Muonekano mzuri wa Stendi mpya ya Mbezi umeharibiwa na Siasa zetu za kutafuta sifa kwa Wanyonge waliobatizwa Masikini

Muonekano mzuri wa Stendi mpya ya Mbezi umeharibiwa na Siasa zetu za kutafuta sifa kwa Wanyonge waliobatizwa Masikini

Attachments

  • IMG_0098.jpg
    IMG_0098.jpg
    20.3 KB · Views: 1
Shida hapa ni kwamba serikali ikiwaondoa tu,

Vyama vya upinzani vitawatumia watu hawa kuomba kura watawaambia kuwa watawaruhusu kufanya watakalo kwenye stendi hiyo.

Kwahiyo mpaka tutakapo jifunza siasa zenye tija ndipo tutakapo pata tunachokitaka.
 
Labda miradi ya kinyesi, kama neno lenyewe kujiajiri limekushinda kuandika sembuse kujilipa 80k
Nilichelewa Kusoma hii post yako Ndugu. Nimecheka hadi Kuanguka katika Kiti changu. Kuna Watu (JF Members) hapa mna Majibu ya Shombo mno. Umenivunja Mbavu!!!
 
Umesema ujinga kwa sababu maeneo yote mawili yanahudumia wasafiri wenye mahitaji sawa ya safari yanayopatikana kwa Machinga na Mamalishe. Msafiri Msukuma kama wewe anasafiri toka Dar es Salaam madege ya Magufuli yapo Uwanja wa Ndege wa Kimataifa anakata tiketi yake, atanunua zawadi huyooo anatelemka Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Chato na zawadi alizonunua kwa Machinga. Mlugulu anakwenda kwao Mji kasoro Bahari kusalimia ndugu anakata Tiketi yake Magufuli Bus Stand huyooo na Hood Bus Service mpaka Moro Stand ya Kisasa iliyofunguliwa na Magufuli, anatelemka na zawadi alizonunua kwa Mamantilie. Kila kitu Magufuli hata ile Nyumba ya TANU Lumumba iliyofunguliwa karibuni!
Ficha ujinga wako
 
Inabidi hata wapiga debe waruhusiwe kuingia ndani na pembezoni mwa Hiyo stand maana ndio shughuli yao inayowaingizia kipato. Wasafiri wataibiwa kwa Sana.
 
Inabidi hata wapiga debe waruhusiwe kuingia ndani na pembezoni mwa Hiyo stand,maana ndo shughuli yao inayowaingizia kipato.Wasafiri wataibiwa kwa Sana.
Kupiga Debe ni Ajira rasmi nchini Tanzania? Kuibiwa kwa Wasafiri hapo Stendi ndiyo Fursa ya Kiuchumi ( Kimaisha ) kwa Wanyonge waliobatizwa Masikini hapo Stendi Mpya Mbezi? Kuna Vitu Vinakera mno na havivumiliki kama kweli Kichwani mwako kuna Akili za Kutosha na Uwerevu usio na Shaka.
 
Ofsi sio sehemu inafanyika biashara

Stend ni sehemu ya watu kufanya biashara, ni haki ya kila mtu kufanya biashara, stend ni ya Watanzania wote maskini na tajiri, kama unaona huo ni uchafuzi na unakuboa, Jenga stend yako ama boresha nyumbani kwako pakuvutie ili uvinjali zaidi
Sitendi sio sehemu ya biashara..ni sehemu ya usafiri. Hebu tusichanganye mada hapa..kule ni sehemu pekee ya kupata usafiri..kuuza na kununua ni MADUKANI na sio standi..nani aliye tuloga? Nani kasema msafiri lazima anunue kitu standi....mbona uwanja wa ndege hatununui wala kula kwa mama lishe??
 
Kama hakuna utaratibu hao wamachinga wanaingiaje stand?
Au kwako utaratibu ni kuona wamachinga hawaruhusiwi kuingia stand🤔🤔🤔🤔
Wanaingia bila utaratibu na kufanya biashara bila utaratibu. Unajua kidogo Mipango miji? Hakuna anayewachukia, tunachukia pale utaalamu umapozidiwa na wanasiasa. Hivi pale Congo kkoo kituo cha basi kimevamiwa na machinga hakuna tena pakrking ya daladala, njia za watembea kwa miguu kkoo ni majiko ta supu, na mamalishe, msongamano usiokuwa na sababu wakati tuna watu wa mipango miji, maafisa biashara n.k si AIBU hii.
 
Mnataka mbaki wachache wenye biashara hapo mtukandamize na bei zenu acha wanyonge wanaosafiri wahudumiwe na wanyonge wenzao
 
Ona haoo acha niwaweke na ushahidi hao wazee wa kuzungumzia mambo bila kujua uhalisia wowote
mama D

Ova
View attachment 1715371
Shauri yenu..mtaishia hadi kuuziwa mayai vinza ndo akili labda zitawarudia . hahahahaaaa.. jamani kila kitu ni bora kiwe ' terms and conditions' otherwise itakuwa vurugu tu..na ustaarabu na mipangilio makini na sheria kufuatwa ndo maendeleo yatakuwepo.
 
Zamani mtu akikuita mnyonge, ni tusi, ila awamu hii imelifanya kuwa ni sifa!!na ZUZU kuitwa mnyonge anajisikia rahaaa!!!
Si afadhali hata neno mnyonge kidogo lina heshima. Mtu anaitwa masikini..mlala hoi anashangilia na kupiga makofi. Jamani ni Upogo gani huu?? Mmesahau maneno matakatifu ya Mungu yakisema ...."Mungu hafanyi maagizo na Masikini?" Sasa vipi wanasiasa wanawaita masiki na mnashangilia...?? Wanyonge ..amina bwana..amakweli tumekuwa matutusa..sikamakwamba nawatusi..lahasha..mwajitusi wenyewe.
 
Back
Top Bottom