Muundo wa Muungano: Tanganyika tunataka 'Serikali moja, nchi moja, taifa moja'!

Muundo wa Muungano: Tanganyika tunataka 'Serikali moja, nchi moja, taifa moja'!

Maanakijiji acha ujanjaujanja,

Unachosema hapa hakina tofauti na wanachokifanya CUF aka UAMSHO,

SERIKALI MOJA + SERIKALI TATU NA MUUNGANO WA MKATABA HUKU SERIKALI ZA ZANZIBAR NA TANGANYIKA ZIKIWA NA MAMLAKA KAMILI = KUVUNJA MUUNGANO

Kuweni na uthubutu wa kusema yaliyomo moyoni na sio kutumia lugha za kiujanjaujanja. Thubutu kusema kuwa hautaki Muungano. Waambieni ukweli wafuasi wenu kuwa hamtaki Muungano uendelee kuwepo kuliko kuwadanganya wapiganie kisichoweza kupatikana.

Kwani wewe maoni yako ni yapi?,
 
Nonda,
kuna kitu kimoja Wzn wameshindwa kukielewa. Wanadai mamlaka kamili 100%. Wakati huo huo wanadai kuwe na serikali 3 au mkataba. Kuwepo kwa vitu hivyo tayari kutaondoa asilimia 100 na kuirudisha chini. Zanzibar watakubali hilo? Kama hawakubali, mamlaka kamili wanayodai ni yapi yatakayowaacha na uhuru wa mamlaka kamili 100%

Ukishasema mamlaka kamili hapo tayari umeshaondoa uwezekano wa mkataba au serikali 3. Labda unieleweshe utakuwaje na mamlaka kamili halafu ukawa na mkataba au serikali 3?

Pili, kuna kitu kinaitwa serikali 3, nauliza kila siku na huwa ndio mwisho wa mjadala hasa kwa WZNZ. Serikali ya tatu ya muungano itashughulikia nini ili ihakikishe kuwa ZNZ inabaki na mamlaka kamili 100%. Na hiyo ya tatu inaendeshwaje kwa gharama ikiwa ZNZ yenye mamlaka kamili 100% ni mbia sawa na Tanganyika itakayokuwa na mamlaka kamili?

Tatu, katika mkataba unaongelewa kuna siri gani ya mkataba ambayo WZNZ hawataki kuiweka wazi? Nina maana mkataba ushughulikie mambo gani yenye faida kwa pande zote zikiwa wabia sawa?

Nne, kitu gani kinachowazuia kusema mnataka kuvunja muungano? Kwanini mnakimbilia serikali 3 au mkataba na si kuvunja bughudha hii ya muungano inayowanasabisha na wabantu ili hali ninyi ni waarabu? Kwanini msitamke LET Tanganyika GO! kama sisi tulivyo na uthubutu wa kusema LET ZNZ GO!

Nomba safari hii usikimbie, uwe na uthubutu wa kujibu. Ukikimbia utakuwa umepoteza uhalali wa kulizungumzia hili jambo kwasababu utakuwa sawa na yule kijana wa mtaani anayeimba mayenu na bolingo ambaye ukimuuliza maana yake hajui, lakini anaimba vema sana.
Nonda, ukiweza kujibu maswali hayo hapo juu utakuwa na uhalali wa kusema ninyamaze, vinginevyo sitavutika katika udhaifu wa kujenga hoja kwa njia ya dharau au matusi. Matusi ni silaha nzuri na nyespesi kuitumia kwa asiye na hoja na hoja ni kinga nzuri kwa mwerevu

Nikukumbushe kuwa mjadala huu umeanza takribani miaka miwili tukiwa na akina Takashi, Baru baru na Zomba. Nimekuwa consistent na maswali kadha wa kadha ambayo majibu yake yamekuwa ni kukimbia thread na kuanzisha nyingine.
Nitaendelea kuwaambia wazanzibar kuwa hoja yao kubwa ni uonevu na njia ya kuondoka katika uonevu ni kuvunja muungano.

Wazanzibar wana kila namna na silaha ya kuvunja muungano. Tumewasikia wakisema kila wanalotaka.
Ukweli uliodhahiri ni kuwa hatawaki muungano uvunjike kwa hofu ya kuwa losers. Wazanzibar wameingizwA mkenge na sasa wanatapa tapa hawana pa kutokea ndio maana wanabaki na hoja ya serikali 3 au mkataba.

Makamu wa Rais Idd Seif amewaambia mchana kweupe, hawajui na hawakuandaliWa kudai wanchokitaka.
Hawawezi kutetea mkataba au serikali 3. Haya ni baadhi ya mambo yaliyoandikwa JF miaka 2 iliyopita.

Nakuhakikishia kuwa, Maalimu Seif Shariff Hamada ambaye ni kinara wa uchochezi wa kuvunja muungano naye pia kabadili msimamo na kubaki na nyimbo ile ile ya taifa la ZNZ serikali 3 au mkataba.

Ahmed Rajab ambaye ni mwandishi naye pia katika kipindi cha miaka 3 ameshindwa kutamka hata neno moja kuhusiana na mkataba au serikali tatu.

Juzi Jusa kabadili msimamo anataka serikali 3, CUF wamebadili msimamo wanataka serikali 2 .
Wakati wazanzibar wakitapa tapa kutafuta mahali pa kushika kwa hofu ya kuvunjika muungano, Watanganyika wameSimama kidete kusema hawatakai Serikali 3 kwasababu ni kubeba zigo lisilo na manufaa.
Hawataki mkataba maana hauna tija na hawaoni mkataba wa nini.

Hayo yakiendelea, Washirazi wamekuja na makala za kuonyesha asili yao ni ZNZ wala siyo Uarabuni na Persian. Wanasema wao ni wengi na wanataka ZNZ ya Sultani. Hili linazidisha hofu miongoni mwa Wazanzibar kwasababu hawajui hatima yao baada ya wenye nchi washiriza kudai mapinduzi ni upuuzi, ZNZ bora ni ile ya Sultani.

Tunachokiona sasa ni kutapa tapa kwa wazanzibar ndio maana hawana majibu ya kile wanachokitetea.
Tutasimama kidete kuhakikisha kuwa unyonyaji unafika mwisho na Watanganyika wanaelewa hilo.

LET ZNZ GO! We have nothing to lose, they have lot to lose
 
Zanzibar ni ndogo sana kijiografia,hofu yao kukiwa na serikali moja dola yake. Pia ikikubali serikali 3 itapoteza nguvu na rasilimali kwali kila serikali lazima ichangie na itapata kulingana na mchango. Bara (serikali iliyopo madarakani) inataka serikali mbili ili iendelee kuficha maovu yake. Ukweli ni kwamba iff we can't have a single government better have 3 for the sake of the union otherwise @ country abstain Union.
 
Nonda,......
Nikukumbushe kuwa mjadala huu umeanza takribani miaka miwili tukiwa na akina Takashi, Baru baru na Zomba. Nimekuwa consistent na maswali kadha wa kadha ambayo majibu yake yamekuwa ni kukimbia thread na kuanzisha nyingine.
Nitaendelea kuwaambia wazanzibar kuwa hoja yao kubwa ni uonevu na njia ya kuondoka katika uonevu ni kuvunja muungano.


LET ZNZ GO! We have nothing to lose, they have lot to lose
Mkuu nguruvi3,

Unaionaje hiyo rai ya Mwalimu Nyerere ya kuwa na serikali mbili Tanzanaia? Serikali ya Tanganyika na serikali ya Zanzibar badala ya serikali ya Tanzania na serikali ya Zanzibar?

Nia ya mjadala/ mijadala hii sio lazima iwe Simba na Yanga. Bali ni kutafuta suluhisho( dawa mjarabu) ya usanii wetu(Muungano wetu). Hii dawa aliyoitoa Mwalimu itatibu matatizo sugu ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.
Itatatua tatizo la kuibebesha mzigo Tanganyika( Tzbara/ bara) na akina sisi tunaotaka kujinasibisha na utanganyika wetu tutatembea na kifua mbele, itamaliza kelele za washirazi(masultani,watwana,watumwa,Znz) na itakidhi tunu yetu ya umajumui wa kiafrika(pan-africanism) tuliyonayo; kuwa na nchi kubwa yenye members wengi, Kenya, Uganda, Tanganyika, Zanzibar, Rwanda na Burundi. Yaani nchi yetu itakuwa na wanachama 6. Bila shaka mfumo wake utakuwa mfumo wa shirikisho. Serikali 7, serikali za majimbo 6 na serikali ya shirikisho 1.

Au wewe unataka kubaki na mazingaombwe yaliyodumu kwa miaka 48 ambayo yanazalisha kero tu?

Tazama picha kubwa, usijikite kwenye masimulizi ya Jussa, Seif, Barubaru, Hizbu, ASP, Usultani,mapinduzi daima nk.

Tanabahisho.Litakapoundwa Shirikisho la Afrika Mashariki, utanzania utakufa, utaifa mpya utakuwa Uafrika Mashariki, lakini majina ya maeneo(territories) yatabaki.

Naomba wanajf, tuipokee hii rai, tuifikirie kwa utuo na kama tutaona itatusogeza mbele basi, kampeni ianze mara moja ya Tanzania yenye serikali mbili, ya Tanganyika na ya Zanzibar.

Atakapokuja Warioba na tume/kamati yake tudai, Tanzania yenye serikali ya Tanganyika na Serikali ya Zanzibar.
Tunaua dege bili kwa jiwe moja tu.

Soma post #88 hapo juu.
 
The EAC aims to facilitate cooperation among its Partner States in political, economic and social fields for their mutual benefit. To this extent the EAC countries established a Customs Union in 2005 and are working towards the establishment of a Common Market in 2010, subsequently a Monetary Union by 2012 and ultimately a Political Federation of the East African States.

Huko ndiko tunakoelekea.

Link East African Community (EAC)
 
Nonda,
Moja ya hoja za Wazanzibar ni kuwa na serikali yao yenye mamlaka kamili. Kero za muungano hazipo ZNZ hata Tanganyika zipo. Kinachoudhi ni kitendo cha WZN kuona kuwa wanaonewa na wamekula koloni la Watanganyika.
Katika dunia ya sasa nchi kuwa koloni si jambo jema na hapo ndipo tunasema, basi ZNZ iondoke katika muungano halafu tukutane katika shirikisho la EA.

Huko kwenye shrikisho ZNZ haitabaki na mamlaka kamili. Ukishakubali kuwa na shirikisho tayari umekubali kuuza uhuru wako kwa shirikisho. Sijui kama Rwanda watakubali kutoa ajira kwa WZNZ wakati wznz hawatakuabali kutoa jaira kwa Warwanda. Sijui kama Tanganyika itaruhusu ardhi ya bwerere kwa wznz wakati Watanganyika hawana haki hiyo ZNZ.
Kwa lolote liwalo ZNZ haitaweza kubaki na mamlaka kamili kama inavyodhani. Ni kujidanganya.

Kwa vile WZNZ wanasema Nyerere Laanatullah(laana ya mwenyezi mungu iwe naye) na kwa vile wengi wanaamini yeye ndiye chimbuko la mapinduzi na muungano wa kuimeza ZNZ, hakuna hoja ya Nyerere itakayokuwa na mashiko kwa MZNZ hata kwa bahati mbaya. Nashangaa hata unamnukuu na sina uhakika swaumu yako itaswihi ,kwasababu Nyerere ni 'shetani' kwa Wazanzibar. Kwanini tujadili mawazo yake tusijadili yetu. Kwanini tumfikirie huyu 'shetani' kwa mustakabali wa nchi yetu ya ZNZ yenye waumini na binadamu kamili?

Kibaya zaidi ni chuki iliyojengwa na WZNZ dhidi ya Watanganyika. Sheria zote za kazi zinazowekwa, ardhi n.k hazimlengi raia mwingine isipokuwa Mtanganyika. Huku bara wapo raha mustarehe ingawa uvumilivu umekwisha na ni suala la muda tu watatimuliwa, watabaguliwa na watatendewa kama wanavyotenda.

Na kwa vile muungano huu hauna faida kwa ZNZ, swali linabaki pale pale, ni faida gani Mzanzibar anaitaraji ndani ya serikali 3 au mkataba? kwanini tusivunje muungano, nini ZNZ inaogopa?

Kinachosikistisha sana ni kuwa hoja za WZNZ hazina kichwa wala miguu. Soma makala ya Seif utabaini kuwa hana hoja ila kutapa tapa. Kama mnataka mamlaka kamili mtayapataje mkiwa katika mkataba au serikali 3?

Mimi nadhani kabla ya mtu kutamka serikali 3 lazima kwanza aangalie maana ya serikali 3, kazi za serikali 3 na uendeshaji wa serikali 3. Kama ni mkataba nao pia uangaliwe vivyo hivyo.

Kutamaka tu serikali 3 au mkataba ni kiwango cha chini sana cha elimu, kufikri ua kutafakari. Ni lazima watu waende zaidi ya hapo. Hadi sasa hakuna MZNZ aliyewahi kuja na proposal ya vitu hivyo ila wote wanaimba kibwagizo cha kwaya, tatu mkataba.

Narudia Zitto kabwe ametoa maoni yake juu ya serikali 3, hata kama sikubaliani na proposal yake ninamsifu kwa kuwa na kitu chenye mantiki (substance). Amejiweka tofauti na WZNZ wasioweza kusema lolote kuhusu wanachokidai.

Chuki kati ya Tanganyika na ZNZ sasa ni kubwa sana na kabla watu hawajaendelea kuchinjana (znz wameanza kwachinja Wabara) ni afadhali muungano uvunjike kila mtu ashughulikie matatizo yake.

Hamuwezi kuwa na ushirikiano na makafir ikiwa ninyi ni watu safi. Mkataba au serikali 3 utawaletea ushenzi, ujambazi, ubazazi n.k. Ninyi hampo tayari kwa kuwa ni taifa teule. Sisi hatupo tayari kubaguliwa kunyanyaswa na WZNZ.

Wakati umefika sasa tunawataka WZNZ waondoke warudi kwenye nchi ya asali na neema.
Wasipoondoka kwa amani tutawaondoa kwa hila. Tutafanya kile wanachofanya. Hili halinamjadala linasubiri wakati tu.

LET ZNZ GO!
 

Nyie ndiyo mnapotosha dhana ya Muungano. Ni vipi Zanzibar itakuwa Mkoa wa Tanganyika kwa mfumo wa serikali moja wakati Tanganyika na yenyewe itakuwa imekufa?

Ok Wanzibara hawataki serikali moja, swali langu linakuja nini mantiki ya Muungano kama bado kila nchi itakuwa na srikali yake. Huo utakuwa Muungano au Ushirikiano baina ya nchi mbili? Huwa nawashangaa sana Wanzinzibar Muungano hawautaki ila faida za Muungano wanataka! What's this Paradox?!

TUMBIRI (PhD, Hull University, HULL City - United Kingdom),
tumbiri@jamiiforums.com



Kumbuka mwaka jana December (9/December 2011) tulisherehekea miaka 50 ya uhuru wa Tanzania (for the majority of people and media, and me included) AND THAT WAS OFFICIAL! - 50TH ANNIVERSARY OF TANZANIA INDEPENDENCE (watu wachache walisherehekea miaka 50 ya uhuru wa Tanzania bara). Sikumsikia aliyesherehekea miaka 50 ya uhuru wa tanganyika.


Jiulize kwa nini tulisherehekea miaka 50 ya UHURU WA TANZANIA au UHURU WA TANZANIA BARA, wakati Tanzania iliasisiwa mwezi April mwaka 1964 kwa muungano wa mataifa huru mawili - Hiyo miaka 50 ilitokea wapi?. Kwa nini tusherekee Uhuru wa Tanzania nchi ambayo haikupata/haikuwahi kutawaliwa? Jibu ni rahisi, TANGANYIKA ndio TANZANIA ndio MUUNGANO, na SERIKALI YA TANGANYIKA ndio SERIKALI YA MUUNGANO. kwa mfano, Tanzania yajipanga kuiadabisha malawi kwa kadhia ya ziwa Nyasa, jee zanzibar inashirikishwa kwenye kadhia hiyo - hapana. Jee ni nini msimamo wa zanzibar juu ya hilo? utasikilizwa? TANGANYIKA NDIO TANZANIA. Na muungano si lolote zaidi ya ukoloni wa wa tanganyika kwa zanzibar. Tanganyika yaweza kuiingiza Tanzania kwevye vita, dhidi ya Amini, au Malawi (mungu apitishie mbali), zanzibar haiwezi jambo kama hilo. Haiwezi hata kujiunga na OIC hadi siku Tanganyika watapopenda.
Kwa hali hiyo basi Mfumo wa serikali moja hautakuwa na jengine zaidi ya kuitumbukiza/kuimeza/kuiyeyusha zanzibar katika Tanganyika. Tanganyika wont have nothing to lose. BASI IWE KWA CONSENT YAO wazanzibari.
 
Kimsingi Muungano huu haukupaswa kuwa na serikali mbili kama zilivyo hivi. Ingawa kwa sasa tayari kuna mambo mengi sana yataleta mgogoro katika kuvunja au kuuendeleza muungano, kwa serikali mbili au tatu...chaguzi zote hizo ingawa Zina matatizo yake, lakini ni afadhali tuamue kupambana na changamoto zitakazojitokeza kwa kufanya serikali MOJA ya nchi Moja ya Tanzania. TOSHA!!! Zanzibar iwe tu kisiwa ndani ya Tanzania chenye uongozi kama mikoa mingine tu huku Tanganyika.Najua wale wazawa wa Zanzibar haswa wataona ni kupoteza utaifa wao na wanaweza wasikubali kabisa na sababu watatoa.

Sidhani kama kuna hasara nyingine kubwa zaidi ya kijamii ambapo watu wenyewe sasa kuanza kuyumba hasa ambao wamehamia kule au wameoana kule, au wazazi wao wametoka pande mbili, je waitwe wakimbizi, je warudi kwao, au je wakae huko kama wageni, je wachukue Uraia wa huko, au waachwe kuamua wenyewe n.k. Kwa kweli kijamii hiyo ni changamoto.
Mi nadhani Zanzibar ikubali tu seriikali moja in real sense kama United States of America, siyo tu kisiasa tu wakati nao wanakuwa na seriikali na kila kitu.
Lakini mi nadhani Zanzibar ikijitenga kabisa, will make friends with Arabic world and Tanganyika will not be their best friend and (with all that they know about Tanganyika securitywise, etc, ) they can easily be ready to even betray Tanganyika for their own prosperity
Something worth fighting, worth facing its challenges ahead is only ONE COUNTRY, ONE GOVERNMENT, ONE PRESIDENT, ONE PEOPLE.
 
MCHAKATO KATIBA MPYA
Tusipoujadili muungano kwa makini, utavunjika II
Joseph Mihangwa
Toleo la 253
8 Aug 2012
Kelele za Zanzibar kama za Eritrea
KATIKA sehemu ya kwanza ya makala haya toleo lililopita, tuliona jinsi Muungano wowote wa nchi uliofikiwa bila ridhaa ya wananchi unavyoweza kuvunjika kwa urahisi, ukiwamo Muungano kati ya Uingereza na Ireland Kaskazini ambao Muungano wa Tanzania umenakili na kuiga mengi, ulivyoanza kuyumba.
Tuliona pia dalili zinazoashiria kuvunjika kwa Muungano wetu, zikiwamo, kukosekana nahodha makini wa kuendesha meli ya Muungano iweze kuvuka salama bahari iliyochafuka; kuanzishwa kwa Muungano wa kitaifa wa Wazanzibari ambao umefufua umoja wao wa kitaifa na kudai kurejeshewa hadhi yao kama nchi; na kuvunjika kwa mihimili mitatu iliyoshikilia Muungano, ambayo ni Rais dikteta asiyeambilika (imperial presidency), mfumo wa Chama kimoja, Azimio la Arusha na Siasa ya Ujamaa na Kujitegemea.
Kabla hatujaichambua kwa kina athari ya kuvunjika kwa mihimili hii mitatu, tuangalie kifananisho cha Muungano wa Ethiopia – Eritrea ulivyovunjika kwa sababu, kama ilivyokuwa Eritrea kwa Ethiopia, ndivyo ilivyo Zanzibar kwa Tanzania. Eritrea ilijitoa kwenye Muungano kati yake na Ethiopia na kuwa nchi huru mwaka 1993.
Harakati za Zanzibar kujitoa kwenye Muungano, kama zilivyokuwa harakati za Eritrea kujitoa kwenye Muungano kati yake na Ethiopia kunatishia na kujenga hofu kwa Watanzania juu ya hatima ya Muungano, hasa baada ya kuundwa kwa Serikali ya Kitaifa (SUK) kwamba sasa hofu hiyo na yenye kuogofya ni dhahiri na yenye kuzua hofu.
Kwa mfano, nani alitarajia kabla ya hapo, kwamba siku moja Zanzibar itakuwa na bendera yake ya Taifa, Wimbo wake wa Taifa, Ngao ya Taifa, “Jeshi” la Taifa, Katiba yake yenye kulinda ukuu wa nchi na maslahi ya Wazanzibari bila kuingiliwa na Katiba wala taasisi yoyote ya Muungano?
Nani alitarajia siku moja Zanzibar itazuia rasilimali zake kutumika kwenye Serikali ya Muungano kama mafuta, ardhi na bahari, ila kwa matumizi na maslahi ya Wazanzibari pekee?
Nani alitarajia kwamba Zanzibar ingeweza kujiunga na Shirikisho la Mpira la Bara la Afrika (CAF) kama nchi nje ya Muungano wa Tanzania na sasa inataka ijiunge na Shirikisho/Jumuiya ya Afrika Mashariki kama nchi?
Yote haya yanatia hofu na kuogofya juu ya hatima ya Muungano, kama tu hatutarejea upya Mkataba wa Muungano kuona wapi unavunjwa na yapi wanayofanya ni sahihi tuwaachie waendelee, badala ya kuendeleza udikteta wa kizamani kuzima hoja sahihi. Kuna dhambi gani wananchi kupewa Mkataba wa Muungano wakasoma na kujiridhisha na yaliyokusudiwa kwenye Muungano huo?
Hofu hii juu ya SUK inaweza kufananishwa na hofu kama iliyozua Eritrea kwa Serikali ya Muungano wa Ethiopia – Eritrea, pale Eritrea alipoanzisha harakati halali kutaka kujinasua kutoka kwenye Muungano huo, uliodumu tu kwa udikteta wa Mfalme Haile Selassie kama nahodha wa Muungano, na alipoondolewa madarakani, meli ya Muungano iliyumba na kuzama kwa nguvu ya tufani.
Na ndivyo ulivyo Muungano wetu, baada ya kuondoka madarakani kwa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, aliyeshika hatamu zote za Muungano na kuuendesha kwa staili ya mpanda Farasi.
Zanzibar kama Eritrea kwenye Muungano
Eritrea ilitawaliwa na Wataliano kwa miaka 50 hadi 1941 waliposhindwa vita na Waingereza. Baada ya ushindi huo, Uingereza iliruhusu nchi hiyo kujitawala kama nchi huru chini ya usimamizi wake. Hapo vyama vya siasa na vya Wafanyakazi vikaanzishwa, pamoja na vyombo vya habari huru kwa ajili ya elimu kwa umma.
Mwaka 1952, wakati hatima ya Eritrea ilipojadiliwa kwenye Umoja wa Mataifa, Ethiopia ilitaka ipewe nchi hiyo kwa madai kwamba, kihistoria ilikuwa ni sehemu ya ufalme wa Ethiopia. Hapo kukatokea mzozo.
Wakati nchi jirani za Kiarabu zilitaka Eritrea iwe Taifa huru, Waeritrea wenyewe, ambao idadi yao wakati huo ilifikia 3,000,000, waligawanyika; nusu yao ambao ni wa madhehebu ya Kikristo, na wa kabila la Tigraya waishio maeneo ya milimani karibu na Mji Mkuu, Asmara, waliunga mkono Muungano na Ethiopia.
Kwa upande wa pili, nusu ya Waeritrea ambao ni Waislamu, wanaoishi sehemu za jangwa karibu na Bahari ya Sham na bonde la Magharibi, walitaka Eritrea ipewe uhuru.
Mwafaka ukafikiwa chini ya usimamizi wa Umoja wa Mataifa, wa kuunda Shirikisho la Ethiopia na Eritrea ambapo Serikali ya Ethiopia ilipewa kusimamia mambo ya Nje, Ulinzi, Fedha, Biashara, Bandari na Forodha.
Chini ya Muungano huu, ambao muundo wake unafanana na Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, Eritrea, kama ilivyo kwa Zanzibar, iliruhusiwa kuwa na Serikali yake na Bunge huru kusimamia mambo yake. Tena, kama ilivyo Zanzibar ndani ya Muungano, iliruhusiwa kuwa na bendera yake, lugha zake za Taifa, ambazo ni Kitigrinya na Kiarabu.
Tangu mwanzo, Mtawala wa Ethiopia, Mfalme Haile Selasie, aliuona Muungano huo, kama ambavyo Rais Julius K. Nyerere alivyouona Muungano wa Tanzania, kuwa ni hatua ya mwanzo tu kuelekea Muungano kamili kwa kuunda nchi moja.
Kero na kelele juu ya Muungano zilianza kusikika pale Watawala wa Ki-ethiopia, kwa ubaguzi na kujuana, wakisaidiwa na wanasiasa Wakristo wa Kitigraya, walipoanza kuvuka mipaka ya mambo yaliyokubaliwa chini ya Mkataba wa Muungano, kwa kuongeza mambo kwa njia ya shinikizo, vitisho na udhibiti kwa Waeritrea.
Kwa njia hii, uhuru ambao Waeritrea walifurahia kwa muda baada ya ukoloni wa Kitaliano (na kabla ya Muungano), kama vile haki za kisiasa, vyama vya wafanyakazi na uhuru wa vyombo vya habari, vilidhibitiwa. Hapo tena, kelele juu ya Ethiopia kutaka kuimeza Eritrea, kama ambavyo Wazanzibari wanalalamikia kutaka kumezwa na Tanganyika, ikazua moja ya kero za Muungano.
Muungano kati ya Tanganyika na Zanzibar uliofikiwa Aprili 26, 1964, ulibainisha mambo kumi na moja tu ya Muungano, baadhi yakiwa ni yale yale yaliyokuwa chini ya Muungano wa Ethiopia na Eritrea, tuliyoyaeleza hapo mwanzo.
Na kama ilivyokuwa kwa Ethiopia/Eritrea, Serikali ya Zanzibar iliachwa kusimamia mambo yote yasiyo ya Muungano, na vivyo hivyo kwa Serikali ya Tanganyika.
Lakini kama ilivyokuwa kwa Ethiopia/Eritrea, kadri Muungano wa Tanzania ulivyopiga hatua mbele, mambo ya Muungano yalizidi kuongezwa kwa njia ya Amri za Rais (Decrees) kinyume na matakwa ya Mkataba wa Muungano, na kufikia 23.
Katiba ya muda ya 1965 (ibara ya 12), ilimpa Rais wa Jamhuri ya Muungano mamlaka ya utendaji kwa mambo yote (11) ya Muungano na kwa Tanganyika; kwa maana kwamba, Rais wa Muungano alikuwa sasa ndiye Rais wa Muungano na hapo hapo Rais wa Tanganyika.
Vivyo hivyo, ibara ya 49 ya Katiba hiyo, ilitoa mamlaka ya kutunga sheria kuhusu mambo ya Muungano na kwa ajili ya Tanganyika, kwa Bunge la Muungano. Ndiyo kusema kwamba, Bunge hilo la Muungano sasa lilikuwa ndilo Bunge la Tanganyika pia.
Mwaka 1967, Bunge lilitunga Sheria Na 24 ya 1967, iliyompa Rais wa Muungano na Rais wa Tanganyika uwezo wa kupachika jina “Tanzania” katika sheria zote popote pale jina “Tanganyika” liliposomeka hivyo.
Hii ilimaanisha kwamba, “Tanganyika” sasa ndiyo iliyogeuka kuwa “Tanzania”, na “Tanzania” ndiyo Tanganyika, lakini Zanzibar ikabakia kama Zanzibar.
Ni kwa misingi hii kwamba, Sheria ya Tafsiri za Vifungu vya Sheria (Interpretation of Laws and General Cluses Act), Namba 30 ya 1972 (kifungu cha 3), iliweza kutafsiri neno “Jamhuri” kumaanisha “Jamhuri ya Tanganyika, inayojumuisha Jamhuri ya Muungano”.
Tanganyika ndiyo Tanzania?
Sheria Namba 24 ya 1967, iliyofuta jina “Tanganyika” kwenye vitabu vya Sheria; na Sheria Namba 30 ya 1972 iliyotafsiri “Jamhuri ya Tanganyika” kujumuisha “Jamhuri ya Muungano” zilitoa tafsiri mbaya na mitazamo potofu kuwafanya Watanganyika kuamini kwamba nchi yao Tanganyika ilipandishwa hadhi kuwa Tanzania, kama mshirika mwandamizi kwa Zanzibar katika Muungano; wakati ukweli Tanganyika na Zanzibar zina hadhi sawa ndani ya Muungano.
Katiba ya kudumu ya 1977 inayotumika sasa ilitibua mambo zaidi na kuongeza utata na mtafaruku kwa Muungano.
Tunafahamu kwamba, Mkataba wa Muungano (ibara ya 5, 6 na 7) kwa Sheria ya Muungano Namba 22 ya 1964 (kifungu 5, 7 na 8) zinatamka bayana kuendelea kuwapo kwa Serikali za Tanganyika na Zanzibar baada ya nchi hizo kuungana kuunda ubia wa mambo kumi na moja ya “Muungano wa Tanganyika na Zanzibar”, kwa maana ya kuwapo Serikali tatu: Serikali ya Tanganyika, Serikali ya Zanzibar na Serikali ya Muungano.
Kwa mfano, ibara ya tano ya Mkataba huo inasema: “Sheria za sasa za Tanganyika na zile za Zanzibar, zitaendelea kuwa na nguvu katika maeneo (territories) ya nchi hizo”.
Na kifungu cha 8 (1) cha Sheria ya Muungano kinasema:
“….. Kuanzia siku ya Muungano na baada ya hapo na kuendelea, Sheria za Tanganyika na za Zanzibar zitaendelea kuwa Sheria za nchi za Tanganyika na Zanzibar ….. na hazitaathirika au kuathiriwa kwa namna yoyote ile kwa kukoma kutumika kwa Katiba ya Tanganyika kwa Serikali ya Tanganyika kama sehemu ya Jamhuri ya Muungano inayojiongoza na kujitawala…..”.
Tofauti na Mkataba wa Muungano; pia tofauti na Katiba ya Muda ya Jamhuri ya Muungano ya 1965, iliyotambua kuwapo kwa Serikali za Tanganyika na Zanzibar, Katiba ya Jamhuri ya Muungano ya 1977 inayoendelea kutumika sasa haiundi au kutambua kuwepo kwa Tanganyika; wala haimpi mamlaka Rais wa Jamhuri ya Muungano, au mtu au watu wowote wale, kuitawala Tanganyika kwa mambo yasiyo ya Muungano.
Hapa, upungufu huu unazua dhana potofu kuwa, Tanzania ndiyo Tanganyika, na Tanganyika ndiyo Tanzania; na kwa sababu hiyo kwamba hapana haja ya kuwa na Serikali zaidi ya moja kwa Tanzania nzima!.
Vivyo hivyo, kama ambavyo uhuru na uwapo wa vyama vya siasa na vya wafanyakazi ulipigwa marufuku kwa AMRI ya Mtawala wa Ethiopia nchini Eritrea (1959), na bendera ya nchi hiyo kufutwa (1958); ndivyo vivyo hivyo mwaka 1977 hapa kwetu, Chama cha ASP kiliunganishwa na Chama cha Tanganyika National Union (TANU), kuunda “Chama cha Mapinduzi” – CCM, kama moja ya mikakati ya kuimarisha Muungano, wakati ukweli mambo ya Vyama vya siasa si moja au sehemu ya mambo chini Mkataba wa Muungano, wala sehemu ya Sheria za Muungano (Acts of Union) kwa utekelezaji.
Kelele za Wazanzibari kama za Waeritrea
Ni kwamba, kelele za Eritrea, kama zilivyo kelele za Zanzibar juu ya kero za Muungano, hazikuwa za uongo, kwani ubabe wa Ethiopia (kaka mkuu ndani ya Muungano, kama ilivyo Tanganyika) ulianza kujionyesha dhahiri kwa kushinikiza mambo yasiyo ya Muungano.
Kwa mfano, mwaka 1958, bendera ya Eritrea ilifutwa; ambapo mwaka 1959, Sheria za Ethiopia zilishinikizwa pia kutumika Eritrea; vyama vya siasa na vya Wafanyakazi navyo vikapigwa marufuku.
Ubabe huu ulikwenda mbali zaidi kwa kudhibiti habari na vyombo vya habari, lugha za Taifa za Kitigranya na Kiarabu zikapigwa marufuku, na nafasi yake kuchukuliwa na lugha ya Kiethiopia ya “Amhari”, kama lugha ya Taifa.
Kana kwamba hayo yalikuwa hayatoshi, mwaka 1962, Bunge la Eritrea lilishinikizwa kukubali kufutwa kwa Shirikisho, na Bunge hilo kulazimishwa kujifuta lenyewe ili Eritrea imezwe na Ethiopia. Kuanzia hapo, Eritrea ilihesabiwa na kupewa hadhi duni kama moja tu ya majimbo 13 ya Ethiopia.
Kwa miaka yote ya 1960, Serikali ya Haile Selasie ilikabaliwa na maasi pande zote. Kwa mfano, maasi ya Wa-Oromo katika Jimbo la Bale upande wa Kusini, yalidumu kwa miaka sita; nao Wasomali waasi wa Ogaden, waliunda Chama chao cha Ukombozi – “The West Somali Liberation Front” (WSLF) kuwafukuza Waethiopia Ogaden ili kurudisha Serikali ya Kisomali.
Huko Eritrea, vikundi vya wapiganaji wa msituni vilianzisha vita ya ukombozi ambapo Serikali ya Selasie ilitumia silaha nzito na ukatili mkubwa kujaribu kuizima. Ukatili huu ulidhalilisha utaifa wa Waeritrea, wakaapa kutorudi nyuma hadi uhuru upatikane.
Septemba 12, 1974, Mfalme Haile Selasie, alipinduliwa na Kanali Mengistu Haile Mariam, ambaye naye hakuweza kuzima vita ya ukombozi ya Wa-eritrea. Si hivyo tu, itikadi na sera zake za Ki-karl Marx/Ki-Lenin, zilimletea maasi mengine ya ndani na juu ya vita ya Eritrea, kufuatia zoezi lake la utaifishaji wa njia kuu za uchumi kwa kasi ya kutisha; kuanzia na Makampuni ya Bima na Mabenki (Januari 1975), Viwanda vikubwa na Makampuni ya biashara (Februari 1975), ambapo Machi 1975, alitaifisha ardhi yote na hivyo kuharibu kabisa nguvu za kiuchumi za utawala uliopita na masalia yake.
Kwa mfano, katika jimbo la Tigray, waasi waliunda Jeshi la ukombozi la “Tigray People’s Liberation Front” (TPLF) kwa msaada wa Wa-eritria.
Na huko Ethiopia ya Kusini, Wa-Oromo walikuwa na Jeshi la “Oromo Liberation Front” (OLF) likiungwa mkono na Wasomali, ambao nao walifufua Jeshi lao la ukombozi – “The Western Somali Liberation Front” (WSLF) ili kurejesha “ardhi yao iliyopotea”.
Hatimaye, Mei 1991, Kanali Mengistu Haile Mariam alizidiwa nguvu na muungano wa Majeshi ya waasi wa Eritrea na Tigray na kukimbilia uhamishoni.
Matokeo ya kura ya maoni iliyoitishwa Julai 1991 chini ya usimamizi wa Umoja wa Mataifa, kujadili hatima ya Eritrea, yaliwezesha Eritrea kurejeshewa uhuru kamili mwaka 1993, na hivyo kufunga ukurasa wa miaka 30 ya Vita kwa nchi hiyo.
Hatuwezi kuyapuuza malalamiko ya Wazanzibari juu ya uendeshaji wa Muungano wetu wenye kuzua kero. Kama ambavyo Serikali ya Ethiopia ilivyoutumia utengano wa Waeritrea milioni tatu kushinikiza mambo yake yasiyo ya Muungano, na hatimaye Eritrea kumezwa ndani ya Ethiopia; ndivyo nasi tulivyo na kila sababu ya kuhofu juu ya SUK, iwapo Wazanzibari wataungana na baadaye kutaka tafsiri sahihi ya Muundo wa Muungano wetu, ambao kwa muda mrefu, kero zake zimekosa utashi wa kuzitafutia ufumbuzi.
Na ingawa SUK haiwezi kuzua mtafaruku mkubwa kwa sasa kwa Muungano wetu kama ilivyokuwa kwa Ethiopia na Eritrea, lakini lazima tujiandae kwa mazingira mapya Visiwani chini ya SUK, ambayo kwa vyovyote vile, yatagusa mustakabali wa Muungano


Tusikubali kwenda serikali tatu. Kwa vile tumekatazwa kutaka kuvunja Muungano - japo waliotukataza hawana uwezo huo - na kwamba tunaweza kujadili "muundo" bora wa Muungano. Ninawasihi watu wa bara kudai "Serikali moja, taifa moja, na nchi moja". Haya mambo ya serikali mbili nchi mbili au serikali tatu nchi mbili hayaingii kichwani na ni jitihada za kujaribu kuibeba Zanzibar. Wakati umefika tudai uwepo wa serikali moja tu ya kitafa kwenye nchi moja.

Ninafahamu kabisa matokeo ya watu wa bara kutaka hili. Jambo pekee ambalo tusikubali kuuziwa (CCM na upiinzani wanataka hili) ni serikali tatu. Serikali tatu ni mzigo ambao hatuwezi kuubeba na wala hatupaswi kuubeba. Nawasihi wenzangu tukate kuongezewa mizigo. Tuwe na serikali moja, taifa moja na nchi moja. Sasa kama hili lina maana Zanzibar iwe "serikali moja, taifa moja na nchi moja" na bara iwe "serikali moja, taifa moja na nchi moja" basi na iwe.

Tuwasaidie Zanzibar watoke kwenye Muungano kama hawataki serikali moja kwani mbili hawataki na tatu tutajipa mzigo zaidi!

SAY NO TO SERIKALI TATU!!

Iambie tume ya Warioba - hatutaki serikali tatu!!
 
Kimsingi Muungano huu haukupaswa kuwa na serikali mbili kama zilivyo hivi. Ingawa kwa sasa tayari kuna mambo mengi sana yataleta mgogoro katika kuvunja au kuuendeleza muungano, kwa serikali mbili au tatu...chaguzi zote hizo ingawa sina matatizo yake, lakini ni afadhali tuamue kupambana na changamoto zitakazojitokeza kwa kufanya serikali MOJA ya nchi Moja ya Tanzania. TOSHA!!! Zanzibar iwe tu kisiwa ndani ya Tanzania chenye uongozi kama mikoa mingine tu huku Tanganyika.
Zanzibar ikijitenga kabisa, will make friends with Arabic world and Tanganyika will not be their best friend and (with all that they know about Tanganyika securitywise, etc, )
they can easily be ready to even betray Tanganyika for their own prosperity
Something worth fighting, worth facing its challenges ahead is only ONE COUNTRY, ONE GOVERNMENT, ONE PRESIDENT, ONE PEOPLE.

For the reasons of the same EGOCENTRIC SENTIMENTS (highlighted in red), zanzibaris will never accept THE ONE COUNTRY, ONE GOVERNMENT,ONE PRESIDENT DEVILISH, . Hapo hujatafuna maneno, the purpose is to contain (colonize?) Zanzibar for the security of Tanganyika. Sina tatizo na mawazo yako, hiyo ndio dhambi ya awali, hiyo ndio sababu ya muungano wenyewe miaka 48 iliyopita.
 
Mwanakijiji si kweli kwamba serikali tatu ni ghali kuliko serikali 2 tuliyo nayo sasa,
Chadema wakichukua nchi kutakuwa na mawaziri wa muungano wasiozidi watano (ulinzi, mambo ya nje, fedha, nimesahau nyingine) Kwa hiyo utakapokuwa na mawaziri 12 na manaibu mawaziri ni 24 na 10 wa Tanganyika = 34. Sasa linganisha mawaziri tulio nao. Just an example kwa kuwa hoja yetu ni lazima serikali iwe ndogo.

Pili, ukipunguza wizara maana yake unapunguza watumishi waliojazwa ktk wizara hizo. Mabilioni yanaokolewa.

Tatu, ukifuta (ukimerge mkuu wa wilaya na meya/mkurugenzi + wakuu wa mikoa) maana lazima mmoja aondoke kati yao, maana yake ume serve mabilioni mengi sana pia.
Kwa hiyo, pamoja na heshima zote nilizo nazo kwako, sikubaliani na hoja ya gharama pamoja na kuwa iliwahi pia kutumiwa pia na mtu ninayemheshimu sana ktk nchi late Mwl Nyerere.
kama hukubaliani na mimi lete calculation hapa.
 
Kwanza Mzee Mwanakijiji Muungano wa serekali tatu ni wazo la kinafiki kwa wasioutaka huo muungano kwa dhati kwani si tu gharama zitaongezeka bali tutakaribissha mivutano isiyokwisha na serekali ya muungano itakuwa inaelea tu juu kwa juu...

I support you kuwa muungano wa kweli ni wa serekali moja....lazima kila mmoja akubbali kupoteza autonomy ndiyo sacrifice ya muungano vinginevyo ni kichekesho cha serekali mbili kitaendelea....moja ya wote na nyingine ya wachache....Umefika mda watanganyika tuamke sasa na tusimamie hili...ama serekali moja au kila mtu akusanye kilicho chake
....

Kwani Wadanganyika mlikuwa mumelala!!!

Kumbukeni waswahili wanasema Alalae ... na ukimwamsha ....

Poleni sana

 
Nonda,
Moja ya hoja za Wazanzibar ni kuwa na serikali yao yenye mamlaka kamili. Kero za muungano hazipo ZNZ hata Tanganyika zipo. Kinachoudhi ni kitendo cha WZN kuona kuwa wanaonewa na wamekula koloni la Watanganyika.
Katika dunia ya sasa nchi kuwa koloni si jambo jema na hapo ndipo tunasema, basi ZNZ iondoke katika muungano halafu tukutane katika shirikisho la EA.

Huko kwenye shrikisho ZNZ haitabaki na mamlaka kamili. Ukishakubali kuwa na shirikisho tayari umekubali kuuza uhuru wako kwa shirikisho. Sijui kama Rwanda watakubali kutoa ajira kwa WZNZ wakati wznz hawatakuabali kutoa jaira kwa Warwanda. Sijui kama Tanganyika itaruhusu ardhi ya bwerere kwa wznz wakati Watanganyika hawana haki hiyo ZNZ.
Kwa lolote liwalo ZNZ haitaweza kubaki na mamlaka kamili kama inavyodhani. Ni kujidanganya.

Kwa vile WZNZ wanasema Nyerere Laanatullah(laana ya mwenyezi mungu iwe naye) na kwa vile wengi wanaamini yeye ndiye chimbuko la mapinduzi na muungano wa kuimeza ZNZ, hakuna hoja ya Nyerere itakayokuwa na mashiko kwa MZNZ hata kwa bahati mbaya. Nashangaa hata unamnukuu na sina uhakika swaumu yako itaswihi ,kwasababu Nyerere ni 'shetani' kwa Wazanzibar. Kwanini tujadili mawazo yake tusijadili yetu. Kwanini tumfikirie huyu 'shetani' kwa mustakabali wa nchi yetu ya ZNZ yenye waumini na binadamu kamili?

Kibaya zaidi ni chuki iliyojengwa na WZNZ dhidi ya Watanganyika. Sheria zote za kazi zinazowekwa, ardhi n.k hazimlengi raia mwingine isipokuwa Mtanganyika. Huku bara wapo raha mustarehe ingawa uvumilivu umekwisha na ni suala la muda tu watatimuliwa, watabaguliwa na watatendewa kama wanavyotenda.

Na kwa vile muungano huu hauna faida kwa ZNZ, swali linabaki pale pale, ni faida gani Mzanzibar anaitaraji ndani ya serikali 3 au mkataba? kwanini tusivunje muungano, nini ZNZ inaogopa?

Kinachosikistisha sana ni kuwa hoja za WZNZ hazina kichwa wala miguu. Soma makala ya Seif utabaini kuwa hana hoja ila kutapa tapa. Kama mnataka mamlaka kamili mtayapataje mkiwa katika mkataba au serikali 3?

Mimi nadhani kabla ya mtu kutamka serikali 3 lazima kwanza aangalie maana ya serikali 3, kazi za serikali 3 na uendeshaji wa serikali 3. Kama ni mkataba nao pia uangaliwe vivyo hivyo.

Kutamaka tu serikali 3 au mkataba ni kiwango cha chini sana cha elimu, kufikri ua kutafakari. Ni lazima watu waende zaidi ya hapo. Hadi sasa hakuna MZNZ aliyewahi kuja na proposal ya vitu hivyo ila wote wanaimba kibwagizo cha kwaya, tatu mkataba.

Narudia Zitto kabwe ametoa maoni yake juu ya serikali 3, hata kama sikubaliani na proposal yake ninamsifu kwa kuwa na kitu chenye mantiki (substance). Amejiweka tofauti na WZNZ wasioweza kusema lolote kuhusu wanachokidai.

Chuki kati ya Tanganyika na ZNZ sasa ni kubwa sana na kabla watu hawajaendelea kuchinjana (znz wameanza kwachinja Wabara) ni afadhali muungano uvunjike kila mtu ashughulikie matatizo yake.

Hamuwezi kuwa na ushirikiano na makafir ikiwa ninyi ni watu safi. Mkataba au serikali 3 utawaletea ushenzi, ujambazi, ubazazi n.k. Ninyi hampo tayari kwa kuwa ni taifa teule. Sisi hatupo tayari kubaguliwa kunyanyaswa na WZNZ.

Wakati umefika sasa tunawataka WZNZ waondoke warudi kwenye nchi ya asali na neema.
Wasipoondoka kwa amani tutawaondoa kwa hila. Tutafanya kile wanachofanya. Hili halinamjadala linasubiri wakati tu.

LET ZNZ GO!

Nguruvi3,

Ahali yangu umekuwa hodari sana wa kusukumia matatizo na malalamiko yako kwa waZnz na kusahau kabisa kuwa historia ndio inayokuhukumu. Mimi kama mtaaluma nakushauri sana soma historia yenu Tanganyika kwa uzuri sana utaliona nini unachokificha ambacho JKN aliwaokoa nacho.

Kumbuka kuwa Tanganyika imegubikwa na UNAFIKI na Znz ipo wazi ndio maana mchana kweupeeeee wanasema ubaya na madhara ya Muungano kwa mustakabali wa Taifa Lao.

Lakin unasahau kuwa Tanganyika hakuna Uzalendo. Kila mtu mlafi na yupo kwa maslahi binafsi jambo linalopelekea nchini mwenu kuongoza sio tu kwa ufisadi lakin hata dhulma.

Nafikiri kama utapitia historia za nchi hizo mbili za Tanganyika na Znz utaona wazi makutano yake ni membamba sana kuliko utando wa Buibui jambo ambalo viongozi hususan kutoka Bara wanalazimisha na kulinda utando huo wa buibui kwa gharama zote.

Nakupa pole.



 
Mkuu nguruvi3,

Unaionaje hiyo rai ya Mwalimu Nyerere ya kuwa na serikali mbili Tanzanaia? Serikali ya Tanganyika na serikali ya Zanzibar badala ya serikali ya Tanzania na serikali ya Zanzibar?

Nia ya mjadala/ mijadala hii sio lazima iwe Simba na Yanga. Bali ni kutafuta suluhisho( dawa mjarabu) ya usanii wetu(Muungano wetu). Hii dawa aliyoitoa Mwalimu itatibu matatizo sugu ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.
Itatatua tatizo la kuibebesha mzigo Tanganyika( Tzbara/ bara) na akina sisi tunaotaka kujinasibisha na utanganyika wetu tutatembea na kifua mbele, itamaliza kelele za washirazi(masultani,watwana,watumwa,Znz) na itakidhi tunu yetu ya umajumui wa kiafrika(pan-africanism) tuliyonayo; kuwa na nchi kubwa yenye members wengi, Kenya, Uganda, Tanganyika, Zanzibar, Rwanda na Burundi. Yaani nchi yetu itakuwa na wanachama 6. Bila shaka mfumo wake utakuwa mfumo wa shirikisho. Serikali 7, serikali za majimbo 6 na serikali ya shirikisho 1.

Au wewe unataka kubaki na mazingaombwe yaliyodumu kwa miaka 48 ambayo yanazalisha kero tu?

Tazama picha kubwa, usijikite kwenye masimulizi ya Jussa, Seif, Barubaru, Hizbu, ASP, Usultani,mapinduzi daima nk.

Tanabahisho.Litakapoundwa Shirikisho la Afrika Mashariki, utanzania utakufa, utaifa mpya utakuwa Uafrika Mashariki, lakini majina ya maeneo(territories) yatabaki.

Naomba wanajf, tuipokee hii rai, tuifikirie kwa utuo na kama tutaona itatusogeza mbele basi, kampeni ianze mara moja ya Tanzania yenye serikali mbili, ya Tanganyika na ya Zanzibar.

Atakapokuja Warioba na tume/kamati yake tudai, Tanzania yenye serikali ya Tanganyika na Serikali ya Zanzibar.
Tunaua dege bili kwa jiwe moja tu.

Soma post #88 hapo juu.

Nonda.

Moja ya matatizo yenu ni kuwa badala ya kuzungumzia mustakabali wa nchi yenu nje ya muungano na namna ya kurejesha utaifa wenu , Mumekuwa vinara wa kuwasamea waZnz na Znz kijumla.

Nakushauri itazame nchi yako nje ya muungano itakuwa namna gani? Nafikiri kengele imeshalia huko watu hawataki kuhisabiwa na mengine mengi ikiwa pamoja na kugundulika kwa uwepo wa Bakwata kwenye nchi isiyo na dini.

Nakushauri ONDOA BORITI KWENYE JICHO LAKO KABLA KUANGALIA LA MWENZIO.

Pole sana

 
Nonda.

Moja ya matatizo yenu ni kuwa badala ya kuzungumzia mustakabali wa nchi yenu nje ya muungano na namna ya kurejesha utaifa wenu , Mumekuwa vinara wa kuwasamea waZnz na Znz kijumla.

Nakushauri itazame nchi yako nje ya muungano itakuwa namna gani? Nafikiri kengele imeshalia huko watu hawataki kuhisabiwa na mengine mengi ikiwa pamoja na kugundulika kwa uwepo wa Bakwata kwenye nchi isiyo na dini.

Nakushauri ONDOA BORITI KWENYE JICHO LAKO KABLA KUANGALIA LA MWENZIO.Pole sana
Ahlan Baru baru, swaumu inaendeleaje sheikh.
Hapa hoja iliyopo si matatizo ya Tanganyika. Tanganyika kama taifa lina matatizo yake na hayo yanapaswa kushughukiwa na Watanganyika. Ni makubwa au madogo kiasi gani hilo ni tatizo la Watanganyika.
Hata ZNZ nao wanapaswa kushughulikia yao.

Kinachotuunganisha hapa ni muungano ambao ni kero na bughudha kwa WZNZ.
Hoja kubwa ya WZNZ waliounga mkono UAMSHO ni kuwa na taifa lao lenye mamlaka kamili.
Hili naliunga mkono kwasababu kuondoka kwa ZNZ kutatoa nafasi za kushughulikia matatizo ya Tanganyika kama nchi.

Kama unafuatilia kwa siku za karibuni kumekuwa na mabadiliko ya ghafla sana kwa wenzetu.
Wametupa jalalani hoja yao ya kuvunja muungano, wameshindwa kutumia vyombo vyao kuvunja muungano na wamegeuga kwa kasi ya ajabu sana kudai serikali 3 au mkataba.
Ninashangaa hata CUF ambao sasa twajaua ni Washirazi na wakazi walio wengi wa ZNZ, wakiongozwa na akina Maalim na Jusa nao pia wameitosa ajenda ya kuvunja muungano!

Kila MZNZ mke au mume kijana na mtoto wanaimba serikali 3 au mkataba. Wasichosema ni kuwa hivyo vitu tunavihitaji kwanini. Nimeweka maswali hapo juu hakuna anayejibu bali wote wanazungunguka na kuleta hadithi.

Ninarudia, utawezaje kuwa na mamlaka kamili ukiwa ndani ya mkataba au serikali 3?
Katika hayo mawili ni mambo gani mnadhani yawe ya mkataba au serikali 3?
Na mnadhani uendeshaji wa serikali 3 au mkataba uzingatie nini, kwa vipi na namna gani.

Ni ujinga uliotopea kuamaka asubuhi na kuandika au kusema serikali 3 au mkataba bila kufafanunua.
Nafahamu ugumu wa kuteteaa hoja hii maana hata Seif Mshirazi hakuweza, Ahmed Rajab mshirazi hawezi, kwa muimba kwaya atabaki na kibwagizo cha mkataba na 3.

Kwanini msirejee kwenye mkakati wenu wa awali wa kuvunja muungano.
Mbona Tanganyika hawababaiki na kusema muungano basi kila mtu aende zake!

Kiwewe cha serikali 3 au mkataba ni cha nini? Kwanini hamjibu hoja zinazohusu serikali 3 au mkataba manakimbilia hoja nje ya mada? Kuna siri gani msiotaka ijulikane kuhusu serikali 3 au mkataba mnabaki na maneno mawili 'serikali 3' mkataba?

Hebu tujikite hapa pa serikali 3 au mkataba, mtufahamishe nini hasa mnadhani kitatokea au kitokee kwa hilo. Tujikite hapa kwasababu ni dhahiri shahiri WZNZ wanatapa tapa hasa baada ya Tanganyika kusema enendeni kwa amani.
WZNZ wanatapa tapa, sasa tusaidiane nini siri ya serikali 3 au mkataba. WZNZ wametosa hoja ya kuvunja muungano! hawataki kuvunja muungano, wanautaka muungano kwa udi na uvumba! kibao kimegeuga but it is too late!

LET ZNZ GO! We have absolutely nothing to lose, we wish they could leave us today before Iftar

 
Ahlan Baru baru, swaumu inaendeleaje sheikh.
Hapa hoja iliyopo si matatizo ya Tanganyika. Tanganyika kama taifa lina matatizo yake na hayo yanapaswa kushughukiwa na Watanganyika. Ni makubwa au madogo kiasi gani hilo ni tatizo la Watanganyika.
Hata ZNZ nao wanapaswa kushughulikia yao.

Kinachotuunganisha hapa ni muungano ambao ni kero na bughudha kwa WZNZ.
Hoja kubwa ya WZNZ waliounga mkono UAMSHO ni kuwa na taifa lao lenye mamlaka kamili.
Hili naliunga mkono kwasababu kuondoka kwa ZNZ kutatoa nafasi za kushughulikia matatizo ya Tanganyika kama nchi.

Kama unafuatilia kwa siku za karibuni kumekuwa na mabadiliko ya ghafla sana kwa wenzetu.
Wametupa jalalani hoja yao ya kuvunja muungano, wameshindwa kutumia vyombo vyao kuvunja muungano na wamegeuga kwa kasi ya ajabu sana kudai serikali 3 au mkataba.
Ninashangaa hata CUF ambao sasa twajaua ni Washirazi na wakazi walio wengi wa ZNZ, wakiongozwa na akina Maalim na Jusa nao pia wameitosa ajenda ya kuvunja muungano!

Kila MZNZ mke au mume kijana na mtoto wanaimba serikali 3 au mkataba. Wasichosema ni kuwa hivyo vitu tunavihitaji kwanini. Nimeweka maswali hapo juu hakuna anayejibu bali wote wanazungunguka na kuleta hadithi.

Ninarudia, utawezaje kuwa na mamlaka kamili ukiwa ndani ya mkataba au serikali 3?
Katika hayo mawili ni mambo gani mnadhani yawe ya mkataba au serikali 3?
Na mnadhani uendeshaji wa serikali 3 au mkataba uzingatie nini, kwa vipi na namna gani.

Ni ujinga uliotopea kuamaka asubuhi na kuandika au kusema serikali 3 au mkataba bila kufafanunua.
Nafahamu ugumu wa kuteteaa hoja hii maana hata Seif Mshirazi hakuweza, Ahmed Rajab mshirazi hawezi, kwa muimba kwaya atabaki na kibwagizo cha mkataba na 3.

Kwanini msirejee kwenye mkakati wenu wa awali wa kuvunja muungano.
Mbona Tanganyika hawababaiki na kusema muungano basi kila mtu aende zake!

Kiwewe cha serikali 3 au mkataba ni cha nini? Kwanini hamjibu hoja zinazohusu serikali 3 au mkataba manakimbilia hoja nje ya mada? Kuna siri gani msiotaka ijulikane kuhusu serikali 3 au mkataba mnabaki na maneno mawili 'serikali 3' mkataba?

Hebu tujikite hapa pa serikali 3 au mkataba, mtufahamishe nini hasa mnadhani kitatokea au kitokee kwa hilo. Tujikite hapa kwasababu ni dhahiri shahiri WZNZ wanatapa tapa hasa baada ya Tanganyika kusema enendeni kwa amani.
WZNZ wanatapa tapa, sasa tusaidiane nini siri ya serikali 3 au mkataba. WZNZ wametosa hoja ya kuvunja muungano! hawataki kuvunja muungano, wanautaka muungano kwa udi na uvumba! kibao kimegeuga but it is too late!

LET ZNZ GO! We have absolutely nothing to lose, we wish they could leave us today before Iftar


Bw Nguruvi3

Taratibu usuje ukadondoka chini naona povu linakutoka...Kitu kimoja unajichanganya kuhusu maoni ya wznz kuhusu Muungano. Ukweli wa mambo waznz wa kawaida wameshachoka na huu muungano wa ulaghai na ujanja ujanja. Tatizo la wanasiasa wa tngka na znz wamebanwa nasheria ya usajili wa vyama kwamba hakuna chama kitakacho sajiliwa kikiwa na sera ya kuvunja muungano. Kikifanya hivyo maana yake ni kupoteza uhalali wa kuwa chama cha siasa.

Kwahiyo maoni ya vyama vya siasa yanaishia kwenye serikali 2(mkataba) au tatu . Hii ni kwa sababu tu za kisiasa ,lakini hao watu wengi wao hawataki kabisa muungano . Sisi (mimi) tunaunga mkono Uamsho kwasababu wako wazi na hakuna sheria inayowabana kutamka hadharani kuukataa muungano. Kwahiyo hivi sasa kundi la Uamsho limekuwa na nguvu kubwa ya kiushawishi kuliko chama chochote cha siasa ZNZ.

Kabla ya kuanza kuwafanyia hila hao wznz wanaishi Tanganyka mungekuwa na utaratibu mzuri wa kuwaondosha wa tngka wanaishi ZNZ kwasababu wengi wao ni masikini zaidi ya wznz wanaishi tngka.

LET ZNZ GO!
 
Bw Nguruvi3

Taratibu usuje ukadondoka chini naona povu linakutoka...Kitu kimoja unajichanganya kuhusu maoni ya wznz kuhusu Muungano. Ukweli wa mambo waznz wa kawaida wameshachoka na huu muungano wa ulaghai na ujanja ujanja. Tatizo la wanasiasa wa tngka na znz wamebanwa nasheria ya usajili wa vyama kwamba hakuna chama kitakacho sajiliwa kikiwa na sera ya kuvunja muungano. Kikifanya hivyo maana yake ni kupoteza uhalali wa kuwa chama cha siasa.

Kwahiyo maoni ya vyama vya siasa yanaishia kwenye serikali 2(mkataba) au tatu . Hii ni kwa sababu tu za kisiasa ,lakini hao watu wengi wao hawataki kabisa muungano . Sisi (mimi) tunaunga mkono Uamsho kwasababu wako wazi na hakuna sheria inayowabana kutamka hadharani kuukataa muungano. Kwahiyo hivi sasa kundi la Uamsho limekuwa na nguvu kubwa ya kiushawishi kuliko chama chochote cha siasa ZNZ.

Kabla ya kuanza kuwafanyia hila hao wznz wanaishi Tanganyka mungekuwa na utaratibu mzuri wa kuwaondosha wa tngka wanaishi ZNZ kwasababu wengi wao ni masikini zaidi ya wznz wanaishi tngka.LET ZNZ GO!
Watanganyika wanaoishi ZNZ ni wangapi sheikh na wao kama wataamua kubaki huko hiayari yao, lakini sidhani kuwa wanafiki 1000.

Mimi nawaunga mkono UAMSHO na WZNZ wanapaswa kuwaunga mkono UAMSHO. Njia bora ya kuwaunga mkono ni kuacha kuongelea serikali 3 au mkataba. Hadi hapo kutakuwa hakuna chaguo ila kuvunja muungano.

Kuhusu vyama vya siasa na usajili hilo si kweli kwasababu ZNZ ina BLW. Kuna CUF na CCM, kuna Spika kuna mwanasheria mkuu, wana bendera na wimbo wa taifa, mahakama kuu. Hakuna mtu yoyote yule aliyejaribu kufikisha mswada wa kuvunja muungano kwa njia za kisheria kama walivyoleta mswada wa GNU au mabadiliko ya katiba.

Nani aliwazuia WZN Kuanzisha SUK au kubadili katiba yao? Jusa hajawahi kushtakiwa kwa kusema anachodhani ni sahihi.
Wazanzibar wanatumia mwanya tu kukwepa ukweli kuwa hawataki kuvunja muungano.

Ndiyo maana leo tunasikia serikali 3 au mkataba. Sasa kama hutaki muungano unataka serikali 3 au makataba wa nini.
Sisi Tanganyika tumeshaona hatuna manufaa na huu muungano na sasa hatutaki serikali 2, 3 au mkataba tunataka ZNZ iondoke zake kwa amani.

Tusaidieni basi ili tuvunje hili dudu kwa amani kwa kukaa kimya ili asijetokea mtu na kusema upo uwezekano ABC.


LET ZNZ GO!
 
Mwanakijiji si kweli kwamba serikali tatu ni ghali kuliko serikali 2 tuliyo nayo sasa,
Chadema wakichukua nchi kutakuwa na mawaziri wa muungano wasiozidi watano (ulinzi, mambo ya nje, fedha, nimesahau nyingine) Kwa hiyo utakapokuwa na mawaziri 12 na manaibu mawaziri ni 24 na 10 wa Tanganyika = 34. Sasa linganisha mawaziri tulio nao. Just an example kwa kuwa hoja yetu ni lazima serikali iwe ndogo.

Pili, ukipunguza wizara maana yake unapunguza watumishi waliojazwa ktk wizara hizo. Mabilioni yanaokolewa.

Tatu, ukifuta (ukimerge mkuu wa wilaya na meya/mkurugenzi + wakuu wa mikoa) maana lazima mmoja aondoke kati yao, maana yake ume serve mabilioni mengi sana pia.
Kwa hiyo, pamoja na heshima zote nilizo nazo kwako, sikubaliani na hoja ya gharama pamoja na kuwa iliwahi pia kutumiwa pia na mtu ninayemheshimu sana ktk nchi late Mwl Nyerere.
kama hukubaliani na mimi lete calculation hapa.

Aweda,

..kuna gharama za kuwepo kwa bunge la muungano ambalo hauja-account for.

..hivi unajua kabla ya mapinduzi na muungano ZNZ ilikuwa na wabunge wangapi?

..binafsi nina hakika walikuwa hawazidi 50. sasa hebu jiulize leo ZNZ wana wawakilishi wangapi na wabunge wangapi?

..pia wa-ZNZ wanataka mamlaka kamili katika masuala ya mambo ya nje, fedha na sarafu, ulinzi[raisi ambaye ni amiri jeshi mkuu], mafuta etc. wameeleza bayana kwamba wanataka mamlaka kamili ya kuamua mambo yao.

..kwanini CDM mnajaribu kuwaletea longolongo la serikali 3?? waZNZ wamesema wanataka waachwe wampumue!!

..sisi wengine tunaamini tutaokoa gharama kubwa zaidi ikiwa Tanganyika na Zanzibar zitakuwa ni nchi/dola tofauti zinazoshirikiana kupitia EAC au SADC.

..labda ungetueleza faida za kuwa na serikali 3 vs Tanganyika na ZNZ kuwa separate ni zipi?
 
Ahlan Baru baru, swaumu inaendeleaje sheikh.
Hapa hoja iliyopo si matatizo ya Tanganyika. Tanganyika kama taifa lina matatizo yake na hayo yanapaswa kushughukiwa na Watanganyika. Ni makubwa au madogo kiasi gani hilo ni tatizo la Watanganyika.
Hata ZNZ nao wanapaswa kushughulikia yao.

Kinachotuunganisha hapa ni muungano ambao ni kero na bughudha kwa WZNZ.
Hoja kubwa ya WZNZ waliounga mkono UAMSHO ni kuwa na taifa lao lenye mamlaka kamili.
Hili naliunga mkono kwasababu kuondoka kwa ZNZ kutatoa nafasi za kushughulikia matatizo ya Tanganyika kama nchi.

Kama unafuatilia kwa siku za karibuni kumekuwa na mabadiliko ya ghafla sana kwa wenzetu.
Wametupa jalalani hoja yao ya kuvunja muungano, wameshindwa kutumia vyombo vyao kuvunja muungano na wamegeuga kwa kasi ya ajabu sana kudai serikali 3 au mkataba.
Ninashangaa hata CUF ambao sasa twajaua ni Washirazi na wakazi walio wengi wa ZNZ, wakiongozwa na akina Maalim na Jusa nao pia wameitosa ajenda ya kuvunja muungano!

Kila MZNZ mke au mume kijana na mtoto wanaimba serikali 3 au mkataba. Wasichosema ni kuwa hivyo vitu tunavihitaji kwanini. Nimeweka maswali hapo juu hakuna anayejibu bali wote wanazungunguka na kuleta hadithi.

Ninarudia, utawezaje kuwa na mamlaka kamili ukiwa ndani ya mkataba au serikali 3?
Katika hayo mawili ni mambo gani mnadhani yawe ya mkataba au serikali 3?
Na mnadhani uendeshaji wa serikali 3 au mkataba uzingatie nini, kwa vipi na namna gani.

Ni ujinga uliotopea kuamaka asubuhi na kuandika au kusema serikali 3 au mkataba bila kufafanunua.
Nafahamu ugumu wa kuteteaa hoja hii maana hata Seif Mshirazi hakuweza, Ahmed Rajab mshirazi hawezi, kwa muimba kwaya atabaki na kibwagizo cha mkataba na 3.

Kwanini msirejee kwenye mkakati wenu wa awali wa kuvunja muungano.
Mbona Tanganyika hawababaiki na kusema muungano basi kila mtu aende zake!

Kiwewe cha serikali 3 au mkataba ni cha nini? Kwanini hamjibu hoja zinazohusu serikali 3 au mkataba manakimbilia hoja nje ya mada? Kuna siri gani msiotaka ijulikane kuhusu serikali 3 au mkataba mnabaki na maneno mawili 'serikali 3' mkataba?

Hebu tujikite hapa pa serikali 3 au mkataba, mtufahamishe nini hasa mnadhani kitatokea au kitokee kwa hilo. Tujikite hapa kwasababu ni dhahiri shahiri WZNZ wanatapa tapa hasa baada ya Tanganyika kusema enendeni kwa amani.
WZNZ wanatapa tapa, sasa tusaidiane nini siri ya serikali 3 au mkataba. WZNZ wametosa hoja ya kuvunja muungano! hawataki kuvunja muungano, wanautaka muungano kwa udi na uvumba! kibao kimegeuga but it is too late!

LET ZNZ GO! We have absolutely nothing to lose, we wish they could leave us today before Iftar

Nguruvi3,

Ahlan wa sahalan.

Ahali yangu kila wakti unakuwa mtu wa kulalama zaidi na kujaribu kusukuma makosa kwa waZnz na kuisahau nafsi yako na wenzako wa tanganyika.

Nashangaa zaidi unaposema waZnz wanataka Serikali tatu au zaidi au pungufu ya hizo. Kumbuka hayo ni maoni ya watu binafsi tu wana haki ya kusema lolote walitakalo. Lakin kumbuka kilio chao kikuu ni kuifanya Znz iwe Doula huru na yenye mamlaka kamili katika Muungano wenu. Hilo lipo wazi dhahir wa shahir. Halina ubishi na wala halikwepeki. Limezungumzwa Barazani (BLW) bila kificho wala kumung'unya maneno.

Na kama utakuwa mpenda haki na msema kweli. Rejea kwenye muungano wenu uone kuwa ulipitishwa na Bunge la Muungano na wala sio BLW. Kwa mantiki hiyo mwenye mamlaka ya mwisho wa kuvunja muungano huo ni Bunge la Muungano na sio BLW. tazama kwenye Bunge la Muungano waZnz ni chini ya 30% tu waliobaki wote ni wa TNG. Sasa ni kitu cha kushawishi tu Bunge lijadili hilo kama walivyojaribu wakti ule wa kudai Serikali huru ya Tanganyika na kuunda G57.
Mimi naamini wazi kama watanganyika wataacha UNAFIKI na UOGA wana nafasi kubwa na pana sana kuzungumzia huu Mvungano wenu. Na kama Znz wangepewa Rungu hilo nafikiri saa hizi mngekuwa mnazungumzia mengine. Kwani siku zote waZnz wana uthubutu na uwezo mkubwa bila woga kuzungumzia mustakabali wa Taifa lao katika Muungano na maslahi ya nchi yao.

Kama mchambuzi wa mambo ya historia nafikiri ungejikita zaidi kuona Ni vipi tanganyika mtaishi nje a muungano wenu. Kwani kuna mengi sana ambayo mlijaribu kwa nguvu zote kuyaficha ambapo sasa yapo dhahir na yanahatarishi mustakabali wa Tanganyika kama taifa mfu ambayo Znz inayapooza kwa muonekano wake.

Nakushauri usijikite kwenye maoni ya watu binafsi bali jikite kwenye ukweli unasemaje. Kila mtu ana haki ya kutoa maoni lakin ukweli huwa haupindiki na siku zote na saa zote unasimama. maoni ya mtu mmoja mmoja usichukulie ndio msimamo wa jamii nzima.
Namaliza kwa kusema ondoa boriti kwenye jicho lako kabla kuliangalia la mwenzako.



 
hapa nilitaka nibainishe kidogo kuhusu suala la kuwafukuza raia pindi muungano wenu ukivunjika.

Naomba mtambue kwamba nyie hamtakuwa wa kwanza kuvunja muungano Duniani. Hata EAC ilivunjika na kuliwekwa taratibu maalum za raia wa kila nchi kuweza kurejea makwao. Na wale waliokuwa wamewekeza vile vile kuna taratibu za kimataifa za uhamiaji na hata zile za kulinda mali za raia pindi muungano unapovunjika.

Ikumbukwe kuwa kuvunja muungano sio uadui. Kwani watu watatumia taratibu za kimataifa za uhamiaji kutembelea au kuishi nchi za nje. Na hilo lipo wazi kabisa.

Mfano mzuri ni mimi ambaye nilikuwa Mtanzania kwa kuzaliwa na nilikuwa raia wa Tanzania. sasa hivi ni raia wa Oman (nimetumia uraia wa kurithi toka kwa wazazi wangu wote wawili) nimeukana uTz lakin kwa kutumia taratibu za Uhamiaji kila siku nikiamua nakuja Tanzania kuona ndugu, jamaa na marafiki zangu na vile vile kuwekeza kama muwekezaji wa kigeni.

Naomba msitie hofu kwa isshu za kufukuzana kama wengi wanavyojaribu kutisha wengine.
 
Back
Top Bottom