Mungu ndiye shetani(?)

Nimefanya ushenzi sana humu duniani ila sikawahi kumkufuru Mungu
Najua Munguu na ni mwingi wa rehema utanisamehe dhambi zangu.
Tenda jambo kwa huyu mtoa mada ehee Mungu nakuomba
😂,Bosi sio kufuru,, shetan hawezi kumzidi mungu nguvu, huyo mnaemwita shetani kama yupo, yupo kwa makusudi maalumu,, yaani hii ni kama game of chance, soma vizuri kisa cha ayub,, wakati shetan na mungu wakiwekeana dau juu ya ayub,
Soma issue ya farao, alietaka kuwaacha wana wa israel waondoke kwa amani,, kisha mungu akaufanya moyo wa farao kuwa mgumu ili tu apate kumuua,
Soma habari ya moses kutomtahiri mwanae, jambo lililopelekea jehova, amnyatie nyatie moses akikwepa kukanyanga mashonde na hadi akampiga kabari ya nguvu moses,, soma jinsi yehova alivyokua akibishana na moses kila wakati yehova alipokuwa akiwateketeza waisrael jangwani , hadi ikafikia hatua yehova anamwamuru moses amkate kichea mfalme wa agag, moses alipogoma, yehova akamwambia hataingia nchi takatifu kwa maana yehova atamuua moses,,
Ofcource hizo habari ni hekaya tu za wazee wa kiyahudi, kwani moses hakuwahi kuwepo🤷🏽‍♂️
 
Daaah bro sjawah kuwaza ivi najiulza mamb meng ila ww n noma
 
Msitoe povu sana...jibuni hoja...mnaweza mkakasirikiana bure...kumbe Mungu na Shetani huwa wanakutana na kupiga stori, mfano kama mwanzoni mwa kitabu cha Ayubu...Truth is born out of an argument.
 
Hivi upo duniani au ulisha potea... Umekunywa keyvant inakukimbiza nakuona uwandike kile hujuwi umeandika. Angalia sasa hili bandiko litakavyo kutesa mpaka useme pooo Mungu hadhihakiwi na chochote apandacho mtu huvuna... Tafakari utavuna nn na nn itakuwa hatima yako.... Jibu unalo mwenyewe
 
Hakuna Mungu wala Shetani, hizo zote ni hadithi za kutungwa na watu tu.
 
Hapa wagala ndo mnapofeli,, huyo ni mtu wenu, na hiyo mistari kainukuu kutoka kwenye kitabu chenu sasa hiyo dini nyingine unayooita ya kiarabu hapo inaingiaje!!
Alivyooandika umemuelewa? Biblia haisomwi km gazeti na waliojaribu kusoma km gazeti walishindwa kujua maana yake.
Alichoandika ni kama masimulizi ambayo hayana ukweli 100% ndani yake.
Biblia inakutaka unapoielezea uoneshe vifungu kwa mfano ni Mwanzo sura ya 1, mstari wa 4 inasema hivi ndiyo maana imeandikwa kwa lugha nyingi ili watu waeielewe.
Ukweli usiojificha angekuwa ameisema hivyo quran, kuna masheh wangekuwa wanamsomea Albadili sasa hivi, angefahamika ilikuwa ni kuuliwa au kuhukumiwa kifo kwenye mahakama ya kadhi.
Mfano hai
Iran, mwanamke wa dini ya kiislam hakufunika kichwa aliuliwa
Kuna shekh hapo naijeria amehukumiwa kifo. Uzi wake humu JF
Kuna sheh mwingine Uarabuni alihukumiwa kifo
Kuna mwanamke hapo jirani alimbusu mwanaume hadharani alihukumiwa kifo ila kwa kuona watu wa haki za binadamu wataingilia kati wakabadili hukumu na kufungwa jela miezi 6
Siyo kama wakristo wanatetea dhambi
1. Mungu wao ni mwenye nguvu na anaweza kujitetea ndiyo anayetoa hukumu.
2. Usihukumu usije ukahukumiwa. Ambaye hana dhambi awe wa kwanza kumtupia mawe huyu mtoa uzi? Utaenda mbingu ya nani ukimuua mwenzako
 
Mtu akiteseka wanasema ni mapenzi ya Mungu, Ina maana ana uhusiano na shetani. Mimi ninaona Mungu na shetani ni vitu viwili vinavyofanya kazi pamoja. Ni sawa na mwanga na Giza. Wakati wa mchana mimea inatumia jua kutengeneza ule ukijani wake na usiku mimea inatoa hewa kwa binadamu.
 
Mi naona andiko lipo vizuri na mtoa mada ametoa sababu zake..na amemaliza andiko lake Kwa swali...sasa nyie toeni hoja...badala ya vitisho, hukumu si kazi yenu...Muumba pekee ndio mtoa hukumu...nyie jibuni mada...Mungu na Shetani hawana uadui wa kihivyo mnavyofikiria nyie...What is a good man but a bad man's teacher and what is a bad man but a good man's job!
 
Elimu bure inawaharibu watanzania usiku mimea inatoa carbon dioxide mchana inatoa oxygen, unavyosema usiku hewa kwa binadamu kwa hiyo binadamu anatumia carbon dioxide
 
Ukifatilia sana matukio ya mwanzo hadi mwisho wa Biblia unajiuliza haya yalifanyika Mungu akiwa wapi? Au Mungu ni dhaifu? Yaani watu wameuana sana humo kwenye Bible mpala unashangaa ukiwa unasoma kama unasoma kitabu kitakatifu kweli au kitabu cha Kichina cha movie ya vita.

Watu kuchinjana, kuuana, kufirana na uzinzi mpaka mtu anazidi na Dada yake, wasichana wanazini na Baba yao.

Lakini ndio hivyo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…