Mcheza Piano
JF-Expert Member
- Mar 2, 2024
- 562
- 1,339
Achana na porojo za vikundi vinavyo hongwa na watu wenye nia mbaya ili kumhujumu ndugu Murtaza Mangungu (genius wa msimbazi), leo nataka kukumegea siri makini sana.
Ni hivi, ndugu Murtaza Mangungu ni kiongozi makini anayesimamia katiba na sheria ndiyomaana mpaka sasa hajajiingiza kwenye sarakasi za hovyo zinazo endelea pale msimbazi.
Amesema wazi kuwa hawezi kujiuzulu bila kujua kosa lake maana yupo pale kwa matakwa ya katiba ya Simba sio kwa matakwa ya ma popoma kama GENTAMYCINE .
Pili amesema kuwa yuko tayari kutoa fedha zake mfukoni na kupitisha bakuli kwa mashabiki, wapenzi na wanachama wa Simba ili kufanya usajili makini kwaajili ya msimu ujao.
Kwa maneno mengine, Murtaza hataki kulamba viatu vya mwekezaji kisa tu mwekezaji ana fedha. Murtaza anajua kuwa mwekezaji anapata faida na kama hayuko tayari kutumia sehemu ya faida yake kufanya usajili basi asepe watakuja wawekezaji wengine.
Hakika Murtaza ndiyo tumaini letu pekee na yeye ndiye anayeshikilia maslahi ya timu yetu na amesimama imara kuzuia uporaji wa hii timu unaotaka kufanywa na wahuni.
Ikumbukwe kuwa huyu anayetaka kuipora timu yetu, anatuhumiwa kupora mashamba ya serikali kwa kujifanya kuwa mwekezaji anayetaka kuendeleza mashamba hayo baada ya kupewa ametumia hati zake kuchukua mikopo ambayo ameitumia kwa maslahi yake binafsi na serikali imempa muda kutoa maelezo yaliyo nyooka kabla hajashushiwa rungu zito.
Murtaza analifahamu vyema hili sakata na anataka kutusaidia wanasimba kuzuia ujangili kama huu kufanyika pale simba.
Hongera sana Murtaza, kwasasa utatukanwa na kudhihakiwa na mashabiki maandazi, ila mwakani hao hao watakuja hapa kukumwagia sifa. Tafadhali kaza buti, shikilia hapo hapo.
Ni hivi, ndugu Murtaza Mangungu ni kiongozi makini anayesimamia katiba na sheria ndiyomaana mpaka sasa hajajiingiza kwenye sarakasi za hovyo zinazo endelea pale msimbazi.
Amesema wazi kuwa hawezi kujiuzulu bila kujua kosa lake maana yupo pale kwa matakwa ya katiba ya Simba sio kwa matakwa ya ma popoma kama GENTAMYCINE .
Pili amesema kuwa yuko tayari kutoa fedha zake mfukoni na kupitisha bakuli kwa mashabiki, wapenzi na wanachama wa Simba ili kufanya usajili makini kwaajili ya msimu ujao.
Kwa maneno mengine, Murtaza hataki kulamba viatu vya mwekezaji kisa tu mwekezaji ana fedha. Murtaza anajua kuwa mwekezaji anapata faida na kama hayuko tayari kutumia sehemu ya faida yake kufanya usajili basi asepe watakuja wawekezaji wengine.
Hakika Murtaza ndiyo tumaini letu pekee na yeye ndiye anayeshikilia maslahi ya timu yetu na amesimama imara kuzuia uporaji wa hii timu unaotaka kufanywa na wahuni.
Ikumbukwe kuwa huyu anayetaka kuipora timu yetu, anatuhumiwa kupora mashamba ya serikali kwa kujifanya kuwa mwekezaji anayetaka kuendeleza mashamba hayo baada ya kupewa ametumia hati zake kuchukua mikopo ambayo ameitumia kwa maslahi yake binafsi na serikali imempa muda kutoa maelezo yaliyo nyooka kabla hajashushiwa rungu zito.
Murtaza analifahamu vyema hili sakata na anataka kutusaidia wanasimba kuzuia ujangili kama huu kufanyika pale simba.
Hongera sana Murtaza, kwasasa utatukanwa na kudhihakiwa na mashabiki maandazi, ila mwakani hao hao watakuja hapa kukumwagia sifa. Tafadhali kaza buti, shikilia hapo hapo.