Muundo wa Muungano: Tanganyika tunataka 'Serikali moja, nchi moja, taifa moja'!

Muundo wa Muungano: Tanganyika tunataka 'Serikali moja, nchi moja, taifa moja'!

Tutakuwa na mkoa wa pemba na mkuu wa Mkoa Maalim Sharif,
Mkoa wa Unguja na Mkuu wake Dr shein kama ilivoyo mkuu wa mkoa wa mbeya Kandoro.
 
Watanganyika wanaoishi ZNZ ni wangapi sheikh na wao kama wataamua kubaki huko hiayari yao, lakini sidhani kuwa wanafiki 1000.

Mimi nawaunga mkono UAMSHO na WZNZ wanapaswa kuwaunga mkono UAMSHO. Njia bora ya kuwaunga mkono ni kuacha kuongelea serikali 3 au mkataba. Hadi hapo kutakuwa hakuna chaguo ila kuvunja muungano.

. Kuna CUF na CCM, kuna Spika kuna mwanasheria mkuu, wana bendera na wimbo wa taifa, mahakama kuu. HakunKuhusu vyama vya siasa na usajili hilo si kweli kwasababu ZNZ ina BLWa mtu yoyote yule aliyejaribu kufikisha mswada wa kuvunja muungano kwa njia za kisheria kama walivyoleta mswada wa GNU au mabadiliko ya katiba.

Nani aliwazuia WZN Kuanzisha SUK au kubadili katiba yao? Jusa hajawahi kushtakiwa kwa kusema anachodhani ni sahihi.
Wazanzibar wanatumia mwanya tu kukwepa ukweli kuwa hawataki kuvunja muungano.

Ndiyo maana leo tunasikia serikali 3 au mkataba. Sasa kama hutaki muungano unataka serikali 3 au makataba wa nini.
Sisi Tanganyika tumeshaona hatuna manufaa na huu muungano na sasa hatutaki serikali 2, 3 au mkataba tunataka ZNZ iondoke zake kwa amani.

Tusaidieni basi ili tuvunje hili dudu kwa amani kwa kukaa kimya ili asijetokea mtu na kusema upo uwezekano ABC.


LET ZNZ GO!

Naona umesahau kama msajili wa vyama vya siasa ni Bw, TENDWA, sio BLW au spika KIFICHO. Chama cha siasa ili kisajiliwe lazima kiwe na wanachama waanzilishi kutoka Tngka na ZNZ. Ingelikuwa rahisi kama kusingekuwa na ulazima huo, ili znz wawe na vyama vyao bila kuhusisha wtngka.

Usisubiri kauli kutoka katika chama chochote kile cha siasa ya kuvunja Muungano. Halita tokea mpaka hapo katiba mpya ikiruhusu hivyo. Hata CHADEMA hawataki Muungano, ila kwa sasa hivi wanaishia serikali 3 au majimbo.

Vile vile sijakusikia kuwasakama CHADEMA kwa kutaka serikali 3 ila umekuwa ile hanagaiko la moyo"obsessed with Zanzibar" .
 
[SIZE=3 said:
MAMMAMIA;4255533]Hapo kwenye RED - Kuwakataza wananchi kujadili maslahi ya taifa lao ni KULAZIMISHANA na pia kung'ang'ania serikali tatu ni kulazimishana. Kwa nini kulazimishana huku? Kwa faida ya nani?
[/SIZE]
Kuna waliotoa rai ya kura ya maoni, matokeo yake yatakuwa kwa kasima gani - Tanzania Bara 50+1 na Zanzibar 50+1 iwe ndio uamuzi wa wengi juu ya kile watakachoamua au Tanzania yote wakiamua 50+1 iwe ndio imepita?

Kwa mtazamo wangu ni kuwa MUUNGANO UMESHAKUA KIROBA CHA MISUMARI, hakibebeki tena. Uamuzi wowote utakaoamuliwa sasa - iwe serikali 1,2,3...au kanda 7 au serikali 30 (yaani kila mkoa na serikali yake)...bado kero za Muungano zitazidi na hivyo kuzidi kutobebe
ka.

Kwa maoni yangu, suluhisho pekee la kutatua kero za Muungano ni kuvunja Muungano.


Mkuu nakupa big up uko juu ya mstari
 
In your dreams that will never happen hadi Vatican itapobadilika na kua mkoa pia u know what i mean
 
Tusikubali kwenda serikali tatu. Kwa vile tumekatazwa kutaka kuvunja Muungano - japo waliotukataza hawana uwezo huo - na kwamba tunaweza kujadili "muundo" bora wa Muungano. Ninawasihi watu wa bara kudai "Serikali moja, taifa moja, na nchi moja". Haya mambo ya serikali mbili nchi mbili au serikali tatu nchi mbili hayaingii kichwani na ni jitihada za kujaribu kuibeba Zanzibar. Wakati umefika tudai uwepo wa serikali moja tu ya kitafa kwenye nchi moja. labda yeye hana akili kwa sababu nionavyo mimi raisi wetu hana hata hadhi ya kuwa monitor wa darasa yeye aligombea uraisi kama zamu mbona hao washauri hawamshauri amwache mkewe bogus ni bogus tu.

Ninafahamu kabisa matokeo ya watu wa bara kutaka hili. Jambo pekee ambalo tusikubali kuuziwa (CCM na upiinzani wanataka hili) ni serikali tatu. Serikali tatu ni mzigo ambao hatuwezi kuubeba na wala hatupaswi kuubeba. Nawasihi wenzangu tukate kuongezewa mizigo. Tuwe na serikali moja, taifa moja na nchi moja. Sasa kama hili lina maana Zanzibar iwe "serikali moja, taifa moja na nchi moja" na bara iwe "serikali moja, taifa moja na nchi moja" basi na iwe.

Tuwasaidie Zanzibar watoke kwenye Muungano kama hawataki serikali moja kwani mbili hawataki na tatu tutajipa mzigo zaidi!

SAY NO TO SERIKALI TATU!!

Iambie tume ya Warioba - hatutaki serikali tatu!!
kwenye signature hapo kwanini hao washauri wasimshauri amwache mkewe, kwangu mimi kikwete aligombea urais kama zamu tu lakini hana hata hadhi ya kuwa monitor wa darasa,bogus ni bogus tu.wanatenganishwa mapacha nini vinchi hivi viwili vibovu.naunga mkono hoja asilimia mia.
 

Mkuu nakupa big up uko juu ya mstari
wamepata fursa ya kuujadili muungano kwa amani wanalazimisha matakwa yao we waache hakuna kitu kitakachodumu milele kwa kulazimishana.tatizo lao wanaamini katika jeshi na polisi na kwa uchache mahakama lakini naamini kwa dhati kabisa ipo siku watu wataudai kwa mapanga hawatojali bunduki wala singe we kaka subiri **** hawi **** milele na siku akishtuka anayejihisi mjanja hutafuta sehemu ya kujificha.na hii sio kwa muungano tu bali kwa yote ambayo wanayatekeleza kwa kuwakandamiza wengine.
 
Naona umesahau kama msajili wa vyama vya siasa ni Bw, TENDWA, sio BLW au spika KIFICHO. Chama cha siasa ili kisajiliwe lazima kiwe na wanachama waanzilishi kutoka Tngka na ZNZ. Ingelikuwa rahisi kama kusingekuwa na ulazima huo, ili znz wawe na vyama vyao bila kuhusisha wtngka.

Usisubiri kauli kutoka katika chama chochote kile cha siasa ya kuvunja Muungano. Halita tokea mpaka hapo katiba mpya ikiruhusu hivyo. Hata CHADEMA hawataki Muungano, ila kwa sasa hivi wanaishia serikali 3 au majimbo.

Vile vile sijakusikia kuwasakama CHADEMA kwa kutaka serikali 3 ila umekuwa ile hanagaiko la moyo"obsessed with Zanzibar" .
Takashi, nadhani kuna jambo umelielewa vibaya tena vibaya sana.
Msajili wa vyama vya siasa anasajili vyama na kusimamia taratibu za usajili.
Haongozi vyama au sera za vyama.

Chadema au CUF wakisema wanataka serikali 3 hakuna msajili atakayewaondolea usajili ili mradi tu hayo yawe maoni yao.
CCM wakisema serikali 2 hakuna msajili atakayeondoa usajili wa CCM.

CUF/CCM/CDM Bado wana haki ile ile ya kutoa maoni ya kuvunja muungano bila kuathirika kwa namna yoyote ile. Hapa ndipo unapokosea ukidhani kuwa kusema muungano uvunje ni sawa na uhaini. Hapo ndipo ulipojichanganya.

Maalimu Seif Sharif Hamad Mshirazi, jana amesema kuwa ZNZ iwe dola kamili na kiti chake. Hajavunja sheria yoyote kwasababu ametoa maoini yake kwa mujibu wa sheria. Ni kwa msingi huo chama cha CUF ambacho msimamo wake ni kuvunja muungano kina haki kabisa ya kutamka hivyo na wala si uhaini kama unavyodhani.

Jambo lingine ni pale unaposhindwa kuelewa kuwa ndani ya Bunge na kwenye BLW kuna vifungu vinaruhusu wabunge wapeleke hoja za vyama vyao au Hoja zao Binafsi. Zote zinajulikana kama hoja binafsi zikitoka nje ya utaratibu wa serikali.

Kulikuwa hakuna tatizo kwa Wawakilishi kupeleka mswada wa kuvunja muungano.
Raza na Wabunge wengine wakiwa ndani ya BLW walitamka kuwa muungano uvunjwe. Hawakuchukuliwa hatua ya aina yoyote ile kwasababu hawakuvunja sheria yoyote na ukweli ni kuwa walikuwa wanatekeleza wajibu wao.

Mwanasheria mkuu wa SMZ alisema muungano tunaopaswa kuwa nao ni ule wa Uswiss. Ingawa sijui huo wa Uswiss lakini nataka uelewe kuwa unapotaka muungano mwingine ni lazima uvunje huu kwanza. Mwanasheria hakuogopa kusema kwakuwa hakuvunja sheria yoyote ya serikali au usajili wa vyama.

Mswada wa kubadili katiba ya SMZ ulifanyika bila ushauriano na muungano. Mabadiliko hayo yanaathiri sana katiba ya muungano na Zanzibar waliweza kufanya wenyewe. Hawakuchukuliwa hatu na hawakuvunja sheria kwamujibu wao.

Kuanzishwa kwa serikali ya umoja wa kitaifa GNU kwa upande mmoja wa nchi inayoongozwa na msajili wa vyama vya siasa ilikuwa ni kukiuka wazi kwa sheria za usajili wa vyama. ZNZ ilifanya hivyo na haukuwa uhaini.

Kwa mifano hiyo hapo juu nadhani utakuwa umeelewa kuwa hakukuwa na kosa kwa bwana Jusa Ismaili kufikisha mswada wa kuvunja muungo Dodoma.

Hakukuwa na tatizo kwa Mohamed kufikisha mswada wa kuvunja muungano ndani ya BLW.
Hakukuwa na tatizo kwa mwanasheria wa SMZ ambaye hafungamani na vyama wala msajili wa vyama kuleta mswada wa kuvunja muungano.

Ni wazi kuwa Wazanzibar kwa hofu ya kuvunja muungano hawakuwa tayari. Hoja kubwa ya WZNZ si kuvunja muungano bali kuwa na serikali 3 au mkataba ili yale mambo magumu wayaweke katika ushirika huo kwa manufaa ya nchi yao.

Nimalizie kwa kusema kuwa hakukuwa na kikwazo cha aina yoyote kisheria, kijamii au kisiasa kwa Wazanzibar kuleta hoja ya kuvunja muungano! hakuna! na kinachoendelea sasa ni wao kutapa tapa kwa kutambua ukweli kuwa kuvunjika kwa muungano kutapeleka machungu makali sana kiuchumi na kisiasa visiwani.

Kwa kuelewa kuwa kuvunjika kwa muungano kutafunga njia zote za uchumi wa ZNZ na kwamba Tanganyika ambalo ni soko kubwa la biashara na ajira halitafikika.

Kwa kuelewa kuwa Tanganyika ndiyo nchi pekee Duniani iliyopokea Wazaznibar wengi kuliko taifa jingine bila kikwazo au masharti, na kwa kuelewa kuwa bajeti ya visiwani inategemea Tanganyika.

Kwa kuelewa kuwa mzigo wa elimu na ulinzi na usalama hautabebeka na wznz bila kuuza uhuru wao Uarabuni. Kwa kuelewa kuwa Waarabu wanaweza kununua kisiwa hicho na wakazi wake wakageuka vijakazi.

Hayo yanawatisha sana WZNZ, but guess what! it is too late. Matusi sasa basi LET ZNZ GO!
 
Nguruvi3,


Ahali yangu kuna mambo kidogo naona huafahamu ndio maana umeandika yote hapo juu. Kumbuka kuwa Tanzania ni nchi inayoendeshwa na kufuata Katiba yake. Ndani ya katiba zote mbili ile ya JMTz na ile ya Znz zimejipambanua wazi. Sasa ulipaswa kwanza kujua mamlaka ya Bunge la Muungano na Mamlaka ya Baraza la wawakilishi kwa mujibu wa Sharia zenu.

Naona nikusaidie kitu kidogo hapo kutoka kwenye Katiba yenu, hebu pitia kidogo Sheria namba 15 ibara ya 6 ya mwaka 1984 katika kifungu cha 4 cha katiba ya Muungano ya TZ uone utekelezaji wa mamlaka ya nchi.

Lakin pia si vibaya ukapitia na pia na Sheria ya 15 ibara ya 9 ya mwaka 1984 kifungu cha 34 cha Katiba ya Muungano wa Tz uone mamlaka ya JMTz.

Nafikiri kama utapitia vifungu hivyo nilivyobainisha hapo juu vya katiba yenu utakuwa umejiweka vizuri sana katika kujenga hoja zako pasipo kukindamana na sharia mama ya nchi yako.


 
In your dreams that will never happen hadi Vatican itapobadilika na kua mkoa pia u know what i mean
Wewe tena unakimbilia kuharibu hali ya hewa tena! una shida katika ubongo uende MIREMBE! Wenzako wanajadili kuukataa muungano nawe unakimbilia ROME!! psychiatric case!!
 
Tusikubali kwenda serikali tatu. Kwa vile tumekatazwa kutaka kuvunja Muungano - japo waliotukataza hawana uwezo huo - na kwamba tunaweza kujadili "muundo" bora wa Muungano. Ninawasihi watu wa bara kudai "Serikali moja, taifa moja, na nchi moja". Haya mambo ya serikali mbili nchi mbili au serikali tatu nchi mbili hayaingii kichwani na ni jitihada za kujaribu kuibeba Zanzibar. Wakati umefika tudai uwepo wa serikali moja tu ya kitafa kwenye nchi moja.

Ninafahamu kabisa matokeo ya watu wa bara kutaka hili. Jambo pekee ambalo tusikubali kuuziwa (CCM na upiinzani wanataka hili) ni serikali tatu. Serikali tatu ni mzigo ambao hatuwezi kuubeba na wala hatupaswi kuubeba. Nawasihi wenzangu tukate kuongezewa mizigo. Tuwe na serikali moja, taifa moja na nchi moja. Sasa kama hili lina maana Zanzibar iwe "serikali moja, taifa moja na nchi moja" na bara iwe "serikali moja, taifa moja na nchi moja" basi na iwe.

Tuwasaidie Zanzibar watoke kwenye Muungano kama hawataki serikali moja kwani mbili hawataki na tatu tutajipa mzigo zaidi!

SAY NO TO SERIKALI TATU!!

Iambie tume ya Warioba - hatutaki serikali tatu!!
Ukidai serikali moja ni sawa tu na kuuvunja Muungano, Nadhani unawatania wazanzibari.
 
Kumbuka mwaka jana December (9/December 2011) tulisherehekea miaka 50 ya uhuru wa Tanzania (for the majority of people and media, and me included) AND THAT WAS OFFICIAL! - 50TH ANNIVERSARY OF TANZANIA INDEPENDENCE (watu wachache walisherehekea miaka 50 ya uhuru wa Tanzania bara). Sikumsikia aliyesherehekea miaka 50 ya uhuru wa tanganyika.


Jiulize kwa nini tulisherehekea miaka 50 ya UHURU WA TANZANIA au UHURU WA TANZANIA BARA, wakati Tanzania iliasisiwa mwezi April mwaka 1964 kwa muungano wa mataifa huru mawili - Hiyo miaka 50 ilitokea wapi?. Kwa nini tusherekee Uhuru wa Tanzania nchi ambayo haikupata/haikuwahi kutawaliwa? Jibu ni rahisi, TANGANYIKA ndio TANZANIA ndio MUUNGANO, na SERIKALI YA TANGANYIKA ndio SERIKALI YA MUUNGANO. kwa mfano, Tanzania yajipanga kuiadabisha malawi kwa kadhia ya ziwa Nyasa, jee zanzibar inashirikishwa kwenye kadhia hiyo - hapana. Jee ni nini msimamo wa zanzibar juu ya hilo? utasikilizwa? TANGANYIKA NDIO TANZANIA. Na muungano si lolote zaidi ya ukoloni wa wa tanganyika kwa zanzibar. Tanganyika yaweza kuiingiza Tanzania kwevye vita, dhidi ya Amini, au Malawi (mungu apitishie mbali), zanzibar haiwezi jambo kama hilo. Haiwezi hata kujiunga na OIC hadi siku Tanganyika watapopenda.
Kwa hali hiyo basi Mfumo wa serikali moja hautakuwa na jengine zaidi ya kuitumbukiza/kuimeza/kuiyeyusha zanzibar katika Tanganyika. Tanganyika wont have nothing to lose. BASI IWE KWA CONSENT YAO wazanzibari.

Mkuu Jumaane,
Naona kuna mambo mengi unachanganya Mkuu wangu. Kuna makosa mengi yanafanywa na hawa Viongozi wa Serikali ya Muungano lakini Wanzanzibar wanayahusisha moja kwa moja mkakati wa Tanganyika (Nchi iliyokufa) dhidi ya Zanzibar hai. Swala la Tanzania kusheherekea miaka 50 ya uhuru mwaka jana tumelipigia kelele sana hata sisi Watanganyika. Tulitaka itambulike kama sherehe ya miaka 50 ya Uhuru wa Tanganyika. Bahati mbaya hawakutaka kutusikia na wakafanya kama walivyotaka!

Bahati nzuri au Mbaya makosa hayo yanafanywa huku baadhi ya Wazanzibari wakiwemo kwenye hiyo hiyo serikali ya Jamhuri ya Muungano. Hatukuwasikia Mawaziri na Manaibu mawaziri kutoka Zanzibar wakipinga dhana ya miaka 50 ya Uhuru wa Tanzania. Walikuwa kimya wakasheherekea vizuri kama vile kilichotokea ni sahihi.

Kwa hiyo ninachotaka kusema hapa ni kwamba kuna Makosa wanafanya ndugu zetu wachache (Wazanzibari na Watanganyika) kwa wanufaaa yao binafsi lakini tusiyahusishe na dhamira ya Watanganyika au Wazanzibari wote kwa ujumla wao.

Tatizo kubwa tulilonalo sasa hivi ni Serikali za Chama cha Mapinduzi (CCM) kutotaka kuwasikiliza Wanzibari na Watanganyika wajadili kama Muungano wana utaka au hawautaki! Wao wanatusemea sisi eti tunataka Muungano na Muungano tunaoutaka ni wa serikali mbili. Hawa ndio wanaotuchonganisha sisi Watanganyika na Wanzanzibari na hatimae inatafsiriwa na Wazanzibari kwamba ni dhamira ya Watanganyika!

Watu hao hao sasa hivi wameliingiza swala la Muungano kwenye Maoni ya Tume ya katiba ya Jamhuri ya Muungano lakini kimantiki ilipaswa Muungano ndio ujadiliwe kwanza katiba ifuate baadae. Na hili swala limesemwa sana si tu na Wazanzibari hata na baadhi ya Watanganyika kama Mimi.

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kilipambanua sana swala hili ndani na nje ya Bunge lakini kwa sababu ya uchache wao Bungeni walishindwa! Kwa hiyo ni wakati sasa Wanzanzibari na Watanganyika wakashtuka na kuona nani mbaya wao? Ni nani anawachonganisha hadi mmoja kati yao aonekane ni Mkoloni wa mwingine? Na ni nani anawachonganisha hadi mmoja kati yao aonekane anafaidi kuliko mwingine kwenye Mfumo wa Muungano huu? Ni swali la kujiuliza Mimi, Wewe na wengine. Tuendelee kujadiliana!

TUMBIRI (PhD, Hull University, Hull City - United Kingdom),

tumbiri@jamiiforums.com
 
Mwanakijiji si kweli kwamba serikali tatu ni ghali kuliko serikali 2 tuliyo nayo sasa,
Chadema wakichukua nchi kutakuwa na mawaziri wa muungano wasiozidi watano (ulinzi, mambo ya nje, fedha, nimesahau nyingine) Kwa hiyo utakapokuwa na mawaziri 12 na manaibu mawaziri ni 24 na 10 wa Tanganyika = 34. Sasa linganisha mawaziri tulio nao. Just an example kwa kuwa hoja yetu ni lazima serikali iwe ndogo.

Pili, ukipunguza wizara maana yake unapunguza watumishi waliojazwa ktk wizara hizo. Mabilioni yanaokolewa.
kama hukubaliani na mimi lete calculation hapa.

Mkuu Mikael P Aweda,
Usema kweli hata Mimi nakuheshimu sana kuliko hata wewe unavyomuheshimu Mzee Mwanakijiji. Kimsingi tunapozungumzia gharama za kuendesha serikali katika Mfumo wa serikali tatu tunamaanisha Jumla ya gharama (Aggregate Cost) za kuendesha serikali zote tatu. Ya Zanzibar, Tanganyika na ya Muungano. Hatuzungumzii gharama za Serikali ya Muungano pekee. Ingawa nami ni MCHADEMA kama wewe lakini naipinga sana hii sera yetu ya Serikali tatu kwa hoja hiyo hiyo kwamba inaongeza mzigo na gharama kwa wananchi.

Kwa nini nasema hivyo? Nasema hivyo kwa sababu hata Serikali ya Muungano tukisema iwe na Mawaziri Wawili bado kila nchi Tanganyika na Zanzibar itabidi ziwe na Wizara zao binafsi kushughulikia mambo ambayo siyo ya Muungano. Kama Afya siyo jambo la Muungano itabidi Tanganyika na Zanzibar kila nchi ianzishe ya Wizara yake. Kama Kilimo siyo jambo la Muungano the same itabidi Tanganyika na Zanzibar kila nchi ianzishe Wizara yake. The same itakavyokuwa kwa Maji, Nishati, Michezo, Maliasili nk. Na utaona kwamba the way Serikali ya Muungano itakavyokuwa na Wizara Chache ndivyo individual Ministries kwa kila nchi zitakavyoongezeka na hivyo kuongeza gharama kwa ujumla wake.

Lakini tukiwa na serikali moja maana yake ni kwamba hatutakuwa na haja ya kuwa na duplicate Ministries in both sides of Union. Tutakuwa na Wizara ya Moja ya Mambo ya Afya, Wizara moja ya Kilimo, Wizara moja ya Maji, Nishati, Michezo nk. Sasa sijui ni vipi gharama zitapungua ikiwa tutakuwa na serikali tatu contrary na serikali moja ikizingatiwa kwamba possibilities ya kupunguza na kumerge Wizara ipo hata kwa kuwa na Serikali moja.

Kimsingi hoja ya Serikali tatu inakuzwa sana na baadhi ya Wanasiasa kwa hofu ya kukosa vyeto katika Mfumo wa Serikali moja tu. After all tujiulize nini maana ya Muungano kama bado kila nchi ina serikali yake tofauti na ya Muungano? Huo utakuwa Muungano au ushirikiano baina ya nchi mbili kwenye maeneo waliyokubaliana? Kama kweli tunataka Muungano wa kweli utakaoendana na neno lenyewe Muungano ni busara tukawa na serikali moja tu. Kama hatutaafikiana kwa hilo sioni mantiki ya kuungana. Na kuna hatari kubwa sana katika Mfumo wa serikali tatu mnaopendekeza, Serikali ya Muungano kukosa mvuto kutoka kwa wananchi na heshima kutoka kwa serikali ndogo mbili zitakazokuwa pande zote mbili.

Serikali ndogo zitajiona ni Powerful kuliko ya Muungano wakati huo huo Serikali ya Muungano nayo itajiona Poweful than counterparts. Tunatarajia kutakuwa na misuguano ya hapa na pale ambayo sasa hivi misuguano hiyo wanaiita 'kero za Muungano'.

Cc: JokaKuu

TUMBIRI (PhD, HULL University - HULL City, UK),

tumbiri@jamiiforums.com
 
P. Aweda, kwanza huwezi kuwa na wizara tano tu za Muungano; na hata kama inawezekana utaoa kuwa wizara tano za Muungano zitakuwa ndio za muhimu zaidi na zenye gharama zaidi.
 
P. Aweda, kwanza huwezi kuwa na wizara tano tu za Muungano; na hata kama inawezekana utaoa kuwa wizara tano za Muungano zitakuwa ndio za muhimu zaidi na zenye gharama zaidi.
Samahani Mwanakijiji, Unaweza kunambia ni mzigo gani zaidi utawapata Bara kukiwa na serikali tatu?..
 
Mkuu Mikael P Aweda,
Lakini tukiwa na serikali moja maana yake ni kwamba hatutakuwa na haja ya kuwa na duplicate Ministries in both sides of Union. Tutakuwa na Wizara ya Moja ya Mambo ya Afya, Wizara moja ya Kilimo, Wizara moja ya Maji, Nishati, Michezo nk. Sasa sijui ni vipi gharama zitapungua ikiwa tutakuwa na serikali tatu contrary na serikali moja ikizingatiwa kwamba possibilities ya kupunguza na kumerge Wizara ipo hata kwa kuwa na Serikali moja.


Pitia hapa, bado unataka serikali moja?
Unataka kumeza sumu?

link https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...-moja-nchi-moja-taifa-moja-5.html#post4415616
 
Samahani Mwanakijiji, Unaweza kunambia ni mzigo gani zaidi utawapata Bara kukiwa na serikali tatu?..

Mkandara,

Kukiwa na serikali tatu maana yake ni kwamba kila nchi (Tanganyika na Zanzibar) zitapaswa kuchangia pato lao fulani kila mwaka kuiweka Serikali ya Muungano in Operation. Under One Government hakutakuwa na hicho kitu. Kwa hiyo huo mzigo hautakuwa tu kwa Wabara bali hata kwa Wazanzibari

Nakala: Mzee Mwanakijiji.

TUMBIRI (PhD, University of HULL - UK),

tumbiri@jamiiforums.com
 

Mkandara,

Kukiwa na serikali tatu maana yake ni kwamba kila nchi (Tanganyika na Zanzibar) zitapaswa kuchangia pato lao fulani kila mwaka kuiweka Serikali ya Muungano in Operation. Under One Government hakutakuwa na hicho kitu. Kwa hiyo huo mzigo hautakuwa tu kwa Wabara bali hata kwa Wazanzibari

Nakala: Mzee Mwanakijiji.

TUMBIRI (PhD, University of HULL - UK),

tumbiri@jamiiforums.com
Lakini Utaweza vipi kuwa na serikali Moja ikiwa mnajua hili haliwezi kukubaliwa na zanzibar amabo watakuwa wamemezwa haswa na serikal ya bara?..Mnafikiri kweli zanzibar inaweza kubali kuwa mkoa tu ktk Utaifa wa nchi yetu au hilo bunge litakuwa vipi maana ni nchi mbili zilizoungana kuunda Moja. Je ni 50/50 kutoka bara na visiwani, Uongozi wa kiutawala utakuwa vipi 50/50 au ule alioanzisha Nyerere wa rais akitoka bara makamu atoke visiwani, sijui uwwiano. jamani mnatazama vitu kwa picha gani haswa kushauri hata hii serikali moja ikiwa tumeshindwa ktk ushirika huu uliopo..

Mawazo ya serikali moja ni mawazo ya Ubinafsi zaidi na yasiyotakiwa hata kupendekezwa kwa sababu ndio kichochezi cha Ubaguzi huu uloanzishwa na Wazanzibar. Kama nilivyomwelewa Mwanakijiji, hoja hii ina maana tu ya kwamba kama Zanzibar wameanzisha cheche za moto, sasa na sisi bara tunaweka kuni kabisa halafu tuone nani atashindwa kukaa jikoni.

Swala la serikali tatu au moja halihusiani kabisa na cost isipokuwa ni malengo ya kufikia mkataba unaokubalika pande mbili na kusema kweli hakuna iwe serikali moja, mbili au tatu. Tatizo la Muungano hadi sasa ni mgao wa kula meza kuu ktk uongozi, kuna utata mkubwa juu ya maswala yanayohusu muungano na yale yasiyohusu Muungano kiasi kwamba marafiki wa Bara sio marafiki wa visiwani, mapenzi ya bara sio mapenzi ya visiwani hivyo hakuna NDOA hapa mkuu wangu tulale chumba kimoja ama viwili..Hii ni kulazimishana.

The only solution kati yetu na Zanzibar ni kuvunja ndoa hii. Zanzibar itatuletea hatari kubwa sana ya Ubaguzi wa KIDINI kwa madai ya kuwa wao wanabaguliwa kwa sababu ni waislaam na kusema kweli upo ukweli ndani yake tunapoitwa sisi makafir na bomba la mavi. hakuna mapenzi kati yetu na Zanzibar hivyo soluhisho ni - LET ZNZ go!..
 
Kuna swali halijibiwi na pro-serikali 3.
Hivi hiyo serikali ya tatu itashughulikia mambo gani? Tukipata jibu hapo tunaweza kuanza na hesabu, bila jibu unapataje hesabu za gharama za kuendesha kwa kuanzia tu.
 
Kuna swali halijibiwi na pro-serikali 3.
Hivi hiyo serikali ya tatu itashughulikia mambo gani? Tukipata jibu hapo tunaweza kuanza na hesabu, bila jibu unapataje hesabu za gharama za kuendesha kwa kuanzia tu.
Aaaah mkuu wangu, mimi ni pro serikali tatu pia ukiondoa hii ya kuvunja muungano kuliko hiyo serikali moja, lakini najua haiwezekani kutokana na kwamba Zanzibar hawatapenda hii kabisa. Serilkali tatu, kuna serikali za states ambayo zitakuwa mbili na hiyo ya Republic itakuwa na majukumu ktk maswala yote YATAKAYOKUWA YA MUUNGANO kama unavyoona serikali ya Obama au ya Cameron.

Tatizo ni kwamba Wazanzibar hawataki mambo yaliyomo ktk muungano yabakie ktk muungano. wanataka kuyaondoa zaidi mambo ya muungano ili tubakie na jushirika wa kijumuiya tu..wanataka uhuru kamili japokuwa sisi hatuna hata nchi. wanataka kuweka mikataba yao na nchi za nje pasipo kushauriana na rais wa nchi hasa akiwa mbara maana alipokuwa Mwinyi hakushauriana na yeyote na waliosna sawa tu. Kuwa na kiti UN, Kuchagua marafiki, mgao wa keki na ushiriki ktk maswala ya mikopo, misaada na kadhalika. Hivyo hatuwezi kuunda serikali tatu wala moja kutokana nakwmaba kero za Muungano ni kero za Wazanzibar.wakati kero ya Muungano kwa bara ni madai ya Wazanzibar yasiyokwisha..
 
Back
Top Bottom