Muungano: Maalim Seif aipa tume ya jaji Warioba masharti

Muungano: Maalim Seif aipa tume ya jaji Warioba masharti

ni fikira potofu ujinga na uroho wa madaraka, wazanzibar wanaruhusiwa kwenda zao, mtumwa anamkumbuka bwanake sultan ni kipindi kirefu hajamtia bakora,tutakuwa tunaendeleza lile tamasha la pasaka hasa soka mpaka pale uhamsho watakapoiteka zanzibar completely.
 
Mtu akiondoa vihasira kwa sababu yoyote ile, kwa mbaaali, hichi kipengele (2.Kubadili jina la muungano kutoka Jamhuri ya watu wa Tanzania na kuwa muungano wa Jamhuri za Tanzania) kina mantiki: Kinakuwa kama kinaomba federalism, na federalism haina tatizo as such. Tatizo linalokuja ni kwamba Maalim kachanganya vitu kwenye madai. Huwezi kuomba federalism halaf ukaomba na uraia wa pekee, na uwakilishi wa kimataifa wa pekee. Hii ni kama kuchanganya chumvi na sukali kwenye chakula hicho hicho; so confused! Polisi, bendera, baraza la mitihani la pekee, hivi vinaelezeka kujitenga ndani ya federal states. Lakini si uraia na uwakilishi wa kimataifa.
Well said, na kujichanganya huko ndiko kunaleta matatizo.

Huwezi kuwa na federal government yenye commander in chief wawili.
Huwezi kuwa na federal sytem ukawa na rais wenye uraia na hati za kusafiria tofauti.
Huwezi kuwa na federal sytem ukawa na uwakilishi tofauti katika medani ya kimataifa.

Muhimu sana ni kuwa yeye hajasema anataka federal system, yeye aliasisi serikali 3, ghafla akataka mkataba na sasa hatujui anataka nini. Ndio maana tunasema pengine yupo affected psychologically hasa tukizingatia umri wake na nafasi ya urais.
 
sokwe ukijibu haya hata mie ntaelewa!juzi bungen wabunge wa Zanzibar walitaka zanzibar inufaike na gesi ya mtwara (correct me if I am wrong) hapo hapo wao wanasema mafuta sio mambo ya muungano!je Zanzibar inataka kuinyonya Tanzania/Tanganyika?kinachopatikana Zanzibar ni Chao lakini kinachopatikana Bara ni Chetu sote!ndio hivo Mwataka?kama ndio hivo then nafikir hata sie Tanganyika hatuhitaji muungano na nyie!mjikalie na mafuta yenu na sisi tujikalie na tabu zetu!
Kamanda Moshi, wao wanataka ardhi iwe jambo la muungano. Ukweli ni kuwa hakuna Mtanganyika anayepewa fursa hiyo huko kwao.

-Wanataka ajira iwe jambo la muungano, wakati huo huo wameweka sheria za kuzuia ajira kwa Watanganyika visiwani.
-Wanataka kunufaika na gesi ya Mtwara, wakati huo huo wanasheria iliyounda uzuiaji wa gesi kuwa sehemu ya muungano.
-Wanataka gesi na mafuta visiwe vya muungano, wakati hu huo wanataka umeme wa bure
-Wanataka wawe na jeshi la Polisi, wakati huo huo hawajui gharama za jeshi la ulinzi.
-Wanadai hawana mafao BoT, wakati huo huo wanapata 7% ya pato la taifa
-Wana baraza lao la mitihani, wakati huo huo wanataka nafasi za upendeleo kuingia elimu ya juu Tanganyika.
-Wanataka mali asili na utalii visiwe vya muungano, wakati huo huo wanataka elimu ya juu iwe muungano wasomeshe watoto wao bure.

Umimi umewajaa sana hawa wenzetu, ni wakati wapewe nafasi wapumue. Tuwasaidie waondoke katika muungano haraka. Tuwasaidie kwasababu hakuna kitu tutakachopoteza.
 
Chama sio dini wala msahafu, sio kwamba mtu hawezi kubadili kauli au kuenda kinyume na chama chake, katiba ya sio kitu chochote, kiongozi bora huangalia wafuasi nini wanakitaka, ndipo huunga mkono kwa wafuasi hao ili aweze kukubalika, alicho kifanaya maalim kuwangu mkono wazanzibari ambao wengi wanahoja, ukiangalia leo hii wazanzibari asilimia 66 wanaunga mkono kuwepo kwa mamlaka kamili ya zanzibar na muungano wa mkataba, hivi maalim kama ana stik katika katiba ya chama chake ataungwa mkono ? Ndio maana anaunga hoja ya kuwepo muungano wa mkataba.
Kiongozi mzuri ni yule anayeonyesha njia hata kama wafuasi wake hawataki. Ni yule anayesimamia kile kilicho sahihi na wala si kura. Seif si kuwa anafuata wanachosema wznz, anawadanganya kwa kutowaeleza ukweli.

Tume ya Warioba ilimpa fursa ya kutoa maoni yake nyumbani kwake.
Seif akaulizwa kwanini tusivunje muungano na tukutane huko EAC?

Jibu la Maalim ni kuwa muungano wetu ni bora kuliko ule wa EAC kwasababu una umri na umepitia misuko suko mingi.
Ukisoma taarifa ya link hapo juu ni Seif huyo huyo anasema kuwa muungano hauna faida na umedhoofisha znz.

Sasa hapa lazima mtu mwenye akili ajiulize, hivi huyu kiongozi anajua anachosema?
Tulitarajia angemwambia Warioba muungano uvunjwe na wala asingeshtakiwa. Hakufanya hivyo.

Wakati akiwa kibanda maiti Seif alisema muungano umedhoofisha sana upande mmoja ambao ni Zanzibar.
Wakati huo huo anataka kuwe na Jamhuri za muungano wa Tanzania.
Kwamba dakika hii anasema hiki, next minute anakanusha alichokisema.

Hapa ndipo tunashangaa kama Uliberali ndio huo basi kuna tatizo.
Huyu si kiongozi ni mtafuta masilahi tu, kwamba awe rais hata kama mzanzibar wa kawaida ataumia.
 
Well said, na kujichanganya huko ndiko kunaleta matatizo.

Huwezi kuwa na federal government yenye commander in chief wawili.
Huwezi kuwa na federal sytem ukawa na rais wenye uraia na hati za kusafiria tofauti.
Huwezi kuwa na federal sytem ukawa na uwakilishi tofauti katika medani ya kimataifa.

Muhimu sana ni kuwa yeye hajasema anataka federal system, yeye aliasisi serikali 3, ghafla akataka mkataba na sasa hatujui anataka nini. Ndio maana tunasema pengine yupo affected psychologically hasa tukizingatia umri wake na nafasi ya urais.

Correct. He might be 'a case'. Chumvi na sukari kwenye mboga hiyohiyo wapi na wapi....
 
Mkuu Nguruvi3 ,
Maalim Seif anawazuga tu kwa haya anayoyaongea kwa sababu hata ukidadavua neno kwa neno utagundua contradiction nyingi tu.
He's a liability siyo tu kwa Watanganyika, bali hata kwa Wazanzibari kama watapewa hiyo nchi wanayoipigia kelele kila siku. He's gonna sell them.
I can't agree more Ng'wamapalala.
Huyu anataka kuwauza wazanzibar kwasababu ya Urais.
Ukisoma maoni ya tume ya Warioba, wznz wengi wamedai kubadilishwa muundo wa muungano, hawajasema kuvunja. Katika link hapo juu makamu wa rais Seif Idd amesema wazi kuwa wao wanafaidika na muungano.

Vuai aliyekuwa waziri kiongozi alisema wazi kuwa znz inanufaika na muungano.
Rais Shein kasema hayo na hata mznz wa kawaida kabisa anafahamu hivyo.

Seif anadhani kuwa na passport na Uraia wa znz kunatosha kuwa suluhu ya matatizo ya wznz.

Anawauza kwasababu kwa hali yoyote, znz itabaki kuitegemea Tanganyika.
Ni kanuni za asili na wala siyo suala la kisiasa.
Kuwaondoa wznz katika mahusiano kwa kiburi, matusi na kejeli kutawaumiza wznz wa kawaida kabisa.
Seif hatambui kuwa ziaidi ya nusu ya wzn inaishi Tanganyika.

Hatambui kuwa hakuna taifa lolote duniani lililobeba wznz wengi kama Tanganyika.

Anawauza wenzake kwa kusema kuwa baraza la mitihani liondolewe na limeondolewa.
Sasa wale wafanyakazi wa znz NECTA ni lazima waondoke.
Kibaya zaidi ni kuwa hilo baraza lao ambalo halitambuliwi na vyuo vya elimu ya juu Tanganyika litaondoa ule ubwete wa nafasi za upendeleo.

Hapa nifafanue kidogo, wakati wa kuchagua wanafunzi wa kuingia elimu ya juu, mwanafunzi wa znz mwenye div 4 anayonafasi kubwa kuingia elimu ya juu Tanganyika kuliko mwanafunzi wa Tanganyika mwenye div 2.
Hii ni kwasababu wao wanatakiwa wajaze nafasi kadhaa hata kama wataleta mwenye div 4 yenye D moja.

Kwasasa hali itabadilika, wanafunzi wa znz lazima wapimwe kama wale wa Rwanda au Malawi.
Hakuna nafasi za upendeleo wala malipo ya bure kama sasa kwasababu wanatahiniwa na bodi tofauti.
Seif hajaliona hilo anaangalia Urais tu.

Kuhusu contradictions, soma habari nzima ya Kibanda maiti.
Kwa mantiki ya katiba ni kuwa Seif anataka kuvunja muungano. Hilo ni sawa na sisi tunamsaidia iwe hivyo.

Mwisho wa hotuba anasema hataki jina la JMT anataka Muungano wa Jamhuri za Tanzania.
Haa! sasa huyu hataki muungano halafu anataka muungano tena

Anasema bendera ya Tanzania ni kinyaa. Juzi akiwa Morogoro alisindikizwa na ving'ora vya bendera hiyo hiyo.
Ndege anayopanda ina bendera hiyo hiyo asiyoitaka. Sasa hapa anakataa nini na anataka nini.

Anataka Uraia wa kila nchi. Miezi michache alikuwa Karimjee kachukua chake mapema sasa anauza wenzake.
Hajawahi kuwaambia kwanini alichukua kitambulisho cha JMT asiyoitaka to begin with!!

Kuhusu vyama vya siasa, anadai kuwe na separation kila sehemu iwe na chama chake.
Mwezi wa pili sasa anzunguka Tanganyika kuanzia Singida, Arusha, Morogoro n.k. kuimarisha uliberali.
Huyu ndiye asiyetaka kuwe na vyama vya siasa pamoja.

Hoja kubwa hapa si kusema eti wznz wasikatae muungano, in fact hapa tulipo tumeshafanya kila jitihada za wao kujinasua. Kinachowashinda wznz ni ukweli kuwa maisha bila Tanganyika ni maumivuy makali sana.
Wanafikiria hivi nusu ya nchi ikirudi kwao ni kitu gani kitatokea?

Wanafikiria,hivi shughuli zao za uchumi ambazo asilimia 90 inategemea soko la bara zitakuwaje baada ya kutengana?
Na wale walioko bara wanajiuliza, wakirudi znz wataanzia wapi maana wengine wanawajukuu,warudi kufanya nini na kwa kuanzia wapi.

Hayo yanawatisha ndio maana utasikia wakisema hawataki muungano kwenye viunga vya minazi, wakija Tanganyika wanataka serika 3 au mkataba.

Wakiambiwa mkataba uwe wa EAC wanasema tuna undugu.
Wakiulizwa undugu wa vipi wanasema kuoleana.
Mbona kuna watu wa Kenya, Uganda, Norway na filipine wameoleana bila muungano. Yote hayo ni uoga tu.

Ni kweli Sief si kiongozi wa kumchukulia serious kwa watu wenye akili zao.
Kwabahati mbaya si wote kundi lake linazidi kupiga kelele hovyo.
Eti Tanganyika inanyonya znz! hayo ndiyo Seif anapita akihubiri.

We don't need that, tuna matatizo mengi sana ya kushughulikia, hawa ni kuwaacha waondoke.
Nasikitika hawakupa uhuru juzi kama redio zao zilivyosema, lakini tupo bega kwa bega na wao hadi wapate uhuru.

Uhuru huo ni pamoja na kuiacha Tanganyika ipumue.
Hakuna cha Jamhuri za Tanzania wala wizara fulani iwe au isiwe.

Tuacheni tupumue miaka 50 ya kubeba mtoto inatosha, sasa tunawatua chini.
This time around hakuna ujanja, lazima kila kitu kiwekwe mezani.

Natoa wito hiyo rasimu ikitoka, kama kuna kipenegele cha kuwabeba ipigwe chini haraka sana.

Mtanganyika lazima kwanza ujiulize, kitu ABCD kinakusaidiaje wewe. Ukikubali bila kufikiri utaishia kulipa bill ya umeme elfu 50 kwa mwezi kumbe elfu 20 unamlipia mznzibar.

Ukikubali bila kufikiri utashangaa huna zahanati, kumbe bilioni 32 zimepelekwa tu kwasababu kuna sehemu inaitwa znz
Ukikubali bila kufikiri, baba yako na mama yako watakatwa kodi za mshahara, wadogo zako washinde na njaa kumbe pesa hizo ni kumsomesha mtoto wa kizanzibar.

Ukikubali bila kutafakari, utapita barabarani na bahasha za khaki ukitafuta ajira, kumbe ajira yako kapewa mtu kwasababu tu ni mnzanzibar.

Tafakari
 
JokaKuu,

Kumekuwa na kampeni za kumchafua Maalim hapa JF, hasa kutoka kwa wale waabudu Nyerere. Lakini ukweli wa mambo Tz inahitaji viongozi kama Maalim Seif. Kiongozi anaejiamini na kutamka hadharani yale anayo yaamini katika ulimwengu huu wa siasa. Tanganyika inahitaji kiongozi kama Maalim , atamke hadharani msimamo wa Tanganyika katika Muungano.

Tanganyika na Tanzania zitofautishwe, huu uhuni wa kutumia mali za Muungano kwa maslahi ya Tanganyika umalizike. Tunako elekea ni kubaya simba wa Uamsho wamemaliza kazi yao ya kuamsha wznz, sasa wanajitayarisha kwa hatua ya pili ya Ukombozi.
Msimamo wa Seif hakuna anayeujua. Anabadili goli kila siku. Hata habari hiyo hapo juu ni mnajimu peke yake anayeweza kutabiri maalim alilenga nini. Hakuna msomi anayeweza kujua anasema nini.

Hakuna kampeni za kumchafua Seif, bali maneno yake chini ya viunga vya minazi yanamchafua.
Tukubaliane kuwa Seif kachoka kifikra, mawazo na kiakili. Naogopa kumuuliza leo anafikiri nini kuhusu Muungano maana anaweza kutoa jibu la aina yake. Mshauri ajitulize na asome mambo kabla ya kutamka hadharani.
Anajichafua sana mliberali huyu.
 
Kamanda Moshi, wao wanataka ardhi iwe jambo la muungano. Ukweli ni kuwa hakuna Mtanganyika anayepewa fursa hiyo huko kwao.

-Wanataka ajira iwe jambo la muungano, wakati huo huo wameweka sheria za kuzuia ajira kwa Watanganyika visiwani.
-Wanataka kunufaika na gesi ya Mtwara, wakati huo huo wanasheria iliyounda uzuiaji wa gesi kuwa sehemu ya muungano.
-Wanataka gesi na mafuta visiwe vya muungano, wakati hu huo wanataka umeme wa bure
-Wanataka wawe na jeshi la Polisi, wakati huo huo hawajui gharama za jeshi la ulinzi.
-Wanadai hawana mafao BoT, wakati huo huo wanapata 7% ya pato la taifa
-Wana baraza lao la mitihani, wakati huo huo wanataka nafasi za upendeleo kuingia elimu ya juu Tanganyika.
-Wanataka mali asili na utalii visiwe vya muungano, wakati huo huo wanataka elimu ya juu iwe muungano wasomeshe watoto wao bure.

Umimi umewajaa sana hawa wenzetu, ni wakati wapewe nafasi wapumue. Tuwasaidie waondoke katika muungano haraka. Tuwasaidie kwasababu hakuna kitu tutakachopoteza.

mkuu yani haya matakwa yao yanaudhi sana...bora waende zao, wakaungane na Kenya au Comoro...lakini kama hivi ndivo wanavotaka, hata mie nitakwenda kupiga kura ya NO kwenye hiyo rasimu ya muungano wa kiunyonyaji.
Waende zao kwa kweli.
 
Ukweli ni kwamba viongozi wengi WA Tanganyika hawapendi muungano lakini hawataki historia iwaandike wao kama chanzo cha kufa muungano.Kiukweli hakuna Mtanganyika yeyote anaefaidika na muungano,especially uwepo au kutokuwepo kwa zanzibar kwenye muungano.HAKUNA!
Yuko mtu aweza kunifahamisha kama sisi wananchi wa kawaida wa Tanganyika twafaidika na zanzibar?Tuko wengi ambao hata kufikiria kwenda kutembea zanzibar,fikra hizo hazipo akilini mwetu,lakini wa Pemba na w Unguja wa tele huku kwetu,meli zikienda Zanzibar na zikirudi asilimia 99.9 ni wao wa Wazaabaa.
 
Kumbe mkuu ile tume ya warioba ni kijiwe?unajiona bora kwa kuto lidai au kulilia taifa lako tanganyika lililo kupatia uhuru?

sasa kama mnaona tume ya warioba inatosha na mlishatoa maoni yenu mle mkutano now sijui tume ya maridhiano sijui kitu gani wa nini sasa?si mkalale msubiri tume ya Warioba ije na rasimu yake...
Unatufundisha sie kuidai nchi yetu???amazing, wewe ya kwako iko wapi?na unamdai nan?sisi hatuna shida maana nchi yetu ipo
 
mkuu yani haya matakwa yao yanaudhi sana...bora waende zao, wakaungane na Kenya au Comoro...lakini kama hivi ndivo wanavotaka, hata mie nitakwenda kupiga kura ya NO kwenye hiyo rasimu ya muungano wa kiunyonyaji.
Waende zao kwa kweli.
Kenya ipi inayotaka kuwabeba hawa,wasiokuwa na shukran,wamejazana tele Tanganyika,na ndio pia wanaoleta migogoro miskitini,wakiwa miskitini pia ndio hivi hivi,wakiwa katika taasisi za kiislam,kama shule,vyuo,miskiti,pia wana ubaguzi wa hali ya juu,watafanya juu chini kama kuna mtanganyika,hata kama ni waina gani lakini kazaliwa Tanganyika,watahakikisha anaondoka madarakani,ashike
Mzaabaa mwenzake.
 
ZANZIBAR ni vyema wakasikilizwa na kupewa wakitacho kwakuwa asilimia kubwa hawati muungano, muungano una magumashi makubwa sana na hata upatikanaji wake ulikuwa wa kimagumashi. Ni muungano gani ambao hata mkataba wake hauonekani?
Wapewe na nani nchi yao?si waondoke huku Tanganyika warudi kwao,mume humtaki,kuondoka hawaondoki,wewe wafikiri wa Tanganyika ni watu wa vipi wanaowavumilia hawa,je na hawa Wa Tanganyika wakiamuwa kuwafukuza hawa Wazaabaa,patakalika huko kwao?waache wamwaamshe aliyelala,watatamani warudi,lakini wapi,wao waseme kila mzaabaa arudi kwao Pemba au Unguja,mbona hapo hasemi huyu Hamad,akisema hapo ndio nitajuwa kweli.Huku wametuzibia nafasi nyingi za ajira na biashara,wanafaidika na soko kubwa la bidhaa la Tanganyika,Uganda,Malawi,Rwanda,Zambia,Burundi,kupitia Tanganyika,waondoke.
 
JokaKuu,

Kumekuwa na kampeni za kumchafua Maalim hapa JF, hasa kutoka kwa wale waabudu Nyerere. Lakini ukweli wa mambo Tz inahitaji viongozi kama Maalim Seif. Kiongozi anaejiamini na kutamka hadharani yale anayo yaamini katika ulimwengu huu wa siasa. Tanganyika inahitaji kiongozi kama Maalim , atamke hadharani msimamo wa Tanganyika katika Muungano.

Tanganyika na Tanzania zitofautishwe, huu uhuni wa kutumia mali za Muungano kwa maslahi ya Tanganyika umalizike. Tunako elekea ni kubaya simba wa Uamsho wamemaliza kazi yao ya kuamsha wznz, sasa wanajitayarisha kwa hatua ya pili ya Ukombozi.

Hapo kwenye red ndipo Wazenj mnapochemka, mnata msimao wa Tanganyika upi? kuvunjika kwa ndoa/muungano kuna nmna tatu. Zanzibar isipoutaka Muungano, automatically utavunjika; Tanganyika isipoutaka muungano automatically utavunjika na wote wawili kwa pamoja yaani ikitokea Tanganyika na Zanzibar kutoutaka muungano (simultaneously) pia utavunjika. kutaka msimamo wa Tanganyika ni kama kutaka suluhu (to request negotiation to strengthen union). muelewe kwamba katika masuala ya kimataifa mnapokubaliana ndipo kuna "reciprocity" lakini mnapotofautiana hakuna 'reciprocity'. Kwa hiyo nyie hamna haja ya kuwataka watanganyika kauli yao juu ya muungano, nyie watu na akili zenu na wawakilishi wenu. Nakuhakikishia wabunge kutoka Zanzibar wote, serikali ya mapinduzi ya zanzibar yote na watumishi wazanzibari waioko Tanganyika 'waamue' tu kurejea zanzibar then uone kama kutabaki muungano, Lakini huku kutaka kusikia kiongozi gani wa Tanganyika kutoa msimamo wa muungano ni kama kutishia nyau au kutafuta 'justification' au kutokuwa tayari. Kimsingi nyerere alishatoa msimamo huu. Aliwahi kusema kama zanzibar inaona inabanwa katika muungano sio tatizo waweza kujitoa, hivyo jitoeni. Kitendo cha kusubiri tume ya warioba ni kuleta machafuko nchini kwa sababu Katiba mpya haina jukumu la kutimiza matakwa ya wazanzibar tu bali pia ya watanganyika.
Maalim Seif ni kiongozi mwandamizi zanzibar na ana kura za wananchi karibu 50% na pia ndio mshgauri wa karibu wa Rais Shein, kwa maana (Shein+Seif) ni 100% ya ridhaa ya wazanzibari wote. Amshauri wakae chini na kuwataka wataalamu wao watoe technical proposal ya kuvunja muungano si technical proposal ya kuwa "selective" katika muungano. Huu mungano watu wa kawaida wa Tanganyika hawataona tofauti yyte kuwapo kwake au kutokuwapo kwake. Au fanya kautafiti kako Bandarini hapo ujue katika kila boti inayoelekea au kutoka Zanzibar ni asilimia ngapi ya wanaoitumia sana kati ya Wazanzibari na watanganyika? utapata majibu kama ni nani 'active' katika muungano huu. Jitoeni jumla bila kuwa selective na bila kutaka kauli mpya kutoka Tanganyika, la kama mtataka kauli kutoka Tanganyika, mtasahau na kuchelewa kujitoa. Hizi kauli za Nguruvi3, Big Show, na wengineo zatosha kuwa kauli za Tanganyika.
 
Hapo kwenye red ndipo Wazenj mnapochemka, mnata msimao wa Tanganyika upi? kuvunjika kwa ndoa/muungano kuna nmna tatu. Zanzibar isipoutaka Muungano, automatically utavunjika; Tanganyika isipoutaka muungano automatically utavunjika na wote wawili kwa pamoja yaani ikitokea Tanganyika na Zanzibar kutoutaka muungano (simultaneously) pia utavunjika. kutaka msimamo wa Tanganyika ni kama kutaka suluhu (to request negotiation to strengthen union). muelewe kwamba katika masuala ya kimataifa mnapokubaliana ndipo kuna "reciprocity" lakini mnapotofautiana hakuna 'reciprocity'. Kwa hiyo nyie hamna haja ya kuwataka watanganyika kauli yao juu ya muungano, nyie watu na akili zenu na wawakilishi wenu. Nakuhakikishia wabunge kutoka Zanzibar wote, serikali ya mapinduzi ya zanzibar yote na watumishi wazanzibari waioko Tanganyika 'waamue' tu kurejea zanzibar then uone kama kutabaki muungano, Lakini huku kutaka kusikia kiongozi gani wa Tanganyika kutoa msimamo wa muungano ni kama kutishia nyau au kutafuta 'justification' au kutokuwa tayari. Kimsingi nyerere alishatoa msimamo huu. Aliwahi kusema kama zanzibar inaona inabanwa katika muungano sio tatizo waweza kujitoa, hivyo jitoeni. Kitendo cha kusubiri tume ya warioba ni kuleta machafuko nchini kwa sababu Katiba mpya haina jukumu la kutimiza matakwa ya wazanzibar tu bali pia ya watanganyika.
Maalim Seif ni kiongozi mwandamizi zanzibar na ana kura za wananchi karibu 50% na pia ndio mshgauri wa karibu wa Rais Shein, kwa maana (Shein+Seif) ni 100% ya ridhaa ya wazanzibari wote. Amshauri wakae chini na kuwataka wataalamu wao watoe technical proposal ya kuvunja muungano si technical proposal ya kuwa "selective" katika muungano. Huu mungano watu wa kawaida wa Tanganyika hawataona tofauti yyte kuwapo kwake au kutokuwapo kwake. Au fanya kautafiti kako Bandarini hapo ujue katika kila boti inayoelekea au kutoka Zanzibar ni asilimia ngapi ya wanaoitumia sana kati ya Wazanzibari na watanganyika? utapata majibu kama ni nani 'active' katika muungano huu. Jitoeni jumla bila kuwa selective na bila kutaka kauli mpya kutoka Tanganyika, la kama mtataka kauli kutoka Tanganyika, mtasahau na kuchelewa kujitoa. Hizi kauli za Nguruvi3, Big Show, na wengineo zatosha kuwa kauli za Tanganyika.
Zinedine,
Wabunge wao wamemchachamalia Wenje kwa nukuu halali ya filosofi ya uliberali hadi bunge likaahirishwa mara 2.

Haujawahi kutokea wabunge wao hasa waliberali kuchachamaa ili mswada wao wa kuvunja muungano usomwe.
Hakujawahi kutokea mswada wa BLW kuvunja muungano.

Hapo juu umeweka vema sana. Ndoa inaweza vunjika kama mke hamtaki mume, mume hamtaki mke au wote hawatakani.
Sasa hili la kusubiri Tanganyika itoe msimamo ni kituko. Msimamo upi wakati njia zote tumewaonyesha hapa Jamvini?

Mwambieni Gharibu Bilal arudi nyumbani
Wabunge wenu wasije Dodoma au wakija waje na mswada
Wawakilishi walete mswada
Viongozi wa serikali ya muungano wajiuzulu
Wznz wote wanaofanya kazi katika muungano waondoke
wznz wote waliopo vyuoni waondoke.

Hadi hapo muungano kwishney wanavyosema vijana. Haya ya kuongelea katika viunga vya minazi ni woga na unafiki wa hali ya juu.

Njia mbona nyeupe, wansita nini.
 
Unawezaje kuwa na nchi mbili, moja ikabaki na serikali yake na nyingine ikafa.....?! Hakuna muungano kama huu dunia nzima....
Kweli kabisa mkuu. Mnapoungana kwa mambo yote basi serikali lazima iwe moja, kama ilivokuwa Ethiopia na Eritrea, lakini kama mmeungana kwa baadhi ya mambo tu basi ni lazima serikali ziwe TATU kama The Great Britain. Muda umefika sasa kukataa kuburuzwa.
 
sasa kama mnaona tume ya warioba inatosha na mlishatoa maoni yenu mle mkutano now sijui tume ya maridhiano sijui kitu gani wa nini sasa?si mkalale msubiri tume ya Warioba ije na rasimu yake...
Unatufundisha sie kuidai nchi yetu???amazing, wewe ya kwako iko wapi?na unamdai nan?sisi hatuna shida maana nchi yetu ipo

Iko wapi?
 
Njia rahisi ni kuifufua tanganyika ikae meza moja na z'br ijadili muungano,kinyume na hapo ni magumashi tu.
 
Msimamo wa Seif hakuna anayeujua. Anabadili goli kila siku. Hata habari hiyo hapo juu ni mnajimu peke yake anayeweza kutabiri maalim alilenga nini. Hakuna msomi anayeweza kujua anasema nini.

Hakuna kampeni za kumchafua Seif, bali maneno yake chini ya viunga vya minazi yanamchafua.
Tukubaliane kuwa Seif kachoka kifikra, mawazo na kiakili. Naogopa kumuuliza leo anafikiri nini kuhusu Muungano maana anaweza kutoa jibu la aina yake. Mshauri ajitulize na asome mambo kabla ya kutamka hadharani.
Anajichafua sana mliberali huyu.
Mkuu, Takashi hapo kazungumza kweli. Maalimu Seif yupo muwazi zaidi ya kile anachofikiri/anachotaka, kwa mfano alisema atabadilisha Sauti ya Tanzania Zanzibar na TVZ kuwa ZBC na imekuwa sasa katika nchi moja kuwa ni mashirika mawili ya serikali ya habari maana yake nini? Maalim huwa anazumgumzia marekebisho ya muundo huu wa muungano akiwa visiwani lakini akiwa bara muungano anausifu hii inamaana Maalimu si kuwa hautaki muungano ila muundo wake urekebishwe na hii hawezi kuisema bara maana wao wanafaidi matunda yake. Chukulia bonanza la CECAFA timu ya Tanganyika inatumia kila kitu cha muungano mpaka jina la nchi, hii si sawa kabisa.
 
Nakubaliana na wewe lakini tusisahau pamoja na kuwa Watanganyika wako kimya sana na Muungano haimaanishi kuwa wanakosa maamuzi, ni kama vile mtu anawaza 'hivi nikijishughulisha na kuvunja muungano napata nini?". Wengi wana Tanganyika (kwa maoni yangu) wanaona sarakasi za Wazanzibari kwa mashangao au wakati mwingine kwa daharau ingawa wapo Wazanzibari wanawaona akina Maalim Seif kama mashujaa.

Hebu angalia hiki kichekesho; Wazanzibari wapinga Muungano mara ya kwanza walikuwa wanataka serikali tatu (hata CUF Msimamo wao ulikuwa hivyohivyo), baada ya muda wakataka Mkataba (hata kuuelezea walikuwa wanapata shida), na tena mpaka "miungu wao" wanaowaamini akina Ahmed Rajabu haya yalikuwa maoni yao. Ghafla baada ya maswali magumu kuhusu huo mkataba wanaoutaka wakakaa kimya.

Sasa hivi kinara wao Maalim Seif anataka Muungano wa "Jamhuri za Tanzania", tena kuwepo na passport zao na mambo yao ya Ulinzi na Mambo ya nje - kichekesho cha karne.

Wanajua vizuri sana kuwa hayo ni lazima wayapate nje ya Muungano, na dawa yake ni kuuvunja. Hwataki kuvunja lakini wanataka Muungano!!

Hawa ni kupe tu, na huo ukupe ndiyo unawafanya mara sitaki nataka. Na usishangae ikaja single nyingine tena!!
Mark my word: Nyerere pamoja na dosari zoote hakukosea; hawa ni wanajiona wamoja kwa sababu ya Tanganyika, nje ya Tanganyika wanachukiana vibaya sana - nawafahamu.

Lets Zanzibar go, hatutaki "Jamhuri za Tanzania"........Ondokeni kuanzia Dodoma Bungeni, Ofisi ya Makamu wa Rais na acheni fadhila zoote mnazopata............Maana naona mke mwenyewe analishwa lakini kutwa kiguu na njia kulalama.

Hizi lawama wapelekee viongozi wa CCM ,Dodoma. Hao ndio walioapa kuulinda Muungano kwa gharama yeyote ile. Hao ndio wanaosubiri ruhusa kutoka kwa Mungu wao Nyerere. Wa znz wameeleza matakwa yao , na inshaallah kwa uwezo wa Allah , ukombozi hauko mbali. Hakika hakuna chenye mwanzo kisichokua na mwishi.
 
Back
Top Bottom