Mungu ndiye shetani(?)

Mungu ndiye shetani(?)

Alivyooandika umemuelewa? Biblia haisomwi km gazeti na waliojaribu kusoma km gazeti walishindwa kujua maana yake.
Alichoandika ni kama masimulizi ambayo hayana ukweli 100% ndani yake.
Biblia inakutaka unapoielezea uoneshe vifungu kwa mfano ni Mwanzo sura ya 1, mstari wa 4 inasema hivi ndiyo maana imeandikwa kwa lugha nyingi ili watu waeielewe.
Ukweli usiojificha angekuwa ameisema hivyo quran, kuna masheh wangekuwa wanamsomea Albadili sasa hivi, angefahamika ilikuwa ni kuuliwa au kuhukumiwa kifo kwenye mahakama ya kadhi.
Mfano hai
Iran, mwanamke wa dini ya kiislam hakufunika kichwa aliuliwa
Kuna shekh hapo naijeria amehukumiwa kifo. Uzi wake humu JF
Kuna sheh mwingine Uarabuni alihukumiwa kifo
Kuna mwanamke hapo jirani alimbusu mwanaume hadharani alihukumiwa kifo ila kwa kuona watu wa haki za binadamu wataingilia kati wakabadili hukumu na kufungwa jela miezi 6
Siyo kama wakristo wanatetea dhambi
1. Mungu wao ni mwenye nguvu na anaweza kujitetea ndiyo anayetoa hukumu.
2. Usihukumu usije ukahukumiwa. Ambaye hana dhambi awe wa kwanza kumtupia mawe huyu mtoa uzi? Utaenda mbingu ya nani ukimuua mwenzako
Watenda mabaya wanahukumiwa Broo.
Acheni Siasa kwenye Imani za watu.

Unapotaja Dini ya Kikristo unazungumzia ufalme Wa Mungu hapa Duniani na wanadamu ndio waliowekwa Ili waujenge juu ya msingi Wa Kristo.

Hakuna ufalme unaojengwa kirahisi. Ukristo imejengwa kwa upanga kama ulivyo uislamu. Waliotangulia walipambana sana kuleta utawala Wenye Sheria za Kikristo.
Una bahati umezaliwa kwenye nchi ambayo tayari watu walipambana na kujenga misingi hiyo ! Mshukuru Mungu kuzaliwa zama ambazo unakaa pembeni serikali inakulipia Kisasi.

Leo hii unaweka ukaona Wakristo wakikaa pembeni wanaona Makanisa yananajisiwa na watu wanaoana na kufunga ndoa za jinsia Moja wanasema kuwa Vita yetu si juu ya damu na Nyama Huku ushoga ukiwa unaenea Kwa Kasi.
Sasa unajiuliza ni Mungu Yupi wanataka aje ajipiganie Wakati amewaweka hapa Duniani Ili wafanye KAZI yake Kwa utukufu wake?

Wakristo wamejazana kwenye mabaa na madanguro wanalewa na uzinzi halafu wanawaachia Mashoga na Mabasha wanapanga Nani aongoze na kutawala na kutunga Sheria za Dunia kinyume na Mipango ya Mungu. Wakristo Wa Sasa wamepotoka na ni waoga?
Biblia inasema waoga na wasioamini sehemu yake ni Katika lile Ziwa liwakalo moto na Kiberiti.
Wakristo watatupwa Nje Kwa sababu wameondoka kwenye Jukumu la kuujenga ufalme Wa Mungu Duniani. Hakuna ufalme Wa Mungu unaotawaliwa na waovu.
Wakristo wanapaswa kuwa Chachu ya Utawala Wa Haki isiyotoka Nje ya Neno la Mungu. Hakuna haki Kwa watenda dhambi.

Basi tuache kuwa na Majeshi mana hatuna vita ya kimwili . Haiwezekani mana tuna KAZI ya kuujenga ufalme Wa Mungu kimwili na KIROHO. Paulo alitaka watu wale wanafunzi wake wazame zaidi kwenye ulimwengu Wa roho Ili vita ianzie Rohoni na kuonekana mwilini Katika kukemea dhambi na kujenga misingi ya Kikristo kwenye Tawala na mamlaka za kimwili ambazo zitasimama Katika kulipa kisasi Badala ya Mungu.
Serikali ni Watu na zinapaswa kuadhibu Kwa haki Badala ya Mungu.
Serikali zinapaswa kuwa chini ya Kristo .
Ukiona serikali hazitendi haki Ujue Wakristo wamelala.
Dunia imefikia ilipo Kwa sababu Wakristo Wa kweli wamelala na ni waoga. Wanazipenda nafsi zao matokeo yake wanajificha Nyuma ya mistari ya kuwa YESU alisema asiye na dhambi awe Wa kwanza kumpiga . Lakini Nenda mahakamani uone walivyojazana kwenye kesi za kugombania mpaka maiti kuzika.[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Nikisoma historia ya ukoloni baran Africa,
Hasa role ya wamisionari na waarabu ktk kutuletea huu ukoloni.

Nakosa kabisa imanj na hizi dini zilizokuja na meli Islamic& Christianity [emoji22]

Sent using Jamii Forums mobile app
Tatizo umezaliwa juzi na ukakulia mjini hujawahi kukaa na Bibi au Babu aliyeishi Miaka 140 iliyopita akakusimulia maisha yaliyokuwa kabla ya Kuja wamisionari.

Wamisionari ni Kama unavyoona leo Wanasiasa na Viongozi Wa Dini?

Wamisionari walileta mwanga Afrika na Duniani kote .
Watu jeuri waliojaribu kuwaua ndio chanzo Cha serikali zao kuleta utawala Wa Kikoloni.
Wamisionari walipokuja walikuta Tawala za asili zilikuwa na Sheria zisizofaa na walipojaribu kuwakosoa walioshia kuuawa. Mfano Sheria za Machifu kupora wake za watu Huku wakiwa na wake wengi . Machifu kupora mifugo ya watu. Kabila Moja kuvamia kabila jingine na kuteka wanawake na kuua wanaume na watoto BILA sababu Huku wakiwa na nia ya kupora Mali na mifugo.

Kuua walemavu , makafara ya watoto. Sheria NYINGI zilikua ni mwenye nguvu mpishe.
Waafrika wangewapokea Wamisionari na kuyafanyia KAZI yale mema waliyokuja nayo na kujifunza Namna Bora ya kujitawala Kwa haki Majeshi na serikali za Kikoloni zisingekuja Kirahisi.
Wangetetea Mila zao na dini zao kwa hoja Badala ya kutumia nguvu kuzilinda Wakati hawakua wanatendeana haki matokeo yake pakawa na kusalitiana kutokana na Chuki KUBWA iliyokuwepo miongoni mwa MAKABILA ,Koo,na Hata familia. Ikawa ni chanzo Cha kutawaliwa kirahisi.

Waafrika kabla ya mkoloni WALIKUA wamegawanyika sana ndio Maana Kuna Koo NYINGI na MAKABILA Mengi ambayo mpaka Sasa hayaelewani Kwa lugha na Hata Tabia. Dini za Kikoloni NDIZO zilizosababisha Leo Msambaa anaoana na na Mchaga. Kabla ya Hapo haikuwezekana kamwe. Mgogo kamwe haikuwezekana akaoa mmasai au Mzaramo akamuoa Mmeru. Watu waliokuwa wamegawanyika kwa kiwango hicho hawangeweza kuwa na Taifa Moja BILA kuwa na serikali yenye nguvu ambayo ilikuwa ni ya Mkoloni Hapo mwanzo kabla ya uhuru.

Historia ya Mwafrika kabla ya mkoloni inajaribu kuficha madhaifu ya waafrika ambayo mpaka Leo yapo wazi na Ndiyo yanaturudisha Nyuma tunabaki kudanganyana Badala ya Kukaa chini na Kuja na será zetu za Elimu ,mitaala Bora ya Elimu, Kariba Bora ,kuwasimamia watawala Ili watekeleze majukumu Yao Kwa maslahi ya umma, Kupinga wachache kuhodhi Mali za umma Kwa mgongo Wa madaraka. Kupinga Kodi KUBWA kwenye rasilimali zinazotokana na juhudi ya wananchia kuzalisha Mfano Ushuru Wa mazao n.k.Huu ni mwendelezo Wa ukoloni.
 
Una bahati unamkufuru Mungu mwenye nguvu, anayeweza kujitetea na mwingi wa rehema.
Ungekuwa ndiyo wale wenye dini ya Kiarabu sasa hivi ungekiwa kwenye mahakama ya kadhi au wamekuchinja kichwa.
Karibu kanisani, ujifunze zaidi. Vita vyetu ni vya kiroho na si vya damu na nyama.
Mwamba unakerekwa na Uislam ee?!!!!! Hoja mama wala haijataja uislamu.....Pole sana, we mjibu tu mtoa mada!
 
Kuna watu niliwahi kuwambia Mungu na Shetani ni marafiki sana. Wakaniona kama nakufuru.

Sisi ndio tunawagombanisha ila wao wanaelewana vizuri.

Rejea tukioa la Ayoub. Pia wakati Babeli inaenda kuvamia Wayahudi ktk kitabu cha Yeremia Mungu akasema nilimtumia Mtumishi wangu Nebukadineza awatie mikononi mwake........

Inawezekana vipi Shetani apigane vita Mbinguni dhidi ya Mungu?

Na bado akafanikiwa kushawishi 1/3 ya malaika zake?

Inawezekana vipi Shetani aliye na nguvu kiasi hiki aletwe duniani kupamna na sisi viumbe dhaifu tulioumbwa na udongo na utegemee ushindi??

Why Mungu asingemalizana na shetani kabisa? Sasa mlolongo wa matukio ukaanza mara namtuma Yesu aje kuwakomboa, mara chinjeni kafara toeni sadaka ziwasafishe dhambi.....huu mzunguko wa nini wakati anatakiwa kufyekelea mbali shetani?
Duniani tunakadiriwa kuwa 7bn. Watakaoenda mbinguni hawafiki 1mIlioni.

Iweje 6bn inapotea hivi hivi sababu ya shetani mmoja?
Siasa zinakufaa lakini huku ktk dini unapuyanga sana.

Itoshe kusema huna uelewa wowote kuhusu ukuu wa MUNGU.
 
Nikisoma historia ya ukoloni baran Africa,
Hasa role ya wamisionari na waarabu ktk kutuletea huu ukoloni.

Nakosa kabisa imanj na hizi dini zilizokuja na meli Islamic& Christianity [emoji22]

Sent using Jamii Forums mobile app
Kizuri zaidi MUNGU wa Wakristo halazimishi kumuabudu yeye.

Kimbembe ni mungu wa imani ile ambapo waamini wake humueleza kuwa ni muumbaji wa viumbe vyote na ana uwezo wa kufanya yote lakini anashindwa tu kujitetea anapodhihakiwa, na hutetewa na aliyeumbwa na yeye (Mtu)...[emoji849][emoji124]
 
Ni
Ukisoma kwa umakini biblia Mwanzo mpaka ufunuo utaelewa kuwa kitabu kimebadilisha wahusika, Sehtani ameitwa Mungu na Mungu ameitwa shetani.

Mungu wa kwenye biblia anaelezewa kuwa Mungu mwenye wivu anayechukia kuona unamsifu au kumfuata mungu mwingine, Anataka wewe tokea unaamka hadi unalala uwe unamuwaza yeye tu na kufanya kila kitu anachotaka yeye, wakati biblia haijaonesha kama Shetani ana wivu au anataka watu wafuate itikadi zake lasivyo atakasirika.

Kutokana na huu wivu, Mungu wa kwenye biblia ukihesabu ameua wanaume takribani millioni na ushee; 2, 345, 439 (Hapa hatujahesabu wanawake na watoto). Ukiconsider na source za nje ya biblia idadi inafika mpaka 22, 743, 746.

Watu alioua mungu ni wengi, kama wale vijana 42 aliowaua kwasababu walimtania Elisha kuwa ana upaa... Watu 147, 000 aliowaua kwasababu walitaka demokrasia maana walichoka kupelekeshwa na Mussa n.k.

Lakini Shetani wa kwenye biblia ameua watu 10 tu, tena hao 10 aliwaua kwasababu alishinikizwa na Mungu, Mungu alimbinya vidole shetani awaue wale watoto wa Ayubu.

Na muda huo huo, Mungu anasema atakuja siku ya mwisho kuchukua watu wake wachache tu na Kuwachoma kwa moto mkali wengine wote ambao hawakumsikiliza mchana na usiku.

Nani ni shetani apo? Na nani ni Mungu?
Ni sawa kwa kuwa ni ujinga unakusumbua ila ujinga ukikutoka utajitambua japo utakuwa umepoteza muda.
 
Watenda mabaya wanahukumiwa Broo.
Acheni Siasa kwenye Imani za watu.

Unapotaja Dini ya Kikristo unazungumzia ufalme Wa Mungu hapa Duniani na wanadamu ndio waliowekwa Ili waujenge juu ya msingi Wa Kristo.

Hakuna ufalme unaojengwa kirahisi. Ukristo imejengwa kwa upanga kama ulivyo uislamu. Waliotangulia walipambana sana kuleta utawala Wenye Sheria za Kikristo.
Una bahati umezaliwa kwenye nchi ambayo tayari watu walipambana na kujenga misingi hiyo ! Mshukuru Mungu kuzaliwa zama ambazo unakaa pembeni serikali inakulipia Kisasi.

Leo hii unaweka ukaona Wakristo wakikaa pembeni wanaona Makanisa yananajisiwa na watu wanaoana na kufunga ndoa za jinsia Moja wanasema kuwa Vita yetu si juu ya damu na Nyama Huku ushoga ukiwa unaenea Kwa Kasi.
Sasa unajiuliza ni Mungu Yupi wanataka aje ajipiganie Wakati amewaweka hapa Duniani Ili wafanye KAZI yake Kwa utukufu wake?

Wakristo wamejazana kwenye mabaa na madanguro wanalewa na uzinzi halafu wanawaachia Mashoga na Mabasha wanapanga Nani aongoze na kutawala na kutunga Sheria za Dunia kinyume na Mipango ya Mungu. Wakristo Wa Sasa wamepotoka na ni waoga?
Biblia inasema waoga na wasioamini sehemu yake ni Katika lile Ziwa liwakalo moto na Kiberiti.
Wakristo watatupwa Nje Kwa sababu wameondoka kwenye Jukumu la kuujenga ufalme Wa Mungu Duniani. Hakuna ufalme Wa Mungu unaotawaliwa na waovu.
Wakristo wanapaswa kuwa Chachu ya Utawala Wa Haki isiyotoka Nje ya Neno la Mungu. Hakuna haki Kwa watenda dhambi.

Basi tuache kuwa na Majeshi mana hatuna vita ya kimwili . Haiwezekani mana tuna KAZI ya kuujenga ufalme Wa Mungu kimwili na KIROHO. Paulo alitaka watu wale wanafunzi wake wazame zaidi kwenye ulimwengu Wa roho Ili vita ianzie Rohoni na kuonekana mwilini Katika kukemea dhambi na kujenga misingi ya Kikristo kwenye Tawala na mamlaka za kimwili ambazo zitasimama Katika kulipa kisasi Badala ya Mungu.
Serikali ni Watu na zinapaswa kuadhibu Kwa haki Badala ya Mungu.
Serikali zinapaswa kuwa chini ya Kristo .
Ukiona serikali hazitendi haki Ujue Wakristo wamelala.
Dunia imefikia ilipo Kwa sababu Wakristo Wa kweli wamelala na ni waoga. Wanazipenda nafsi zao matokeo yake wanajificha Nyuma ya mistari ya kuwa YESU alisema asiye na dhambi awe Wa kwanza kumpiga . Lakini Nenda mahakamani uone walivyojazana kwenye kesi za kugombania mpaka maiti kuzika.[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Respect!
Nafsini nilikuwa naona kabisa majibu haya ya 'vita vyetu vya roho, si vya nyama' yana walakini katika matumizi yake........ni kama watu wanatumia ktk kujificha tu na maovu yao lakini nilikosa utaalamu wa kulisema vizuri; umefafanua vizuri kabisa kwa mifano hai.
 
Dhambi ya Kumkufuru Mungu, hata ufanyeje, Huwa ni yamelele, Haina msamaha!!.
Kwahyo wewe hujawahi kufikiria kumtukana Mungu??
Em jaribu sasa...
Mungu ni..............malizia apo tusi lililokuja kichwan

Mungu ni..................
Mungu ni....................
Huwezi??? Huwezi??
Akili yako ina kuta.
 
Kwahyo wewe hujawahi kufikiria kumtukana Mungu??
Em jaribu sasa...
Mungu ni..............malizia apo tusi lililokuja kichwan

Mungu ni..................
Mungu ni....................
Huwezi??? Huwezi??
Akili yako ina kuta.
Hivi hii jeuri unaitoa wapi kuhoji kuhusu Mungu humu?
 
Ukisoma kwa umakini biblia Mwanzo mpaka ufunuo utaelewa kuwa kitabu kimebadilisha wahusika, Sehtani ameitwa Mungu na Mungu ameitwa shetani.

Mungu wa kwenye biblia anaelezewa kuwa Mungu mwenye wivu anayechukia kuona unamsifu au kumfuata mungu mwingine, Anataka wewe tokea unaamka hadi unalala uwe unamuwaza yeye tu na kufanya kila kitu anachotaka yeye, wakati biblia haijaonesha kama Shetani ana wivu au anataka watu wafuate itikadi zake lasivyo atakasirika.

Kutokana na huu wivu, Mungu wa kwenye biblia ukihesabu ameua wanaume takribani millioni na ushee; 2, 345, 439 (Hapa hatujahesabu wanawake na watoto). Ukiconsider na source za nje ya biblia idadi inafika mpaka 22, 743, 746.

Watu alioua mungu ni wengi, kama wale vijana 42 aliowaua kwasababu walimtania Elisha kuwa ana upaa... Watu 147, 000 aliowaua kwasababu walitaka demokrasia maana walichoka kupelekeshwa na Mussa n.k.

Lakini Shetani wa kwenye biblia ameua watu 10 tu, tena hao 10 aliwaua kwasababu alishinikizwa na Mungu, Mungu alimbinya vidole shetani awaue wale watoto wa Ayubu.

Na muda huo huo, Mungu anasema atakuja siku ya mwisho kuchukua watu wake wachache tu na Kuwachoma kwa moto mkali wengine wote ambao hawakumsikiliza mchana na usiku.

Nani ni shetani apo? Na nani ni Mungu?
Watu wa dini ndio wamemfanya Mungu aonekane hivi unavyomsema.

Mungu ni pendo,na amejaa rehema na neema kubwa.Ni machache sana yameandikwa kumuhusu,ndio maana kama utayasoma kwa hisia za chuki,hutamwelewa.

Kile tu tunachoweza kusema,ni kwamba akili yetu haina uwezo wa kuutafakari ukuu wake,maana ni Mkuu sana.

Hakuna anayejua alipokuwa tumboni kwa mamaye aliishije,kama tu mtoto mchanga asivyoweza kumwelewa mzazi,yawezekana nasi ndivyo tulivyo kwa Mungu wetu muumba mbingu na nchi.
Mungu azidi kuturehemu ili tumjue zaidi.Atupe mioyo ya unyenyekevu na uvumilivu.
Ni yeye tu ajuaye siri ya kifo.
Yesu Kristo ametupatia tumaini la uzima wa milele na kifo amekiita "kulala tu"

Mungu akuhurumie ili ukatangaze ukuu wake

Sent from my Infinix X626 using JamiiForums mobile app
 
Ukiwa na afya njema, husumbuliwi na madeni, na una vijifedha vya kubadilisha mlo, UTAONGEA MENGI
Jibu hoja kwa hoja, sio kujificha kwenye kivuli cha kutisha watu
Huyo Mungu wenu miaka 300 iliyopita hakuna mtu aliyekuwa anamfahamu hapa Africa, so usitishe sana watu wanaoichallenge masimulizi ya Biblia
 
Maana yeye anafahamu kwamba fulani ata uruke ruke vipi utaishia kufa katika uzinzi au ujambazi sasa kwa nini tena iwe anakuandalia adhabu wakati alijua huwezi mtii.

Iweje akulete duniani kuja kuhitimisha safari ya uhai wa watu wengi.

Tunaomba Mungu tujaailie tuwe na safari njema. Ila baada ya km 230 tunaanguka tunatoa sababu shetani kaingilia kati ya safari yetu. Inaleta maswali
Maswali ni mengi kuliko majibu kwakweli.

Soma hii warumi uniambie kama Paulo anamake sense



https://www.bible.com/sw/bible/1818/ROM.10.SRUV

WARUMI 9​

10. Wala si hivyo tu, lakini Rebeka naye, akiisha kuchukua mimba kwa mume mmoja, naye ni Isaka, baba yetu, 12. aliambiwa hivi, Mkubwa atamtumikia mdogo 11.(kwa maana kabla hawajazaliwa wale watoto, wala hawajatenda neno jema wala baya, ili lisimame kusudi la Mungu la kuchagua, si kwa sababu ya matendo, bali kwa sababu ya nia yake Mungu),
13.Kama ilivyoandikwa, Nimempenda Yakobo, bali Esau nimemchukia.

14.Tuseme nini basi? Kuna udhalimu kwa Mungu? La hasha! 15 Maana amwambia Musa, Nitamrehemu yeye nimrehemuye, nitamhurumia yeye nimhurumiaye. 16 Basi, kama ni hivyo, si katika uwezo wa yule atakaye, wala wa yule apigaye mbio; bali wa yule arehemuye, yaani, Mungu.

17 Kwa maana Maandiko yasema juu ya Farao, ya kwamba, Nilikusimamisha kwa kusudi hili, ili nioneshe nguvu zangu kwako, jina langu likatangazwe katika nchi yote. 18 Basi, kama ni hivyo, atakaye kumrehemu humrehemu, na atakaye kumfanya mgumu humfanya mgumu.


19. Basi, utaniambia, Mbona angali akilaumu? Kwa maana ni nani ashindanaye na kusudi lake?
20. La! Sivyo, Ee binadamu; wewe u nani umjibuye Mungu? Je! Kitu kilichoumbwa kimwambie yeye aliyekiumba, Kwa nini umeniumba hivi?
21. Au mfinyanzi je! Hana amri juu ya udongo, kwa fungu moja la udongo kuumba chombo kimoja kiwe cha heshima, na kimoja kiwe hakina heshima?
 
Zilongwa mbali,, zitendwa mbali, hapa hatuko kujadili Iran, Quran, wala kadhi. Mleta uzi ni mgala mwenzenu na amesoma biblia na kukiona hicho alichokiona, suala la kusema biblia aisomwi kama gazeti usiniambie mimi bali mwambie huyo mgala mwenzio kwa kuwa yeye ndio alieleta uzi,, shida yangu mimi kwako ni kuingiza Quran, iran, kadhi, sijui albadir kwenye uzi ambao hata hivyo vitu havihusika, na ukitaka kujadili hayo fungulia uzi wako kama alivyofanya mleta uzi,, ila kwa leo jadiliana na mgala mwenzio juu ya kile alichokiona kwenye biblia.
[emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16]

Mkuu tuwache Wagala pulizi
 
Nimesikitika sana kuona watu wasio na shukrani wanavyoishi na kujihisi wapo sahihi. Hakuna mahali popote Shetani alipoweka upatanisho ila ni Mungu aliyefanya hivyo na alitupatisha kupitia kwa damu ya Yesu.

Ingekuwa Mungu ni Shetani kipindi Abrahamu ameambiwa amtoe sadaka isaka naamini asingezuia na angeacha ila kuzuia maana ya kitendo hicho ni kuelezea moja ya sifa ya Mungu nayo ni huruma..

Kizazi kichafu kiliangamizwa ili dunia iwe mahali salama pa kuishi. Shetani ni baba wa ukahaba ,uzinzi na mengineyo kama Mungu angekuwa Shetani inawezekanaje achukizwe na tabia hizo na kuangamiza?

Tuache kukufuru Imani ni nuru ya moyo na wewe tayari Shetani kakujaribu na ukatumbukia majaribuni. Jaribu kila siku ukiamka usali sala hii"Baba yetu uliye Mbingu.......", ni sala ya kuongeza imani
 
Back
Top Bottom