Mungu Yuko wapi?

Mungu Yuko wapi?

Mungu ni mada pana sana maana kuna miungu mingi mno mengine ikiwa watu, vitu na roho, nafsi ila aliyeumba kila kitu ni MMOJA.

Ndo maana ikaandikwa katika Yeremia 10:11 kuwa wakati ukifika Miungu isiyoumba mbingu na nchi lazima iangamizwe.

Je, kwanini kumekuwa na sintofahamu nyingi kuhusu aliyeumba vyote, wote na yote kuwepo ama kutokuwepo?

Kwa sababu uumbaji wote ulitekwa nyara baada ya aliyekasimiwa uumbaji kuvamiwa (Moyo Wa Mwanzo, Mwanzo 1:1)ndo maana ukija soma katika 1korintho 15:24-28 “Hapo ndipo mwisho, atakapompa Mungu Baba ufalme wake; atakapobatilisha utawala wote, na mamlaka yote, na nguvu.”

“Maana sharti amiliki yeye, hata awaweke maadui wake wote chini ya miguu yake.”

Tuki soma hapo tunaelewa kwamba kumbe Ufalme, mamlaka na nguvu havikuwa kwa muumba baada ya uumbaji kutekwa, ndo maana hata ibilisi alikuwa na uwezo wa kumpandisha Yesu kwenye kinara na kumwambia hii yote unayoona ni miliki yangu nisujudie nikupe yote katika Luka 4:6 “Ibilisi akamwambia, Nitakupa wewe enzi hii yote, na fahari yake, kwa kuwa imo mikononi mwangu, nami humpa ye yote kama nipendavyo.”


Kitu ambacho wengi hawajui ni kuwa aliyetuumba anaenda kwa majira na wakati na habaki palepale kila lango (siku). Mfano habari za Yesu ziliandikwa tangia kipindi cha nabii Isaya lakini alipokuja wayahudi wakamkataa na kusema ni mtoto wa seremala tu wao wanamsubiri masihi paka leo 90% ya waisrael hawamkiri Kristo.
Wakristo mmekuta dini ya wayahudi mmeiba mmeongeza story zenu mnajigamba. Ukimaliza uniambie aliyemuumba Mungu Ni nani?
 
Wakristo mmekuta dini ya wayahudi mmeiba mmeongeza story zenu mnajigamba. Ukimaliza uniambie aliyemuumba Mungu Ni nani?

Ukikaa kwenye kituo cha dini sijui ukristo na uislam au dini yeyote hutamwelewa aliyeumba maana yeye hana dini wala dhehebu. Na aliyeumba yeye hajaumbwa bali yeye ndo CHANZO HALISI (Real Source) wa kila kitu.
 
𝐓𝐡𝐞𝐫𝐞 𝐢𝐬 𝐒𝐮𝐩𝐞𝐫 𝐍𝐚𝐭𝐮𝐫𝐚𝐥 𝐏𝐨𝐰𝐞𝐫(𝐄𝐱𝐚𝐥𝐭) 𝐟𝐨𝐫 𝐞𝐚𝐜𝐡 𝐚𝐧𝐝 𝐞𝐯𝐞𝐫𝐲𝐭𝐡𝐢𝐧𝐠 𝐭𝐡𝐢𝐧𝐤 𝐡𝐨𝐰 𝐢𝐬 𝐡𝐞𝐦𝐢𝐬𝐩𝐡𝐞𝐫𝐞 𝐚𝐧𝐝 𝐭𝐡𝐞 𝐞𝐧𝐭𝐢𝐫𝐞 𝐩𝐥𝐚𝐧𝐞𝐭𝐬.
 
Usitake kuonekana mwelevu kufanya kufuru ili ufurahishe watu au kikundi fulani nakushauri usijitafutie laana kwa haya maandiko yako maana hasira ya Mungu ni kali sana tubu jiepusha na hizi kauli (acha kumfanyia kazi shetani kupotosha kondoo wa Mungu ) usipo sikia ipo siku na saa utakumbuka maandishi haya
Usimtishe mueleweshe ila kwa mwenye akili na vilivyomo humu duniani mwenye akili lazima ajue vina mwenyewe
 
Nimesoma Biblia na inamakosa kuhusu dunia, viumbe, historia, Sayansi na utu kuliko kitabu chochote katika historia ya binadamu. Ukitaka uache ukristo soma Biblia. Hata mtoto wa la pili anaweza akatengeneza storybook na ikaeleweka kuliko Biblia. Kama unabisha nitajie Babu yake Yesu mzaa baba ni nani?
Tatizo lako una soma Biblia kama story book.

Biblia ni kitabu kilichokamilika tena kwa matukio mengi haswa..Jibu lako lipo kitabu cha Mathayo 1:1-17
 

Attachments

  • Screenshot_20230514-213746.png
    Screenshot_20230514-213746.png
    48 KB · Views: 19
Usitake kuonekana mwelevu kufanya kufuru ili ufurahishe watu au kikundi fulani nakushauri usijitafutie laana kwa haya maandiko yako maana hasira ya Mungu ni kali sana tubu jiepusha na hizi kauli (acha kumfanyia kazi shetani kupotosha kondoo wa Mungu ) usipo sikia ipo siku na saa utakumbuka maandishi haya
Pole sana!
 
Tatizo lako una soma Biblia kama story book.

Biblia ni kitabu kilichokamilika tena kwa matukio mengi haswa..Jibu lako lipo kitabu cha Mathayo 1:1-17
Umejiona mjanja ee ndo maana nakuambia soma Biblia nzima ndo urudi. Haya nenda kasome luka 3 23 mpaka 38 uniambie Babu yake Yesu Ni nani. Jacob au Heli. Ukija na jibu moja nishtue
 
Kuna mtu alisema ubongo ni receiver tu, kuna master brain ipo ambayo inatunza kumbukumbu zako na ikifika siku ya mwisho ndo tutajua hatujui pale utakaposhangaa una mwili mpya na ubongo mpya usioungua ukaisha ila maumivu hayazoeleki.

INASIKITISHA MNO.
Hii simulizi na hekaya umeitoa wapi ? Uliwahi kua na huo mwili mpya ukaonja joto ya jiwe au umesimuliwa na waliowahi kufanywa hivyo ? Mda mwingine tuwe na kiasi Cha kuogopeshana jaman, usiwajaze watu uoga swali ni kwamba ukifa unaenda wapi ?
 
Ushaambiwa ukiondoa DINI hakuna MUNGU, kwa hio jiongezee unataka kua mpagani au unataka kua mtu wa dini zilizoletwa na Majahazi ?

Sio kweli maana hata kipindi cha Ibrahim ambapo wakristo kwa waislam wanaamini ndo Baba yao kila mtu akivutia kwake hakukuwa na DINI na Ibrahimu hakuwa na DINI.

Dini zimeanza baada ya Isaka na Ishamael kumzika baba yao Ibrahim na kila mmoja kwenda njia yake akifundishwa namna ya kuabudu na mama yake ndo ukatokea ukristo na uislam kabla ya hizi zengine zote.

Muumba wa vyote, wote na yote hana DINI.
 
Sio kweli maana hata kipindi cha Ibrahim ambapo wakristo kwa waislam wanaamini ndo Baba yao kila mtu akivutia kwake hakukuwa na DINI na Ibrahimu hakuwa na DINI.

Dini zimeanza baada ya Isaka na Ishamael kumzika baba yao Ibrahim na kila mmoja kwenda njia yake akifundishwa namna ya kuabudu na mama yake ndo ukatokea ukristo na uislam kabla ya hizi zengine zote.

Muumba wa vyote, wote na yote hana DINI.
Ndio maana nikasema ukiondoa DINI hakuna MUNGU, wewe hizo habari kusingekua na Biblia au Qur'an ungezijulia wapi ?
 
Umejiona mjanja ee ndo maana nakuambia soma Biblia nzima ndo urudi. Haya nenda kasome luka 3 23 mpaka 38 uniambie Babu yake Yesu Ni nani. Jacob au Heli. Ukija na jibu moja nishtue
Wapi pamekuchanganya hapo. hakuna ujanga wowote hapo ni kuelimishana
 

Attachments

  • Screenshot_20230514-215411.png
    Screenshot_20230514-215411.png
    44.6 KB · Views: 23
  • Screenshot_20230514-213746.png
    Screenshot_20230514-213746.png
    48 KB · Views: 24
Hakuna ambaye haabudu chochote yaani wapagani kama wanavyoitwa,ndo maana ikaandikwa hazina ya mtu ilipo ndipo na moyo wake ulipo.

So kama unaabudu sana hela basi huyo ndo mungu wako maana hela ni Roho.
 
Wapi pamekuchanganya hapo. hakuna ujanga wowote hapo ni kuelimishana

Usisome Kitabu (biblia) kama historia ndo maana kuna majira na wakati wa kila jambo katika Kitabu mfano, Katika 1Korintho 15:28 inasema mwana naye yaani Yesu atawekwa Chini ya Muumba wa vyote,wote na yote “Basi, vitu vyote vikiisha kutiishwa chini yake, ndipo Mwana mwenyewe naye atatiishwa chini yake yeye aliyemtiishia vitu vyote, ili kwamba Mungu awe yote katika wote.”

Na katika Zekaria 14:9 inasema Majira ikifika “Naye Bwana atakuwa Mfalme juu ya nchi yote; siku hiyo Bwana atakuwa mmoja, na jina lake moja.”

Lakini wengi wanaamini aliyeumba anamajina meeengiiii but hayo majina yote ni nafsi zinazojitegemea katika majira husika ilikuwa sawa.
 
Ndio maana nikasema ukiondoa DINI hakuna MUNGU, wewe hizo habari kusingekua na Biblia au Qur'an ungezijulia wapi ?

Biblia sio kitabu cha dini ndo maana nakiita KITABU but kupitia mabadiliko ya majira na wakati mbalimbali ikafanywa ya dini ila hata kabla ya ukristo kilikuwepo kipindi cha Mussa ambaye ndie ameandika kitabu cha MWANZO,Isaya na manabii wengi tu wakubwa.
 
Back
Top Bottom