Jinsi hii thread ilivyoandikwa kwa munkari, inaifanya kuwa biased na kuonyesha chuki binafsi na siasa za MAJITAKA ( Kitchen sink politics)
 
Now I do confirm that "light travels faster than sound.....until you hear them speak".Ha,ha,haaa!
 
The ishu hapa sio what Mwakyembe amesema au hakusema, tatizo hapa ni Muungano na matatizo yake, na huku muafaka, sisi bara we could care less kama hivi vyote viwili vipo au havipo,

Kama una akili ya kutukana kiasi hiki kwa nini usirushie matusi viongozi wako huko visiwani waliokufikisha hapa, yaani kukubali taifa lako liwe mkoa wa Bara, maana you can jump and cry lakini ukweli unaosimama kisheria ni kwamba nchi yako ni mkoa tu wa bara, na rais wako hana tofauti yoyote na RC, ndio maana hata asipokuwepo kwenye mikutano ya cabinet huwa hasubiriwi kwa sababu rais wa jamhuri hawezi subiri RC,

Hatuipendi sana hiii lugha lakini ni wewe mwenyewe unai-provoke na maneno yako ya ubara na uvisiwani, yaani untaka na sisi bara tuanze kutanganza kwenye radio na TV ya taifa maneno ya kuwaomba watoto wasichezee mchanga wa mbele ya nyumba ya Mzee Jang'ombe kama huko kwenu? na viongozi kuanza kuitana kwenye madirisha huko Ikulu kama vile wako mtaaani?

Huko visiwani mnahitaji ku-grow up! sisi Bara tunaondoka hivyo hatuna muda wa kuwasubiri kwanza mpaka mbebane kwenye mikokoteni!
 
Mkuu FMES

Hapa mbavu sina umemkoma nyani Giladi na sifikirii kama atarudi, Du! ubarikiwe tu hizi dana dana nyingine hazina hata mkia.
 
SASA NIMEELEWA, NILIDHANI NAJIBIZANA NA MWIBA, KUMBE MWIBA HUYO NINAYEDHANIA NI MTU NI KITENGO CHA PROPAGANDA CHA CUF NA MJAHIDINA. MIMI SIENDELEI TENA. HAPA HAKUNA HOJA, HAKUNA MANTIKI WALA HAKUNA MAUDHUI - NI CHUKI BINAFSI TUPU NA UDINI. HATUTAFIKA, KWAHERINI! Lazaros
 

asta.............Mkuu pole pole mkuu.......hapo hapo inatosha mkuu......maana unaua.........duuh
 


Sema sema sema !!!!! kaka usiposema tutajuaje ulivyo, tutathibitishaje kuwa hata watu wa dini fulani wakiwa wasomi bado elimu haiwasaidii!!!! sema kaka ili uwe wa mfano humu JF wote tukiwa na akili walimu na viongozi watapatikana vipi??
 

Jee kuna kipengere kwenye Katiba kinachosema kuwa kumpinga Waziri Mkuu ni KOSA? Na jee Mwakyembe au Bunge linauwezo gani juu ya Shamuhuna na nini adhabu ya"kosa" la Shamuhuna kwa kanuni za Bunge?
Usipoyajibu hayo basi Mwakyembe ni fyongo.



Haya yote yangekuwa kuzungumzia umaskini Zanzibar,miundo mbinu mibovu,elimu duni, makazi duni, umeme, hospitali, maji n. tungekuwa mbali sana.Great mind discuss idea.Awe Mwakyembe amekosea awe hajakosea mambo yote ya muungano yana maswali ambayo kuyajibu kwake ni kuvunja muungano.wakati wenzetu ulaya wanaungana Afrika wanagawanyika.JAMANI TUJIONEE HURUMA NCHI YETU IMO KATIKA NCHI ZINAZOONGOZA KWA UMASKINI.KUMBUKENI NYERERE ALISEMA TUKIVUNJA MUUNGANO HUKO VISIWANI NA NYIE LAZIMA MGAWANYIKE. BARA WATAKUWA STABLE.

BADALA YA MWIBA KUFIKIRI MJINASUE KWENYE HALI MLIYONAYO WEWE UNAPIGA KELELE NA MWAKYEMBE HAYA...WAKATI WENZENU WANAWAZA KUFUNGUA SHULE WEWE UNAHIMIZA MADRASA!!!!

MIAKA YOTE HII TANGU 60s Mwiba unagundua leo kuwa muungano una matatizo, mwakyembe amekosea POLE SANA!!!!!!!!!!!!!
 
Watu wenye nguvu nyingi sana za kiuchumi duniani( Ulaya) wanaungana.
Sisi watu duni wa mawazo na tulio nyuma kiuchumi tunataka kugawana vipande vya ardhi ili kila mtu awe Sultan.

Hoja ya msingi inayopelekea Wazanzibari kulalama imefichama kwenye imani yao na asili ya kundi fulani la watu huko visiwani.

Muungano una matatizo hakuna anayebisha, lakini wenzetu wanang'ang'ania suluhisho la namna moja tu.

Mkifanikiwa kuachana na wanabara mtaanza kuwasaka wazanzibara wote visiwani na kuwatimua, wazanzibara wakimalizika wanguja wataambiwa damu yao nao si ya asili ya huko, wanguja wakiisha wapemba wataambiwa kwao ni somalia kismayu, wapemba wakiisha watabakia waarabu wenye damu ya asili ya Omani.

Mwendo huo mie nauita "kwenda Kisengere nyuma" kama Kifulukombe.
 
It is obvious to me that the ill-equipped Shamhuna is either a hopeless zealot, almost Zionistic in nature, or positing himself to be flung into a higher office.It is obvious that Mwakyembe is one of the "Defenders of The Faith" stressing on collective responsibility, a concept I doubt Shamhuna knows the smell of, let alone its intricacies, philosophy and history.

Like a Catholic Cardinal or a Swiss Guard, Mwakyembe faithfully lays down the rules and reminds jokers that you cannot be against your own government. If you do not believe in the leadership of the pontiff and the Pontifex Maximus you cannot be Catholic by definition.Anybody seeing this position as contradictory to his Lowassa indictments misses the important fact that he was acting in a capacity as a Chairman of a presidential Commitee.

While this does not mean he was right in all aspects of his prosecution, if not persecution, of Lowassa, it clearly disqualifies the analogy presented by Mkuu Mwiba.

The big question is, with Shamhuna being a hazy but aspiring pawn in SMZ, is he bound to the concept of collective responsibility to the Union Government?

When the central question is Zanzibari autonomy, this becomes a vicious cycle of two arguments.

Shamhuna believes, or forwards the impression anyway, that Zanzibar is sovereign [sic], Mwakyembe obviously does not subscribe to that.Mwakyembe's criticism is inherently self serving and insufficient as he is imposing collective responsibility on a person disputing the legality of the stated status quo without addressing the facts of the disputed hierarchy.

I call on the article(s) of the Union and their possible ratifications, What are the facts?
 
Kwi kwi kwi chi chi chi!!! heri mimi njomba nisiseme kitu kwenye hii thread.
 
Pundit, there you are! This is the right kind of interaction we need, sober, sound and articulate - not the diatribe we are subjected to by people suffering from paranoia like Mkuu Mwiba and company who see in Dr. Mwakyembe a devil incarnate simply because he did a historical wonderful job of showing Lowassa the door. Wengine tutaendelea kumheshimu kwa hilo, aendelee kufanya hivyo tena na tena!
The question you raise here is pertinent: are the Shamhunas bound by collective ministerial responsibility to the Union Government? My answe is in the affirmative, YES, on grounds which Dr. Mwakyembe may not necessarily subscribe to. I wish he comes forward to elaborate his position as we are doing here.
Let me begin by saying that although the constitutional set up in Tanzania provides for a central government and a regional government for Zanzibar (Wazanzibari msiniue kwa kutumia neno regional, hiyo ni lugha ya kikatiba isiyo na maana ya mkoa), that set-up does not make the system confederal in which the regional government "alone operates directly" upon Zanzibaris. The situation we have is that the central government also operates directly upon Zanzibaris on matters singled out as "union" by the Union Constitution, hence the federal element in the set-up. It is this interactive nature of government operations in Tanzania and Zanzibar in particular which makes the two governments not mutually exclusive, contrary to Shamhuna's thinking.
Wananchi wa Zanzibar wanajua kuwa wanaunda Serikali mbili zinazowahusu moja kwa moja na zenye madaraka tofauti. Hivyo basi Katiba inaweka mazingira kuhakikisha kuwa wananchi hawapewi maagizo yanayokinzana; hawapelekewi ujumbe unaotofautiana na serikali hizi mbili! Hence, Articles 6,8(1)(c),8(2),47(1)(a),126 - 128 etc of the Union Constitution.
Nitoe mfano wa Art.6 inasema: "Katika Sehemu hii ya sura hii, isipokuwa kama maelezo yahitaji vinginevyo neno "Serikali" maana yake ni pamoja na Serikali ya Jamhuri ya Muungano, Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar..." Art.8(1)(c) nayo inasema:"Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni Nchi inayofuata misingi ya demokrasia na haki ya kijamii, na kwa hiyo Serikali itawajibika kwa wananchi".
Hivi akina Shamhuna wanadhani wanawajibika kwa wananchi gani? Wanawajibika kwa wananchi wa Zanzibar kupitia wawakilishi wao walioko Baraza la Wawakilishi na walioko Bunge la Jamhuri ya Muungano! Wawakilishi wa wapigakura wa Zanzibar walioko Bungeni hushiriki katika mchakato wa uteuzi wa Waziri Mkuu. Hivyo Pinda ni waziri Mkuu wa Wazanzibari na Waziri Mkuu wa Watanzania bara! Shamhuna akimtia kidole machoni, anawatia kidole machoni wananchi wake waliomchangua hata yeye kuingia BLW!
Let me end here by thinking aloud on one other aspect. Hivi Shamhuna akija bara, anadhani kwa nini anapokewa kwa ving'ora vya Serikali ya Jamhuri ya Muungano (pamoja na kwamba nafasi yake haiko hata kwenye Katiba ya Zanzibar)? Kwa nini mawaziri wa Zanzibar wakitembelea Tanzania Bara wanatetemekewa na vyombo vya Muungano? It is simply because they are part of the Union set-up, broadly thinking
Nilimsoma juzi Dk. Mwakyembe kwenye gazeti la The African akisema kuwa Katiba imempa Waziri Mkuu madaraka makubwa ya kuwaongoza mawaziri wote wa Jamhuri ya Muungano. Sasa akina Shamhuna hawajui kuwa wanawapa taabu sana mawaziri wenzao kuwapokea wakija bara kutokana na wao kuonyesha kiburi cha kipuuzi kabisa kwa mtu aliyewazidi madaraka?
Niwaombe Wabunge wetu waendelee kuhoji kila kitu kwa uwazi na ukweli. Mambo ya kufichaficha na kuoneana aibu hayatusaidii. Akina Mwakyembe endeleeni na kazi hiyo, hata kama mtatukanwa na akina Mwiba. Ningependa mhoji faida ya kuendelea na structure hii ya Muungano wakati Wazanzibari (akiwemo Karume mwenyewe, ingawa anawatumia akina Shamhuna) waziwazi wanaonyesha hawataki. Hawasemi moja kwa moja kutokana na unafiki na ubabaishaji walionao viongozi tulionao. Siku moja nakumbuka Shamhuna alitamka: "Muungano gani mnauongelea, hivi nyie watu wa bara hamuioni bahari?" Kazi tunayo!
 
Inabidi wakuu wa nchi wakubali kurekebisha kasoro zilizopo. Acheni ubabaishaji bwana. Kama yamewashinda, tuambieni kuliko mara hivi mara vile. Usanii mtupu.
 
Wazanzibar tunawabembeleza mno, waacheni waende zao, kama hawataki waache malumbano na bara waseme wazi. Waziri mkuu amenukuu katiba kwamba Zenj sio nchi, sasa wanataka aseme nchi wakati aliapa kuilinda katiba? Acheni ubabaishaji. Basi semeni katiba ifanyiwe marekebisho ili zanzibar iwe nchi kwa mujibu wa katiba na sio kulalamika kwa mambo yasiyo na msingi. mbona wabara wamepoteza Tanganyika yao na hawalalamiki. Ina maana nyie Zanzibar yenu ni muhimu sana kuliko Tanganyika yetu_
 
Mkumbuke nyie Wazenj bila Muungano mnaoubeza kwa sasa mziki wa Pemba kutaka kujitenga hamtaweza kuuzima. Muwe makini sana msije juta baadae.
 
Tutabaki kulumbana na akina Shamhuna wakati tatizo hasa ni namna RAIS wa Zanzibar anavyopatikana. Sote tumekuwepo na tumeshuhudia jinsi chaguzi za Zanzibar zimekuwa na utata mwingi tangu mwaka 1990.
Kwa jinsi Karume alivyoupata Uraisi, mtu mwenye AKILI timamu hawezi kusema kuwa Zanzibar ni NCHI! Hawa aloowateua wanaelekea KUSAHAU na kuendelea kuropokaropoka tu. Tukiacha uchaguzi HURU ufanyike Zanzibar, wote hawa kesho yake wataihama Zanzibar.
 

Mkuu mwenzangu kwa hapa sikukurupuka kwani ulichosema wewe ni kuwa ni matakwa ya Karume tu kutengeneza nafasi iliyo nje ya katiba kwa makusudi ya Shamuhuna. Nashukuru kuwa umeeleza mwenyewe kuwa kitendo hichi kilishafanywa kabla na hivyo Karume alikuwa akifuata na wala sio utashi wake.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…