Mungu na Shetani: Nani kaua zaidi?

Mungu na Shetani: Nani kaua zaidi?

Je na wale wanaojilipua mabomu kwa jina la Mungu wao?
Hao pia wanaongezeka kwenye list ya mauaji yanayosababishwa na Mungu.
Laiti concept ya Mungu ingelikuwa tofauti na bora, wasingeua.

Sasa Mungu mwenyewe anaua, watu wake hawana sababu ya kutokuua.
 
Wew ni mfugo tu mbele za Mungu huna umuhimu wowote kama ufati amri zake atakuchinja tu....

We ufunge kuku alafu wakuletee zarau mara wanatoroka mara wanapigana lazima utawachinja na utaacha wale wastarabu........
Mnaomuamini ndiyo mifugo. Watunzi wa bible wanawaita kondoo nanyi mmekubaliana na hali.
Mungu wenu ni character muuaji na psychopath.
 
Jamaa analalamika kwa tunda moja yeye ndiye mbaya kuliko aliyeuwa mamilioni.
Yaani kwenye kitabu kinachoitwa Cha mungu, shetani kaua watu 10 tu, tena kwa ruhusa ya mungu.

Lakini hawa waamini hawataki kuisikia ukweli kwamba mungu ni muuaji.
 
Hakimu anapopitisha hukumu ya kifo yule hakimu anakua ni muuji ???
Mfano wako hauna uhalisia. Mungu hayupo kwenye nafasi ya hakimu.
Maandiko hapo juu yanaonesha waziwazi kwamba mungu ndiyo anawaua watu kwa kutumia moto, maji na wanyama.
Si kama anahukumu tu kisha aje mwingine ndiye aue kama wafanyavyo mahakimu.
 
Mungu na shetani waliwahi kukubaliana kujaribu muumini, sikumbuki Ni kifungu gan
Kitabu cha Ayubu hicho mkuu.
Mungu alikuwa amekaa anatazama Shetani akiua watoto 10 wa Ayubu bila kosa lolote.
 
Mpaka sasa mtoa mada anaongoza tatu bila, ngoja tuendelee kuona mtanange unavyoendelea kuwa.
 
Ni Mungu, ile gharika haikuwa mchezo. Ningekuwa nuhu, kwa kuwa kila kiumbe ni wawili tu, ningeuwa vile viumbe waharibifu kama mbu, nyoka, na baadhi ya wanyama wakali.
 
Ndugu WanaJF,

Mungu ni muuaji ambaye amefanya mauaji ya halaiki mara kwa mara na wote tumeyasoma kwenye simulizi za biblia.

Pamoja na hivyo, bado shetani analaumiwa zaidi kwa kudaiwa kusababisha mauaji, magonjwa na mambo ya hivyo yasiyompendeza binadamu.


Tutumie agano la kale kujionea wenyewe jinsi huyu mungu mwenye 'huruma' alivyowatenda wanadamu.


Matukio Ambapo Mungu Aliua Watu Katika Agano la Kale


1. Gharika – Idadi ya vifo: Haijulikani, inakadiriwa 1,000,000+


Rejea: Mwanzo 6:5-7


“BWANA akaona ya kuwa maovu ya mwanadamu ni makubwa duniani, na kwamba kila kusudi analoliwaza moyoni mwake ni baya tu sikuzote. BWANA akasema, Nitamfuta mwanadamu, niliyemuumba, usoni pa nchi; mwanadamu, na mnyama, na kitambaacho, na ndege wa angani; maana, najutia ya kwamba nimewafanya.”




2. Uharibifu wa Sodoma na Gomora – Idadi ya vifo: 1,000

Rejea: Mwanzo 19:24-25

“Ndipo BWANA akanyesha juu ya Sodoma na Gomora kiberiti na moto toka mbinguni kwa BWANA; akaangusha miji hiyo, na Bonde lote, na wote waliokaa katika miji hiyo, na yote yaliyomea katika nchi ile.”

3. Mke wa Lutu – Mtu 1

Rejea: Mwanzo 19:26
“Lakini mkewe Lutu akaangalia nyuma akawa nguzo ya chumvi.”


4. Mapigo ya Misri – Idadi ya vifo: Inakadiriwa 50,000

Rejea: Kutoka 12:29-30
“Ikawa usiku wa manane, BWANA akawapiga wazaliwa wa kwanza wote katika nchi ya Misri, tangu mwana wa kwanza wa Farao aketiye juu ya kiti chake cha enzi, hata mwana wa kwanza wa mfungwa aliyekuwa gerezani; na wazaliwa wote wa kwanza wa wanyama. Farao akaondoka usiku huo, yeye na watumwa wake wote, na Wamisri wote; kukawa na kilio kikuu katika Misri, maana hapakuwa na nyumba pasipokuwa na maiti.”

5. Kisa cha Ndama wa Dhahabu – Watu 3,000

Rejea: Kutoka 32:27-28
“Akaawaambia, BWANA, Mungu wa Israeli, asema hivi, Kila mtu na ajifunge upanga wake pajani mwake; mpitieni na kuupitia marago toka lango hili mpaka lango lile, kila mtu amwue ndugu yake, na rafiki yake, na jirani yake. Wana wa Lawi wakafanya kama vile Musa alivyosema; wakaanguka watu kama elfu tatu siku ile.”

6. Uasi wa Kora – Watu 14,950

Rejea: Hesabu 16:31-35, 49
"Ikawa, alipokwisha kusema maneno hayo yote, nchi ikapasuka iliyo chini yao; nchi ikafunua kinywa chake, na kuwameza, na nyumba zao, na watu wote waliokuwa wa Kora, na vyombo vyao vyote. Wakatumbukia ndani ya shimo, wao na wote waliokuwa nao hai, nchi ikawafunikiza, wakapotea katika mkutano.”


“Nao waliokufa kwa ile tauni walikuwa watu kumi na nne elfu na mia saba, zaidi ya wale waliokufa kwa sababu ya Kora.”


7. Malalamiko Katika Jangwa – Idadi ya vifo: Inakadiriwa 100

Rejea: Hesabu 11:1-3
“Watu walikuwa kama wanaonung’unika kwa ajili ya mabaya masikioni mwa BWANA; BWANA akasikia, hasira zake zikawaka, moto wa BWANA ukawaka kati yao, ukateketeza katika mipaka ya marago.”


8. Tauni kwa Kulalamikia Mana – Idadi ya vifo: Inakadiriwa 500

Rejea: Hesabu 11:33-34
“Kama nyama ilikuwa bado kati ya meno yao, kabla haijatafunwa, hasira za BWANA zikawaka juu ya watu, BWANA akawapiga watu kwa mapigo makuu sana. Kwakuo walipaita pale Kibroth-Hataava, kwa sababu hapo ndipo walipowazika watu waliokuwa na tamaa.”


9. Adhabu kwa Kuabudu Baali-Peori – Watu 24,000

Rejea: Hesabu 25:9
“Nao waliokufa kwa hiyo tauni walikuwa ishirini na nne elfu.”


10. Nyoka Wenye Moto – Idadi ya vifo: Inakadiriwa 200

Rejea: Hesabu 21:6
“BWANA akatuma nyoka za moto kati ya watu, wakawauma; wakaanguka watu wengi katika Israeli.”

11. Adhabu kwa Sababu ya Sensa – Watu 70,000

Rejea: 2 Samweli 24:15

“Basi BWANA akaleta tauni katika Israeli tangu asubuhi hata wakati ulioagizwa; wakafa watu sabini elfu miongoni mwa watu toka Dani mpaka Beer-Sheba.”

Jumla ya Vifo Vilivyosababishwa na Mungu: Inakadiriwa 1,100,000+

-
Vifo vilivyosababishwa na Shetani Katika Agano la Kale


1. Watoto wa Ayubu – Watu 10

Rejea: Ayubu 1:18-19


“Alipokuwa bado akinena, akaja mwingine, akasema, Wana wako na binti zako walikuwa wakila na kunywa divai katika nyumba ya ndugu yao mkubwa; kumbe, upepo mkubwa ukatoka upande wa jangwani, ukaipiga hiyo nyumba pembe zake nne, ikaanguka juu ya hao vijana, nao wamekufa; nami peke yangu nimepona ili nikuambie.”


Jumla ya Vifo Vilivyosababishwa na Shetani: 10


Kwa mantiki hii, Mungu ni muuaji mkubwa sana. Anachojali ni kuogopwa tu. Ni mkatili na ana tabia za psychopaths.


Mungu ni dikteta, character yake ni kama ya wakina Adolf Hitler au wale drug lords wa cartels za Amerika ya kusini.


Anyways, ni fiction tu. Waamini msijenge chuki. Twajua hata ninyi hamumpendi Mungu, ni hofu tu imewatawala, mnaogopa kuchomwa moto.​

Siku njema mkiendelea kutafakari ukatili wa Mungu wa Yakobo.
Kaua aliowaumba,ana haki za kufanya atakalo.muhoji wewe mbona kaua wengi?sa si yeye ndo kaua wengi yeye ndo umuulize sasa
 
Ndugu WanaJF,

Mungu ni muuaji ambaye amefanya mauaji ya halaiki mara kwa mara na wote tumeyasoma kwenye simulizi za biblia.

Pamoja na hivyo, bado shetani analaumiwa zaidi kwa kudaiwa kusababisha mauaji, magonjwa na mambo ya hivyo yasiyompendeza binadamu.


Tutumie agano la kale kujionea wenyewe jinsi huyu mungu mwenye 'huruma' alivyowatenda wanadamu.


Matukio Ambapo Mungu Aliua Watu Katika Agano la Kale


1. Gharika – Idadi ya vifo: Haijulikani, inakadiriwa 1,000,000+


Rejea: Mwanzo 6:5-7


“BWANA akaona ya kuwa maovu ya mwanadamu ni makubwa duniani, na kwamba kila kusudi analoliwaza moyoni mwake ni baya tu sikuzote. BWANA akasema, Nitamfuta mwanadamu, niliyemuumba, usoni pa nchi; mwanadamu, na mnyama, na kitambaacho, na ndege wa angani; maana, najutia ya kwamba nimewafanya.”




2. Uharibifu wa Sodoma na Gomora – Idadi ya vifo: 1,000

Rejea: Mwanzo 19:24-25

“Ndipo BWANA akanyesha juu ya Sodoma na Gomora kiberiti na moto toka mbinguni kwa BWANA; akaangusha miji hiyo, na Bonde lote, na wote waliokaa katika miji hiyo, na yote yaliyomea katika nchi ile.”

3. Mke wa Lutu – Mtu 1

Rejea: Mwanzo 19:26
“Lakini mkewe Lutu akaangalia nyuma akawa nguzo ya chumvi.”


4. Mapigo ya Misri – Idadi ya vifo: Inakadiriwa 50,000

Rejea: Kutoka 12:29-30
“Ikawa usiku wa manane, BWANA akawapiga wazaliwa wa kwanza wote katika nchi ya Misri, tangu mwana wa kwanza wa Farao aketiye juu ya kiti chake cha enzi, hata mwana wa kwanza wa mfungwa aliyekuwa gerezani; na wazaliwa wote wa kwanza wa wanyama. Farao akaondoka usiku huo, yeye na watumwa wake wote, na Wamisri wote; kukawa na kilio kikuu katika Misri, maana hapakuwa na nyumba pasipokuwa na maiti.”

5. Kisa cha Ndama wa Dhahabu – Watu 3,000

Rejea: Kutoka 32:27-28
“Akaawaambia, BWANA, Mungu wa Israeli, asema hivi, Kila mtu na ajifunge upanga wake pajani mwake; mpitieni na kuupitia marago toka lango hili mpaka lango lile, kila mtu amwue ndugu yake, na rafiki yake, na jirani yake. Wana wa Lawi wakafanya kama vile Musa alivyosema; wakaanguka watu kama elfu tatu siku ile.”

6. Uasi wa Kora – Watu 14,950

Rejea: Hesabu 16:31-35, 49
"Ikawa, alipokwisha kusema maneno hayo yote, nchi ikapasuka iliyo chini yao; nchi ikafunua kinywa chake, na kuwameza, na nyumba zao, na watu wote waliokuwa wa Kora, na vyombo vyao vyote. Wakatumbukia ndani ya shimo, wao na wote waliokuwa nao hai, nchi ikawafunikiza, wakapotea katika mkutano.”


“Nao waliokufa kwa ile tauni walikuwa watu kumi na nne elfu na mia saba, zaidi ya wale waliokufa kwa sababu ya Kora.”


7. Malalamiko Katika Jangwa – Idadi ya vifo: Inakadiriwa 100

Rejea: Hesabu 11:1-3
“Watu walikuwa kama wanaonung’unika kwa ajili ya mabaya masikioni mwa BWANA; BWANA akasikia, hasira zake zikawaka, moto wa BWANA ukawaka kati yao, ukateketeza katika mipaka ya marago.”


8. Tauni kwa Kulalamikia Mana – Idadi ya vifo: Inakadiriwa 500

Rejea: Hesabu 11:33-34
“Kama nyama ilikuwa bado kati ya meno yao, kabla haijatafunwa, hasira za BWANA zikawaka juu ya watu, BWANA akawapiga watu kwa mapigo makuu sana. Kwakuo walipaita pale Kibroth-Hataava, kwa sababu hapo ndipo walipowazika watu waliokuwa na tamaa.”


9. Adhabu kwa Kuabudu Baali-Peori – Watu 24,000

Rejea: Hesabu 25:9
“Nao waliokufa kwa hiyo tauni walikuwa ishirini na nne elfu.”


10. Nyoka Wenye Moto – Idadi ya vifo: Inakadiriwa 200

Rejea: Hesabu 21:6
“BWANA akatuma nyoka za moto kati ya watu, wakawauma; wakaanguka watu wengi katika Israeli.”

11. Adhabu kwa Sababu ya Sensa – Watu 70,000

Rejea: 2 Samweli 24:15

“Basi BWANA akaleta tauni katika Israeli tangu asubuhi hata wakati ulioagizwa; wakafa watu sabini elfu miongoni mwa watu toka Dani mpaka Beer-Sheba.”

Jumla ya Vifo Vilivyosababishwa na Mungu: Inakadiriwa 1,100,000+

-
Vifo vilivyosababishwa na Shetani Katika Agano la Kale


1. Watoto wa Ayubu – Watu 10

Rejea: Ayubu 1:18-19


“Alipokuwa bado akinena, akaja mwingine, akasema, Wana wako na binti zako walikuwa wakila na kunywa divai katika nyumba ya ndugu yao mkubwa; kumbe, upepo mkubwa ukatoka upande wa jangwani, ukaipiga hiyo nyumba pembe zake nne, ikaanguka juu ya hao vijana, nao wamekufa; nami peke yangu nimepona ili nikuambie.”


Jumla ya Vifo Vilivyosababishwa na Shetani: 10


Kwa mantiki hii, Mungu ni muuaji mkubwa sana. Anachojali ni kuogopwa tu. Ni mkatili na ana tabia za psychopaths.


Mungu ni dikteta, character yake ni kama ya wakina Adolf Hitler au wale drug lords wa cartels za Amerika ya kusini.


Anyways, ni fiction tu. Waamini msijenge chuki. Twajua hata ninyi hamumpendi Mungu, ni hofu tu imewatawala, mnaogopa kuchomwa moto.​

Siku njema mkiendelea kutafakari ukatili wa Mungu wa Yakobo.
Wavuta bangi wamezidi JF
 
Back
Top Bottom