Muungano: Maalim Seif aipa tume ya jaji Warioba masharti

Muungano: Maalim Seif aipa tume ya jaji Warioba masharti

Nguruvi3

Platinum Member
Joined
Jun 21, 2010
Posts
15,773
Reaction score
32,431
Chanzo cha habari hii ni kutoka katika gazeti la Habari leo
(http://www.habarileo.co.tz/index.php/habari-za-kitaifa/12645-makamu-wa-rais-atikisa-muungano)

Makamu wa Rais wa Zanzibar bw Seif Sharif Hamada ametoa masharti ya mambo 10 yanayopaswa kuondolewa katika mambo ya muungano. Amesema tume ya maridhiano ya Wazanzibar imeamua yafuatayo yasiwe ndani ya katiba mpya.
Ufuatao ni muhtasari wa habari hiyo

1.Zanzibar kuwa na uraia
2.Kubadili jina la muungano kutoka Jamhuri ya watu wa Tanzania na kuwa muungano wa Jamhuri za Tanzania
3.Znz kuwa na sarafu yake na benki kuu yake
4.Zanzibar kuwa na ushirika wa mambo ya kimataifa pekee
5.Zanzibar kuwa na baraza lake la mitihani
6.Kuwa na jeshi lake la Polisi
7.Kuwa na mamlaka zake za kodi zisizofungamana na upande mwingine
8.Usajili wa vyama vya siasa kila upande usiotegemeana
9.Hati za kusafiria
10. Bendera ya znz kule New York, Adis Ababa na Commonwealth.


Maalim ametoa masharti kuwa katiba mpya lazima iwe na marekebisho makubwa katika mambo ya muungano.
Amesema Wazanzibar wataiangalia rasimu ya katiba kwa masharti yaliyotolewa na tume ya maridhiano
.

My take:
Maalim seif sina hana uelewa wa kile anachozungumzia. Kama anao,atakuwa anafahamu kuwa hadhra''audience'' yake haina uelewa na anaweza kuongea atakavyo na kupigiwa makofi.

Kwanza, Maalim Seif lazima atambue katiba ni chombo cha umma na si kwa ajili ya kundi au sehemu moja ya jamii.
kusema anaweka masharti ni dharau kwa wananchi wa Taifa hili.

Pili,tume ya Jaji Warioba ilipoundwa(wengine tulikataa), maalim na wabunge wake wa CUF waliridhia na chama chake kuwa sehemu ya wajumbe wa tume
Alikubalina na taratibu zilizopo na hawezi kuiwekea masharti tume alioridhia kwa kila hali.

Tatu, tume ya maridhiano ya wzn haina nguvu za kisheria.Kama ina nguvu zinaishia huko visiwani.
Haina mamlaka ya kuzungumza kama au Watanganyika hivyo maoni ya tume yanabaki kuwa maoni ya maskani au vijiweni.

Nne,Kubadili jina la JMT kuwa muungano wa jamhuri za Tanzania. Ni dhahiri anautaka muungano kwa kujificha.
Uwepo wa uraia na hati za kusafiria za znz hauna sababu za kuwa na Muungano wa Jamhuri za Tanzania anazodai.

Tano;Kuondoa jeshi la Polisi katika muungano.Polisi ni sehemu ya majeshi ya ulinzi na usalama yenye Amir jeshi mkuu mmoja tu.

Laukana anataka ulinzi na usalama viondolewe, Seif asema Jeshi na Polisi viondolewe ili kuwa na dola kamili.
Jeshi la Tanzania lina Amir jeshi mmoja tu ambaye ni wa majeshi ya ulinzi na usalama ikiwemo Polisi.

Sita,Baraza la mitihani la znz. Hilo limeshafanyika. Anachopaswa kufanya ni kuwashawishi wajumbe wa znz ndani ya NECTA kujitoa
Atake wizara ya elimu ya juu iondolewe pia

Saba, Mafuta na gesi, vimeshaondolewa kwa kutumia BLW.Mafuta yanachimbwa ardhini,hivyo anapaswa kutamka kuwa Ardhi isiwe katika muungano. Na ili kulinda mafuta na ajira zitokanazo, Maalim aseme kuwa ajira na shughuli za utumishi ziondolewe katika muungano.

Nane,Mamlaka za kukusanya kodi zipo znz (TRA na ZRA) Ushahidi upo mapato ya TRA yanabaki huko.
Znz inapokea pesa za bure kwa kupitia ofisi ya makamu wa Rais wa JMT(Mwaka huu bilioni 32).
Anapaswa azikatae kwanza kabla ya kuongelea mamlaka za kodi.

Tisa,Bendera ya JMT haimpendezi, Seif anatakiwa aache kutumia kitu chenye nembo ya JMT asiyotaka

Kumi, Maalim anapaswa kuwaeleza watu kuhusu mgao wa BoT znz inayoupata.
Na aangalie pengo la bajeti ya znz linavyozibwa na pesa za Muungano.

Kumi na moja,Uraia na hati za kusafiri na mambo ya nje,kwanza awaamuru wznz walioko bara akiwemo makamu wa Rais waache warudi kwenye Uraia. Arudishe kile kitambulisho cha JMT alichochukua Karimjee chini ya jina la JMT

Kumi na mbili,Vyama vya siasa, Maalim alikuwa Morogoro kuzindua kampeni za chama chake juzi.
Ili awe serious na anachosema tunamtaka apige marufu kukanyaga Tanganyika katika mambo ya kisiasa.

Madai ya Seif ni wazi anataka kuvunja muungano. Upo umuhimu wa kumsaidia afikie malengo yake ya kisiasa

kwanza, aache kuogopa kutamka 'vunja muungano''.Adai znz huru bila mkataba au kujibanza katika baadhi ya maeneo

Pili,Apige marufuku wabunge wa kiliberali(CUF) wasije Dodoma na wafanyakazi wa serikali ya muungano waondoke

Tatu,apeleke mswada wa kunja muungano BLW na BLM yeye akiwa makamu wa Rais kwa kushirikiana na Rais ambaye ni mwenyekiti wa baraza la mapinduzi

Nne,amshauri Rais ili kauli zake ziwe za SMZ na si za viunga vya minazi.

Muhimu:Maalimu aheshimu maoni ya wananchi juu ya katiba hana sababu za kuifanya ZNZ iweke masharti ya kisiasa kwa Tanzania.

Maalim aseme kama ni msemaji wa SMZ, kuongelea katika viunga vya minazi hakutaleta suluhu.

Maalim Watanganyika hawapo tayari kuburuzwa na wazanzibar kwa makundi au watu wa nje.
Tanganyika si sehemu na haijawahi kuwa sehemu ya sultan na haitakuwa sehemu ya Sultan

cc. Mwanakijiji, JokaKuu, Jasusi, Mag3, Wickama, Mkandara,EMT,Kichuguu,Mchambuzi,Kigwangalla, Zitto, Jusa,Tundu Lisu, AshaDii, Prishaz,Ngongo, Ms Judith, Ghibuu, Barubaru,Ngambo,Nonda, Ngali,Mwalimu,Nape,Bongolander,Invisible,Mwakalinga Y.R,
Watanganyika na Wanajamvi wote
 
Nguruvi3 nimesoma haraka haraka nawahi kanisani, ila naunga mkono kila harakati za Wazanzibar kurahisisha kuuvunja muungano huu wa kijinga na kipuuzi.

Sijaelewa bado Watanganyika ni kwa nini tunaung,ang,ania Muungano huu wa kipuuzi wakati Wazanzibar hawautaki, nashawishika kwa kila hali kuona viongozi wa CCM Tanganyika ndio wanufaikaji wa Muungano huu.
 
Last edited by a moderator:
Mtoa mada naona unazunguka mbuyu tu,kilicho semwa na seif ni matakwa ya waz'br 66% kwenye tume ya warioba ww unasema eti matakwa ya maskani kijiweni,unachotakiwa kusema hapa ni nini matakwa ya watanganyika kwenye muungano na sio kulaumu maoni ya waz'br,ile tume ya maridhiano ni ya waz'br na mambo kumi yale ndio matakwa ya wazbr.
 
Maalim seif ni kirusi hatari sana kilichojaa nyongo ya unafiki ndani yake!wazanzibar wajiulize what next baada ya Maalim seif kushinikiza muungano uvunjike?wajinga ndo waliwao na madevu yao,kwanza ni bora kubeba gunia la misumari kuliko kuendelea kuwakumbatia hao wasiokuwa na shukrani akina yakhe!
 
Maalim Seif ana hoja za msingi. Mimi sioni sababu ya Watanganyika kutoona haja ya kuzungumzia masuala ya Muungano ili hali sisi tunaoishi Zanzibar tunaona dhahiri tunavyobaguliwa na kuwekewa pingamizi sizizo na maana unapotaka kufanya mambo mbalimbali kama raia wa Tanzania.Huku Watanganyika tunaonekana wageni na wanyonyaji.
 
Nakubaliana na wewe kuhusu huu muungano wa Tanganyika na Zanzibari kuna ajenda ya SIRI kubwa sana ambayo CCM wanaijua na hawataki wadanganyika tuijue.
 
Nikweli mkuu, Maalim anatakiwa atoe kauli halali za Kiserikali sio za kwenye mikutano ya CUF, kama kweli anautaka huo muungao autakao yeye. Lasivyo anakuwa bonge la Mnafki.
 
I Think kama wanataka kuuvunja muungano sawa tuh,ila sasa kama wanaamua kutoka basi watoke moja kwa moja,

Naunga mkono inawezekana kuna vitu vya msingi ambavyo wao wanahis wanavimis kwa kuwa ndan ya muungano huu,kwa mantiq hiyo basi yanapotokea majadiliano,wao wayaseme matakwa yao wazi wazi na bila kuchagua kuegemea kwenye urahis watakaoupata kutoka kwetu,

Kama watafikiria kujitoa basi watambue kwa yale mambo yanayowanufaisha kutoka upande wetu watanganyika nayo yapaswa wajiotoe na hayo pia,

Wasiwe selective,kwa kuwa wao ndio wameona huu muungano unawabana...


Nasisi watanganika hakuna haja ya kuwang'ang'ania wazanzibar kama tumeona wamechoka na sisi tumeyaweka mambo yetu ya msingi ambayo tunataka nao wasinufaike nayo...
 
Maalim seif ni kirusi hatari sana kilichojaa nyongo ya unafiki ndani yake!wazanzibar wajiulize what next baada ya Maalim seif kushinikiza muungano uvunjike?wajinga ndo waliwao na madevu yao,kwanza ni bora kubeba gunia la misumari kuliko kuendelea kuwakumbatia hao wasiokuwa na shukrani akina yakhe!

Jiulize vipi ilikuwa zanzibar kabla ya muungano.
 
Nikweli mkuu, Maalim anatakiwa atoe kauli halali za Kiserikali sio za kwenye mikutano ya CUF, kama kweli anautaka huo muungao autakao yeye. Lasivyo anakuwa bonge la Mnafki.

C matakwa ya maalim ni matakwa ya waz'br,na ndio maoni ya waz'br yaliyotolewa kwenye tume ya warioba.
 
I Think kama wanataka kuuvunja muungano sawa tuh,ila sasa kama wanaamua kutoka basi watoke moja kwa moja,

Naunga mkono inawezekana kuna vitu vya msingi ambavyo wao wanahis wanavimis kwa kuwa ndan ya muungano huu,kwa mantiq hiyo basi yanapotokea majadiliano,wao wayaseme matakwa yao wazi wazi na bila kuchagua kuegemea kwenye urahis watakaoupata kutoka kwetu,

Kama watafikiria kujitoa basi watambue kwa yale mambo yanayowanufaisha kutoka upande wetu watanganyika nayo yapaswa wajiotoe na hayo pia,

Wasiwe selective,kwa kuwa wao ndio wameona huu muungano unawabana...


Nasisi watanganika hakuna haja ya kuwang'ang'ania wazanzibar kama tumeona wamechoka na sisi tumeyaweka mambo yetu ya msingi ambayo tunataka nao wasinufaike nayo...
Exactly!
 
Kama hayo mambo 10 ndio matakwa ya wazanzibar basi muungano ufe, sikubaliani na hoja mtoa mada anazunguka ila seif/wazanzibar wanazunguka waseme hawataki muungano, Mia.

Kama muungano ufe basi maoni yako hayo ilikuwa uyapeleke kwa warioba,
 
Kama hayo mambo 10 ndio matakwa ya wazanzibar basi muungano ufe, sikubaliani na hoja mtoa mada anazunguka ila seif/wazanzibar wanazunguka waseme hawataki muungano, Mia.

Kama muungano ufe basi maoni yako hayo ilikuwa uyapeleke kwa warioba,maoni ya waz'br hayawezi kuwa sawa na ya watanganyika.
 
Kama hayo mambo 10 ndio matakwa ya wazanzibar basi muungano ufe, sikubaliani na hoja mtoa mada anazunguka ila seif/wazanzibar wanazunguka waseme hawataki muungano, Mia.
Hapa naomba usome tena kwa utulivu. Sijazunguka, msome The Big show ameeleza kwa ufasaha nilichokusudia.

Hakuna anayetaka kung'ang'ania znz. Lakini basi znz isijibanze kwa kuchagua mambo.
Hivi anatakaje awe na jeshi la Polisi na wala si Jeshi la ulinzi na usalama. Kwanini asikatae JWT

Kwanini asiseme ardhi siyo sehemu ya mambo ya muungano lakini gesi na mafuta amesema.

Kwavile anataka kuvunja muungano, je anataka muungano wa Jamhuri za Tanzania kwa mambo gani.
 
Kama muungano ufe basi maoni yako hayo ilikuwa uyapeleke kwa warioba,maoni ya waz'br hayawezi kuwa sawa na ya watanganyika.
Watanganyika wametoa maoni, waznz wametoa maoni.

Naomba usome habari katika link hiyo hapo juu. Makamu wa Rais Idd Seif amekataa na kusema wazi kuwa wazanzibar wanafaidika na muungano. Shein aliwahi kusema hayo.

Hakuna sababu maoni ya wazanzibar ndiyo yaunde katiba ya JMT. Kwanini wanaweka masharti ili hali tunajua kuwa wapo wazn akiwemo Seif Idd hawakubaliani na Maalim Seif? Je, wznz wapi unaongelea.

The bottom line ni kuwa Seif Hamad asishinikize maoni yake yenye kiu zake za kisiasa kuwa maoni ya wananchi.
Mimi ni mmoja wa wale wanaosema let znz go! lakini itokee hivyo kwa wznz na si kundi au mtu aliyetumwa eti aweke masharti kwa tume ya Warioba. Who is he by the way.
 
Maalim Seif ana hoja za msingi. Mimi sioni sababu ya Watanganyika kutoona haja ya kuzungumzia masuala ya Muungano ili hali sisi tunaoishi Zanzibar tunaona dhahiri tunavyobaguliwa na kuwekewa pingamizi sizizo na maana unapotaka kufanya mambo mbalimbali kama raia wa Tanzania.Huku Watanganyika tunaonekana wageni na wanyonyaji.
Pingamizi kama zipi.
 
Nguruvi3 nimesoma haraka haraka nawahi kanisani, ila naunga mkono kila harakati za Wazanzibar kurahisisha kuuvunja muungano huu wa kijinga na kipuuzi.

Sijaelewa bado Watanganyika ni kwa nini tunaung,ang,ania Muungano huu wa kipuuzi wakati Wazanzibar hawautaki, nashawishika kwa kila hali kuona viongozi wa CCM Tanganyika ndio wanufaikaji wa Muungano huu.
Matola, tumeunga mkono sana na hata kuwapa mbinu za kujitoa. Wao hawataki wanataka mkataba.
Sasa hivi hata mkataba hawataki wanachagua nini cha muungano nini kisiwe. Hapo ndipo hoja ilipo.

Je, Watanganyika huu si muda muafaka wa kuwasaidia kuondoa kila kitu katika muungano ili wawe huru na dola huru!
Wanachokitaka kiwe cha muungano hakitusaidii sisi, sasa kwanini tukubaliane na matakwa yao na si yetu
 
Back
Top Bottom