Muundo wa Muungano: Tanganyika tunataka 'Serikali moja, nchi moja, taifa moja'!

Muundo wa Muungano: Tanganyika tunataka 'Serikali moja, nchi moja, taifa moja'!

Aaaah mkuu wangu, mimi ni pro serikali tatu pia ukiondoa hii ya kuvunja muungano kuliko hiyo serikali moja, lakini najua haiwezekani kutokana na kwamba Zanzibar hawatapenda hii kabisa. Serilkali tatu, kuna serikali za states ambayo zitakuwa mbili na hiyo ya Republic itakuwa na majukumu ktk maswala yote YATAKAYOKUWA YA MUUNGANO kama unavyoona serikali ya Obama au ya Cameron.

Tatizo ni kwamba Wazanzibar hawataki mambo yaliyomo ktk muungano yabakie ktk muungano. wanataka kuyaondoa zaidi mambo ya muungano ili tubakie na jushirika wa kijumuiya tu..wanataka uhuru kamili japokuwa sisi hatuna hata nchi. wanataka kuweka mikataba yao na nchi za nje pasipo kushauriana na rais wa nchi hasa akiwa mbara maana alipokuwa Mwinyi hakushauriana na yeyote na waliosna sawa tu. Kuwa na kiti UN, Kuchagua marafiki, mgao wa keki na ushiriki ktk maswala ya mikopo, misaada na kadhalika. Hivyo hatuwezi kuunda serikali tatu wala moja kutokana nakwmaba kero za Muungano ni kero za Wazanzibar.wakati kero ya Muungano kwa bara ni madai ya Wazanzibar yasiyokwisha..
Mkuu Mkandara umesema sawia.
Mimi sina tatizo na anayetaka serikali 3, mkataba, serikali 1 au 2 ili mradi tu mtu huyo anishawishi kwanza:
1. Kwanini tunahitaji muungano pande zote
2. Kwanini anapendekeza muundo alioupendekeza.

Kwa upande wangu mimi naamini kuwa MUUNGANO UVUNJWE.
Pamoja na kuwa mnazi wa Pana Africanism, nakiri wazi kuwa umajumuhi si kuunganisha mapenda ya ardhi, ni pamoja na utamaduni mila desturi na viwango vya elimu na ufahamu.

Tanzania bara wametoa sana kwa ZNZ kiasi kwamba ZNZ inadhani ni sehemu muhimu sana ya Tanzania.
Kitu gani ZNZ wametaka na kunywimwa?

Siamini kabisa katika serikali 3 kwasababu ZNZ ina ubinafsi sana.
Mfano tu,tume ya katiba wamepiga kelele iwe na wajumbe sawa, lini umewahi kusikia Mzanzibar akisema kwanini gharama za ulinzi na usalama ziwe sawa!

Imefika mahali hata bili zao wanaamua walipe au wasilipe, sasa serikali 3 au mkataba wataheshimu vipi bili zao?
Angalia, wanasema SUMATRA inawanyonya, lakini huko IMO Hawalipi Bili, ubinafsi, na chuki hawawezi kuviweka kando.

Hoja yangu ni kuwa tuwe na mkataba au serikali 3,Kwa vile znz ina ubinafsi na hairidhiki na ina kitu kinaitwa Narcissism, hawatavumilia formula ya aina yoyote ile itakayoleta uwiano wa mkataba au serikali 3.

Ni lazima tukubali kuwa Tanganyika haina Fao lolote kutoka ZNZ.
Ni WZNZ ndio wanahitaji huu muungano na ndio wenye hofu ya kifo cha muungano. Hoja zote za serikali 3 au mkataba ni Kutapa tapa tu kwa kuchelea kuwa wanaachwa mayatima na watatanunuliwa na Wawaekezaji wa Ki-Oman.Period

Labda tena nitupe swali jingine:
Mtanganyika anahitaji Mkataba au serikali 3 na ZNZ ili zimsaidieje?
Tanzania bara inaihitaji ZNZ kwa kitu gani, for what! Ili ipate nini
 
Serikali mbili tu sasa hivi ni mzigo mkubwa kwa nchi ambapo Kikwete ana mawaziri zaidi ya hamsini na Shein naye ana mawaziri zaidi ya 30 (sina uhakika), wabunge wa muungano zaidi ya 400 na wawakilishi zaidi ya 100 (sina uhakika). Mzigo huo uko mabegani mwa wananchi ambao wengi wao hawaathiriki na kuwepo kwa serikali moja, mbili, tatu, nne au hata serikali kumi. Inabidi katiba mpya iweke serikali moja tu na idadi ya mawaziri iwe inajulikana kwa mujibu wa KLatiba, siyo kila rais anaunda baraza la mawaziri kubwa kusudi kila rafiki yake apate nafasi kwenye baraza hilo.

Vyeo vya wakuu wa wilaya vifutwe halafu wakuu wa mikoa wapatikane kwa njia ya uchaguzi tu.

Makatibu wakuu wa wizara zote wasiteuliwe na rais ila waombe nafazi hizo na kupitia usaili wa wazi; nafasi ya katibu mkuu iwe ya mkataba wa miaka miwili au mitatu.
 
Lakini Utaweza vipi kuwa na serikali Moja ikiwa mnajua hili haliwezi kukubaliwa na zanzibar amabo watakuwa wamemezwa haswa na serikal ya bara?..Mnafikiri kweli zanzibar inaweza kubali kuwa mkoa tu ktk Utaifa wa nchi yetu au hilo bunge litakuwa vipi maana ni nchi mbili zilizoungana kuunda Moja. Je ni 50/50 kutoka bara na visiwani, Uongozi wa kiutawala utakuwa vipi 50/50 au ule alioanzisha Nyerere wa rais akitoka bara makamu atoke visiwani, sijui uwwiano. jamani mnatazama vitu kwa picha gani haswa kushauri hata hii serikali moja ikiwa tumeshindwa ktk ushirika huu uliopo..

Mawazo ya serikali moja ni mawazo ya Ubinafsi zaidi na yasiyotakiwa hata kupendekezwa kwa sababu ndio kichochezi cha Ubaguzi huu uloanzishwa na Wazanzibar. Kama nilivyomwelewa Mwanakijiji, hoja hii ina maana tu ya kwamba kama Zanzibar wameanzisha cheche za moto, sasa na sisi bara tunaweka kuni kabisa halafu tuone nani atashindwa kukaa jikoni.

Swala la serikali tatu au moja halihusiani kabisa na cost isipokuwa ni malengo ya kufikia mkataba unaokubalika pande mbili na kusema kweli hakuna iwe serikali moja, mbili au tatu. Tatizo la Muungano hadi sasa ni mgao wa kula meza kuu ktk uongozi, kuna utata mkubwa juu ya maswala yanayohusu muungano na yale yasiyohusu Muungano kiasi kwamba marafiki wa Bara sio marafiki wa visiwani, mapenzi ya bara sio mapenzi ya visiwani hivyo hakuna NDOA hapa mkuu wangu tulale chumba kimoja ama viwili..Hii ni kulazimishana.

The only solution kati yetu na Zanzibar ni kuvunja ndoa hii. Zanzibar itatuletea hatari kubwa sana ya Ubaguzi wa KIDINI kwa madai ya kuwa wao wanabaguliwa kwa sababu ni waislaam na kusema kweli upo ukweli ndani yake tunapoitwa sisi makafir na bomba la mavi. hakuna mapenzi kati yetu na Zanzibar hivyo soluhisho ni - LET ZNZ go!..

Mkuu Mkandara,
Hapa ndipo watu wengi mnachanganya madesa. Sawa Zanzibar haitaki Mfumo wa serikali moja lakini nia yetu ni kuiridhisha Zanzibar au kujiridhisha wadau wote wa Muungano juu ya Mfumo wanaoupenda? Alafu hii ishu ya kumezwa Zanzibar ni Propaganda tu ya wanazi wachache wanaohofia Mfumo wa serikali moja kuwatoa nje ya ulingo wa kisiasa. Kwani nikuulize kwenye Mfumo wa serikali moja Serikali ya Bara haitamezwa? Itaendelea kuwepo?

Tatu, ishu ya Uongozi wa kiutawala itamuliwa na wadau wote kama wakishakubaliana Mfumo wa Serikali moja. Kama wataamua iwe Rotation au otherwise hiyo siyo ishu.

Unasema mawazo ya serikali moja ni mawazo ya Ubinafsi zaidi na yasiyotakiwa hata kupendekezwa kwa sababu ndio kichochezi cha Ubaguzi huu uloanzishwa na Wazanzibar. Mi nakukatalia ndugu yangu. Nikuulize tu leo rafiki yako mmoja akija akikuambia tuchange pesa tununua kiwanja tujenge ghorofa tuishi pamoja alafu mwingine akakuambia kila mtu atafute pesa zake ajenge ghorofa lake kivyake. Ni wazo lipi ni la kiubinafsi? Kujenga nyumba moja pamoja au kujijengea nyumba kivyako vyako?

Pia unasema swala la serikali tatu au moja halihusiani kabisa na cost lakini kwa bahati mbaya umeshindwa kudemonstrate ni jinsi gani serikali tatu haitaleta impact in terms of Operation Cost.

Hata hivyo nakubaliana na wazo lako la kuvunja ndoa hii kati ya Tanganyika na Zanzibar maana kwa sasa tunalazimishana tu.

TUMBIRI (PhD, University of HULL - UK),

tumbiri@jamiiforums.com
 
Inabidi Katiba mpya iweke serikali moja tu na idadi ya mawaziri iwe inajulikana kwa mujibu wa Katiba, siyo kila rais anaunda baraza la mawaziri kubwa kusudi kila rafiki yake apate nafasi kwenye baraza hilo.
Kichuguu,
Kumbe na wewe umezolewa na hii Propaganda kwamba Mchakato wa Sasa wa Katiba Mpya unaweza amua Mfumo wa serikali tunaouhitaji? Ukweli ni kuwa mchakato wa sasa hauna Legal Authority ya kuamua aina ya Muungano tunaoutaka. Kama tunataka hivyo inabidi kwanza Muungano wa sasa uvunjwe ili Tanganyika irudi kwanza. Tanganyika ikisharudi iwaulize Wananchi wake kama wanautaka Muungano, na katika huo mchakato pia itawauliza kama watautaka Muungano watataka uwe wa aina gani? Wa Serikali moja, mbili, tatu, nne, tano nk. Then Wazanzibar nao wataulizwa the same kama Watanganyika walivyoulizwa.

Ikiwa katika kura zote mbili za maoni zitakazofanyika Tanganyika na Zanzibar zitaonyesha kwamba Wananchi wa pande zote wanataka Muungano na wote wamekubaliana uwe Mfumo fulani basi hapo tutakuwa na Muungano wa raha, amani na starehe. Hata hivyo ikiwa katika hizo kura za maoni, maoni yatatofautiana baina ya pande. Mfano labda Wazanzibar wanataka Mfumo wa Serikali tatu wakati Watanganyika wamependekeza Mfumo wa Serikali moja maana yake Muungano hautakuwepo kwa sababu tumetofautiana juu ya Mfumo wa serikali.

Then baada ya kukubaliana Mfumo wa Muungano ndipo itapaswa sasa iundwe Tume ya Kukusanya maoni ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Sasa kinachofanywa sasa hivi na Tume ya Mzee Sinde Warioba ni as if hizo Step hapo juu zimeshafanyika wakati kiukweli bado.

TUMBIRI (PhD, University of HULL - UK),

tumbiri@jamiiforums.com
 
Mkuu Mkandara,
Hapa ndipo watu wengi mnachanganya madesa. Sawa Zanzibar haitaki Mfumo wa serikali moja lakini nia yetu ni kuiridhisha Zanzibar au kujiridhisha wadau wote wa Muungano juu ya Mfumo wanaoupenda? Alafu hii ishu ya kumezwa Zanzibar ni Propaganda tu ya wanazi wachache wanaohofia Mfumo wa serikali moja kuwatoa nje ya ulingo wa kisiasa. Kwani nikuulize kwenye Mfumo wa serikali moja Serikali ya Bara haitamezwa? Itaendelea kuwepo?

Tatu, ishu ya Uongozi wa kiutawala itamuliwa na wadau wote kama wakishakubaliana Mfumo wa Serikali moja. Kama wataamua iwe Rotation au otherwise hiyo siyo ishu.

Unasema mawazo ya serikali moja ni mawazo ya Ubinafsi zaidi na yasiyotakiwa hata kupendekezwa kwa sababu ndio kichochezi cha Ubaguzi huu uloanzishwa na Wazanzibar. Mi nakukatalia ndugu yangu. Nikuulize tu leo rafiki yako mmoja akija akikuambia tuchange pesa tununua kiwanja tujenge ghorofa tuishi pamoja alafu mwingine akakuambia kila mtu atafute pesa zake ajenge ghorofa lake kivyake. Ni wazo lipi ni la kiubinafsi? Kujenga nyumba moja pamoja au kujijengea nyumba kivyako vyako?

Pia unasema swala la serikali tatu au moja halihusiani kabisa na cost lakini kwa bahati mbaya umeshindwa kudemonstrate ni jinsi gani serikali tatu haitaleta impact in terms of Operation Cost.

Hata hivyo nakubaliana na wazo lako la kuvunja ndoa hii kati ya Tanganyika na Zanzibar maana kwa sasa tunalazimishana tu.

TUMBIRI (PhD, University of HULL - UK),

tumbiri@jamiiforums.com
Kwanza nitakujibu swali lako la Ubinafsi ktk kujenga Nyumba. Mtu yeyote anayetaka mimi tuchange fedha ili tununue nyumba wakati najua fika yeye ndiye atafaidika zaidi ktk nyumba hiyo kwa sababu ana watoto 40 wakati mimi nina watoto 2 anipe vyumba vitatu ilihali yeye atachukua vyumba 41.. Mbinafsi ni yule anayekazania kuchanga na kuishi nyumba moja ili kukidhi interest zake bila kujali kwamba miye pia nina mke na watoto nahitaji Uhuru fulani sio wa kupewa chumba cha kulala. UBinafsi sii kuishi pamoja bali ni ubinafsi ni pale mtu anapoweka interest zake mbele ya mtu mwingine. kama unataka utishi pamoja unaweza kuwa mbinafsi usipotaka kusikia mawazo ya mwenza.. Ubinafsi pamoja na kusema it's My way or the highway! - Hakuna mjadala.

Kuhusu swala la Operating cost, mkuu wangu lazima kwanza unielewe. nachosema mimi sababu ya kufikia maamuzi ya kuwa na nyumba moja, mbili au mbili katika uzio mmoja ni kutokana na kutoelewana kwetu. Swala la cost ni secondary maaa the prime thing ni kutafuta suluhu ya mahusiano kwa sababu kama ingekuwa rahisi tungejenga nyuma ya nyumba sita tu badala ya ghrofa. Minimum cost, choo ya kiswahili, kutumia mkaa na kadhalika ingetu gharimu kidogo zaidi ya kujenga ghorofa...
Ubishi wetu sio aina gani ya nyumba tunataka kuijenga bali ni mahusiano gani baina yetu yanayoweza kudumisha uhuru, haki na usawa wa wananchi wa pande mbili.

Sjui kama umewahi kuishi na watu as roommate, kuishi na hata ndugu mkiwa watu waizma mnaojitegemea kimaisha ukaona ugumu wake. Siku zote sisi miafrika tumeshindikana hata ndugu wawili hawawezi kuishi nyumba moja..lazima ugonvi utatokea na wengine urafiki huvunjika wanapoishi pamoja na sababu siku zote huwa ni mmoja wao kujifanya mtawala wa nyumba na mwenye mdomo mchafu wa kumsema mwenzake mchafu, haogi, haoshi vyombo na kadhalika japokuwa huyu mwenye mdomo anayasema haya kwa sababu ya kutazama interest zake na mambo gani yanamkwaza yeye..

Na mara zote ktk hali hii huwa hakuna salama baina yao isipokuwa kutengana ama huyu mmoja awe babu jinga kukubali matusi yote na wala kutoweka madai lakini akipiga mahesabu yake. Hapa hakuna Urafiki wala undugu mkuu wangu ni kuzidanganya nafsi..HIVI NDIVYO TULIVYO na tulivyokuwa muda wote wa muungano wetu japokuwa watu wengi wanachanganya sana kati ya MUUNGANO na JUMUIYA maana hii tulonayo sio ushirika amajumuiya ila ni NDOA baina ya nchi mbili hufungwa kwa mkataba na huachika kwa mkataba na sababu ya kuvunja ndoa..Unaweza kulivua koti ukisikia joto, lakini huwezi kulitupa koti maana utalihitaji siku nyingine ya baridi.

Ujenzi wa nyumba moja ulitushinda kwa sababu tuligawana vyumba, mamlaka na hata tuligawana hadi ujenzi wa msingi isipokuwa kushiriki pamoja ktk kufunika paa na kuta za ujenzi wa gate la kuingia wageni. Tatizo lipo kwenye finishing ya nyumba hii, Living room bara tumeweka furniture, Jikoni tumenunua vyombo hadi majiko tukisema ni ya bara japokuwa chakula tunakula wote. Zanzibar wanajitazama wanasema what do we own ndani ya nyumba hii?.. hawana kitu sasa imetokea kuna uwezekano wa wao kununua gari, bara tunasema hilo gari litakuwa letu sote maana tuna share kila kitu ndani, unakula, kupika na hata kunakalia makochi yangu na kadhalika.

Wazanzibar wenzetu wanataka nao wawe na chao, makochi yao, vuyombo vyao maana hii habari ya mali ni ya mnunuzi aloanza hawaikubali.. Tusiwachagulie marafiki wanaokuja watembeklea kwa sababu tu tuna shre nyumba wakati sisi hatutaki wageni ambao pengine wanaweza kuwa wezi ama wahuni wavuta Bangi wenye malengo ya kuchafua nyumba hii.

Hivyo hizi hitilafu zinazojitokeza ktk muungano wetu ndizo zinazo tuonyesha UBINAFSI wa mtu (nchi) maana tunatoka ktk kushare nyumba. Madai ya Zanzibar ktk mfano wako ni ndivyo Zanzibar wanafikiri ya kuwa tunashare nyumba tu..Wakati ukweli ni kwamba Muungano ni NDOA yetu sio uhsirikiano wa kushare au roomate.. Wanadai ktk nyumba hii wamepewa tu chumba lakini living room kuna TV ya MTanganyika, picha za ukoo wa Mtanganyika, furniture za Tanganyika hadi chooni kila kitu kinahesabuka ni cha Mtanganyika, Mzanzibar hana kitu ndani ya nyumba hii, kiasi kwamba hata akitaka kuleta mgeni wake ni lazima umuombe huyu Tanganyika ruksa!. Katika ndoa mali ya bwana ama mke ni mali ya mwenza pia, hili hawaliafiki kutokana na tabia ya bara kudai hizi ni mali zake sio za muungano wakati hakuna serikali ya bara - hapa kuna ukweli fulani.

Haya ndio madai ya zanzibar sasa wewe unapotaka ifikie hata kile chumba sio chake tena ni nyumba yetu wote ilihali Utaweka masharti ya kugawa kwa kutazama watoto wako. Wewe una watoto 40 mwenzako ana mmoja ama wawili, halafu unataka nyumba hii iwe yenu wote. Mkuu watoto 40 lazima watapunguza kipato cha huyu mtoto mmoja ambaye aliingiza mtaji ktk ujenzi wa nyumba hii..Na njia pekee inayoweza kutufaa ni kila mmoja wetu ajikate tu.

Aidha ni BORA sana kama mna uwezo kila mtu ajenge nyumba yake kivyake (Let Zanzibar Go) ama Ujamaa wa Kikafrika pale nyumba mbili za familia zinajenga ndani ya uzio mmoja - Ukienda kwa Mkandara (Tanzania) utakuta nyumba kadhaa za wazazi na watoto wakiishi na familia zao..(serikali tatu)
 
Kwanza nitakujibu swali lako la Ubinafsi ktk kujenga Nyumba. Mtu yeyote anayetaka mimi tuchange fedha ili tununue nyumba wakati najua fika yeye ndiye atafaidika zaidi ktk nyumba hiyo kwa sababu ana watoto 40 wakati mimi nina watoto 2 anipe vyumba vitatu ilihali yeye atachukua vyumba 41.. Mbinafsi ni yule anayekazania kuchanga na kuishi nyumba moja ili kukidhi interest zake bila kujali kwamba miye pia nina mke na watoto nahitaji Uhuru fulani sio wa kupewa chumba cha kulala. UBinafsi sii kuishi pamoja bali ni ubinafsi ni pale mtu anapoweka interest zake mbele ya mtu mwingine. kama unataka utishi pamoja unaweza kuwa mbinafsi usipotaka kusikia mawazo ya mwenza.. Ubinafsi pamoja na kusema it's My way or the highway! - Hakuna mjadala.

Kuhusu swala la Operating cost, mkuu wangu lazima kwanza unielewe. nachosema mimi sababu ya kufikia maamuzi ya kuwa na nyumba moja, mbili au mbili katika uzio mmoja ni kutokana na kutoelewana kwetu. Swala la cost ni secondary maaa the prime thing ni kutafuta suluhu ya mahusiano kwa sababu kama ingekuwa rahisi tungejenga nyuma ya nyumba sita tu badala ya ghrofa. Minimum cost, choo ya kiswahili, kutumia mkaa na kadhalika ingetu gharimu kidogo zaidi ya kujenga ghorofa...
Ubishi wetu sio aina gani ya nyumba tunataka kuijenga bali ni mahusiano gani baina yetu yanayoweza kudumisha uhuru, haki na usawa wa wananchi wa pande mbili.

Mkuu Mkandara,
Umejitahidi sana kujenga hoja ingawa ulilenga kuitetea Zanzibar na hoja yao ya Serikali tatu lakini umeishia kuitetea Tanganyika bila kujijua. Katika ubinafsi wa kujenga nyumba tukichukulia Tanganyika na Zanzibar kama Familia mbili ambazo zina contemplating on whether build and one house or each one to build his own house.

Katika mfano wako hakika Tanganyika ndiyo yenye watoto 40 huku Zanzibar ina watoto 2. Bahati mbaya umesahau kwamba wingi wa Watoto wa Kitanganyika siyo kwamba wote ni wategemezi hapana. Wengi ni vijana, wababa, wamama nk. Yani ni nguvu kazi. Kwa hiyo katika ujenzi wa hiyo nyumba moja haina maana kwamba Wazanzibar watatoa sawa na Tanganyika ili kukamilisha nyumba hiyo.

Mchango wa Tanganyika katika kujenga Tanzania ni mkubwa kuliko mchango wa Zanzibar. Chukulia tu makusanyo ya mapato ya Mkoa mmoja wa Tanganyika mfano Dar es Salaam na linganisha Jumla ya mapato ya nchi nzima ya Zanzibar, alafu uniambie. Bajeti ya nzima ya Zanzibar sijui hata kama inalingana na bajeti ya Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii ambayo kimsingi siyo ya Muungao. Ni wizara ya Tanganyika. Kwa hiyo linavyokuja swala la kugawana vyumba kwenye nyumba moja ni wazi kabisa Tanganyika itabidi ichukue vyumba vingi kwa sababu familia yake ni kubwa na imetoa mchango mkubwa kuliko Zanzibar katika kujenga hiyo nyumba.

Tanganyika haijapenda iwe na familia kubwa bali mwenyezi Mungu ndiye alieibariki iwe hivyo. It's a Nature. Ingekuwa ishu sana kama ungeniambia Zanzibar ina mapato sawa na Tanganyika huku Tanganyika ikiwa na familia kubwa kuliko familia ya Zanzibar – So hapa hakuna mjadala.

Kuhusu swala la Operating cost unasema sababu ya kufikia maamuzi ya kuwa na nyumba tatu katika uzio mmoja ni kutokana na kutoelewana kwetu lakini unashindwa kutambua kwamba kitakachotuwezesha kujenga na kumantain hizo nyumba ni pesa na siyo maelewano. Kwa hiyo siyo busara ku undermine swala la Operating cost katika kumantain hizo nyumba tatu. Maana nyumba inahitaji kufagiliwa kila asubuhi, ilipiwe bili za maji, ulinzi na umeme. Ikarabatiwe rangi na sakafu pale zinapochoka. Tusipo consider hiki kitu tunaweza kujikuta tunaanza kujenga nyumba ya tatu siku inafika kwenye linta wadau wanakwambia hawana pesa za kuchangia uendelezaji wa ujenzi wa hiyo nyumba. Na watakwambia wamebanwa na bajeti na hivyo vipaumbele vyao wamevielekeza kwenye nyumba zao binafsi.

Hata hivyo kuna para naona umeandika hoja ya msingi sana kwa kusema 'ubishi wetu sio aina gani ya nyumba tunataka kuijenga bali ni mahusiano gani baina yetu yanayoweza kudumisha uhuru, haki na usawa wa wananchi wa pande mbili'. Hili nakuunga mkono. Na kwa kukusaidia ni kwamba wenzetu kutoka Zanzibar wanataka mahusiano yao na Tanganyika yawe ya ujirani mwema tu kama ilivyo Kenya na Uganda au Rwanda na Burundi. Wanataka wajitoe, wajitegemee lakini wakubwa hawataki kusikia. Mimi kama Mtanganyika nawakubalia. Hata mimi napenda iwe hivyo.

Kimsingi mambo mengi umeonyesha msimamo kama wangu hivyo sijaona mahala pa kukukosoa. Tofauti yangu na wewe ni pale unapokuwa Pro-Serikali tatu badala ya Pro-Serikali moja.

TUMBIRI (PhD, University of HULL - UK),
tumbiri@jamiiforums.com
 
Mkuu Mkandara,
Umejitahidi sana kujenga hoja ingawa ulilenga kuitetea Zanzibar na hoja yao ya Serikali tatu lakini umeishia kuitetea Tanganyika bila kujijua. Katika ubinafsi wa kujenga nyumba tukichukulia Tanganyika na Zanzibar kama Familia mbili ambazo zina contemplating on whether to share and build one house or each one to build his own house. Katika mfano wako hakika Tanganyika ndiyo yenye watoto 40 huku Zanzibar ina watoto 2. Bahati mbaya umesahau kwamba wingi wa Watoto wa Kitanganyika siyo kwamba wote ni wategemezi hapana. Wengi ni vijana, wababa, wamama nk. Yani ni nguvu kazi. Kwa hiyo katika ujenzi wa hiyo nyumba moja haina maana kwamba Wazanzibar watatoa sawa na Tanganyika ili kukamilisha nyumba hiyo.

Mchango wa Tanganyika katika kujenga Tanzania ni mkubwa kuliko mchango wa Zanzibar. Chukulia tu makusanyo ya mapato ya Mkoa mmoja wa Tanganyika mfano Dar es Salaam na linganisha Jumla ya mapato ya nchi nzima ya Zanzibar, alafu uniambie. Bajeti ya nzima ya Zanzibar sijui hata kama inalingana na bajeti ya Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii ambayo kimsingi siyo ya Muungao. Ni wizara ya Tanganyika. Kwa hiyo linavyokuja swala la kugawana vyumba kwenye nyumba moja ni wazi kabisa Tanganyika itabidi ichukue vyumba vingi kwa sababu familia yake ni kubwa na imetoa mchango mkubwa kuliko Zanzibar katika kujenga hiyo nyumba.

Tanganyika haijapenda iwe na familia kubwa bali mwenyezi Mungu ndiye alieibariki iwe hivyo. It's a Nature. Ingekuwa ishu sana kama ungeniambia Zanzibar ina mapato sawa na Tanganyika huku Tanganyika ikiwa na familia kubwa kuliko familia ya Zanzibar – So hapa hakuna mjadala.

Kuhusu swala la Operating cost unasema sababu ya kufikia maamuzi ya kuwa na nyumba tatu katika uzio mmoja ni kutokana na kutoelewana kwetu lakini unashindwa kutambua kwamba kitakachotuwezesha kujenga na kumantain hizo nyumba ni pesa na siyo maelewano. Kwa hiyo siyo busara ku undermine swala la Operating cost katika kumantain hizo nyumba tatu. Maana nyumba inahitaji kufagiliwa kila asubuhi, ilipiwe bili za maji, ulinzi na umeme. Ikarabatiwe rangi na sakafu pale zinapochoka. Tusipo consider hiki kitu tunaweza kujikuta tunaanza kujenga nyumba ya tatu siku inafika kwenye linta wadau wanakwambia hawana pesa za kuchangia uendelezaji wa ujenzi wa hiyo nyumba. Na watakwambia wamebanwa na bajeti na hivyo vipaumbele vyao wamevielekeza kwenye nyumba zao binafsi.

Hata hivyo kuna para naona umeandika hoja ya msingi sana kwa kusema 'ubishi wetu sio aina gani ya nyumba tunataka kuijenga bali ni mahusiano gani baina yetu yanayoweza kudumisha uhuru, haki na usawa wa wananchi wa pande mbili'. Hili nakuunga mkono. Na kwa kukusaidia ni kwamba wenzetu kutoka Zanzibar wanataka mahusino yao na Tanganyika yawe ya ujirani mwema tu kama ilivyo Kenya na Uganda au Rwanda na Burundi. Wanataka wajitoe, wajitegemee lakini wakubwa hawataki kusikia. Mimi kama Mtanganyika nawakubalia. Hata mimi napenda iwe hivyo.

Kimsingi mambo mengine naona unamsimamo kama wangu hivyo sijaona mahala pa kukukosoa. Tofauti yangu na wewe ni pale unapokuwa Pro-Serikali tatu badala ya Pro-Serikali moja.

TUMBIRI (PhD, University of HULL - UK),
tumbiri@jamiiforums.com
Ahaaa mkuu wangu mbona siku zote nasema tuunde serikali tatu kwa sababu ya Bara!.. nimechoka na wazanzibar mbona siku nyingi sana na najua fika kwamba Zanzibar hawatakubali serikali tatu kama ilivyokuwa madai ya CUF ya zamani.. Hakuna wakati wowote hapa JF nimetetea madai ya Wazanzibar ktk swala la Muungano isipokuwa hutetea nafasi na uhalali wao kuwepo ktk muungano wetu. na nimesema sana waje hapa Canada watazame muungano wa British ambayo ni kubwa kama bara na Quebec ambayo ni ndogo na visiwa muhimu sana vya Wafaransa.

Haya ya kulazimishana hata ktk mila na desturi za watu kusema kweli sikubaliani nalo..hawana freedom ya kuchagua marafiki wala kujiunga na jumuiya isipokuwa kwa ruksa ya bara kutokana na serikali mbili au moja kuwabana zaidi. Hali hii itaondoka tu tukiwa na serikali tatu na watakuwa na uhuru wao kama ilivyo Quebec ktk maswala yanayowahusu kijimbo..haijalishi bara tunachangia kiasi gani maana hii ni NDOA hivyo huwezi kusema mume au mke ndio anaendesha familia...Kinachotakiwa ni kutazama mahitaji ya kila mmoja wetu na kuyatatua sio umeweka ngapi hivyo tugawane kwa nguvu ya uwekezaji. Zanzibar wanataka nyumba yao wao wenyewe kama urithi wao haya maswala ya kuchangia nyumba moja hawataki ni utumwa kwao hivyo wanaitaka talaka...

Mkuu wangu huwezi kupima hivyo ama umuhimu wa kuwa na Jeshi ama viwanda kwa kupima uzalishaji bali umuhimu wa kitu hicho ndio unatangulia..Mchango wa zanziba ni mdogo kutiokana na population, udogo wa nchi na yawezekana kuwa mkubwa zaidi kiasilimia ikiwa utapima mchango wao against their population na matumizi machache.


Haya madai ya kina Maalim Seif ama Jussa hata siku moja siyatetei japokuwa naelewa kuna mapungufu ktk nmfumo wa serikali mbili ambao hakuna kiongozi wa Zanzibar huyazungumzia..Hivyo kutokana na madia ya hawa wjainga ndio maana nasema serikali TATU kwa faida ya kurudisha identity ya serikali ya Tanganyika ama kujitenga kabisa tuwaache Wazanzibar japokuwa najua fika baada ya miaka mitano tu itakuwa Afghanstan ya Afrika na itabidi twende kuwaokoa ndugu zetu tena kama mapinduzi ya mwaka 1964..
 
Well said...serikali moja ni chaguo zuri,kwani mantiki ya kuwa na nchi moja inakuwepo,na gharama zake ni nafuu.
Wazanzibar wakihisi ni usumbufu,tutawasaidia waende salama.
 
Mkuu Mkandara,
Hapa ndipo watu wengi mnachanganya madesa. Sawa Zanzibar haitaki Mfumo wa serikali moja lakini nia yetu ni kuiridhisha Zanzibar au kujiridhisha wadau wote wa Muungano juu ya Mfumo wanaoupenda? Alafu hii ishu ya kumezwa Zanzibar ni Propaganda tu ya wanazi wachache wanaohofia Mfumo wa serikali moja kuwatoa nje ya ulingo wa kisiasa. Kwani nikuulize kwenye Mfumo wa serikali moja Serikali ya Bara haitamezwa? Itaendelea kuwepo?

Tatu, ishu ya Uongozi wa kiutawala itamuliwa na wadau wote kama wakishakubaliana Mfumo wa Serikali moja. Kama wataamua iwe Rotation au otherwise hiyo siyo ishu.

Unasema mawazo ya serikali moja ni mawazo ya Ubinafsi zaidi na yasiyotakiwa hata kupendekezwa kwa sababu ndio kichochezi cha Ubaguzi huu uloanzishwa na Wazanzibar. Mi nakukatalia ndugu yangu.
Nikuulize tu leo rafiki yako mmoja akija akikuambia tuchange pesa tununua kiwanja tujenge ghorofa tuishi pamoja alafu mwingine akakuambia kila mtu atafute pesa zake ajenge ghorofa lake kivyake. Ni wazo lipi ni la kiubinafsi? Kujenga nyumba moja pamoja au kujijengea nyumba kivyako vya

Pia unasema swala la serikali tatu au moja halihusiani kabisa na cost lakini kwa bahati mbaya umeshindwa kudemonstrate ni jinsi gani serikali tatu haitaleta impact in terms of Operation Cost.

Hata hivyo nakubaliana na wazo lako la kuvunja ndoa hii kati ya Tanganyika na Zanzibar maana kwa sasa tunalazimishana tu.

TUMBIRI (PhD, University of HULL - UK),

tumbiri@jamiiforums.com


Mkuu kama rafikiako atatoa pesa sawa na wewe na mukashirikiana kujenga basi itakua sawa hakuna ubinafsi. Lakini wewe unazo milioni arubaini halafu umwambie rafikiako mwenyemilioni moja muchanganye pesa mujenge basi huo ni ujanja na huenda ikawa unania ya kumzulumu kile kidogo chake na baadae utasema nyumba ni yako kwavile wewe ndie uliotoa nyingi.

Labda niongeze suali kwa watu kama Mwanakijiji!na Mkanda, ikiwa serekali tatu au mkataba hazinafaida na tanganyika labda mutueleze Tanganyika itafaidika na nini katika muungano wa serekali moja?
 
Mkuu kama rafikiako atatoa pesa sawa na wewe na mukashirikiana kujenga basi itakua sawa hakuna ubinafsi. Lakini wewe unazo milioni arubaini halafu umwambie rafikiako mwenyemilioni moja muchanganye pesa mujenge basi huo ni ujanja na huenda ikawa una nia ya kumzulumu kile kidogo chake na baadae utasema nyumba ni yako kwavile wewe ndie uliotoa nyingi.

Labda niongeze suali kwa watu kama Mwanakijiji!na Mkanda, ikiwa serekali tatu au mkataba hazinafaida na tanganyika labda mutueleze Tanganyika itafaidika na nini katika muungano wa serekali moja?

Mkuu hiyo nyumba niliyosema kujengwa haitajengwa kwa shuruti. Kama Wazanzibari wataona watadhuliwa kwa nini waingie kwenye Muungano? Hatuwalazimishi kwenye Muungano wa Serikali moja! Na sisi hatutaki watulazimishe kwenye Muungano wa serikali tatu. Kama inashindikana nimesema is better tuvunje Muungano. Kwa hiyo hoja ya Tanganyika kudhuru Zanzibar haina mashiko!

Hoja yako ya pili unauliza 'Tanganyika itafaidika na nini katika muungano wa serekali moja?'. Katika swala la serikali moja lengo si kufaidisha Tanganyika wala Zanzibar. Lengo ni kunufaisha Tanzania yote kwa ujumla. Tanganyika kama Tanganyika hatutakuwa na haja ya ku run our private government. The same to Zanzibar they will not incur cost to run their own independent government under one Union Government System.

TUMBIRI (PhD, University of HULL - UK),

tumbiri@jamiiforums.com
 
Nonda, Nguruvi3, Jasusi, Mwanakijiji, Kichuguu, zomba, takashi,

..kuhusu hizi tuhuma au shutuma za "kumezwa" na muungano.

..hivi kweli wa-Tanganyika hatujamezwa na huu muungano?

..manake sisi ndiyo tume-sacrifice utaifa wetu na kuchukua utaifa wa Tanzania.

..pia hatuna serikali yetu wenyewe, na zaidi ikitokea Raisi wa muungano akawa Mzanzibari, basi huwa na mamlaka ya kutuingilia mpaka ktk zile wizara zisizohusu muungano.

..pia imetokea, na siyo mara moja, kwa wa-Zanzibari kuteuliwa kuongoza wizara ambazo zinahusiana na masuala ya wa-Tanganyika. wakati huohuo sisi hatuna ruksa ya kuongoza wizara ktk serikali ya wa-Zanzibari.

..hivi wanaostahili kulalamika kwamba wamemezwa na muungano ni wa-Tanganyika au wa-Zanzibari??
 
Last edited by a moderator:
jokaKuu,
Mimi nadhani hii dhana ya kumezwa inatokana na ubaguzi. Tanzania bara ingekuwa ni nusu Waarabu, sidhani ungesikia malalamiko ya Wazanzibari. Lakini kwa sababu ya ubaguzi wao--rejea majina yao kuhusu muundo wa vichwa vyetu-- wanaona tumewapunguzia Uarabu wao na hence tumewameza. Ni ubaguzi tu.
 
jokaKuu,
Mimi nadhani hii dhana ya kumezwa inatokana na ubaguzi. Tanzania bara ingekuwa ni nusu Waarabu, sidhani ungesikia malalamiko ya Wazanzibari. Lakini kwa sababu ya ubaguzi wao--rejea majina yao kuhusu muundo wa vichwa vyetu-- wanaona tumewapunguzia Uarabu wao na hence tumewameza. Ni ubaguzi tu.
Hapana Jasusi, Wazanzibar mimi nawajua sana na wangetubafua hata kama tungekwua WaOman..Kumbuka historia yao ilitokana na Ubaguzi japokuwa wao utawaskia wakisema ati Muingereza ndiye aliyewalazimisha kuunda matabaka ya vyama.. Chama kinaandikishwa na Wazanzibar wenyewe na kujipa jina wao wenyewe wakijita Washiraz, Waafrika, Waarabu lakini lawama kapewa Muingereza.

Hawa hata mzazi akipoteza mimba basi lazima kuna mkono wa mtu..ndivyo walivyo mkuu wangu huwezi kumkuta Mpemba anajichanganya na Wangazija na kama utamwona basi labda kaoa/kaolewa kwa Wangazija..Yaani hata sijui nikwambie nini lakini of all Mpemba ndiye wa kumwogopa zaidi waunguja wanafuata tu mkumbo maana Mpemba ndiye Myahudi. JokaKuu mkuu wangu umelonga!
 
Last edited by a moderator:
Mwanakijiji si kweli kwamba serikali tatu ni ghali kuliko serikali 2 tuliyo nayo sasa,
Chadema wakichukua nchi kutakuwa na mawaziri wa muungano wasiozidi watano (ulinzi, mambo ya nje, fedha, nimesahau nyingine) Kwa hiyo utakapokuwa na mawaziri 12 na manaibu mawaziri ni 24 na 10 wa Tanganyika = 34. Sasa linganisha mawaziri tulio nao. Just an example kwa kuwa hoja yetu ni lazima serikali iwe ndogo.

Pili, ukipunguza wizara maana yake unapunguza watumishi waliojazwa ktk wizara hizo. Mabilioni yanaokolewa.

Tatu, ukifuta (ukimerge mkuu wa wilaya na meya/mkurugenzi + wakuu wa mikoa) maana lazima mmoja aondoke kati yao, maana yake ume serve mabilioni mengi sana pia.
Kwa hiyo, pamoja na heshima zote nilizo nazo kwako, sikubaliani na hoja ya gharama pamoja na kuwa iliwahi pia kutumiwa pia na mtu ninayemheshimu sana ktk nchi late Mwl Nyerere.
kama hukubaliani na mimi lete calculation hapa.

Naona watu wengi wanachanganya idadi ya mawaziri pekee siyo kipimo cha ukubwa wa serikali!!!. Ukubwa wa serikali unapimwa kwa vitu vifuatavyo je asilimia ngapi ya mapato yanatumika kulipa wafanyakazi na shughuli za kiserikali? na je ni asilimia ngapi zinatumiaka kulipa shughuli za maendeleo. Mfano serekali kumiliki biashara kama ATC na Tanesco ni ukubwa wa serikali kwani wafanyakazi hao pesa ya budget yake inatoka serikalini!!. Hivyo naona tubadilike na kufikiria kwa undani maana ya ukubwa wa serikali siyo idadi ya mawaziri pekee!!. Kwasasa serikali ni kubwa sana.
 
Naona watu wengi wanachanganya idadi ya mawaziri pekee siyo kipimo cha ukubwa wa serikali!!!. Ukubwa wa serikali unapimwa kwa vitu vifuatavyo je asilimia ngapi ya mapato yanatumika kulipa wafanyakazi na shughuli za kiserikali? na je ni asilimia ngapi zinatumiaka kulipa shughuli za maendeleo. Mfano serekali kumiliki biashara kama ATC na Tanesco ni ukubwa wa serikali kwani wafanyakazi hao pesa ya budget yake inatoka serikalini!!. Hivyo naona tubadilike na kufikiria kwa undani maana ya ukubwa wa serikali siyo idadi ya mawaziri pekee!!. Kwasasa serikali ni kubwa sana.
Kamundu,
Pia kuna suala jingine ambalo Aweda hajalizungumzia. Nani atakuwa kamanda in chief? Rais wa Tanganyika au rais wa serikali ya muungano? Zanzibar sasa hivi hawana national army, lakini tukiwa na rais wa Tanganyika, rais wa Zanzibar na rais wa muungano nani atakuwa na mamlaka juu ya jeshi letu? Nyerere was right.
 
Nonda, Nguruvi3, Jasusi, Mwanakijiji, Kichuguu, zomba, takashi,

..kuhusu hizi tuhuma au shutuma za "kumezwa" na muungano.

..hivi kweli wa-Tanganyika hatujamezwa na huu muungano?

..manake sisi ndiyo tume-sacrifice utaifa wetu na kuchukua utaifa wa Tanzania.

..pia hatuna serikali yetu wenyewe, na zaidi ikitokea Raisi wa muungano akawa Mzanzibari, basi huwa na mamlaka ya kutuingilia mpaka ktk zile wizara zisizohusu muungano.

..pia imetokea, na siyo mara moja, kwa wa-Zanzibari kuteuliwa kuongoza wizara ambazo zinahusiana na masuala ya wa-Tanganyika. wakati huohuo sisi hatuna ruksa ya kuongoza wizara ktk serikali ya wa-Zanzibari.

..hivi wanaostahili kulalamika kwamba wamemezwa na muungano ni wa-Tanganyika au wa-Zanzibari??
JokaKuu

Watanganyika tunajifanya tu kumezwa lakini wengi kati yetu tunaelewa ukiini macho/ usanii uliopo.

Tuhuma ni Zanzibar kumezwa na Tanganyika na sio muungano.

Hiyo ni kwa sababu, Muungano huu una wanachama wawili tu kwa miaka 48. Na kama alivyosema mwalimu.Mfumo wa muungano ungekuwa Shirikisho kama Kenya au Uganda wangekubali Kuungana na Tanganyika na Zanzibar.

Kuna siku niliandika mchango nikiwa "sober" kama mkuu Nguruvi3.
Mchango huu uko hapa.link https://www.jamiiforums.com/great-t...ni-na-kwa-manufaa-ya-nani-33.html#post1906050

Unayosema hapa ni kweli tupu na mimi naona ndio kiini macho chenyewe/mazingaombwe. je huo ni mkakati maalum kuwa Tanganyika ipate hasara sasa lakini ivune faida baada ya kupatikana serikali moja? Kama inavyodai eneo zaidi la bahari?

Je baada ya kupata serikali moja, tutakuwa tunatumia mfumo wa UK? Au ndio mfumo tunaoutumia sasa?

Kwa nini hatudai mfumo wa shirikisho?

JokaKuu, ingawaje umesema "utanganyika" ulipotea(kumezwa) au bunge la Tanganyika chini ya Mwalimu lilifuta serikali ya Tanganyika lakini sehemu iliyoitwa Tanganyika kulikuwa na umuhimu gani kulibadili na kuwa Tzbara au bara?

Halafu kama Tanganyika ilimezwa kwa nini yamekuwepo mambo ya Muungano na yasiyo ya muungano?(Wizara za masuala ya Tanganyika)

Nikichukulia huo mfano wa UK, England haina serikali yake lakini jina England lipo, wangeweza kufanya usanii kama wetu, kuita England, Britain bara au UK bara. Uk kuna utaifa mama mmoja, Britain/British na kuna utaifa wa nchi nyengine tatu/nne, English,Irish, Welsh na N.Irelanders

Hapa Tz upo utaifa mama mmoja,Utanzania na utaifa wa wabia( wabara)watanganyika, wazanzibari...utanganyika/ubara na uzanzibari
Ndani zipo nchi mbili Tanganyika na Zanzibar..nje ipo Tanzania.
Hapa utata unajitokeza mambo ambayo si ya muungano, Serikali ya Tanzania inayatoa wapi mamlaka ya kuiwakilisha Zanzibar?
Tanganyika imekasimu mamlaka yake; kwa hiyo inawakilishwa na serikali ya Muungano(Tanzania).Muungano haueleweki, utata mwingi sana.

Kwa maelezo ya Nguvuri3, Tanganyika haikufa na kwa hivyo utanganyika haukufa pia.
https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...wa-serikali-3-ni-bora-sana-4.html#post4451717

Lakini pia mantiki ni kuwa mjusi(lizard)Zanzibar hawezi kummeza mamba(crocodile)Tanganyika. Lakini Kinyume chake ni kama chatu(Tanganyika) kula/kummeza kuku(Zanzibar).

https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...-moja-nchi-moja-taifa-moja-5.html#post4415616

Nchi mbili zinapoungana na kuwa Nch i moja mifumo ya kawaida ya miundo ya Katiba ni miwili: Muungano wa Serikali Moja, au Shirikisho la serikali Tatu. Kwa mfumo wa kwanza kila nchi itafuta serikali yake na nchi mpya inayolizaliwa itakuwa ni nchi moja yenye Serikali moja. Katika mfumo wa pili kila nchi itajivua madaraka ambayo yatashikwa na serikali ya shirikisho na itakuwa na serikali ambayo ambayo itakuwa na mamlaka juu ya mambo yaliyobaki.

Kwa hiyo mimi nilipinga mfumo wa Serikali Moja. Shirikisho la Serikali Tatu lingekuwa ni gharama kubwa mno kwa Tanganyika. Zanzibar ingeendesha Serikali yake na kuchangia gharama za kuendesha Serikali ya Shirikisho; na Tanganyika ingefanya vivyo hivyo. Lakini ni dhahiri kwamba mchango wa Tanganyika ndio hasa ungeendesha SerikaIi ya Shirikisho.
Kwa hivyo ilitupasa tujiulize kwa nini tunataka kuibebesha Tanganyika gharama zote hizo; na hasa kwa nini tunataka Serikali ya Tanganyika? Hivi tuna hofu ya kwamba Tanganyika, bila kuwa na SerikaIi yake, itaoekana kuwa imemezwa na Zanzibar ? Hofu yetu ni kwamba tukiwa na Serikali Moja Tanganyika itaonekana kuwa imeimeza Zanzibar.

Labda ni vizuri kukumbusha kwamba shabaha ya baadhi yetu ilikuwa ni kuunganisha nchi za Afrika Mashariki ziwe nchi moja. Na wakati Zanzibar na Tanganyika zinaungana, Kenya, Uganda na Tanganyika zilikuwa katikati ya mazungumzo ya kutafuta uwezekano wa kuungana. Kama jambo hilo, lingetokea, nina hakika kabisa kwamba mfumo wa nchi mpya ambayo ingezaliwa ungelikuwa ni Shirikisho; au la Shirikisho la Nchi Tatu zenye Serikali Nne, na Shirikisho la Nchi Nne zenye Serikali Tano.

Kwa kweli hata kesho Nchi za Afrika ya Mashariki zikiamua kuungana, na Tanzania ikawa ni mshiriki, naamini kuwa ni rahisi zaidi kushirikisha Tanzania yenye Serikali Mbili - ya Zanzibar na ya Tanganyika - kuliko Tanzania yenye Serikali Mbili, ya Tanzania na ya Zanzibar. Wapendao Utanganyika watakuwa wazalendo zaidi, badala ya kuwa wasaliti, wakiazimia Afrika ya Mashariki iliyoungana kuwa Nchi Moja. kuliko Tanzania iliyotengana ikawa nchi mbili.

Uk10-12 link Uongozi Wetu Na Hatma Ya Tanzania (by Nyerere)



Sasa tunaotaka serikali moja na Zanzibar, je tuko tayari pia kuunda serikali moja na Kenya au Uganda? Au tutapenda kuunda serikali ya shirikisho na nchi hizo?
Hapo jipime nia yako na dhamira yako mchangiaji. Nini nia ya kutaka kuifuta serikali ya Zanzibar?

Kuna kitu katika maandiko ya mwalimu Nyerere ambacho hakifahamiki? Ni kipi?

Kila tunavyojifanya mafundi zaidi ndio tunazidi kulikoroga!!!

Tuunde serikali ya Tanganyika na Serikali ya Zanzibar, tuanze safari ya EA federation.
Tutakuwa na nchi ya Tanzania ambayo itakuwa na hadhi kama ilivyo Tanganyika leo ndani ya Muungano na kila upande utapata kujiwakilisha vyema katika EAC/EAF. Mazingaombwe yatakuwa yamepata dawa yake.
 
Mkuu kama rafikiako atatoa pesa sawa na wewe na mukashirikiana kujenga basi itakua sawa hakuna ubinafsi. Lakini wewe unazo milioni arubaini halafu umwambie rafikiako mwenyemilioni moja muchanganye pesa mujenge basi huo ni ujanja na huenda ikawa unania ya kumzulumu kile kidogo chake na baadae utasema nyumba ni yako kwavile wewe ndie uliotoa nyingi.

Labda niongeze suali kwa watu kama Mwanakijiji!na Mkanda, ikiwa serekali tatu au mkataba hazinafaida na tanganyika labda mutueleze Tanganyika itafaidika na nini katika muungano wa serekali moja?
Mkuu wangu, tulichiokubaliana hakitokani na Urafiki bali ni Undungu wetu iwe ni ndoa ama kula yamini. Hivyo kinachotangulia ni UNDUGU wetu haya maswala ya madai ya kujenga nyumba ni ziada kama watu wengine wanavyogombania Mirathi..

Binafsi yangu sikubaliani na kuvunja Undugu kwa sababu ya mabishano ya ujenzi wa nyumba moja ama matumizi yetu.. Tukisha kuwa ndugu haina maana kila mmoja wetu amtegemee mwingine ama mmoja kuyaendesha maisha ya mwingine. Kila mmoja wetu atakuwa na maisha yake kama binadamu na yale ya Undugu wetu ndio tunakusanyika kuyajadili..

Mwisho nadhan sijasema serikali tatu hazina faida kwa Tanganyika.. Hapana nimesema nataka serikali tatu ili Tanganyika irufishe uhalali wake wa UHuru wa mwaka 1961 na siku zote nitaendelea kusherehekea Kuzaliwa kwa Tanganyika maana sijasikia ndoa ya mume na mke mmoja haruhusiwi kusherehekea siku yake ya kuzaliwa, hata kama sisi tumeolewa na Zanzibar tukabadilisha Ubini wetu..Wao waislaam walimuoa mke mkristu kwani hawakujua?.. utasikia ati walilazimishwa jamani watu wenyewe wangemalizana, yule Jaluo Okello angetawala mwaka mmoja tu sijui ingekuwa vipi..wamshukuru Bi Khadija mwenye radhi za Bin Adam kuja waokoa toka mdomo wa mamba leo wamesahau yote..
 
Back
Top Bottom