Muungano: Maalim Seif aipa tume ya jaji Warioba masharti

Muungano: Maalim Seif aipa tume ya jaji Warioba masharti

JokaKuu,

Kumekuwa na kampeni za kumchafua Maalim hapa JF, hasa kutoka kwa wale waabudu Nyerere. Lakini ukweli wa mambo Tz inahitaji viongozi kama Maalim Seif. Kiongozi anaejiamini na kutamka hadharani yale anayo yaamini katika ulimwengu huu wa siasa. Tanganyika inahitaji kiongozi kama Maalim , atamke hadharani msimamo wa Tanganyika katika Muungano.

Tanganyika na Tanzania zitofautishwe, huu uhuni wa kutumia mali za Muungano kwa maslahi ya Tanganyika umalizike. Tunako elekea ni kubaya simba wa Uamsho wamemaliza kazi yao ya kuamsha wznz, sasa wanajitayarisha kwa hatua ya pili ya Ukombozi.

Saluti mkuu!
 
Mkuu Nguruvi3 ,

Hivi bado huwa mnazichukua kauli za Maalim Seif serious?

Mimi nilishamfuta katika ulimwengu wa wanasiasa wanasema na kutenda. Huyu jamaa anatumia ujinga wetu katika siasa zake za kitapeli. He stands only for his own skin. Maslahi na nafsi yake ni zaidi ya maslahi ya wananchi wake. He's a political prostitute. He's willing to prostitute himself for his political personal gain. Karagabaho!.

Wazee wetu walioleta hili "dudu" linaloitwa muungano pamoja na kufanya hivyo kwa nia nzuri, madhara yake yamekuwa makubwa na yanaendelea kuwa makubwa zaidi ya jinsi walivyotegemea.

CCM wako kwenye matope na hili "dudu" na ninaamini wengi wanapenda sana kuachana nalo lakini kivuli cha Mwl. Nyerere kinawaogopesha kuchukua maamuzi. MwanaCCM gani yuko tayari kuingia kwenye historia kama aliuvunja muuungano ambao kwa mujibu wa katiba iliyopo ni usaliti katika kiapo?.

Hotuba ya Mwl. Nyerere pale kilimanjaro hotel tarehe 14th March 1995 kuhusu kumpata Rais bora ilipigilia nyundo historia ya nchi kuhusiana na hili "dudu" muungano. Maneno yake hayo yamekuwa kama zimwi kwa CCM. Watakaoweza kupambana na hili ZIMWI na kulitupilia mbali ni watu kutoka nje ya nyumba ya CCM peke yake.

Ninaamini kitakachopatikana katika katiba hii mpya ni serikali tatu kwa vile kuna wanaCCM wengi ambao wanapenda iwe hivyo na hata mapendekezo ya CCM katika tume kuhusiana na hili "dudu" yalikuwa VAGUE.

Maalim Seif anawazuga tu kwa haya anayoyaongea kwa sababu hata ukidadavua neno kwa neno utagundua contradiction nyingi tu.

He's a liability siyo tu kwa Watanganyika, bali hata kwa Wazanzibari kama watapewa hiyo nchi wanayoipigia kelele kila siku.

He's gonna sell them.

Nakubaliana na wewe lakini tusisahau pamoja na kuwa Watanganyika wako kimya sana na Muungano haimaanishi kuwa wanakosa maamuzi, ni kama vile mtu anawaza 'hivi nikijishughulisha na kuvunja muungano napata nini?". Wengi wana Tanganyika (kwa maoni yangu) wanaona sarakasi za Wazanzibari kwa mashangao au wakati mwingine kwa daharau ingawa wapo Wazanzibari wanawaona akina Maalim Seif kama mashujaa.

Hebu angalia hiki kichekesho; Wazanzibari wapinga Muungano mara ya kwanza walikuwa wanataka serikali tatu (hata CUF Msimamo wao ulikuwa hivyohivyo), baada ya muda wakataka Mkataba (hata kuuelezea walikuwa wanapata shida), na tena mpaka "miungu wao" wanaowaamini akina Ahmed Rajabu haya yalikuwa maoni yao. Ghafla baada ya maswali magumu kuhusu huo mkataba wanaoutaka wakakaa kimya.

Sasa hivi kinara wao Maalim Seif anataka Muungano wa "Jamhuri za Tanzania", tena kuwepo na passport zao na mambo yao ya Ulinzi na Mambo ya nje - kichekesho cha karne.

Wanajua vizuri sana kuwa hayo ni lazima wayapate nje ya Muungano, na dawa yake ni kuuvunja. Hwataki kuvunja lakini wanataka Muungano!!

Hawa ni kupe tu, na huo ukupe ndiyo unawafanya mara sitaki nataka. Na usishangae ikaja single nyingine tena!!
Mark my word: Nyerere pamoja na dosari zoote hakukosea; hawa ni wanajiona wamoja kwa sababu ya Tanganyika, nje ya Tanganyika wanachukiana vibaya sana - nawafahamu.

Lets Zanzibar go, hatutaki "Jamhuri za Tanzania"........Ondokeni kuanzia Dodoma Bungeni, Ofisi ya Makamu wa Rais na acheni fadhila zoote mnazopata............Maana naona mke mwenyewe analishwa lakini kutwa kiguu na njia kulalama.
 
sokwe ukijibu haya hata mie ntaelewa!juzi bungen wabunge wa Zanzibar walitaka zanzibar inufaike na gesi ya mtwara (correct me if I am wrong) hapo hapo wao wanasema mafuta sio mambo ya muungano!je Zanzibar inataka kuinyonya Tanzania/Tanganyika?kinachopatikana Zanzibar ni Chao lakini kinachopatikana Bara ni Chetu sote!ndio hivo Mwataka?kama ndio hivo then nafikir hata sie Tanganyika hatuhitaji muungano na nyie!mjikalie na mafuta yenu na sisi tujikalie na tabu zetu!

Mkuu hayo yote yanatokana na tanganyika haipo,idaini kwanza tanganyika muone kama wazenj wataingia,huoni kule baraza la wakilishi mtanganyika hatii mguu?
 
Last edited by a moderator:
Mkataba wa nini?hebu niambie wewe unaona mimi kama mtanganyika nafaidika vipi na uwepo wa Zanzibar kama sehemu ya Muungano?hakuna sababu ya mkataba,daini nchi yenu na muondoke jumla.

Zanzibar washadai nchi yao je tanganyika mnadai nn?
 
Umesahau kumi na tatu; kwanini viongozi wa ki-tanganyika waoga kupita kiasi. au ndio kile tunacho kiamini kuwa wao ndio wanaonufaika na Muungano huu wa kidhalimu.

Sasa ninyi majasiri si mjiondoe kabisa, vunjeni Muungano hata mimi nitakuunga mkono. Ninyi masema tunawanyonya na tunawazibia neema zenu lakini kwa nini hamtaki kutoka na sasa hivi manataka Jamhuri za Tanzania?

Halafu usituite waoga, hivi kuna muoga gani anaweza kumdhulumu mtu jasiri?

Kwa mtazamo wako (na Wazanzibar wenzako).

1. Tunawanyonya rasilimali zenu (kama zipo)
2. Tunawazibia neema zenu
3. Tunawachagulia viongozi nk nk

Sasa hapo nani jasiri!! Anayedhulimiwa ama anayedhulumu?
 
  • Thanks
Reactions: ral
Mkuu hayo yote yanatokana na tanganyika haipo,idaini kwanza tanganyika muone kama wazenj wataingia,huoni kule baraza la wakilishi mtanganyika hatii mguu?
Serikali tatu itakuwa "pasua kichwa" vilevile!; Kwanza gharama zitakuwa kubwa kwa nchi changa kama hizi, halafu uchangiaji wa gharama za kuendesha serikali ya muungano matatizo yatajitokeza kama vile anayechangia kikubwa katika Muungano ataka naye apate mgao au sauti kubwa, kuna suala la ardhi na mengineyo.

Kuukata mzizi wa fitina ni kuuvunja Muungano tu, kila mtu afe na chake.
 
Zanzibar washadai nchi yao je tanganyika mnadai nn?

Sasa mnamdai nani nchi yenu?kwan hamjui procedure za kudai nchi yenu?tuwakumbushe?kazi ya baraza la wawakilishi ni nini?si muende mahakama ya katiba kudai nchi yenu?mnadai kwenye vijiwe mkuu?mtadai sana kama ndo hivo..kelele nyingi lakini kuchukua hatua hamchukui!poleni zenu,heri sie ambao hatujadai nchi yetu!
 
mchakato wa katiba mpya unaoendelea sasa unazidi kupata vikwazo vingi kiasi cha kuonekana labda wakati wake ulikuwa bado,lakini kutokana na msuguano wa kiuchumi na hali halisi ya dunia ya leo ikaonekana kwamba wakati wa kubadilisha katiba ni sasa.Kwa upande wangu sidhani kama viongozi wa serikali na wale kisiasa ndio wanawajibika kuwasilisha maoni ya watu,mwananchi ndio mwenye kutoa maoni.Viongozi hawa wakijifanya kuwasilisha maoni ya watu wataaribu kila kitu chema walichokianzisha wao wenyewe kwa manufaa ya wote,na hapo itaonesha kuwa hicho walichokianzisha hakikuwa cha watu bali chao wenyewe.Kikubwa wakuu hawa wajitahidi kuwa wavumilivu ili ile tume walioichagua na kuiamini iweze kuleta mwongozo ule wananchi wanautaka (katiba).Hii ikiwa ni pamoja na kutojihusisha na matamko au maelezo ambayo wakati mwingine tayari walikwisha wasilisha kwenye tume,kwani kufanya hivyo ni sawa na kuishinikiza/kuishurutisha tume ifuate kile ambacho wanataka wao na si vinginevyo.K
 
hapa ndipo kwenye tatizo Yericko!

Watanganyika wengi siku hizi wanataka Muungano uvunjwe lakini tatizo wapo peke yao hawana support ya viongozi (labda unitajie viongozi wawili tu wa juu serikalini wanaotaka muungano uvunjike) tofauti na wenzao Wazanzibar hawautaki Muungano na wana support kutoka kwa viongozi wao.

Bila ya kushirikisha uongozi au viongozi wa kiserikali sioni kama mtafanikiwa kuipata Tanganyika.
Ukweli ni kwamba viongozi wengi WA Tanganyika hawapendi muungano lakini hawataki historia iwaandike wao kama chanzo cha kufa muungano.Kiukweli hakuna Mtanganyika yeyote anaefaidika na muungano,especially uwepo au kutokuwepo kwa zanzibar kwenye muungano.HAKUNA!
 
ZANZIBAR ni vyema wakasikilizwa na kupewa wakitacho kwakuwa asilimia kubwa hawati muungano, muungano una magumashi makubwa sana na hata upatikanaji wake ulikuwa wa kimagumashi. Ni muungano gani ambao hata mkataba wake hauonekani?
 
Mkuu hayo yote yanatokana na tanganyika haipo,idaini kwanza tanganyika muone kama wazenj wataingia,huoni kule baraza la wakilishi mtanganyika hatii mguu?

Kama tanganyika haipo sasa nyie mwadai uhuru kutoka wapi?je waweza kudai uhuru kutoka kwenye nchi yako mwenyewe(maana ndicho mnachofanya)and its treason mnachokifanya!
 
Nakubaliana na wewe lakini tusisahau pamoja na kuwa Watanganyika wako kimya sana na Muungano haimaanishi kuwa wanakosa maamuzi, ni kama vile mtu anawaza 'hivi nikijishughulisha na kuvunja muungano napata nini?". Wengi wana Tanganyika (kwa maoni yangu) wanaona sarakasi za Wazanzibari kwa mashangao au wakati mwingine kwa daharau ingawa wapo Wazanzibari wanawaona akina Maalim Seif kama mashujaa.

Hebu angalia hiki kichekesho; Wazanzibari wapinga Muungano mara ya kwanza walikuwa wanataka serikali tatu (hata CUF Msimamo wao ulikuwa hivyohivyo), baada ya muda wakataka Mkataba (hata kuuelezea walikuwa wanapata shida), na tena mpaka "miungu wao" wanaowaamini akina Ahmed Rajabu haya yalikuwa maoni yao. Ghafla baada ya maswali magumu kuhusu huo mkataba wanaoutaka wakakaa kimya.

Sasa hivi kinara wao Maalim Seif anataka Muungano wa "Jamhuri za Tanzania", tena kuwepo na passport zao na mambo yao ya Ulinzi na Mambo ya nje - kichekesho cha karne.

Wanajua vizuri sana kuwa hayo ni lazima wayapate nje ya Muungano, na dawa yake ni kuuvunja. Hwataki kuvunja lakini wanataka Muungano!!

Hawa ni kupe tu, na huo ukupe ndiyo unawafanya mara sitaki nataka. Na usishangae ikaja single nyingine tena!!
Mark my word: Nyerere pamoja na dosari zoote hakukosea; hawa ni wanajiona wamoja kwa sababu ya Tanganyika, nje ya Tanganyika wanachukiana vibaya sana - nawafahamu.

Lets Zanzibar go, hatutaki "Jamhuri za Tanzania"........Ondokeni kuanzia Dodoma Bungeni, Ofisi ya Makamu wa Rais na acheni fadhila zoote mnazopata............Maana naona mke mwenyewe analishwa lakini kutwa kiguu na njia kulalama.
Sijaona neno ambalo nitalipinga katika bandiko lako hili. Hawa jamaa kama nilivyosema, kigugumizi chao katika matamko na kwenye majukwaa ya kisiasa zinadhihirisha kabisa hawana hata tone la political will kujitoa kwenye muungano.

Wanajificha kwenye katiba ya nchi kama kujitoa ni kosa ya uhaini ili kuficha madhaifu yao.

Kama unavyosema, kwa sababu wao siyo wamoja, hata wale wanaotegemea maisha yao kwa kodi za Watanganyika hawawezi kukubali kuachia posho na malupu lupu wanayoyapata. Hata Wabunge, wafanyakazi waandamizi wa serikali, wafanyabiashara, n.k. Hawawezi kukubaliana na mawazo yao.

Kitu ninachokifahamu, hawa jamaa ni weakling na hawawezi kujitoa kwenye muungano lakini nchi yetu itakuwa na serikali tatu.

I can't wait to read rasimu kujua mwelekeo wa taifa letu katika maswala yanayopigiwa kelele sana ambazo zingine mpaka zinakuwa na crocodile tears.
 
Its enough to say Maalim Seif ISN'T NORMAL! Sorry
 
Ukweli ni kwamba viongozi wengi WA Tanganyika hawapendi muungano lakini hawataki historia iwaandike wao kama chanzo cha kufa muungano.Kiukweli hakuna Mtanganyika yeyote anaefaidika na muungano,especially uwepo au kutokuwepo kwa zanzibar kwenye muungano.HAKUNA!
Unafikiri ni njia gani zinaweza kutumika kuwapata hawa viongozi waje hadharani na kuweka msimamo wao?
 
Mtoa mada naona unazunguka mbuyu tu,kilicho semwa na seif ni matakwa ya waz'br 66% kwenye tume ya warioba ww unasema eti matakwa ya maskani kijiweni,unachotakiwa kusema hapa ni nini matakwa ya watanganyika kwenye
muungano na sio kulaumu maoni ya waz'br,ile. tume ya maridhiano ni ya waz'br na mambo kumi yale ndio matakwa ya wazbr.

Pendekezeni (au niseme amueni) kujitegemea 100%! Na mkubali pia kulipa mnachodaiwa na Tanganyika na upande huu tuwalipe madai yenu yote yaliyopo ( kama yapo). Then Mzanzibar aliepo Tanganyika aehesabiwe kuwa ni raia wa kigeni
 
Hahahaha alhamdullah leo umekubali na umeelewa nini wanachokitaka wazanzibari ? Mungu awafungue na awangoe hawa walio baki wanaowabeza wazanzibari

Mkataba, jamuhuri zote mezani.
Nguruvi3,

..wa-Znz wameweka ya kwao mezani.

..na sisi wa-Tanganyika tuweke ya kwetu mezani.

..suala la ardhi, Maalim Seif amelielezea ktk taarifa waliyotoa baada ya kongamano lao.

..kwa upande wangu madai ya kina Maalim yanabeba 90% ya matamanio yangu.

..naunga mkono msimamo wa Maalim Seif na wenzake.

cc: Barubaru, THE BIG SHOW, takashi, GHIBUU, Nonda
 
Chama sio dini wala msahafu, sio kwamba mtu hawezi kubadili kauli au kuenda kinyume na chama chake, katiba ya sio kitu chochote, kiongozi bora huangalia wafuasi nini wanakitaka, ndipo huunga mkono kwa wafuasi hao ili aweze kukubalika, alicho kifanaya maalim kuwangu mkono wazanzibari ambao wengi wanahoja, ukiangalia leo hii wazanzibari asilimia 66 wanaunga mkono kuwepo kwa mamlaka kamili ya zanzibar na muungano wa mkataba, hivi maalim kama ana stik katika katiba ya chama chake ataungwa mkono ? Ndio maana anaunga hoja ya kuwepo muungano wa mkataba.
Kitu kinachoshangaza ni kuona kuwa Maalim hana kitu alichokisimamia na kukiamini kwa dhati.
Anabadilika kila uchao

Yeye na chama chake cha Uliberali walitaka serikali 3
Mara akabadilika anataka mkataba bila kukubaliana na Waliberali
Sasa hivi anataka dola huru ya znz kwa kutumia kamati ya maridhiano na wala si BLW au BLM
Ukisoma vizuri anataka federalism kwa hilo la Muungano wa Jamhuri za Tanzania
Maudhui ya habari zake ni kuwa hataki muungano.
Wakati hataki muungano, yupoo bize Morogoro na Singida akiimarisha CUF
Haieleweki anaSema kama MaaliM, Makamu wa Rais au Katibu mkuu wa CUF.
Maneno na majungu huyasema viungani Znz, akija Tanganyika ni muumini wa muungano.
Hataki Tanzania na bendera zake ni mbaya hazimpendezi, mfukoni anakitambulisho cha Tanzania.

In short huyu jamaa anayumba yumba sana.
Watanganyika tuwaunge mkono hawa jamaa haraka sana.
Wakishakuwa na Passport zao maana yake ni kuwa hawa ni raia wa nje hakuna mkataba wala mashiriikiano kila mtu kivyake
 
Sasa mnamdai nani nchi yenu?kwan hamjui procedure za kudai nchi yenu?tuwakumbushe?kazi ya baraza la wawakilishi ni nini?si muende mahakama ya katiba kudai nchi yenu?mnadai kwenye vijiwe mkuu?mtadai sana kama ndo hivo..kelele nyingi lakini kuchukua hatua hamchukui!poleni zenu,heri sie ambao hatujadai nchi yetu!

Kumbe mkuu ile tume ya warioba ni kijiwe?unajiona bora kwa kuto lidai au kulilia taifa lako tanganyika lililo kupatia uhuru?
 
Back
Top Bottom