Mungu ndiye shetani(?)

Mungu ndiye shetani(?)

Afrika Tena nawakati Ethiopian wanamfahamu tokea miaka hiyo ya before Christ (B.C) kwa hiyo Ethiopian haipo Africa
Ni Waafrika wangapi kipindi hicho walikuwa wakristo?
Mwaka 1400 ni watanzania wangapi walikuwa wakristo?
Mnaona Ukristo kama ndio imani universal vile wakati imekuja tu juzi,
 
Nimefanya ushenzi sana humu duniani ila sikawahi kumkufuru Mungu
Najua Munguu na ni mwingi wa rehema utanisamehe dhambi zangu.
Tenda jambo kwa huyu mtoa mada ehee Mungu nakuomba
....najua Mungu ni mwingi wa rehema utanisamehe dhambi zangu.

Ishia hapo, itapendeza.
 
Jamaa mmoja aliwaita watu kadhaa kutoka mataifa tofauti na Kila mmoja alimtaka ataje jina la Mungu wake...ikawa Kila mmoja akataja jina tofauti na basi mzozo ukaibuka miongoni mwao...Kila mmoja akisema kuwa jina la Mungu wake ndilo sahihi...wakati hayo yakiendelea chizi mmoja alikuwa akipita maeneo hayo na mara yule jamaa akamuuliza: " na wewe Mungu wako ni yupi" . Yule chizi bila kusema neno alinyoosha kidole kuelekea Jua....na Kisha akaondoka. Basi wale waliobaki walicheka sana...
It is a characteristic of a great mind to entertain a thought without accepting it.
 
Mawazo yake hayachunguziki, akili zake sio kama za kwetu.
Maana yeye anafahamu kwamba fulani ata uruke ruke vipi utaishia kufa katika uzinzi au ujambazi sasa kwa nini tena iwe anakuandalia adhabu wakati alijua huwezi mtii.

Iweje akulete duniani kuja kuhitimisha safari ya uhai wa watu wengi.

Tunaomba Mungu tujaailie tuwe na safari njema. Ila baada ya km 230 tunaanguka tunatoa sababu shetani kaingilia kati ya safari yetu. Inaleta maswali
 
Huu ni mfano mbaya
Hivi mfano wewe umeamua kufuga kuku Kisha siku moja ukaamua kuwachinja kuku wote uwale supu na nyama nyingine ugawe,hapo kuna dhambi au lawama kuchinja Mali yako?

Sasa Mungu akiamua kuua watu wake aliowaumba mwenyewe wewe unakerekwa na nini? Akiamua siku moja kuijaza maji dunia ili wahuni wafe Kisha wengine wabaki kwenye safina si maamuzi ya kwake? Usimpangie Mungu Cha kufanya mzee baba.
 
Umeandika pumba tupu hapa.
Pointless.
Watenda mabaya wanahukumiwa Broo.
Acheni Siasa kwenye Imani za watu.

Unapotaja Dini ya Kikristo unazungumzia ufalme Wa Mungu hapa Duniani na wanadamu ndio waliowekwa Ili waujenge juu ya msingi Wa Kristo.

Hakuna ufalme unaojengwa kirahisi. Ukristo imejengwa kwa upanga kama ulivyo uislamu. Waliotangulia walipambana sana kuleta utawala Wenye Sheria za Kikristo.
Una bahati umezaliwa kwenye nchi ambayo tayari watu walipambana na kujenga misingi hiyo ! Mshukuru Mungu kuzaliwa zama ambazo unakaa pembeni serikali inakulipia Kisasi.

Leo hii unaweka ukaona Wakristo wakikaa pembeni wanaona Makanisa yananajisiwa na watu wanaoana na kufunga ndoa za jinsia Moja wanasema kuwa Vita yetu si juu ya damu na Nyama Huku ushoga ukiwa unaenea Kwa Kasi.
Sasa unajiuliza ni Mungu Yupi wanataka aje ajipiganie Wakati amewaweka hapa Duniani Ili wafanye KAZI yake Kwa utukufu wake?

Wakristo wamejazana kwenye mabaa na madanguro wanalewa na uzinzi halafu wanawaachia Mashoga na Mabasha wanapanga Nani aongoze na kutawala na kutunga Sheria za Dunia kinyume na Mipango ya Mungu. Wakristo Wa Sasa wamepotoka na ni waoga?
Biblia inasema waoga na wasioamini sehemu yake ni Katika lile Ziwa liwakalo moto na Kiberiti.
Wakristo watatupwa Nje Kwa sababu wameondoka kwenye Jukumu la kuujenga ufalme Wa Mungu Duniani. Hakuna ufalme Wa Mungu unaotawaliwa na waovu.
Wakristo wanapaswa kuwa Chachu ya Utawala Wa Haki isiyotoka Nje ya Neno la Mungu. Hakuna haki Kwa watenda dhambi.

Basi tuache kuwa na Majeshi mana hatuna vita ya kimwili . Haiwezekani mana tuna KAZI ya kuujenga ufalme Wa Mungu kimwili na KIROHO. Paulo alitaka watu wale wanafunzi wake wazame zaidi kwenye ulimwengu Wa roho Ili vita ianzie Rohoni na kuonekana mwilini Katika kukemea dhambi na kujenga misingi ya Kikristo kwenye Tawala na mamlaka za kimwili ambazo zitasimama Katika kulipa kisasi Badala ya Mungu.
Serikali ni Watu na zinapaswa kuadhibu Kwa haki Badala ya Mungu.
Serikali zinapaswa kuwa chini ya Kristo .
Ukiona serikali hazitendi haki Ujue Wakristo wamelala.
Dunia imefikia ilipo Kwa sababu Wakristo Wa kweli wamelala na ni waoga. Wanazipenda nafsi zao matokeo yake wanajificha Nyuma ya mistari ya kuwa YESU alisema asiye na dhambi awe Wa kwanza kumpiga . Lakini Nenda mahakamani uone walivyojazana kwenye kesi za kugombania mpaka maiti kuzika.[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Ni Waafrika wangapi kipindi hicho walikuwa wakristo?
Mwaka 1400 ni watanzania wangapi walikuwa wakristo?
Mnaona Ukristo kama ndio imani universal vile wakati imekuja tu juzi,
Even kwenye agano la kale Ethiopian au kush wametajwa na wametoa baadhi ya watumish wa Mungu huyu Mungu ambaye unamtuhumu ameletwa na wazungu, ndo maana hata Leo Ethiopia ni nchi yenye wakristo wengi
 
Una bahati unamkufuru Mungu mwenye nguvu, anayeweza kujitetea na mwingi wa rehema.
Ungekuwa ndiyo wale wenye dini ya Kiarabu sasa hivi ungekuwa kwenye mahakama ya kadhi au wamekuchinja kichwa.
Karibu kanisani, ujifunze zaidi. Vita vyetu ni vya kiroho na si vya damu na nyama.
Usisahau mleta uzi ni J Makamba mlamba asali amevimbiwa na kukufuru
 
Hakika kungekuwa na Mungu, mateso hayangekuwapo, ni shetani kabeba ulimwengu akitaka umsujudu ili mambo yako yanyooke. Chunguza walionyoosha maisha yao wanafanya nini, hata kama anajiita mlokole.
 
Umeandika pumba tupu hapa.
Pointless.
Leta pointi zako achana na Pointless na Pumba za watu Wengine halafu unasema unamwamini Mungu.

Nyie ndio waumini Uchwara wanaopotosha maandiko Kwa uelewa MDOGO Wa maneno. Jadili mambo Kwa uelewa mpana kitabu Chako unachokisoma hakina majibu ya mambo Yote yanayoulizwa Kwa Ujumla wake.
Mfano Majibu ya sayansi hayajibiwi kirahisi rahisi. Serikali za kidunia zinafanya KAZI ya Mungu au Hilo huamini ? unafikiri KAZI ya mungu ni kushika vitambaa tu na Chumvi na mafuta ya upako Wa waonyesha mazingambwe?
 
Siku ukimjua Mungu ni nani, huyo hatakuwa Mungu tena...
 
Msitoe povu sana...jibuni hoja...mnaweza mkakasirikiana bure...kumbe Mungu na Shetani huwa wanakutana na kupiga stori, mfano kama mwanzoni mwa kitabu cha Ayubu...Truth is born out of an argument.
Kama vile Samia na mbowe[emoji1787]
 
Zilongwa mbali,, zitendwa mbali, hapa hatuko kujadili Iran, Quran, wala kadhi. Mleta uzi ni mgala mwenzenu na amesoma biblia na kukiona hicho alichokiona, suala la kusema biblia aisomwi kama gazeti usiniambie mimi bali mwambie huyo mgala mwenzio kwa kuwa yeye ndio alieleta uzi,, shida yangu mimi kwako ni kuingiza Quran, iran, kadhi, sijui albadir kwenye uzi ambao hata hivyo vitu havihusika, na ukitaka kujadili hayo fungulia uzi wako kama alivyofanya mleta uzi,, ila kwa leo jadiliana na mgala mwenzio juu ya kile alichokiona kwenye biblia.
Inshort: ajibu hoja,aache Mbambamba[emoji28]
 
Elimu yako na uelewa wako juu yako ya Mungu uko limited na sio wewe ni tatizo la watu wengi, mwanadamu kupitia adamu alimkataa Mungu na mfumo wake wa maisha ndo maana wewe na wenzako mnatukana Mungu na hawafanyi chochote sababu Mungu hawez shindana na binadamu ambaye atakufa
Tatzo lenu hamujibu hoja za mleta
Mi sio mleta uzi,ukinishambulia sikuelewi[emoji4]
 
Tatizo umezaliwa juzi na ukakulia mjini hujawahi kukaa na Bibi au Babu aliyeishi Miaka 140 iliyopita akakusimulia maisha yaliyokuwa kabla ya Kuja wamisionari.

Wamisionari ni Kama unavyoona leo Wanasiasa na Viongozi Wa Dini?

Wamisionari walileta mwanga Afrika na Duniani kote .
Watu jeuri waliojaribu kuwaua ndio chanzo Cha serikali zao kuleta utawala Wa Kikoloni.
Wamisionari walipokuja walikuta Tawala za asili zilikuwa na Sheria zisizofaa na walipojaribu kuwakosoa walioshia kuuawa. Mfano Sheria za Machifu kupora wake za watu Huku wakiwa na wake wengi . Machifu kupora mifugo ya watu. Kabila Moja kuvamia kabila jingine na kuteka wanawake na kuua wanaume na watoto BILA sababu Huku wakiwa na nia ya kupora Mali na mifugo.

Kuua walemavu , makafara ya watoto. Sheria NYINGI zilikua ni mwenye nguvu mpishe.
Waafrika wangewapokea Wamisionari na kuyafanyia KAZI yale mema waliyokuja nayo na kujifunza Namna Bora ya kujitawala Kwa haki Majeshi na serikali za Kikoloni zisingekuja Kirahisi.
Wangetetea Mila zao na dini zao kwa hoja Badala ya kutumia nguvu kuzilinda Wakati hawakua wanatendeana haki matokeo yake pakawa na kusalitiana kutokana na Chuki KUBWA iliyokuwepo miongoni mwa MAKABILA ,Koo,na Hata familia. Ikawa ni chanzo Cha kutawaliwa kirahisi.

Waafrika kabla ya mkoloni WALIKUA wamegawanyika sana ndio Maana Kuna Koo NYINGI na MAKABILA Mengi ambayo mpaka Sasa hayaelewani Kwa lugha na Hata Tabia. Dini za Kikoloni NDIZO zilizosababisha Leo Msambaa anaoana na na Mchaga. Kabla ya Hapo haikuwezekana kamwe. Mgogo kamwe haikuwezekana akaoa mmasai au Mzaramo akamuoa Mmeru. Watu waliokuwa wamegawanyika kwa kiwango hicho hawangeweza kuwa na Taifa Moja BILA kuwa na serikali yenye nguvu ambayo ilikuwa ni ya Mkoloni Hapo mwanzo kabla ya uhuru.

Historia ya Mwafrika kabla ya mkoloni inajaribu kuficha madhaifu ya waafrika ambayo mpaka Leo yapo wazi na Ndiyo yanaturudisha Nyuma tunabaki kudanganyana Badala ya Kukaa chini na Kuja na será zetu za Elimu ,mitaala Bora ya Elimu, Kariba Bora ,kuwasimamia watawala Ili watekeleze majukumu Yao Kwa maslahi ya umma, Kupinga wachache kuhodhi Mali za umma Kwa mgongo Wa madaraka. Kupinga Kodi KUBWA kwenye rasilimali zinazotokana na juhudi ya wananchia kuzalisha Mfano Ushuru Wa mazao n.k.Huu ni mwendelezo Wa ukoloni.
Ha ha ha....
JamiiForums-1086713271.jpg
 
Kizuri zaidi MUNGU wa Wakristo halazimishi kumuabudu yeye.

Kimbembe ni mungu wa imani ile ambapo waamini wake humueleza kuwa ni muumbaji wa viumbe vyote na ana uwezo wa kufanya yote lakini anashindwa tu kujitetea anapodhihakiwa, na hutetewa na aliyeumbwa na yeye (Mtu)...[emoji849][emoji124]
Ngumu kumeza[emoji28]
 
Nimesikitika sana kuona watu wasio na shukrani wanavyoishi na kujihisi wapo sahihi. Hakuna mahali popote Shetani alipoweka upatanisho ila ni Mungu aliyefanya hivyo na alitupatisha kupitia kwa damu ya Yesu.

Ingekuwa Mungu ni Shetani kipindi Abrahamu ameambiwa amtoe sadaka isaka naamini asingezuia na angeacha ila kuzuia maana ya kitendo hicho ni kuelezea moja ya sifa ya Mungu nayo ni huruma..

Kizazi kichafu kiliangamizwa ili dunia iwe mahali salama pa kuishi. Shetani ni baba wa ukahaba ,uzinzi na mengineyo kama Mungu angekuwa Shetani inawezekanaje achukizwe na tabia hizo na kuangamiza?

Tuache kukufuru Imani ni nuru ya moyo na wewe tayari Shetani kakujaribu na ukatumbukia majaribuni. Jaribu kila siku ukiamka usali sala hii"Baba yetu uliye Mbingu.......", ni sala ya kuongeza imani
Mitume wa mungu kina daudi,yakobo, Suleiman n.k wote walizini ila mungu bado akawa upande wao.

Imekaaje hii unaposema shetan ndo baba wa uzinzi[emoji848]
 
Nilikuwa na hili wazo ila nikasita kulitoa, "ulimwengu wote ni wa shetani, ukicheza nae vizuri utakula Bata. Tafakari kwa makini kila penye maendeleo shetani yupo. Utasikia Mungu kanipa, kakupa wewe una vichwa viwili? Una nini zaidi akupendelee? My friend "life is a game"
Wachina walijitambua mapema sana
ndo maana wanapata maendeleo kwa Kasi sana na kufanya Yale tuliyozani kwa uwezo wao yasingewezekana

Hizi Islamic& Christianity zimetulemaza Sana waafrika na ndo tools za kutufanya tuzid kuamaskini forever.

Rejea yanayoendelea nyumba za ibada,
Ni michango michango Kwenda mbele.
Watu hawafanyi kazi siku nzima wanasali

Kwa mwendo huu,
Taifa linasongaje mbele Sasa, tujitafakari[emoji848]
JamiiForums-1086713271.jpg
 
Back
Top Bottom