa na nini?
Aidha, wazo hakuna Mungu limetoka wapi na limetokana na sababu gani? Na linapendekeza au linaelezea nini vitu vilivyopo?
Lakini pia, hii elimu tunayokwenda kusoma shuleni na vyuoni: kufundishwa na kusoma, (fizikia, hisabati, bailojia, kemia, jogorafia, sheria, uraia, historia, lugha, uhandisi, taalimungu (theology), elimu ya mtima (psychology), nakadhalika), imetoka wapi? Nani aliileta? Nani aliipangilia na kuiweka katika utaratibu huo? Kwa nini?
Kwa sababu kama ikiwa kila binadamu anapelekwa shule na chuo kujifunza na kusoma, maana yake hayo masomo tunayo kwenda kusoma au hiyo elimu tunayofundishwa shuleni na vyuoni hatukuwa tunaijua au tunaifahamu. Na hii maana yake ni kwamba kuna mtu aliyeijua hiyo elimu ambayo sisi tunakwenda kusoma na kufundishwa.
Sasa basi, huyo mtu aliipata wapi hiyo elimu au hayo masomo tunayofundishwa shuleni na vyuoni yalitoka wapi?
Na je, ni kweli kwamba hiyo ndio elimu (yaani hayo masomo) na kwamba hakuna kitu kingine bora zaidi au utaratibu mwingine wa kupima na kuelewa ulimwengu, ila isipokuwa kwa masomo au elimu hiyo tu?
Unauelezeaje ulimwengu: vitu vyote vilivyopo
Kadiri ya ufahamu wako na kadiri ya unavyoona na unavyoelewa, unaona vitu vilivyopo (ulimwengu ) vimefanyika kwa akili au havijafanyika kwa akili? Na je, unagundua hilo kwa jinsi gani? Je, ni baada ya kufundishwa au ni kabla? Au hugundui hivyo, badala yake unagundua nini?
Na hali hiyo ya vitu vya asili kuwa au kufanyika hivyo vilivyofanyika, inaashiria nini au unaieleza kuwa ni hali gani: yenye ufahamu au haina ufahamu?
Kwa binadamu, vitu vyote vilivyopo angalau vitu vyote anavyoweza kuviona akiwemo na mtu mwenyewe, anaona kuwa vitu hivyo au viumbe hivyo kuanzia na miundo yao ya nje na ya ndani, mpangilio wao, na jinsi yao ya utendaji kazi; ama ni kiungo kimoja kimoja katika kitu au kiumbe kimoja; au ni vitu mbalimbali, vinaonekana kufanyika kwa akili nyingi na upatano wao ni wa hali ya juu sana.
Kwa lugha rahisi, binadamu anaona ulimwengu kuwa umefanyika kwa akili nyingi na upatano wao ni wa hali ya juu sana. Hali hiyo ya mtu ya kufikiri au ya kuona kuwa ulimwengu, yaani vitu vyote vilivyopo vinaonekana kuwa na kufanyika kwa akili nyingi na akijiangalia na yeye mwenyewe - asijuwe ni hali gani hiyo imesababisha vitu sio tu kuwa kwa akili lakini na kwa jinsi gani, anajitiisha na kutambua hali hiyo kwa kuiita "Mungu".
Tunapojiuliza kuna Mungu au hakuna Mungu, tunapaswa kimsingi kufahamu kuwa neno hilo (Mungu) tunaita uwepo wa hali ya akili ambao hauonekani lakini tumeufahamu au tumeujua kwa jinsi tunavyoona vitu vyote vya asili vilivyofanyika kwa akili nyingi na upatano wao ulivyo wa hali ya juu sana.
Hivyo basi, "Mungu", ni nini? Au Mungu maana yake ni nini? Mungu maana yake ni, Uwepo wa Hali ya Juu Wenye Akili. Kumbe, tunaposema Mungu au tunaposema kuna Mungu, ni Neno tunaloita "Uwepo wa Hali ya Juu Wenye Akili". Na maana hii inatokana na jinsi tunavyoona na kustaajabia vitu vya asili vilivyofanyika kwa akili nyingi na upatano wao ulivyo wa hali ya juu sana.
Tunasikia mara zote watu wakizungumza juu ya akili na kuhusu akili. Kwa hakika watu huzungumza kuhusu akili wakielezea mpangilio na miundo na ufanyaji kazi wa vitu na upatano wao jinsi ulivyo na unavyoeleweka, mkamilifu na wenye matokeo chanya.
Na tunasema akili kuelezea uwezo wa hali ya juu wa kujua, wa kufahamu, wa kuelewa, wa ujuzi, wa maarifa na wa kufanya vitu, yaani kutatua matatizo na kufanya mageuzo yenye maendeleo. Lakini hatahivyo akili ni nini? Je, akili ipo wapi? Je, akili inaonekana?
Akili ni kipawa kinachomwezesha mtu kufikiri kujifunza, kuwasiliana kuamua na kutatua matatizo. Kwa maneno mengine, akili ni ufahamu. Kwa kuchukua wanyama na hata mimea kama viumbe wenye ufahamu tunaweza kuelewa akili ya wanyama na mimea, akili ya binadamu, na tunaposema Mungu - Uwepo wa Hali ya Juu Wenye Akili.
Kimsingi wanyama wote wana ubongo ambamo mna ufahamu yaani akili. Lakini hatahivyo, wote tunakubali kwamba ubongo wa binadamu una akili kuliko ubongo wa wanyama wengine.
Kwa hiyo hatuwezi kuhitimisha kuwa akili ni shughuli au kazi za ubongo kwa sababu ubongo wa wanyama wengine nao vile vile unafanya shughuli za ufahamu. Lakini hatahivyo, wanyama wameendelea kubaki katika mstali wa ulalo (horizontal) wanadamu wako katika msatali wa wima (vertical).
Na kwa kweli binadamu pia anaweza kutokuwa na akili. Akabaki tu na ufahamu wa kawaida kama wanyama. Akawa tu kama wanyama anatekeleza kile mwili unamuasilishia kupitia milango yake mitano ya fahamu.
Kimsingi, akili ni ile hali ya kuwa na ufahamu wa kina wa mambo jinsi yalivyo na elimu ya vitu, yaani maarifa kamilifu au ushahidi wao wa ndani, na hivyo akili ni tofauti na ufahamu unaotokana na unaotegemea mwili, yaani milango mitano ya fahamu, ambao huo hautupatii maarifa kamilifu ya kitu au vitu, ya jambo au mambo jinsi yalivyo na yanavyotakiwa kuwa. Lakini hatahivyo, kama bado tungali hapa duniani tunahitaji mwili (hali safi ya ndani na ya mwili), ili kuunganika na Mungu, yaani Uwepo wa Hali ya Juu Wenye.
Unaweza kujiuliza au kufikiri ni nini kinakufanya uone au usema kitu hiki au jambo hili au hali fulani ni ya kiakili au imefanyika kwa akili; au jambo hili haliingii akilini? Unaposema kwa mfano, kitu hiki au jambo hili haliingii akilini unakuwa unajaribu kueleza nini?
Pengine wewe mwenyewe unaweza usijue jinsi mwili wako ulivyofanyika na unavyofanya kazi, labda ni vigumu sana. Lakini fikiria kwa mfano, kama umewahi kuona mitambo mbalimbali iwe ni ya viwandani au hospitalini ilivyotengenezwa na inavyofanya kazi, ni hali gani hiyo, na unaweza kuielezeaje?
Iwe ni mashine rahisi mpaka tata. Vivyo hivyo kuanzia na viumbe vidogo kabisa mpaka vikubwa kabisa vinaeleza hali ambayo mtu anaona na anaiita akili. Ingawa hakuna aliyeona akili ila ubongo ambao ni mahali pa ufahamu lakini hatahivyo, tunakubali kuwa vitu vyote vilivyopo vinaonekana kuwa na kufanyika kwa akili nyingi na upatano wao ni wa hali ya juu.
Kwa hiyo kama hivi ndivyo binadamu anaona ulimwengu, yaani vitu vyote vilivyopo vinaonekana kuwa na vimefanyika kwa akili, na sayansi haikatai hilo la vitu vya asili kuonekana kufanyika kwa akili nyingi na upatano wao kuwa wa hali ya juu isipokuwa inatafuta hali hiyo, na kwa jinsi gani.
Basi wazo kwamba kuna Mungu (idea that there is God is absolutely true), ni la kweli na hakika kwa sababu ambazo ni wazi na bayana. Kwanza vitu vya asili vilivyofanyika kwa akili nyingi na upatano wao kuwa wa hali ya juu. Na Pili mtu alivyo bora angalau katika viumbe wanaoonekana. Ubora huo ndio unaoelezwa katika biblia ikimtaja mtu kuwa "amefanyika kwa mfano na sura ya Mungu."
"Mfano na sura ya Mungu", mwandishi wa simulizi hilo la kweli za akili anamaanisha kuwa mtu amefanyizwa kwa mwili na roho - anayo hali ya akili hivi kwamba anaweza kuunganika na Uwepo wa Hali ya Juu Wenye Akili, yaani Mungu.
Dini inafundisha kuwa Mungu ndiye amesababisha uhai na ulimwengu kuwepo na kwamba Yeye ndiye tokeo la uhai na ulimwengu na ulimwengu unatawaliwa na uwepo Wake. Sayinsi inasema mianzo ya vitu vilivyopo: ulimwengu, umesababisha na mlipuko mkubwa uliotokea zamani. Nadharia hii ambayo ni msingi mkuu wa nadharia zote za sayansi na ambayo inakubalika na wanasayansi wengi jinsi vitu vilivyotokea inafundisha kuwa vitu vilitokana na nishati au nguvu (energy).
Kwa sababu sayansi inashughulikia jinsi vitu vilivyopo vilitokea, katika muktadha huo imetusaidia sio tu kuelewa ulimwengu, lakini pia kumjua Mungu. Na hivyo kwa sababu inashughulika na vitu vinavyoonekana na vinavyoweza kupimika, sayansi haitufundishi kwamba nishati hiyo ambayo imesababisha vitu kutokea ni kama nishati tunayoitumia kwa mitambo au inayopatikana kwa vyakula, jua nakadhalika. Lakini (Sayansi) inatufundisha kwamba nishati hiyo ni zaidi ya hali tunayoweza kuielezea kama mlipuko au kama nishati inayoupa mwili nguvu, au inayowezesha mitambo kufanya kazi au jua kustawisha na kuwezesha uhai wa viumbe duniani, ni Nishati Yenye Ufahamu wa Hali ya Juu wa Akili.
Kitabu cha Mwanzo kinasema kuwa Mungu aliumba ulimwengu pasipo kutumia kitu chochote. Simulizi hilo linachoeleza ni kuwa ulimwengu uliumbwa au ulifanyizwa kwa kutumia akili. Na hii ni sayansi iliyowazi kwamba vitu vyote vilivyopo vinaonekana na vimefanyika kwa akili.
Kwa jinsi ufahamu wetu ulivyo na unavyotokana na kujifunza au kusoma au kufuatilia vitu vilivyopo kwa karibu yaani maarifa yetu yanayotuwezesha kuelewa na hatimaye kupima ulimwengu, haiwezekani kukataa au hata kukana kwamba ulimwengu yaani vitu vyote vilivyopo havionekani kuwa na kufanyika kwa akili nyingi na upatano wao ni wa hali ya juu sana.
Labda kama kutakuja utaratibu mwingine, yaani elimu au ufahamu au uelewa mwingine, ambao utaeleza kwa namna nyingine isiyo hii tunayoiona au tulionao kwamba, ulimwengu kuonekana na kufanyika kwa akili nyingi na upatano wao kuwa wa hali ya juu, unaashiria Uwepo wa Hali ya Juu Wenye Akili tunaouita Mungu.
Na kwa upande mwingine, Ukana Mungu ambao msingi wake ni kutokuwa na uelewa wa kina wa mambo na elimu ya vitu umewavutia watu wengi katika mwelekeo huo kwa sababu ya kutokujua kama ambavyo ilivyo pia kwa wafuasi wengi wa dini.
Kile kinachoweza kuonekana kama kutoelewana - wengine wakikubali kuna Mungu na wengine wakikana hakuna Mungu, kimeendelea hata wakati ambao kuna ukuaji mkubwa wa maarifa ya sayansi na teknolojia. Na kwa kweli ni kama, kwa baadhi wasio na uelewa wa imani na sayansi, na walio na uelewa wa imani na sayansi, sayinsi imeimarisha mwelekeo wao.
Si kweli kwamba sayansi haibainishi kweli za akili, yaani kweli zilizotufikia kwa njia ya imani: mfano kuna Mungu na tokeo la uhai na ulimwengu, kwanini kuna ouvu duniani, nini hutokea baada ya kifo, nakadhalika.
Hatahivyo, pamoja na sayansi kuweka wazi mambo mengi ya imani (dini), ni dhahiri watu wengi bado hawajaelewa, na hivyo wanajiuliza:-
Je , ni kweli Mungu yupo au hayupo? Au Je, ni kweli Mungu yupo mahali pote (omnipresent)? Je, Mungu anauwezo wote (omnipotent)? Je, Mungu anajua yote, ana ujuzi wote; ana maarifa yote (omniscience)?
Na kama ni kweli! Kwa nini Mungu ambaye ni upendo, anauwezo wote, anajua yote, ana maarifa yote, ana nguvu na mamlaka yote, aumbe na aruhusu dunia ambayo inawezekana uovu kufanyika?
Kimsingi mjadala huu au maswali hayo hayawezi kuwa na maana au kujibika kama hatujui msingi wa neno Mungu, (au Hali hiyo) ambaye Ndiye mjadala wenyewe na ambaye Ndiye maswali yanaelekezwa kwake, umetokana na ni nini.
Ndugu zangu:-
Ni nini hutufanya tuseme Mungu? Yaani ni nini tunakirejelea tunapoita Mungu? Neno Mungu au wazo Mungu; au wazo kuna Mungu tumelitoa wapi? Sababu gani zimetusababisha kusema kuna Mungu; au wazo Mungu limesababishwa na nini?
Aidha, wazo hakuna Mungu limetoka wapi na limetokana na sababu gani? Na linapendekeza au linaelezea nini vitu vilivyopo?
Lakini pia, hii elimu tunayokwenda kusoma shuleni na vyuoni: kufundishwa na kusoma, (fizikia, hisabati, bailojia, kemia, jogorafia, sheria, uraia, historia, lugha, uhandisi, taalimungu (theology), elimu ya mtima (psychology), nakadhalika), imetoka wapi? Nani aliileta? Nani aliipangilia na kuiweka katika utaratibu huo? Kwa nini?
Kwa sababu kama ikiwa kila binadamu anapelekwa shule na chuo kujifunza na kusoma, maana yake hayo masomo tunayo kwenda kusoma au hiyo elimu tunayofundishwa shuleni na vyuoni hatukuwa tunaijua au tunaifahamu. Na hii maana yake ni kwamba kuna mtu aliyeijua hiyo elimu ambayo sisi tunakwenda kusoma na kufundishwa.
Sasa basi, huyo mtu aliipata wapi hiyo elimu au hayo masomo tunayofundishwa shuleni na vyuoni yalitoka wapi?
Na je, ni kweli kwamba hiyo ndio elimu (yaani hayo masomo) na kwamba hakuna kitu kingine bora zaidi au utaratibu mwingine wa kupima na kuelewa ulimwengu, ila isipokuwa kwa masomo au elimu hiyo tu?
Unauelezeaje ulimwengu: vitu vyote vilivyopo
Kadiri ya ufahamu wako na kadiri ya unavyoona na unavyoelewa, unaona vitu vilivyopo (ulimwengu ) vimefanyika kwa akili au havijafanyika kwa akili? Na je, unagundua hilo kwa jinsi gani? Je, ni baada ya kufundishwa au ni kabla? Au hugundui hivyo, badala yake unagundua nini?
Na hali hiyo ya vitu vya asili kuwa au kufanyika hivyo vilivyofanyika, inaashiria nini au unaieleza kuwa ni hali gani: yenye ufahamu au haina ufahamu?
Kwa binadamu, vitu vyote vilivyopo angalau vitu vyote anavyoweza kuviona akiwemo na mtu mwenyewe, anaona kuwa vitu hivyo au viumbe hivyo kuanzia na miundo yao ya nje na ya ndani, mpangilio wao, na jinsi yao ya utendaji kazi; ama ni kiungo kimoja kimoja katika kitu au kiumbe kimoja; au ni vitu mbalimbali, vinaonekana kufanyika kwa akili nyingi na upatano wao ni wa hali ya juu sana.
Kwa lugha rahisi, binadamu anaona ulimwengu kuwa umefanyika kwa akili nyingi na upatano wao ni wa hali ya juu sana. Hali hiyo ya mtu ya kufikiri au ya kuona kuwa ulimwengu, yaani vitu vyote vilivyopo vinaonekana kuwa na kufanyika kwa akili nyingi na akijiangalia na yeye mwenyewe - asijuwe ni hali gani hiyo imesababisha vitu sio tu kuwa kwa akili lakini na kwa jinsi gani, anajitiisha na kutambua hali hiyo kwa kuiita "Mungu".
Tunapojiuliza kuna Mungu au hakuna Mungu, tunapaswa kimsingi kufahamu kuwa neno hilo (Mungu) tunaita uwepo wa hali ya akili ambao hauonekani lakini tumeufahamu au tumeujua kwa jinsi tunavyoona vitu vyote vya asili vilivyofanyika kwa akili nyingi na upatano wao ulivyo wa hali ya juu sana.
Hivyo basi, "Mungu", ni nini? Au Mungu maana yake ni nini? Mungu maana yake ni, Uwepo wa Hali ya Juu Wenye Akili. Kumbe, tunaposema Mungu au tunaposema kuna Mungu, ni Neno tunaloita "Uwepo wa Hali ya Juu Wenye Akili". Na maana hii inatokana na jinsi tunavyoona na kustaajabia vitu vya asili vilivyofanyika kwa akili nyingi na upatano wao ulivyo wa hali ya juu sana.
Tunasikia mara zote watu wakizungumza juu ya akili na kuhusu akili. Kwa hakika watu huzungumza kuhusu akili wakielezea mpangilio na miundo na ufanyaji kazi wa vitu na upatano wao jinsi ulivyo na unavyoeleweka, mkamilifu na wenye matokeo chanya.
Na tunasema akili kuelezea uwezo wa hali ya juu wa kujua, wa kufahamu, wa kuelewa, wa ujuzi, wa maarifa na wa kufanya vitu, yaani kutatua matatizo na kufanya mageuzo yenye maendeleo. Lakini hatahivyo akili ni nini? Je, akili ipo wapi? Je, akili inaonekana?
Akili ni kipawa kinachomwezesha mtu kufikiri kujifunza, kuwasiliana kuamua na kutatua matatizo. Kwa maneno mengine, akili ni ufahamu. Kwa kuchukua wanyama na hata mimea kama viumbe wenye ufahamu tunaweza kuelewa akili ya wanyama na mimea, akili ya binadamu, na tunaposema Mungu - Uwepo wa Hali ya Juu Wenye Akili.
Kimsingi wanyama wote wana ubongo ambamo mna ufahamu yaani akili. Lakini hatahivyo, wote tunakubali kwamba ubongo wa binadamu una akili kuliko ubongo wa wanyama wengine.
Kwa hiyo hatuwezi kuhitimisha kuwa akili ni shughuli au kazi za ubongo kwa sababu ubongo wa wanyama wengine nao vile vile unafanya shughuli za ufahamu. Lakini hatahivyo, wanyama wameendelea kubaki katika mstali wa ulalo (horizontal) wanadamu wako katika msatali wa wima (vertical).
Na kwa kweli binadamu pia anaweza kutokuwa na akili. Akabaki tu na ufahamu wa kawaida kama wanyama. Akawa tu kama wanyama anatekeleza kile mwili unamuasilishia kupitia milango yake mitano ya fahamu.
Kimsingi, akili ni ile hali ya kuwa na ufahamu wa kina wa mambo jinsi yalivyo na elimu ya vitu, yaani maarifa kamilifu au ushahidi wao wa ndani, na hivyo akili ni tofauti na ufahamu unaotokana na unaotegemea mwili, yaani milango mitano ya fahamu, ambao huo hautupatii maarifa kamilifu ya kitu au vitu, ya jambo au mambo jinsi yalivyo na yanavyotakiwa kuwa. Lakini hatahivyo, kama bado tungali hapa duniani tunahitaji mwili (hali safi ya ndani na ya mwili), ili kuunganika na Mungu, yaani Uwepo wa Hali ya Juu Wenye.
Unaweza kujiuliza au kufikiri ni nini kinakufanya uone au usema kitu hiki au jambo hili au hali fulani ni ya kiakili au imefanyika kwa akili; au jambo hili haliingii akilini? Unaposema kwa mfano, kitu hiki au jambo hili haliingii akilini unakuwa unajaribu kueleza nini?
Pengine wewe mwenyewe unaweza usijue jinsi mwili wako ulivyofanyika na unavyofanya kazi, labda ni vigumu sana. Lakini fikiria kwa mfano, kama umewahi kuona mitambo mbalimbali iwe ni ya viwandani au hospitalini ilivyotengenezwa na inavyofanya kazi, ni hali gani hiyo, na unaweza kuielezeaje?
Iwe ni mashine rahisi mpaka tata. Vivyo hivyo kuanzia na viumbe vidogo kabisa mpaka vikubwa kabisa vinaeleza hali ambayo mtu anaona na anaiita akili. Ingawa hakuna aliyeona akili ila ubongo ambao ni mahali pa ufahamu lakini hatahivyo, tunakubali kuwa vitu vyote vilivyopo vinaonekana kuwa na kufanyika kwa akili nyingi na upatano wao ni wa hali ya juu.
Kwa hiyo kama hivi ndivyo binadamu anaona ulimwengu, yaani vitu vyote vilivyopo vinaonekana kuwa na vimefanyika kwa akili, na sayansi haikatai hilo la vitu vya asili kuonekana kufanyika kwa akili nyingi na upatano wao kuwa wa hali ya juu isipokuwa inatafuta hali hiyo, na kwa jinsi gani.
Basi wazo kwamba kuna Mungu (idea that there is God is absolutely true), ni la kweli na hakika kwa sababu ambazo ni wazi na bayana. Kwanza vitu vya asili vilivyofanyika kwa akili nyingi na upatano wao kuwa wa hali ya juu. Na Pili mtu alivyo bora angalau katika viumbe wanaoonekana. Ubora huo ndio unaoelezwa katika biblia ikimtaja mtu kuwa "amefanyika kwa mfano na sura ya Mungu."
"Mfano na sura ya Mungu", mwandishi wa simulizi hilo la kweli za akili anamaanisha kuwa mtu amefanyizwa kwa mwili na roho - anayo hali ya akili hivi kwamba anaweza kuunganika na Uwepo wa Hali ya Juu Wenye Akili, yaani Mungu.
Dini inafundisha kuwa Mungu ndiye amesababisha uhai na ulimwengu kuwepo na kwamba Yeye ndiye tokeo la uhai na ulimwengu na ulimwengu unatawaliwa na uwepo Wake. Sayinsi inasema mianzo ya vitu vilivyopo: ulimwengu, umesababisha na mlipuko mkubwa uliotokea zamani. Nadharia hii ambayo ni msingi mkuu wa nadharia zote za sayansi na ambayo inakubalika na wanasayansi wengi jinsi vitu vilivyotokea inafundisha kuwa vitu vilitokana na nishati au nguvu (energy).
Kwa sababu sayansi inashughulikia jinsi vitu vilivyopo vilitokea, katika muktadha huo imetusaidia sio tu kuelewa ulimwengu, lakini pia kumjua Mungu. Na hivyo kwa sababu inashughulika na vitu vinavyoonekana na vinavyoweza kupimika, sayansi haitufundishi kwamba nishati hiyo ambayo imesababisha vitu kutokea ni kama nishati tunayoitumia kwa mitambo au inayopatikana kwa vyakula, jua nakadhalika. Lakini (Sayansi) inatufundisha kwamba nishati hiyo ni zaidi ya hali tunayoweza kuielezea kama mlipuko au kama nishati inayoupa mwili nguvu, au inayowezesha mitambo kufanya kazi au jua kustawisha na kuwezesha uhai wa viumbe duniani, ni Nishati Yenye Ufahamu wa Hali ya Juu wa Akili.
Kitabu cha Mwanzo kinasema kuwa Mungu aliumba ulimwengu pasipo kutumia kitu chochote. Simulizi hilo linachoeleza ni kuwa ulimwengu uliumbwa au ulifanyizwa kwa kutumia akili. Na hii ni sayansi iliyowazi kwamba vitu vyote vilivyopo vinaonekana na vimefanyika kwa akili.
Kwa jinsi ufahamu wetu ulivyo na unavyotokana na kujifunza au kusoma au kufuatilia vitu vilivyopo kwa karibu yaani maarifa yetu yanayotuwezesha kuelewa na hatimaye kupima ulimwengu, haiwezekani kukataa au hata kukana kwamba ulimwengu yaani vitu vyote vilivyopo havionekani kuwa na kufanyika kwa akili nyingi na upatano wao ni wa hali ya juu sana.
Labda kama kutakuja utaratibu mwingine, yaani elimu au ufahamu au uelewa mwingine, ambao utaeleza kwa namna nyingine isiyo hii tunayoiona au tulionao kwamba, ulimwengu kuonekana na kufanyika kwa akili nyingi na upatano wao kuwa wa hali ya juu, unaashiria Uwepo wa Hali ya Juu Wenye Akili tunaouita Mungu.