MUONGOZO: Mambo ya kuzingatia unaponunua gari lililotumika ndani ya Tanzania

MUONGOZO: Mambo ya kuzingatia unaponunua gari lililotumika ndani ya Tanzania

Kuna mdau fulani anahusika sana na magari aliniambia kama unataka gari ya kununua hapa bongo bora ununue kwa wahindi au waarabu wa kkoo. Wale jamaa wanatunza sana magari yao halafu pia hayapati dhoruba sana kama haya mengine. Utakuta gari inazunguka hapohapo kkoo au posta na upanga.

Na pia hao jamaa wanauza gari nzuri sana kwa bei chee kwasababu wanataka kuleta nyingine mpya zaidi.
Upate connection zao vizuri. Wengi wao huwa wanawapa kazi madereva wao ya kuuza na mwisho wa siku madereva wanawatonywa madalali au wenyewe wanakuwa madalali. Hii kitu huwa inaboa sana.....

Mimi madalali huwa siwapendi hata kidogo.
 
Watu wengi huwa kuagiza gari ni zoezi zito sababu ya uoga wa zile procedures, paperworks na pia associated costs za kuagiza..... But ukitazama kuagiza kunakupa guarantee ya kupata gari unayohitaji na kukupunguzia changamoto zinazohusiana na ulaghai wa baadhi ya wauza magari.
 
Katika hizo, namba 8 na 10 zimenikuna. Unakuta mtu ana nunua gari namba C limechoka vibaya! Kwa wanaojua gari, body na Engine na Gear Box ni vitu vya msingi sana. Unakuta gari ni namba C lakini body limetoboka hadi unajiuliza kulikoni.

Watanzania wanapaswa kuelewa kwamba zile namba B,C, na D kwa sasa ni herufi tu na ni kiashiria kuwa gari limeingia nchini limekuta mfululizo gani wa namba( number Serie) lakini haina maana upya wa gari!
Kwa kuongezea tu. Kuna gari zimeingizwa ila usajiri zinatumia wa gari ambazo zimeshasajiriwa ila hazipo barabarani tena. Aidha kwa ajari au changamoto zinginezo.
 
Nahitaji Vitz New Model Number D au C zile za cc 990 Anayeuza au Anayemfahamu muuzaji tafadhali nijulishe ASAP kupitia pm
 
Habari wakuu,

Naombeni ushauri wenu. Nimejichanga nimefanikiwa kufikisha 5M sasa nimeona ni wakati muafaka na mimi nimiliki chombo cha usafiri.Je, aina gani ya gari inafaa haswa kwa kijana anayeanza maisha?

Mambo gani ya kuzingatia wakati wa kununua gari second hand hapahapa Bongo (Hususan hapa Dar es salaam).Kwa budget hiyo naweza kupata hitaji langu?

Mambo gani ya kuepuka katika mchakato mzima ili kuepuka kununua gari lisilofaa?
 
Kwangu Mimi nakushauri upate gari kama IST,RUNX ,RAUM au VITZ hapo kidogo utapata angalau furaha
 
Hongera Mkuu,Ndiyo Faida Kubwa Za Nchi Kufikia Uchumi Wa Kati, Pesa Tele. Gari Utakayoipata Hakikisha Isiwe Mbovu Ili Ufurahie Maisha
 
Be blessed.

Binafsi ninapenda wenye kuelimisha umma.

Mungu akupe maisha yenye mafanikio zaidi ili uzidi kuwa msaada kwa wanyonge
 
Naomba kufahamu vitu unavyotakiwa kuangalia pale unaponunua gari kwa mtu.

Nmesikia unatakiwa uende TRA, TRA unatakiwa ukafanye nini, pia kuhusu umiliki unabadilishaje.

Na vitu gani mhimu unatakiwa kuvibadili ili uwe mmiliki halali.

na pia naomba kufahamu, mwenye uzoefu vitz new model na passo afadhali kidogo ni nzuri maana nipo dolo nataka nijitupe kwa kati ya hizo mbili, namaanisha utumiaji wa mafuta na kuhimili mateso
 
Naomba kufahamu vitu unavyotakiwa kuangalia pale unaponunua gari kwa mtu.

Nmesikia unatakiwa uende TRA, TRA unatakiwa ukafanye nini, pia kuhusu umiliki unabadilishaje.

Na vitu gani mhimu unatakiwa kuvibadili ili uwe mmiliki halali.

na pia naomba kufahamu, mwenye uzoefu vitz new model na passo afadhali kidogo ni nzuri maana nipo dolo nataka nijitupe kwa kati ya hizo mbili, namaanisha utumiaji wa mafuta na kuhimili mateso
 
Back
Top Bottom