Muungano: Maalim Seif aipa tume ya jaji Warioba masharti

Muungano: Maalim Seif aipa tume ya jaji Warioba masharti

Mimi nawashangaa mnaong'ang'ania Muungano. Tuwaunge mkono Wazanzibari waende zao haraka sana. Tudai na sisi Tanganyika yetu badala ya kukimbizana na kivuli cha Wazanzibari. Kwa hili nawaunga mkono Waliberali 100%
 
Nadhani hakuna mtu anayeweza kupinga muungano kwa maana ya neno na nia ya tendo lenyewe. lakini mtu anaweza kupinga Muungano wa tanganyika na Zanzibarau au muungano mwingine kwa mantiki ya muudo na faida zake kwa kila upande. Ikiwa kama hilo la kuukataa muungano litatokea Watanganyika tuwaachie wazanzibari waamue sisi tukae kimya na uamuzi wowote watakaoamua kama ni kuuvunja au kuendelea nao tuukubali nasi tutabaki salama kama alivokwisha sema mwalimu.
 
Kuna kitu Zanzibar hawakielewi, ila woga wao wa kujitegemea unawafanya kuendelea kung'ang'ania vitu.
Ni hivi, sisi hatutaki aina yoyote na muungano nao, hivyo waituambie habari za Muungani, sisi hatutaki kabisa kuwepo na muungano, na maadam wao wameamua kujitoa na kubeba hilo bango la kujitoa, basi wajitoe jumla badala ya kuleta aina za miungano mezani.
Wanang'ang'ania nini kuwa na sisi, mpaka wanaa kutuletea aina za miungano....wanaogopa ku-stand alone? basi waache kelele.
 
Bahati mbaya upande wetu Tanganyika hakuna hata kiongozi mmoja anaweza kujitokeza wazi na kuyasema kama Mtanganyika nao wanaitaji nini katika huu muungano huu kama uendelee huwe wa aina gani na kama uvunjwe kila nchi ibaki na kwake.
Makamu wa Rais wa Zanzibar bw Seif Sharif Hamada ametoa masharti ya mambo 10 yanayopaswa kuondolewa katika mambo ya muungano. Amesema tume ya maridhiano ya Wazanzibar imeamua yafuatayo yasiwe ndani ya katiba mpya.
Ufuatao ni muhtasari wa habari hiyo

1.Zanzibar kuwa na uraia
2.Kubadili jina la muungano kutoka Jamhuri ya watu wa Tanzania na kuwa muungano wa Jamhuri za Tanzania
3.Znz kuwa na sarafu yake na benki kuu yake
4.Zanzibar kuwa na ushirika wa mambo ya kimataifa pekee
5.Zanzibar kuwa na baraza lake la mitihani
6.Kuwa na jeshi lake la Polisi
7.Kuwa na mamlaka zake za kodi zisizofungamana na upande mwingine
8.Usajili wa vyama vya siasa kila upande usiotegemeana
9.Hati za kusafiria
10. Bendera ya znz kule New York, Adis Ababa na Commonwealth.


Maalim ametoa masharti kuwa katiba mpya lazima iwe na marekebisho makubwa katika mambo ya muungano.
Amesema Wazanzibar wataiangalia rasimu ya katiba kwa masharti yaliyotolewa na tume ya maridhiano
.
Hapa Seif anatetea nchi yake iwe kamili mimi binafsi naungana naye amekuwa muwazi zaidi tatizo kwetu Tanganyika kwa nini viongozi wetu wanawalazimisha watu wa nchi ingine kuungana, viongozi wetu wana maslahi gani ni huu muungano mbona hawasema wapo kimya tu huku wakitumia nguvu nyingi kuulinda.
 
huyo ndo simbaaa.. maalim seif sio wewe jingakubwa..... ndo mwenyewake mzanzibari halisi anaebura milioni kibao nyinyi.... wewe kasirikaaaaaa.. ukisha kucho ndo hivyo analolitaka mzanznibari ndo hilo hilo......u knowwwwwwwwwwwwwwwwwwwwwwwwwwwwwwwwwwwwwwwwwwww

Mkuu wote waliochangia hakuna hata mmoja aliyetoa matusi,wamejitahidi kutoa maoni yao,nashangaa unamshambulia mtoa hoja badala ya kushambulia hoja.
 
Yupo sahihi Mliberali wawaachie Zenji yao mana sioni umuhimu wa Muungano huu ambao wabara hawanufaiki nao na wavisiwani wanadai hivyo hivyo sasa anaenufaika na Muungano ni nani? Kweli akili kumkichwa.
 
Kuna kitu Zanzibar hawakielewi, ila woga wao wa kujitegemea unawafanya kuendelea kung'ang'ania vitu.
Ni hivi, sisi hatutaki aina yoyote na muungano nao, hivyo waituambie habari za Muungani, sisi hatutaki kabisa kuwepo na muungano, na maadam wao wameamua kujitoa na kubeba hilo bango la kujitoa, basi wajitoe jumla badala ya kuleta aina za miungano mezani.
Wanang'ang'ania nini kuwa na sisi, mpaka wanaa kutuletea aina za miungano....wanaogopa ku-stand alone? basi waache kelele.

Hadidu rejea za warioba ni marufuku kuuvunja.
 
Huyu yakhe atupshe mkapa yupo wap akamtandke kwa ffu naskia yeye na karume ni uamsho
 
Watanganyika wametoa maoni, waznz wametoa maoni.

Naomba usome habari katika link hiyo hapo juu. Makamu wa Rais Idd Seif amekataa na kusema wazi kuwa wazanzibar wanafaidika na muungano. Shein aliwahi kusema hayo.

Hakuna sababu maoni ya wazanzibar ndiyo yaunde katiba ya JMT. Kwanini wanaweka masharti ili hali tunajua kuwa wapo wazn akiwemo Seif Idd hawakubaliani na Maalim Seif? Je, wznz wapi unaongelea.

The bottom line ni kuwa Seif Hamad asishinikize maoni yake yenye kiu zake za kisiasa kuwa maoni ya wananchi.
Mimi ni mmoja wa wale wanaosema let znz go! lakini itokee hivyo kwa wznz na si kundi au mtu aliyetumwa eti aweke masharti kwa tume ya Warioba. Who is he by the way.
Kukata mzizi wa fitina hapa ni kura ya maoni iitishwe, wazanzibar wote wapewe fursa ya kutoa maoni yao iwapo wanakubaliana na muungano au la. Kikwazo ni kwamba ccm inaliogopa hili kwa kuwa ina uhakika wazanzibar hawautaki muungano na watapiga kura ya kuukataa. Badala yake wanaamua kuwatawala kimabavu tu.
 
Nguruvi3,

..wa-Znz wameweka ya kwao mezani.

..na sisi wa-Tanganyika tuweke ya kwetu mezani.

..suala la ardhi, Maalim Seif amelielezea ktk taarifa waliyotoa baada ya kongamano lao.

..kwa upande wangu madai ya kina Maalim yanabeba 90% ya matamanio yangu.

..naunga mkono msimamo wa Maalim Seif na wenzake.

cc: Barubaru, THE BIG SHOW, takashi, GHIBUU, Nonda
 
Last edited by a moderator:
Mkuu nakuomba nikusumbue kupata majina ya hiyo tume ya maridhiano na hadidu za rejea kwa tume ya katiba. Nilikuwa 'offline' kwa wiki moja hivi.
 
Chanzo cha habari hii ni kutoka katika gazeti la Habari leo
(http://www.habarileo.co.tz/index.php/habari-za-kitaifa/12645-makamu-wa-rais-atikisa-muungano)

Makamu wa Rais wa Zanzibar bw Seif Sharif Hamada ametoa masharti ya mambo 10 yanayopaswa kuondolewa katika mambo ya muungano. Amesema tume ya maridhiano ya Wazanzibar imeamua yafuatayo yasiwe ndani ya katiba mpya.
Ufuatao ni muhtasari wa habari hiyo

1.Zanzibar kuwa na uraia
2.Kubadili jina la muungano kutoka Jamhuri ya watu wa Tanzania na kuwa muungano wa Jamhuri za Tanzania
3.Znz kuwa na sarafu yake na benki kuu yake
4.Zanzibar kuwa na ushirika wa mambo ya kimataifa pekee
5.Zanzibar kuwa na baraza lake la mitihani
6.Kuwa na jeshi lake la Polisi
7.Kuwa na mamlaka zake za kodi zisizofungamana na upande mwingine
8.Usajili wa vyama vya siasa kila upande usiotegemeana
9.Hati za kusafiria
10. Bendera ya znz kule New York, Adis Ababa na Commonwealth.


Maalim ametoa masharti kuwa katiba mpya lazima iwe na marekebisho makubwa katika mambo ya muungano.
Amesema Wazanzibar wataiangalia rasimu ya katiba kwa masharti yaliyotolewa na tume ya maridhiano
.

My take:
Maalim seif sina hana uelewa wa kile anachozungumzia. Kama anao,atakuwa anafahamu kuwa hadhra''audience'' yake haina uelewa na anaweza kuongea atakavyo na kupigiwa makofi.

Kwanza, Maalim Seif lazima atambue katiba ni chombo cha umma na si kwa ajili ya kundi au sehemu moja ya jamii.
kusema anaweka masharti ni dharau kwa wananchi wa Taifa hili.

Pili,tume ya Jaji Warioba ilipoundwa(wengine tulikataa), maalim na wabunge wake wa CUF waliridhia na chama chake kuwa sehemu ya wajumbe wa tume
Alikubalina na taratibu zilizopo na hawezi kuiwekea masharti tume alioridhia kwa kila hali.

Tatu, tume ya maridhiano ya wzn haina nguvu za kisheria.Kama ina nguvu zinaishia huko visiwani.
Haina mamlaka ya kuzungumza kama au Watanganyika hivyo maoni ya tume yanabaki kuwa maoni ya maskani au vijiweni.

Nne,Kubadili jina la JMT kuwa muungano wa jamhuri za Tanzania. Ni dhahiri anautaka muungano kwa kujificha.
Uwepo wa uraia na hati za kusafiria za znz hauna sababu za kuwa na Muungano wa Jamhuri za Tanzania anazodai.

Tano;Kuondoa jeshi la Polisi katika muungano.Polisi ni sehemu ya majeshi ya ulinzi na usalama yenye Amir jeshi mkuu mmoja tu.

Laukana anataka ulinzi na usalama viondolewe, Seif asema Jeshi na Polisi viondolewe ili kuwa na dola kamili.
Jeshi la Tanzania lina Amir jeshi mmoja tu ambaye ni wa majeshi ya ulinzi na usalama ikiwemo Polisi.

Sita,Baraza la mitihani la znz. Hilo limeshafanyika. Anachopaswa kufanya ni kuwashawishi wajumbe wa znz ndani ya NECTA kujitoa
Atake wizara ya elimu ya juu iondolewe pia

Saba, Mafuta na gesi, vimeshaondolewa kwa kutumia BLW.Mafuta yanachimbwa ardhini,hivyo anapaswa kutamka kuwa Ardhi isiwe katika muungano. Na ili kulinda mafuta na ajira zitokanazo, Maalim aseme kuwa ajira na shughuli za utumishi ziondolewe katika muungano.

Nane,Mamlaka za kukusanya kodi zipo znz (TRA na ZRA) Ushahidi upo mapato ya TRA yanabaki huko.
Znz inapokea pesa za bure kwa kupitia ofisi ya makamu wa Rais wa JMT(Mwaka huu bilioni 32).
Anapaswa azikatae kwanza kabla ya kuongelea mamlaka za kodi.

Tisa,Bendera ya JMT haimpendezi, Seif anatakiwa aache kutumia kitu chenye nembo ya JMT asiyotaka

Kumi, Maalim anapaswa kuwaeleza watu kuhusu mgao wa BoT znz inayoupata.
Na aangalie pengo la bajeti ya znz linavyozibwa na pesa za Muungano.

Kumi na moja,Uraia na hati za kusafiri na mambo ya nje,kwanza awaamuru wznz walioko bara akiwemo makamu wa Rais waache warudi kwenye Uraia. Arudishe kile kitambulisho cha JMT alichochukua Karimjee chini ya jina la JMT

Kumi na mbili,Vyama vya siasa, Maalim alikuwa Morogoro kuzindua kampeni za chama chake juzi.
Ili awe serious na anachosema tunamtaka apige marufu kukanyaga Tanganyika katika mambo ya kisiasa.

Madai ya Seif ni wazi anataka kuvunja muungano. Upo umuhimu wa kumsaidia afikie malengo yake ya kisiasa

kwanza, aache kuogopa kutamka 'vunja muungano''.Adai znz huru bila mkataba au kujibanza katika baadhi ya maeneo

Pili,Apige marufuku wabunge wa kiliberali(CUF) wasije Dodoma na wafanyakazi wa serikali ya muungano waondoke

Tatu,apeleke mswada wa kunja muungano BLW na BLM yeye akiwa makamu wa Rais kwa kushirikiana na Rais ambaye ni mwenyekiti wa baraza la mapinduzi

Nne,amshauri Rais ili kauli zake ziwe za SMZ na si za viunga vya minazi.

Muhimu:Maalimu aheshimu maoni ya wananchi juu ya katiba hana sababu za kuifanya ZNZ iweke masharti ya kisiasa kwa Tanzania.

Maalim aseme kama ni msemaji wa SMZ, kuongelea katika viunga vya minazi hakutaleta suluhu.

Maalim Watanganyika hawapo tayari kuburuzwa na wazanzibar kwa makundi au watu wa nje.
Tanganyika si sehemu na haijawahi kuwa sehemu ya sultan na haitakuwa sehemu ya Sultan

cc. Mwanakijiji, JokaKuu, Jasusi, Mag3, Wickama, Mkandara,EMT,Kichuguu,Mchambuzi,Kigwangalla, Zitto, Jusa,Tundu Lisu, AshaDii, Prishaz,Ngongo, Ms Judith, Ghibuu, Barubaru,Ngambo,Nonda, Ngali,Mwalimu,Nape,Bongolander,Invisible,Mwakalinga Y.R,
Watanganyika na Wanajamvi wote
Nadhani wangekuwa sasa kusema Muungano wa Jamhuri za TanZania, kwani hapo (bolded) pana tofauti ya tafsiri.
 
Nguruvi3,

..wa-Znz wameweka ya kwao mezani.

..na sisi wa-Tanganyika tuweke ya kwetu mezani.

..suala la ardhi, Maalim Seif amelielezea ktk taarifa waliyotoa baada ya kongamano lao.

..kwa upande wangu madai ya kina Maalim yanabeba 90% ya matamanio yangu.

..naunga mkono msimamo wa Maalim Seif na wenzake.

cc: Barubaru, THE BIG SHOW, takashi, GHIBUU, Nonda


Mimi Pia namuunga mkono Maalim Seif kwa asilimia mia moja,

Ila nachokiona mimi kama Mtanganyika ni kwamba kama tumeamua kuuvunja basi tusiwe selective katika namna ya uvunjaji,Maalim Seif asiwe selective,

Kwa mtazamo Wangu mimi Mkuu JokaKuu ni kwamba kila upande uchukue 50 zake kivyake vyake,

Maadam Zanzibar wanaona wamebanwa na huu muungano basi waamue kwa amani kuondoka na sisi tuwaache kwa amani waondoke,lakini sisi tusitake chochote kutoka kwao,na wao wasitake chochote kutoka kwetu,,

Yaani tuuvunje muungano katika kila nyanja,tuifanye zanzibar kamavile tunavoichukulia nchi nyingine mfano kenya,uganda n.k,,maingiliano ambayo yapo na ya kihistoria tutajua namna ya kuyapangilia ili tuendelee na maisha yetu kama kawaida...
 
Last edited by a moderator:
..wa-Znz wameweka ya kwao mezani.

..na sisi wa-Tanganyika tuweke ya kwetu mezani.
Nina wasiwasi kuwa Watanganyika (with all respect to them) bado hawajawa na ujasiri wa kuanzisha makongamano na kuweka ya kwao mezani, sanasana wataishia kwenye "meza za mitandao".

Mpaka leo bado kuna Watanganyika (no offense) wanaotegemea Warioba na tume yake kuleta mabadiliko ya Muungano!
...si rahisi kama unavyofikiria JokaKuu
 
Mtu akiondoa vihasira kwa sababu yoyote ile, kwa mbaaali, hichi kipengele (2.Kubadili jina la muungano kutoka Jamhuri ya watu wa Tanzania na kuwa muungano wa Jamhuri za Tanzania) kina mantiki: Kinakuwa kama kinaomba federalism, na federalism haina tatizo as such. Tatizo linalokuja ni kwamba Maalim kachanganya vitu kwenye madai. Huwezi kuomba federalism halaf ukaomba na uraia wa pekee, na uwakilishi wa kimataifa wa pekee. Hii ni kama kuchanganya chumvi na sukali kwenye chakula hicho hicho; so confused! Polisi, bendera, baraza la mitihani la pekee, hivi vinaelezeka kujitenga ndani ya federal states. Lakini si uraia na uwakilishi wa kimataifa.



Chanzo cha habari hii ni kutoka katika gazeti la Habari leo
(http://www.habarileo.co.tz/index.php/habari-za-kitaifa/12645-makamu-wa-rais-atikisa-muungano)

Makamu wa Rais wa Zanzibar bw Seif Sharif Hamada ametoa masharti ya mambo 10 yanayopaswa kuondolewa katika mambo ya muungano. Amesema tume ya maridhiano ya Wazanzibar imeamua yafuatayo yasiwe ndani ya katiba mpya.
Ufuatao ni muhtasari wa habari hiyo

1.Zanzibar kuwa na uraia
2.Kubadili jina la muungano kutoka Jamhuri ya watu wa Tanzania na kuwa muungano wa Jamhuri za Tanzania
3.Znz kuwa na sarafu yake na benki kuu yake
4.Zanzibar kuwa na ushirika wa mambo ya kimataifa pekee
5.Zanzibar kuwa na baraza lake la mitihani
6.Kuwa na jeshi lake la Polisi
7.Kuwa na mamlaka zake za kodi zisizofungamana na upande mwingine
8.Usajili wa vyama vya siasa kila upande usiotegemeana
9.Hati za kusafiria
10. Bendera ya znz kule New York, Adis Ababa na Commonwealth.


Maalim ametoa masharti kuwa katiba mpya lazima iwe na marekebisho makubwa katika mambo ya muungano.
Amesema Wazanzibar wataiangalia rasimu ya katiba kwa masharti yaliyotolewa na tume ya maridhiano
.

My take:
Maalim seif sina hana uelewa wa kile anachozungumzia. Kama anao,atakuwa anafahamu kuwa hadhra''audience'' yake haina uelewa na anaweza kuongea atakavyo na kupigiwa makofi.

Kwanza, Maalim Seif lazima atambue katiba ni chombo cha umma na si kwa ajili ya kundi au sehemu moja ya jamii.
kusema anaweka masharti ni dharau kwa wananchi wa Taifa hili.

Pili,tume ya Jaji Warioba ilipoundwa(wengine tulikataa), maalim na wabunge wake wa CUF waliridhia na chama chake kuwa sehemu ya wajumbe wa tume
Alikubalina na taratibu zilizopo na hawezi kuiwekea masharti tume alioridhia kwa kila hali.

Tatu, tume ya maridhiano ya wzn haina nguvu za kisheria.Kama ina nguvu zinaishia huko visiwani.
Haina mamlaka ya kuzungumza kama au Watanganyika hivyo maoni ya tume yanabaki kuwa maoni ya maskani au vijiweni.

Nne,Kubadili jina la JMT kuwa muungano wa jamhuri za Tanzania. Ni dhahiri anautaka muungano kwa kujificha.
Uwepo wa uraia na hati za kusafiria za znz hauna sababu za kuwa na Muungano wa Jamhuri za Tanzania anazodai.

Tano;Kuondoa jeshi la Polisi katika muungano.Polisi ni sehemu ya majeshi ya ulinzi na usalama yenye Amir jeshi mkuu mmoja tu.

Laukana anataka ulinzi na usalama viondolewe, Seif asema Jeshi na Polisi viondolewe ili kuwa na dola kamili.
Jeshi la Tanzania lina Amir jeshi mmoja tu ambaye ni wa majeshi ya ulinzi na usalama ikiwemo Polisi.

Sita,Baraza la mitihani la znz. Hilo limeshafanyika. Anachopaswa kufanya ni kuwashawishi wajumbe wa znz ndani ya NECTA kujitoa
Atake wizara ya elimu ya juu iondolewe pia

Saba, Mafuta na gesi, vimeshaondolewa kwa kutumia BLW.Mafuta yanachimbwa ardhini,hivyo anapaswa kutamka kuwa Ardhi isiwe katika muungano. Na ili kulinda mafuta na ajira zitokanazo, Maalim aseme kuwa ajira na shughuli za utumishi ziondolewe katika muungano.

Nane,Mamlaka za kukusanya kodi zipo znz (TRA na ZRA) Ushahidi upo mapato ya TRA yanabaki huko.
Znz inapokea pesa za bure kwa kupitia ofisi ya makamu wa Rais wa JMT(Mwaka huu bilioni 32).
Anapaswa azikatae kwanza kabla ya kuongelea mamlaka za kodi.

Tisa,Bendera ya JMT haimpendezi, Seif anatakiwa aache kutumia kitu chenye nembo ya JMT asiyotaka

Kumi, Maalim anapaswa kuwaeleza watu kuhusu mgao wa BoT znz inayoupata.
Na aangalie pengo la bajeti ya znz linavyozibwa na pesa za Muungano.

Kumi na moja,Uraia na hati za kusafiri na mambo ya nje,kwanza awaamuru wznz walioko bara akiwemo makamu wa Rais waache warudi kwenye Uraia. Arudishe kile kitambulisho cha JMT alichochukua Karimjee chini ya jina la JMT

Kumi na mbili,Vyama vya siasa, Maalim alikuwa Morogoro kuzindua kampeni za chama chake juzi.
Ili awe serious na anachosema tunamtaka apige marufu kukanyaga Tanganyika katika mambo ya kisiasa.

Madai ya Seif ni wazi anataka kuvunja muungano. Upo umuhimu wa kumsaidia afikie malengo yake ya kisiasa

kwanza, aache kuogopa kutamka 'vunja muungano''.Adai znz huru bila mkataba au kujibanza katika baadhi ya maeneo

Pili,Apige marufuku wabunge wa kiliberali(CUF) wasije Dodoma na wafanyakazi wa serikali ya muungano waondoke

Tatu,apeleke mswada wa kunja muungano BLW na BLM yeye akiwa makamu wa Rais kwa kushirikiana na Rais ambaye ni mwenyekiti wa baraza la mapinduzi

Nne,amshauri Rais ili kauli zake ziwe za SMZ na si za viunga vya minazi.

Muhimu:Maalimu aheshimu maoni ya wananchi juu ya katiba hana sababu za kuifanya ZNZ iweke masharti ya kisiasa kwa Tanzania.

Maalim aseme kama ni msemaji wa SMZ, kuongelea katika viunga vya minazi hakutaleta suluhu.

Maalim Watanganyika hawapo tayari kuburuzwa na wazanzibar kwa makundi au watu wa nje.
Tanganyika si sehemu na haijawahi kuwa sehemu ya sultan na haitakuwa sehemu ya Sultan

cc. Mwanakijiji, JokaKuu, Jasusi, Mag3, Wickama, Mkandara,EMT,Kichuguu,Mchambuzi,Kigwangalla, Zitto, Jusa,Tundu Lisu, AshaDii, Prishaz,Ngongo, Ms Judith, Ghibuu, Barubaru,Ngambo,Nonda, Ngali,Mwalimu,Nape,Bongolander,Invisible,Mwakalinga Y.R,
Watanganyika na Wanajamvi wote
 
Mimi ni Mtanganyika na ninasubiri kwa hamu hiyo siku Tanganyika yetu itakaporejea. Kwa mantiki hiyo, ninamuunga mkono Maalim na Wazenj wote na Walibelari wote kudai Zanzibar huru. jamani tuwaunge mkono maana siku Zanzibar itakapopata uhuru wake, moja kwa moja na Tanganyika itakuwa imerejesha uhuru wake. Ushauri wa bure kwa akina Maalim na Walibelari: vunja ndoa na CCM, unga mkono harakati za ukombozi wa pili wa Tanzania zinazoendeshwa chini ya uongozi wa CDM na M4C yake mtakuwa mmejihakikishia uhuru wenu. Muungano kama ulivyo leo hii ni mradi wa CCM kuendelea kuhodhi utawala. As long as mnaendelea na ndoa ya CUF + CCM (sijui kama ni ya jinsia moja au tofauti), basi hizo ngonjera zitabakia hapo hapo Kibanda maiti!!!
 
Back
Top Bottom