Mungu Yuko wapi?

Mungu Yuko wapi?

Kila tamaduni Ina Mungu wake. Umewajua wa kiislamu na kiyahudi kwa sababu ya utumwa na ukoloni, tungetawaliwa na wahindi tungekuwa wahindu tunaabudu masanamu. Hamna Mungu wa ukweli

Miungu ipo mingi kutokana na mambo mbalimbali ila aliyeumba ni MMOJA.
 
Basi na ulimwengu hujaumbwa...ni chanzo halisi. Nipe good argument sio assumption.

Muumba hakuumba ulimwengu wala dunia bali mbingu na nchi Mwanzo 1:1. Na ukitaka uelewe zaidi dunia na ulimwengu sio ili umbo unaloona bali ni mfumo unaotawala watu na vitu.
 
Hiyo dini inaitwa judaism, au uyahudi. Ndo maana nakuambia upo bongo unajua dini mbili tu duniani wakati zipo zaidi ya 10000. Kila mmoja na Mungu wake na sheria zake.

Unasema judaism sababu ndicho ulichokuta kwenye vitabu na article mbalimbali ukaaminishwa hivyo.Najua Dini zipo nyingi sana lakini zote izo hazikupi kweli bali utengano kiimani.
 
Hizi story za kumuambia mtoto ili asiwe anaiba pipi Ila sio mimi. Nenda kasome biology nervous system form 2 alafu urudi.
bro ni heri ukae kmy Uwepo wa Mungu unathibitika na sio mpk yakukute ndo uamin wapo waliokufulu yakawakuta makubwa na ww ni swala la mda tu. so you better shut your mouth
 
Ulimwengu wa Giza ni upi? Upo wapi? Una ushahidi Kama upo? Kama huna kwa Nini huamini tembo wanaopaa usiku Ila unaamini hayo madude

Kama hujui zipo falme na mamlaka za giza ambazo zinatumia watu hawa hawa unaowaona, hata nikifafanua hutaelewa.
 
Vitabu vya mwanzo ni vya dini ya Hinduism ambayo zipo za 3000BC so kusema Biblia ni ya kwanza ni uwongo. Kulikuwa na maandiko ya dini za Persia, ugiriki, Norse, na zingine kabla ya uyahudi na ukristo. So hoja yako sio kweli. Sema ni kitabu Cha kwanza Kati ya viwili unavyoviona bongo. Usiseme uwongo.

Hivyo ndo unavyojua kwa kugoogle lakini Kweli itabaki kweli.
 
We umeamua kuchagua Biblia out of all books in the world kuhusu Mungu. Why? Nipe sababu nje ya ukoloni, kuzaliwa katika ukristo, kudanganya na mchungaji mponyaji, etc. Why umechagua Biblia umeacha zingine. Kama ishu Ni ya kwanza sio kweli Kuna dini zenye maandiko kabla ya Biblia, so nipe sababu ya msingi

Nakupa sababu moja tu ya msingi out of all books KITABU ndo kimetumika na kilitumika kuweka maagano ya siri mengi sana dhidi ya atendaye kwa haki.

Hivyo sio KITABU tu cha kawaida cha story kama wengi wanavyoamini na kujua.

Na mimi nakiita KITABU sio biblia kwakuwa hayo maandiko yako kwenye sehemu nyingi sana.
 
Shetani ni wewe na Mungu Ni wewe. Coz hata kwenye Biblia yako hamna kosa ambalo shetani kafanya, hamna sheria ambayo kavunja, Mungu kaua watu million huko shetani kauwa 10 tu na kwa ruhusa ya Mungu.

Hujasoma kitabu vizuri rudi kasome, akili za wengi zimeaminishwa na dunia na ulimwengu kuwa MUUMBA ndo anaua watu.

KERUBI aliyekuwa malaika wa sifa kabla ya kuasi ukisoma Isaya 14:13-15 utakuta kwanini alitupwa chini.
 
Yes indeed

Tena zimetoka maeneo ya Mesopotamia huko Iraq ya leo.
Jamii za kule zilianza kuja na hekaya hzo za uumbaji na gharika
 
Mi najiuliza maswali mengi. Mungu Ni Nini, anataka Nini na Yuko wapi.

Ukifuatilia historia ya binadamu tokea tukiwa wawindaji maporini miungu ilikuwepo. Wazee walikuwa wanaongoza vijana kwa kuwaambia kuwa Mungu anataka mfanye hivi, na hio miungu ilikuwepo pangoni ambapo wazee tu wanaingia, baadae vijana wakajitoa akili kwenda wakaona wazee ni waongo na hamna kitu mule. Wagiriki wakaja na miungu yao wakasema ipo ya milima ya Olympus, Leo hii watu wamepanda milima yote ugiriki hawajaona miungu hio.

Wakaja wayahudi, wakasema Mungu yupo mawinguni. Ukifuatilia hata Yesu alipaa mawinguni, Mungu alifungua madirisha ya mbinguni kuleta mafuriko, alichungulia kutoka mawinguni kwenye mnara wa babel, etc. Waislamu nao wakaja na mbingu Saba sijui. Anyways wazungu wametengeneza ndege na rocket zimeenda mawinguni, nje ya dunia, mpaka mwezini. Sasa hivi watu wa dini wanasema yupo nje ya ulimwengu.

So nikagundua trend, wanamficha, wanamweka mbali ili watu wasiweze kumfikia, why? Kwa sababu hayupo? Kwa sababu hajasema hizo sheria? Why wanamficha. Afu wanakuambia anataka uamini yupo ndo utapona usipoamini unaunguzwa. Ukiuliza nikimwona afu nikamwamini, anasema no, lazma usimwone ndo uamini. Na wanaweka kifo mwisho wa kumuani ili waweze kuendelea kutunga sheria kwa jina lake na kuweza kuendelea kutawala watu kwa sababu hamna mtu Ashawahi kurudi akasema baada ya kifo kipo hivi.

Mwanasayansi mi nauliza Mbinguni Kuna Nini. Hamna njaa hamna maumivu hamna ndoa hamna chochote zaidi ya kumuabudu Mungu. Watu kanisani na msikitini hawapendi kwenda unategemea watapenda milele ya Ibada. So wakaamua kuanzisha motoni kutishia watu kwamba wataunguzwa milele. Sasa, ukifa unaacha mwili wako hapa, wanasema una roho, roho ni Nini, hoo mawazo sijui pumzi, ukiuliza unajua kazi ya ubongo ni Nini mtu hajui, haya tufanye roho ni ka upepo kanaenda motoni ehe kanaunguaje, hakana nyama, hakana nervous system hakana ngozi, hakana pain receptors, hakana ubongo au spinal cord, maumivu unayasikiaje, na bado hatujauliza huu Moto upo wapi, walisemaga chini kisa mavolcano lakini now hawasemi Tena coz of elimu.

Tukienda kwenye sheria zenyewe sijui usivae nguo tofauti, usile shellfish, usichanganye mazao, usimwage nje, usiabudu sanamu lakini abudu kitu Cha kufikiriwa na myahudi, hivi kwa Nini mtu atengeneze nyota billion 60 na sayari trillion afu aje kujali binadamu wewe ambae ni Kama vumbi kwa huu ulimwengu unamwaga wapi. Na kwa Nini sheria hizi zinaonekana Kama sheria za kabila ya la zamani huko kwenye majangwa na haziendani na sheria za binadamu kuishi na watu vizuri. Na Wanavyosema tumuabudu siku ya Saba.

Siku zimekuja kutengenezewa baadae Sana na zimebadilika badilika Mara kwa Mara katika historia ya Mayans na Romans. Na wamechagua sun day coz ni siku ya pagans kuabudu jua. Ila yote haya tuyaache, why Mungu muweza yote anataka hela, mwisho wa siku wote mnabidi mgundue kuwa binadamu walitengeneza miungu ili kujibu maswali magumu yasiyojibika kipindi kile na ku
Mi najua Mungu yupo, ila kwa hizi hoja zako nasimama na wewe
 
Usitake kuonekana mwelevu kufanya kufuru ili ufurahishe watu au kikundi fulani nakushauri usijitafutie laana kwa haya maandiko yako maana hasira ya Mungu ni kali sana tubu jiepusha na hizi kauli (acha kumfanyia kazi shetani kupotosha kondoo wa Mungu ) usipo sikia ipo siku na saa utakumbuka maandishi haya
Mungu ana hasira na kijiumbe ambacho ni kama kipunje cha vumbi ukilinganisha na matrilioni ya magalax.wazungu na waarabu kweli walituona maboya
 
Ujuaji mwingi braza.
Hivyo vitabu vya shule vilivyo andika una uhakika hao ndio wamiliki halali wa concepts na precepts hizo ndani ya hivyo vitabu.
Vitabu unavyoviona uandishi wake hauna tofauti mana uandishi mmoja vyanzo vya taarifa tofauti... Hujaliona hilo ?
Lakini ukinunua gazeti ukisoma si unalielewa bila mtafsiri. Lakini unahitaji mtafsiri akusomee Biblia. Acheni uoga Biblia sio neno la Mungu ni neno la walimtunga Mungu ndo maana kila kukicha utaskia dhehebu linatokea kwa sababu ni kitabu Kama Malaya kinatafsiriwa kivyovyote vile coz hakijaandikwa vizuri.
 
systems za dunia zilivo zinaonyesha kuwa yupo architect mkuu(mungu) , jua inachomoza inatua in perfect order, the air , life zote hizi ni ishara ya kuwepo kwake mungu,sihitaji mwarabu au myahudi kunidhihirishia bali ni imani yangu
Huyo Mungu nae si perfect katengenezwa na nani?
 
Mungu ana hasira na kijiumbe ambacho ni kama kipunje cha vumbi ukilinganisha na matrilioni ya magalax.wazungu na waarabu kweli walituona maboya
Shida dini zinamweka binadamu kwanza tafkiri ulimwengu ni wake...tuliukuta na tuuacha na ulimwengu utaendelea kuwepo. Kama viumbe vinatoweka sembuse sisi.
 
Back
Top Bottom