Muundo wa Muungano: Tanganyika tunataka 'Serikali moja, nchi moja, taifa moja'!

Muundo wa Muungano: Tanganyika tunataka 'Serikali moja, nchi moja, taifa moja'!

Nonda,

..hoja yangu iko palepale. Je, wa-Tanganyika tumemezwa au hatujamezwa??

..i need a categoric yes or no, with some evidence please.

..je, Tanganyika hatujarudi kuwa koloni la Zanzibar??

..je wa-Zanzibar kutuingilia mpaka kwenye masuala yasiyohusu muungano si ukoloni wa namna fulani?

..ZNZ kutumia umeme toka Tanganyika na baadaye kukataa kulipa madeni siyo uporaji wa rasilimali za Tanganyika?
 
Nonda, Nguruvi3, Jasusi, Mwanakijiji, Kichuguu, zomba, takashi,

..kuhusu hizi tuhuma au shutuma za "kumezwa" na muungano.

..hivi kweli wa-Tanganyika hatujamezwa na huu muungano?

..manake sisi ndiyo tume-sacrifice utaifa wetu na kuchukua utaifa wa Tanzania.

..pia hatuna serikali yetu wenyewe, na zaidi ikitokea Raisi wa muungano akawa Mzanzibari, basi huwa na mamlaka ya kutuingilia mpaka ktk zile wizara zisizohusu muungano.

..pia imetokea, na siyo mara moja, kwa wa-Zanzibari kuteuliwa kuongoza wizara ambazo zinahusiana na masuala ya wa-Tanganyika. wakati huohuo sisi hatuna ruksa ya kuongoza wizara ktk serikali ya wa-Zanzibari.

..hivi wanaostahili kulalamika kwamba wamemezwa na muungano ni wa-Tanganyika au wa-Zanzibari??

JokaKuu,

Hapana shaka yeyote kuhusu Zanzibar kumezwa na Muungano na vile vile kumezwa na Tanganyika. Zanzibar iliyokuwa ya miaka 70s ,80s na 90s sio ya leo. Hujuma dhidi ya Zanzibar zanaendelea hadi hii leo, kiasi amacho kama ni mjusi kumezwa na nyoka, basi kilichobakia ni mkia tu.

Mambo yote muhimu ya ki-nchi yameingizwa katika Muungano ,ukiachilia mbali ya 11 ya awali ya mkataba wa Muungano. Wazanzibari wananyimwa haki zao za msingi na haki hizo kupewa watanganyika, ikiwemo kunyimwa vitambulisho vya Mzanzibari mkaazi. Tumeshuhudia watanganyika wakimiminwa Zanzibar wakati wa uchaguzi ili wakipigie kura chama tawala.

Kuondoshwa kwa Rais wa Zanzibar, kutoka nafasi ya u- makamo wa Rais wa JYM na kuwa waziri asiyekuwa na wizara maalumu. Kuvunjwa kwa idara ya Usalama wa taifa wa Zanzibar, na baadae kuingizwa katika Muungano. Kuvunjwa kwa Jeshi la Zanzibar (NYUKI) na silaha zote nzito kuhamishiwa Tanganyka.

Serikali ya Muungano imefanikiwa kuinyima mamlaka makubwa Zanzibar kaisi kwamba hata Rais wa Zanzibar akitoka nje ya nchi lazima apewe kibali kutoka kwa Bw, MEMBE. Kulazimishwa Zanzibar, kujitoa katika OIC. Kwa kifupi Zanzibar haina mamlaka ya ki-nchi pamoja na kwamba ina wizara zisizokua za Muungano. Baya zaidi ni pale ambapo Rais wa Zanzibar kuteuliwa na watanganyika Dodoma.

Haya yote yanafanywa kwa makusudi na ni mpango wa muda mrefu, lengo ni kuifuta Zanzibar. Wapo wanao amini kuwa Zanzibar ni sehemu ya Tanganyika ,kwahiyo wanayo haki ya kuendeleza hujuma dhidi ya Zanzibar mpaka pale malengo yao kufanikiwa.

Na sisi tunasema kuwa harakati za ukombozi zitaendelea mpaka kieleweke....Mimi naungana na wanaodai kuvunjwa kwa Muungano. Kwa sababu Muungano unaelekea kubaya ,janga la maafa ya kujitakia litaikumba TZ sio muda mrefu, tumuombe M Mungu asitufikishe huko.
 
takashi,

..lakini Tanganyika na sisi hatuna mamlaka yoyote yale. Kila mamlaka tuliyokuwa naye before yameporwa na muungano.

..heri yenu mnaye Raisi ambaye ni waziri asiye na wizara maalum. Sisi wa-Tanganyika hatuna Raisi kabisa. Yaani hatuna nchi, na utaifa wetu umefutiliwa mbali.

..nakumbuka miaka ya 60 Zanzibar iliilazimisha Tanganyika kufunga ubalozi wake na Ujerumani Magharibi. matokeo yake Tanganyika ikakosa fedha za misaada kwa miradi ya maendeleo.

..Tanganyika imevamiwa na wa-Zanzibari wanaokadiriwa kuwa 350,000. kumbuka mwaka 1964 ZNZ ilikuwa na watu 300,000. wakati huohuo wa-Tanganyika wamekuwa wakinyanyaswa na kubaguliwa mara wanapofika ZNZ.

..Vitendo vya kibaguzi na kikatili dhidi ya wa-Tanganyika vimekuwa vikiongezeka siku hadi siku huko ZNZ. Imekuwa jambo la kawaida kwa wa-ZNZ kuwaita wa-Tanganyika majina ya ajabu-ajabu kama machogo. Pia kumekuwa na ubaguzi wa kidini dhidi ya wa-Tanganyika ambao huitwa makafiri, pamoja na nyumba zao za ibada kuchomwa moto.

..Mwisho, wako wa-ZNZ wanaoamini kwamba Tanganyika ni mali ya ZNZ. Watu hao hukumbushia na kutaka kurudisha dola ya Sultani wa ZNZ iliyostawi kutokana na biashara ya watumwa na pembe za ndovu toka Tanganyika and beyond.
 
Mkuu Joka Kuu,
Niseme 'YES' Tumemezwa.

Tumemezwa kwasababu sisi tume sacrifice sana katika huu muuungano bila kuwa na faida.
Leo sitataja tume sacrifice nini, ninachoweza kusema nikuwa ushahidi unajitokeza.
ZNZ wamekuwa wanalalamika sana kuhusu ukoloni, uchumi na kuingiliwa kisiasa.
Wamekuwa wanataka ZNZ kama ya 1963 na wamedai kuvunja muungano.

Kwa muda wote huo Tanganyika walikuwa kimya ikaonekane kana kwamba madai hata ya uzushi ni kweli. Leo tunajua kuwa TRA hawachukui hata senti tano, tunajua kuwa ZMA hawalipi bili IMO n.k.

Kwa WZNZ hii ilikuwa ni fursa adimu sana ya kuvunja muungano. Guess what! Baada ya kusikia Watanganyika wakihoji wananufaika na nini na Baada ya Watanganyika kusema LET ZNZ GO! na baada ya hoja ya Watanganyika serikali moja, tatu hapana na shirikisho hakuna WZNZ wote wamegeuka na kukamata hoja za muungano wa Uswiss, Cuba na Claifronia
Serikali 3, mkataba n.k. Kutapa tapa huku ni ushahidi usio na kificho kuwa wametumeza na tukitoka wanabaki na gamba.

(Soma Raia mwema Ahmed Rajabu hataki tena kuvunja muungano anasema wananchi waulizwe aina ya muungano. Maalimu Seif anataka serikali 3, Jusa 3, Nonda 3, Baru baru 3, takashi mkataba n.k.)

Takashi, hoja zako mbona ni nyepesi sana! Umesema Tanganyika imewanyanyang'a jeshi! kinachowashinda kurudisha ni nini wakati mna bendera, wimbo wa taifa n.k. Lakini jiulize gharama za ulinzi na usalama wa ZNZ nani anabeba.
Katika bajeti ya bilioni 600 ZNZ haina hata senti tano ya ulinzi na usalama. Nani amemezwa ZNZ auTanganyika inayolipa bili?

Takashi umesema ZNZ imeporwa mambo yote muhimu, labda ufafanue ni yapi hayo! Mimi nadhani muhimu ni yale 11 ambayo ZNZ ina ubia usio na malipo.
Kila mara nimekuwa nakuuliza swali lifuatalo na nadhani huu ndio utakuwa mwisho kwasababu huwa unakimbia.

Katika mambo 11 ya muungano yaliyoongezwa hadi 32, nitajie moja tu linalomfaidisha Mtanganyika na kumnyonya Mzanzibar!

Kuondoshwa kwa Rais wa ZNZ kuwa makamu wa Rais kulizingatia mambo ya kikatiba. Mathalani, sheria ikisema kama ilivyokuwa ina maana kuwa ipo siku tungekuwa na Rais wa JMT Mzanzibar, Makamu wa Rais Mzanzibar achilia utitiri wa mawaziri waliopo sasa. Hawa wangekuwa 'Wataalamu viongozi'' waliotoka ugahibuni kuja kuitawala Tanganyika.
Hadi sasa wamejazwa katika bunge na serikali, ushahidi wa Tanganyika kutafunwa kama si kumezwa

Nasema kuitawala Tanganyika kwasababu ZNZ ina serikali yake, mathalani Waziri wa Afya wa JMT kwanini awe MZNZ wakati kuna wizara ya Afya kule.

Niseme ukweli kuwa hata hawa waliopo hawatakiwi kuwepo kwasababu hawana lolote linalowagusa.
Wabunge 50 wanafanya nini Dodoma? Wanamwakilisha nani katika bajeti ya kilimo wakati ZNZ ina wizara yake.

Hatuna sababu ya kufikiri zaidi suala lililopo mbele yetu:
1. Serikali moja ambayo ZNZ haitakubali na muungano utavunjika natural
2. Kuwatenga na kuweka vikwazo kama tulivyosikia wakihaha kuhusu vitambulisho bandarini.
3. Kuvunja muungano kwa staili ya UAMSHO

Serikali 3 au mkataba ni upuuzi maana hauna tija wala faida kwa Mtanganyika.
LET THEM GO !
 
Mimi naamini wazi kama Mtaunda muungano wa Serikali moja tu basi automatic Zanzibar lazima itajitoa na hivyo muungano kufa. Kwa waZnz hawatakubali kuwa mkoa ndani ya Serikali moja.

Lakin kwa upande wa Tanganyika kama Znz ikijitoa katika Muungano wenu lazima kuna haya yatawatokea.

Pitia link hii ya TTB Religion » Tanzania Tourist Board

Hapo utagundua lazima kutakuwa na kupokezana madaraka kwa dini kuu zilizotajwa na kubainishwa na Serikali ya JMTz. Kwani kwa sasa pengo hilo linafichwa na waZnz kwa upande wa dini moja.

Sasa sijui wa Tanganyika mnalionaje hilo ambalo sasa lipo dhwahiri shahir halina siri tena.
 
Mimi naamini wazi kama Mtaunda muungano wa Serikali moja tu basi automatic Zanzibar lazima itajitoa na hivyo muungano kufa. Kwa waZnz hawatakubali kuwa mkoa ndani ya Serikali moja.

Lakin kwa upande wa Tanganyika kama Znz ikijitoa katika Muungano wenu lazima kuna haya yatawatokea.
Pitia link hii ya TTB Religion » Tanzania Tourist Board
Hapo utagundua lazima kutakuwa na kupokezana madaraka kwa dini kuu zilizotajwa na kubainishwa na Serikali ya JMTz. Kwani kwa sasa pengo hilo linafichwa na waZnz kwa upande wa dini moja.
Sasa sijui wa Tanganyika mnalionaje hilo ambalo sasa lipo dhwahiri shahir halina siri tena.
Baru baru, kelele unazosikia si kelele za watu ni kelele za vikundi cha watu. Watanganyika wengi bado ni wamoja na wanaamini katika maisha ya kuvumiliana.

Nikupe mfano, tunasikia watu wa dini fulani iwayo wakisema 'sisi wakristo' au 'sisi waislam' tumeadhamria kadha wa kadha.Ukweli ni kuwa ni kundi linalojivika kofia fulani na kusema 'sisi'. Hivi mtu kama Mtikila au Sheikh Ponda waliwasiliana lini na dini zao na kupewa jukumu la usemaji?

Kama lipo tatizo dawa ni kulitafutia ufumbuzi si kulificha kwa kutumia maumivu na kelele za Wazanzibar.
By the way ni WZN hao hao wanaonyima wenzi wao fursa walizostahiki kupata. Huwezi kunishawishi kuwa akiondoka Hussein Mwinyi wizara ya afya hakuna mtu mwingine wa kaliba yake anayeweza kushika wadhifa huo. Wapo mamilioni ya Watanganyika na uwepo wa Huseein Mwinyi ni kuziba nafasi tu kama alivyoziba Nahodha na wengine wengi.

Hatuwezi kwenda mbele bila ya kuongelea matatizo yanayotukabili kwa kina na kutafuta ufumbuzi.

Huwezi kunishawishi tena ya kuwa tunapaswa kupiga ZNZ mabomu watakapotanganza kukataa muungano.
Hiari hiyo wanayo na yatakayotokana na wao kuondoka katika muungano ni matokeo tu kama yale ya WZNZ wanaotaka kuvunja muungano wakielewa wazi kuwa kuna WZNZ na Washirazi, kuna Wapemba na Watumbatu n.k.

Hoja yako ni kuwa lazima tuwe na waznz wajaze viti vya bunge, wajaze serikali, walipiwe gharama za maisha ili kusiwe na matatizo Tanganyika. Hii ni dhaifu sana, ya kwamba umebeba zigo la misumari kwa kuogopa kubeba furushi la pamba.

Labda uniambie endapo wznz ndio suluhisho, je tutakapokuwa na mkataba au serikali 3 suluhu hiyo itakuwepo?
Je WZNZ wakiamua kuvunja Tanganyika itafanya nini kwa hilo unalosema!

Hoja kubwa iliyopo mbele ni ninyi kushindwa kuvunja nuungano kwa woga, na ZNZ kutumia Tanganyika kama ngazi.
Tutawasadia safari hii:
1. Serikali 1 ambayo hamtaki
2. Vunja muungano.

Mkataba au serikali 3 hutataki kwasababu hazitatusadia kwa hilo unalosema au chochote.
Mumeshindwa kutetea uwepo wa mkataba au serikali 3 na hakuna sababu ya kuwa na kitu msichokijua mnakitaka kwa nini na kwasababu zipi na kiweje.
 
Mwisho, wako wa-ZNZ wanaoamini kwamba Tanganyika ni mali ya ZNZ. Watu hao hukumbushia na kutaka kurudisha dola ya Sultani wa ZNZ iliyostawi kutokana na biashara ya watumwa na pembe za ndovu toka Tanganyika and beyond.........
[/QUOTE]
JokaKuu,

Huu ulaghai ndio wanzanzibari wamechoka nao. Hatuwezi kuwa na Muungano ambao nyinyi (Tanganyika) muwe "partner" na hapo hapo muwe "master". Hapa hapatakuwa na haki. Lazima kuwe na Tanganyika ,Zanzibar na Muungano.

Ubaguzi ni kitu kibaya sana, ila hizi mbegu za Ubaguzi alizipanda Nyerere. Huwezi kuwanyima watu haki zao za msingi na kuwatawala ki-dikteta halafu utegemee mapenzi kutoka kwao.

Huwezi kuwanyima watu uhuru wa kujiunga na OIC halafu utegemee mapenzi kutoka kwao. Hakuna mzanzibari aliyezaliwa kuwachukia watanganyika. Watanganyika wenyewe kwa kiburi chao ndio wanatengeneza mazingira ya chuki baina ya raia.

Hakuna mzanzibari anaetaka kuitawala Tanganyika , bali ni kinyume chake. Mznz anataka aachiwe apumue...
 
Hakuna mzanzibari anaetaka kuitawala Tanganyika , bali ni kinyume chake. Mznz anataka aachiwe apumue....[/QUOTE]

Napendekeza kuwe na serikali moja au nchi mbili zilizo huru, huu ndio ukweli. We need them they dont need us tunawapotezea time, they need to plan their own thing we are obstacle they are targeting Diaspora connections. let them Go let us remain with oue Mwabepande's hangover.
 
@Takashi,

Hivi katika zama hizi Mzanzibari anaposema "ipigwapo zumari ZNZ hucheza walioko maziwa makuu," mtu huyo anakuwa na maana gani kama si kuzitukuza na kuzienzi zama zile za ukatili wa dola ya ZNZ dhidi ya weusi wa Tanganyika?

Hivi unafikiri Mzanzibari, na tena kiongozi kama Seif Sharrif Hamad anapoandika makala ndefu na kutoa nukuu hiyo, unafikiri Mtanganyika wa kawaida anasikia kitu gani hapo?

Nyerere hakupanda ubaguzi. If anything, Nyerere alitaka tuwe kitu kimoja, haki sawa kwa wote. Wenye ubaguzi ni wale walioamua kujitenga waking'ang'ania utaifa wao, na zaidi kuwaita ndugu zao majina ya ajabu-ajabu kama vichogo.

Nieleze ni lini umewasikia wa-Tanganyika wakiwadhihaki wa-ZNZ kutokana na maumbile yao. Sana sana m-ZNZ akifika huku Tanganyika ataitwa Mpemba, sawa na tunavyotambulishana kwa makabila yetu kama Wagogo, Wachaga, Wanyakyusa nk.

Hata sisi wa-Tanganyika tumechoka na ulaghai, tumechoka na unyonyaji, na zaidi tumechoka na UBAGUZI. Zile kampeni za Uamsho zilikuwa zikieneza uongo na ubaguzi wa kutisha. Kuna mikutano wananchi wanadai ukimwi, madawa ya kulevya, ukosefu wa ajira, popobawa, suruali midebwedo, vimesababishwa na wa-Tanganyika. Maneno hayo yanasemwa mbele ya Sheikh bila kurekebishwa au kukanushwa.


Siyo siri kwamba wa-ZNZ mnatutawala ktk muungano huu. Wazanzibari wanawakilishwa na wabunge wengi kulinganisha na sisi wa-Tanganyika. Wabunge wa ZNZ wanajadili bajeti na hoja zinazohusisha wizara zisizo za muungano.

Umeme unazalishwa Tanganyika lakini Mzanzibari anauziwa kwa bei ndogo kuliko wenye mali. Rejea sakata ya EWURA kupandisha bei ya umeme Tanganyika, na serikali kukubali ZNZ kugomea bei mpya.

Mwisho, naunga mkono kampeni ya LET ZANZIBAR GO!!!
 
JokaKuu,
Huu ulaghai ndio wanzanzibari wamechoka nao. Hatuwezi kuwa na Muungano ambao nyinyi (Tanganyika) muwe "partner" na hapo hapo muwe "master". Hapa hapatakuwa na haki. Lazima kuwe na Tanganyika ,Zanzibar na Muungano.
Huwezi kuwanyima watu haki zao za msingi na kuwatawala ki-dikteta halafu utegemee mapenzi kutoka kwao.

Huwezi kuwanyima watu uhuru wa kujiunga na OIC halafu utegemee mapenzi kutoka kwao.
Hakuna mzanzibari anaetaka kuitawala Tanganyika , bali ni kinyume chake. Mznz anataka aachiwe apumue..
We need them they dont need us tunawapotezea time, they need to plan their own thing we are obstacle
Takashi, Sina uhakika kama uliandika kitu ulichokusudia au uliamua kuandika kila neno lilipokuja kichwani.
Hapo mwanzo umesema, tunataka serikali ya Tanganyika, Zanzibar na Muungano. Ukimaanisha kuwa uwepo wa serikali 2 na ile ya muungano. Hadi hapo unataka muungano uwepo.

Kwenye aya hiyo hiyo ya kwanza umesema 'huwezi kuwanyima watu haki zao na kuwatawala kidikteta'
Aya ya pili unasema '' huwezi kuwanyima watu haki yao ya kujiunga na OIC'' na katika aya hiyo hiyo unasema ''Hakuna Mznz anayetaka kuitawala ZNZ bali kinyume chake'' ukimaanisha Tanganyika wanataka kuitawala ZNZ.

Aya ya tatu unasema 'we need them, they don't need us'' ukaongezea ''they need to plan their own thing we are the obstacles''.

Wakati aya ya kwanza ukisema kuwepo muungano aya zingine zinakataa uwepo wa muungano. Umeona jinsi ulivyojichanganya kwa kuanzia tu. Huwezi kutaka muungano wakati unalalamikia udikteta na kunyimwa haki.

Kwa vile umeeleza na kuonyesha wazi kuwa ZNZ inaonewa na kunyima haki zake basi ZNZ haihitaji kuwa na muungano ili ipate haki zake zote na ku-plan bila obstacles. Hilo litawezekana ZNZ ikijitoa katika muungano. Ni haki yao.

Usichokielewa kabisa ni kuwa ZNZ inatapa tapa, wamegoma kuvunja muungano na wanataka muungano tena kwa mbinu na nguvu. Wanataka muungano kupitia serikali 3 au mkataba. Wameshindwa kuandika mswada wa kuvunja muungano.

Maoni ya WZN kwenye tume wote wanataka muungano akiwemo Maalim Seif, Jusa na wachochezi wengine wenye hadhi kubwa sana ZNZ. Maana yake ni kuwa, ZNZ needs Tanganyika.

Kwa kutambua kuwa ZNZ inayimwa haki zake Watanganyika wamesema hivi;
Hawataki serikali 3
Hawataki mkataba

Tunawataka WZNZ nao waseme hivyo ili wapate ZNZ itakayojiunga na OIC kupata mikate, asali na maziwa bila bughudha.

Kama WZNZ hawatkubali kuvunja muungano, Watanganyika waliowabeba watauvunja;
1. Kudai serikali 1 ambayo ZNZ hawatakubali
2. Kukataa mkataba au serikali 3
3. Kuwatimua kwa kubana milango muhimu huku bara.

Ikishindikana basi ZNZ itabaki kuwa koloni na hapo watalazimika kutii amri kutoka Dodoma. Mna chaguo !
 
@Nguruvi3,

..wewe endelea kuwaelimisha hawa mabwana.

..unajua imefika wakati "kero za muungano" zimekuwa kama entitlement ya wa-ZNZ.

..its about time na sisi wa-Tanganyika tuwe na kero zetu.

..umeme unazalishwa Tanganyika, lakini tunaupata kwa bei kubwa kuliko wenzetu wa-ZNZ. katika mazingira hayo nani mkoloni, na nani mtawaliwa???
 
wabunge wa zanzibar inabidi waache kuja dodoma huu ni unyonyaji
 
Serikali moja, na ni sisi watanganyika ndiyo tunavyotaka. Kama wazanzibari hawataki serikali moja, basi waishie hukohuko. Sijui kwa nini hii mizee yetu inawabembeleza hawa wazanzibari, wana nini? Get'em out of our way, wanatujazia miinzi tu na misamaki yao.

Hahahaaa kwanza waondoke kwenye wizara zetu huku bara.
 
@Nguruvi3,

..wewe endelea kuwaelimisha hawa mabwana.

..unajua imefika wakati "kero za muungano" zimekuwa kama entitlement ya wa-ZNZ.

..its about time na sisi wa-Tanganyika tuwe na kero zetu.

..umeme unazalishwa Tanganyika, lakini tunaupata kwa bei kubwa kuliko wenzetu wa-ZNZ. katika mazingira hayo nani mkoloni, na nani mtawaliwa???
Mkuu Joka kuu, siyo tu bei rahisi bali pia hawalipi kabisaaa! hawajui bei ya umeme kama mwananchi wa Kidatu au Ruaha.

Siyo umeme tu hata bili kule IMO hawalipi, elimu ya juu hawalipi na hapo hapo wanapata 7% ya pato la taifa achilia mbali bilioni 32 za ofisi ya makmu wa Rais kupelekwa ZNZ bila sababu ya maana ili mradi tu kuwafurahisha.
Ifike mahali tuone jinsi tunavyonywa na hawa watu milioni 1 na tujiulize tunapata nini kutokana na investment hiyo.

Bandarini wamedai vitambulisho, believe me, WZNZ wanahaha na wameanza kusema mnafunga mpaka. Hiyo ni prelude,tunakwenda kwenye ajira na uwezekezaji sasa.

Kwa vile wameanzisha baraza lao la mitihani ni wakati vyuo vya elimu ya juu vitathmini kama viwango vinakidhi usajili katika vyuo vyetu. Hakuna sababu ya kumnyima mtoto wa Tanganyika haki kwa kisingizio cha nafasi maalumu za ZNZ ambazo hatujui kama zinakidhi viwango. Huu ni uonevu.

Mtoto wa Tanganyika afaidike na rasilimali za nchi yake, siyo anyimwe haki ili kumpendeza mzanzibar halafu baba wa Kitanganyika alipe kodi kumueleimisha mtoto asiye wa nchi hii.Huu ni uonevu

Saint Ivuga, wabunge hao wanalipwa kwa gharama za Mtanganyika kujadili yasiyowahusu.
In other word wamejaza viti na kulamba marupu rupu kwa kazi isiyowahusu. Huu ni uonevu
 
Mimi naamini wazi kama Mtaunda muungano wa Serikali moja tu basi automatic Zanzibar lazima itajitoa na hivyo muungano kufa. Kwa waZnz hawatakubali kuwa mkoa ndani ya Serikali moja.

Lakin kwa upande wa Tanganyika kama Znz ikijitoa katika Muungano wenu lazima kuna haya yatawatokea.

Pitia link hii ya TTB Religion » Tanzania Tourist Board

Hapo utagundua lazima kutakuwa na kupokezana madaraka kwa dini kuu zilizotajwa na kubainishwa na Serikali ya JMTz. Kwani kwa sasa pengo hilo linafichwa na waZnz kwa upande wa dini moja.

Sasa sijui wa Tanganyika mnalionaje hilo ambalo sasa lipo dhwahiri shahir halina siri tena.

Barubaru,

..nakumbuka kuna post ulisema wa-ZNZ mlikuwa mkiteuliwa kushika nyadhifa mbalimbali, huku wa-Tanganyika Waislamu wenye qualifications kubwa zaidi yenu wakiachwa kwenye mataa.

..majuzi hapa nimesoma ripoti ya Tundu Lissu ambapo kuna Jaji wa mahakama ya rufaa ameteuliwa toka ZNZ wakati hana vigezo vya kupewa nafasi hiyo. Yaani wameachwa Watanganyika kama Prof.Abdalah Safari ambao ni highly qualified badala yake ameteuliwa m-Zanzibar kihiyo, kisa muungano.

..pia kuna kikundi cha mashekhe toka ZNZ wanaoleta vurugu huku Tanganyika wakitumia gazeti za an-nuur na radio imaan, lakini hayo tuyaweke kando kwa leo.
 
Naunga mkono serikali moja tu.
Ama ya Tanzania,
Au ya Tanganyika, wengine wachape lapa.
 
Takashi, Sina uhakika kama uliandika kitu ulichokusudia au uliamua kuandika kila neno lilipokuja kichwani.
Hapo mwanzo umesema, tunataka serikali ya Tanganyika, Zanzibar na Muungano. Ukimaanisha kuwa uwepo wa serikali 2 na ile ya muungano. Hadi hapo unataka muungano uwepo.

Kwenye aya hiyo hiyo ya kwanza umesema 'huwezi kuwanyima watu haki zao na kuwatawala kidikteta'
Aya ya pili unasema '' huwezi kuwanyima watu haki yao ya kujiunga na OIC'' na katika aya hiyo hiyo unasema ''Hakuna Mznz anayetaka kuitawala ZNZ bali kinyume chake'' ukimaanisha Tanganyika wanataka kuitawala ZNZ.

Aya ya tatu unasema 'we need them, they don't need us'' ukaongezea ''they need to plan their own thing we are the obstacles''.

Wakati aya ya kwanza ukisema kuwepo muungano aya zingine zinakataa uwepo wa muungano. Umeona jinsi ulivyojichanganya kwa kuanzia tu. Huwezi kutaka muungano wakati unalalamikia udikteta na kunyimwa haki.

Kwa vile umeeleza na kuonyesha wazi kuwa ZNZ inaonewa na kunyima haki zake basi ZNZ haihitaji kuwa na muungano ili ipate haki zake zote na ku-plan bila obstacles. Hilo litawezekana ZNZ ikijitoa katika muungano. Ni haki yao.

Usichokielewa kabisa ni kuwa ZNZ inatapa tapa, wamegoma kuvunja muungano na wanataka muungano tena kwa mbinu na nguvu. Wanataka muungano kupitia serikali 3 au mkataba. Wameshindwa kuandika mswada wa kuvunja muungano.

Maoni ya WZN kwenye tume wote wanataka muungano akiwemo Maalim Seif, Jusa na wachochezi wengine wenye hadhi kubwa sana ZNZ. Maana yake ni kuwa, ZNZ needs Tanganyika.

Kwa kutambua kuwa ZNZ inayimwa haki zake Watanganyika wamesema hivi;
Hawataki serikali 3
Hawataki mkataba

Tunawataka WZNZ nao waseme hivyo ili wapate ZNZ itakayojiunga na OIC kupata mikate, asali na maziwa bila bughudha.

Kama WZNZ hawatkubali kuvunja muungano, Watanganyika waliowabeba watauvunja;
1. Kudai serikali 1 ambayo ZNZ hawatakubali
2. Kukataa mkataba au serikali 3
3. Kuwatimua kwa kubana milango muhimu huku bara.

Ikishindikana basi ZNZ itabaki kuwa koloni na hapo watalazimika kutii amri kutoka Dodoma. Mna chaguo !
Nguruvi3

Nadhani kumefanyika usanii au makosa katika ku-quote maneno yangu. Hiyo sentensi nyekundu sio maneno yangu .Nadhani kuna mchangiaji ali-quote maneno yangu lakini akachanganya na yake. (Kidzude)

Mimi msimamo wangu uko pale pale , SITAKI MUUNGANO NATAKA NI(TU)ACHIWE TUPUMUWE. Niliposema huwezi kuwa na Muungano ambao Tanganyika ,iwe partner na hapo hapo iwe Master. Hii ni kujaribu kuelezea moja ya sababu ambazo mtu kama mimi naukataa Muungano. Kutokuwepo kwa Tanganyika ni chanzo cha ulaghai na uwongo wa Muungano. Nia yenu sio Muungano bali ni utawala...(Ukoloni).

Kuna pesa zinagaiwa mitaani Zanzibar kwa mtu yeyote atakae toa maoni ya kukubali Muungano kama ulivyo kwa Tume ya Katiba.
Pesa hizi zimetoka Tanganyika , kwavile wemeshaona msimamo wa waznz ni tishio kwa Ukoloni wao. Sasa Bw,Nguruvi3, JokaKuu, Mkandara, MM kijiji n,k. Zuwieni rushwa hii ,MZNZ hanunuliwi tena kwa 5,000 Tsh.

Aibu aibu, wabunge wanatembeza bahasha za hela...Kweli hamjiamini.

Mimi naunga mkono harakati zenu za LET ZNZ GO ! ila ninacho waomba muwe na nia dhati.
 
Nguruvi3

Nadhani kumefanyika usanii au makosa katika ku-quote maneno yangu. Hiyo sentensi nyekundu sio maneno yangu .Nadhani kuna mchangiaji ali-quote maneno yangu lakini akachanganya na yake. (Kidzude)

Mimi msimamo wangu uko pale pale , SITAKI MUUNGANO NATAKA NI(TU)ACHIWE TUPUMUWE. Niliposema huwezi kuwa na Muungano ambao Tanganyika ,iwe partner na hapo hapo iwe Master. Hii ni kujaribu kuelezea moja ya sababu ambazo mtu kama mimi naukataa Muungano. Kutokuwepo kwa Tanganyika ni chanzo cha ulaghai na uwongo wa Muungano. Nia yenu sio Muungano bali ni utawala...(Ukoloni).

Kuna pesa zinagaiwa mitaani Zanzibar kwa mtu yeyote atakae toa maoni ya kukubali Muungano kama ulivyo kwa Tume ya Katiba.
Pesa hizi zimetoka Tanganyika , kwavile wemeshaona msimamo wa waznz ni tishio kwa Ukoloni wao. Sasa Bw,Nguruvi3, JokaKuu, Mkandara, MM kijiji n,k. Zuwieni rushwa hii ,MZNZ hanunuliwi tena kwa 5,000 Tsh.

Aibu aibu, wabunge wanatembeza bahasha za hela...Kweli hamjiamini.

Mimi naunga mkono harakati zenu za LET ZNZ GO ! ila ninacho waomba muwe na nia dhati.

Sioni kama hawa uliowataja hapa wanataka muungano uvunjike/uvunjwe.

Mimi nimeshajaribu kuonesha ni lazima tuirudishe serikali ya Tanganyika na jina Tanganyika kama hatua ya kumaliza mazingaombwe lakini kila wanapoandika wanasema "tuwasaidie wazanzibari wajitoe"

Rai niliyotoa mimi ni kuwa tutumie rai ya mwasisi wa Muungano ya kuunda EAF. Huko tupeleke timu mbili.Serikali ya Tanganyika kivyake na serikali ya Zanzibar kivyake. Hapo ni kuwa huu muungano wa kisanii unaisha na tunaanza na Muungano wa kikweli.

Hawa dugu zangu, wananiweka njia panda.wananiona mimi UAMSHO. Bila Tanganyika na serikali ya Tanganyika ni kuendelea na kiini macho halafu tunalalamika Tanganyika inapata hasara. Entity ambayo haipo inapata hasara vipi?

Hakuna kati ya hawa anayetaka serikali ya Tanganyika.

JokaKuu unasema Tanganyika imemezwa? Imemezwa na nani?
Kama jibu ni Muungano, Muungano ni baina ya nchi ipi na nchi ipi?

Ile ngao ya adam na hawa ni nembo ya serikali ipi? Ile katiba ya Muungano imepatikana vipi?

Mkuu Nguruvi3 anasema Tanganyika ni sleeping general....alalae usimwamshe....

Jamani watanganyika tuamke!
 
Nonda kama kuna 'entity' isiyokuwepo sasa ukoloni unatoka wapi? Utakuwaje koloni bila mkoloni na kwa hapa mkoloni ni nani?Kuhusu EAF hoja yetu ni kuvunja muungano kwanza ili kila mmoja aende kivyake. Hakuna serikali 3 au mkataba.

Takashi hao wanaogawa pesa ni Waznz kwasababu hakuna shoka lisilo na mpini. Kuna msukuma gani anaweza kuwasiliana na mznz kwa ubaguzi na dharau mlio nayo. Hivyo waulizeni wale 50 wanaokwenda kulala Dodoma, huenda wamepewa fungu.

Lakini si hata Gharibu bilali naye kapewa bilioni 32?
Maalimu Seif si anachukua pensheni hazina Dar? Karume, Mwinyi je.
Hivi unafikiri Hussein Mwinyi au Nahodha wanawaelewa!

Fikiria pia yule mznz anayeishi raha mstarehe Msasani,Ilala, Mabawa Tanga akisikia kuvunja muungano unadhani atafanya nini!

Juzi wameombwa vitambulisho, hamadi kila mtu analalama tunazuiwa sisi ni Wtanzania, nchi moja n.k.

Tuelimishe watu kuhusu LET ZNZ GO
 
Back
Top Bottom