Pancras Suday
JF-Expert Member
- Jun 24, 2011
- 8,141
- 3,838
Kwa mtazamo wangu watanzania tunahitaji muungano wa serikali moja, yaani Zanzibar na bara zote zikubali kusurrender autonomy zake kwa serikali na nchi moja tu ya Tanzania. Nionavyo mimi, serikali mbili ama tatu zitaturudisha kulekule kwenye matatizo ambayo tunapaswa kuyakimbia tena kwa speed ya 250km/h.
Serikali mbili zitaendeleza migogoro na mivutano ileile ambayo tulishaichoka.
Serikali tatu ndo balaa, yaani muundo huu ni sawa na mwanaume aliyeshindwa ndoa ya wake wawili kisha akaamua kuongeza mke mwingine. Kiukweli muundo huu utatugharimu. Kiusalama kwa mfano, nchi washirika wakigoma kuziwezesha wizara zenye dhamana ya usalama nchi imekwisha!, marais wa nchi washirika wakiamua kuuhujumu muungano ni rahisi sana kwenye serikali tatu. Inshort miungano ya serikali mbili au tatu haifai!
Kama ni hivyo basi, dawa ni muungano wa serikali moja. Faida yake kubwa ni kwamba itaimarisha utaifa wetu haijawahi tokea. Pili itaondoa malalamiko ya kila upande wa muungano kuona unakandamizwa na upande mwingine. Kubwa zaidi itatuongezea nguvu mbele ya maadui kwani "umoja ni nguvu"
Sisi watanganyika tupo tayari hata serikali moja ila sasa upande wa pili ndo balaa lilipo, ndo maana kwa sasa tunataka serikali tatu ili mmoja akisusa muungano tunautupilia mbali, muungano ni kama koti tu, likikubana unalivua!
Kwa mtazamo wangu watanzania tunahitaji muungano wa serikali moja, yaani Zanzibar na bara zote zikubali kusurrender autonomy zake kwa serikali na nchi moja tu ya Tanzania. Nionavyo mimi, serikali mbili ama tatu zitaturudisha kulekule kwenye matatizo ambayo tunapaswa kuyakimbia tena kwa speed ya 250km/h.
Serikali mbili zitaendeleza migogoro na mivutano ileile ambayo tulishaichoka.
Serikali tatu ndo balaa, yaani muundo huu ni sawa na mwanaume aliyeshindwa ndoa ya wake wawili kisha akaamua kuongeza mke mwingine. Kiukweli muundo huu utatugharimu. Kiusalama kwa mfano, nchi washirika wakigoma kuziwezesha wizara zenye dhamana ya usalama nchi imekwisha!, marais wa nchi washirika wakiamua kuuhujumu muungano ni rahisi sana kwenye serikali tatu. Inshort miungano ya serikali mbili au tatu haifai!
Kama ni hivyo basi, dawa ni muungano wa serikali moja. Faida yake kubwa ni kwamba itaimarisha utaifa wetu haijawahi tokea. Pili itaondoa malalamiko ya kila upande wa muungano kuona unakandamizwa na upande mwingine. Kubwa zaidi itatuongezea nguvu mbele ya maadui kwani "umoja ni nguvu"
Kiukweli hayo yoote, 2, 3 ni uzushi tuu, Binafsi napeda kon NCHI MOJA SERIKALI MOJA!
Kwa mtazamo wangu watanzania tunahitaji muungano wa serikali moja, yaani Zanzibar na bara zote zikubali kusurrender autonomy zake kwa serikali na nchi moja tu ya Tanzania. Nionavyo mimi, serikali mbili ama tatu zitaturudisha kulekule kwenye matatizo ambayo tunapaswa kuyakimbia tena kwa speed ya 250km/h.
Serikali mbili zitaendeleza migogoro na mivutano ileile ambayo tulishaichoka.
Serikali tatu ndo balaa, yaani muundo huu ni sawa na mwanaume aliyeshindwa ndoa ya wake wawili kisha akaamua kuongeza mke mwingine. Kiukweli muundo huu utatugharimu. Kiusalama kwa mfano, nchi washirika wakigoma kuziwezesha wizara zenye dhamana ya usalama nchi imekwisha!, marais wa nchi washirika wakiamua kuuhujumu muungano ni rahisi sana kwenye serikali tatu. Inshort miungano ya serikali mbili au tatu haifai!
Kama ni hivyo basi, dawa ni muungano wa serikali moja. Faida yake kubwa ni kwamba itaimarisha utaifa wetu haijawahi tokea. Pili itaondoa malalamiko ya kila upande wa muungano kuona unakandamizwa na upande mwingine. Kubwa zaidi itatuongezea nguvu mbele ya maadui kwani "umoja ni nguvu"
Kiukweli hayo yoote, 2, 3 ni uzushi tuu, Binafsi napeda kon NCHI MOJA SERIKALI MOJA!
Sijakuelewa ndugu! Nikiota niko na Profesor wa ccm maana yake nini? Nani huyo Profesa wa ccm?
Serikali tatu au nil hakuna moja wala mbili!
Nataka serikali moja ili znz iwe kama lindi kwa au serikali tatu ili tanganyika iwepo nadhani huo utakuwa muafaka kamili
Tusikubali kwenda serikali tatu. Kwa vile tumekatazwa kutaka kuvunja Muungano - japo waliotukataza hawana uwezo huo - na kwamba tunaweza kujadili "muundo" bora wa Muungano. Ninawasihi watu wa bara kudai "Serikali moja, taifa moja, na nchi moja". Haya mambo ya serikali mbili nchi mbili au serikali tatu nchi mbili hayaingii kichwani na ni jitihada za kujaribu kuibeba Zanzibar. Wakati umefika tudai uwepo wa serikali moja tu ya kitafa kwenye nchi moja.
Ninafahamu kabisa matokeo ya watu wa bara kutaka hili. Jambo pekee ambalo tusikubali kuuziwa (CCM na upiinzani wanataka hili) ni serikali tatu. Serikali tatu ni mzigo ambao hatuwezi kuubeba na wala hatupaswi kuubeba. Nawasihi wenzangu tukate kuongezewa mizigo. Tuwe na serikali moja, taifa moja na nchi moja. Sasa kama hili lina maana Zanzibar iwe "serikali moja, taifa moja na nchi moja" na bara iwe "serikali moja, taifa moja na nchi moja" basi na iwe.
Tuwasaidie Zanzibar watoke kwenye Muungano kama hawataki serikali moja kwani mbili hawataki na tatu tutajipa mzigo zaidi!
SAY NO TO SERIKALI TATU!!
Iambie tume ya Warioba - hatutaki serikali tatu!!
Hawa ccm wavunje muungano basi ili watu tupumue na kuangalia mambo mengine ya maana kwenye nchi hii. Huu muungano ni wa ccm. Wengine tumeuchoka, hatuutaki, kwani hatuoni hata manufaa yake, wazanzibari pamoja na kubebwabebwa lakini wanauona kama kiini macho kwao.