ah ha ah ha , kijana unafurahisha sana . bara hamna serikali? hebu leo inamisha kichwa chako dakika kumi kisha fikiri na kisha njoo tena na urudie haya maneno kwamba bara hamna serikali.

Nimefikiria sana, sioni mantiki ya malalamiko yenu, mmepea nafasi za upendeleo kibao kama wale wengine bado hamjaona hilo. Unajua kwa nini tunawapa nafasi za upendeleo?

Think mzee think positively.
 
sina chuki na mtanganyika yeyote kwasababu najua ipo siku nitatumbukizwa kaburini na ,who knows? pengine nitazikwa huko huko tanganyika ,lakini la kweli lisemwe ,tusiwe kama wanasiasa wetu kutetea jambo japo kama tunajuwa liko against reality. tunachotaka wazanzibari ni kutendewa haki katika muungano huu na kama haiwezekani basi tugawane mbao. hivi kwanini watanganyika waikimbie sera ya serikali tatu katika muungano? why? hivi wao hawataki serikali yao? or what? nisaidieni.
 
I will go even further and say that the idea of a nation-state ever since the 1648 Westphalia Conference, not only the Tanzanian Union, the idea itself the world over, has never been as plagued by religious -and I am using that word in the most negative connotation possible- sentimentalism and unwarranted redundancy coupled with unnecesary pageantry, utopian ideals, quixotic goals, collectivist illusions and hope mongering of the highest degree where cold and sometimes unpalatable facts would more than suffice.

The only reason the nation-states of the world are surviving is sentimentalism, fear (of nothing but fear) and the designs of machining politburos full of Machiavellian aspirants and career hot air blowers.
 
Nimefikiria sana, sioni mantiki ya malalamiko yenu, mmepea nafasi za upendeleo kibao kama wale wengine bado hamjaona hilo. Unajua kwa nini tunawapa nafasi za upendeleo?

Think mzee think positively.
unaonekana ni mgeni wa siasa? kwenye siasa unaweza ukaona kwa dhahiri ya mambo unapendelewa lakini kumbe deep inside unakandamizwa , waswahili wanasema siasa ni mchezo mchafu. unaweza ukaona tumependelewa kupewa serikali yetu lakini kumbe serikali yenyewe ni bofu (kivuli) na wale unaowaona hawana serikali kumbe ndio wamebeba nyanzo muhimu zote ndani ya ile serikali inayotambulikana ulimwenguni kote (u.n). who is better?
 

..na mchukuwe tandago za kitanda zenu mwende ..tuone alaa!!!....maneno mengi ya nini....INABIDI KURA YA MAONI IITISHWE .....TUANGALIE NI ASILIMIA NGAPI ZANZIBAR WANATAKA MUUNGANO...BARA HATUNA HAJA YA KUFANYA KURA YA MAONI...WAZANZIBAR WAAMUWE WENYEWE KAMA WANATAKA MUUNGANO AU LA WANATAKA KUJITENDA ..BAADA YA HAPO ...WANAWEZA KUENDELEA KUJITENGA...PEMBA NAO WATATAKA TAIFA LAO...HAMJUI KWANINI CUF WANAUNGA MKONO MUUNGANO UVUNJIKE ..WANATAKA BAADA YA HAPO NAO WAJITENGE MAANA UNGUJA WANAWABANA SANA ..WAKATI WAPEMBA NDIO WASOMI NA WACHAPAKAZI....

SISI WENGI TANGANYIKA TUNATAKA SERIKALI MOJA .....SO HILO NDIO MWELEKEO...HII MAMBO YA SERIKALI MBILI ..NI KUPIGA SIASA......
 

Nisingekwambia think positively. Nashukuru kama umejua hilo!. Na hilo jibu lako inaonyesha nani mkomavu wa siasa, mbona hukusema toka mwanzo kwamba mnafanywa kama watoto watakao pipi kisiasa??? kila mtaa mbunge???

Kama ungekomaa kisiasa ungegundua hilo mapema badala ya mimi kukuwekea wazi!!!!
 
my view. serikali 3 kama haliwezekani basi uvunjwe. sio wa kwanza kuvunjika.
 
Jamani Mods.

Hii topic unganisheni na topic ya Zanzibar. Sioni tofauti kabisa!

labda mi nipo tofauti ila naona hivyo!, inaniwia taabu kuchangia huku na kule!!!
 

Kwa nini bara wanyimwe haki ya kutoa mawazo yao kuhusu hiki kitu? Kuna katabia ka kuwa take for granted watu wa bara. Nao waulizwe. Mimi binafsi naona serikali moja haitufai maana matatizo ya wenzetu yatakuwa yetu!
 
Hapa hapanifai tena naona sasa imekuwa ushabiki kwa rangi zenu ...
 
Mkuu labda usome maneno ya Seleli kule maana hayatofautiani na yangu mkuu! kama ni ualimu labda ujisaidie wewe mkuu, Seleli ameweka wazi nenda ujisomee mkuu elimu yabure kwua Zanibar ni mkoa ndani ya muungano, FULL STOP!

Jee nichukulie kuwa huna hoja tena? Usishangae mwanafunzi kugeuka mwalimu.
Hapo ulipo wewe ndipo tulipoanza kuwa Zanzibar si mkoa bali ni nchi na tunafikiria kurejesha kuja Zanzibar kwa Paspoti. Nafikiri hutoweza kuja tena angalau ukaiona zanzibar ilivyo kwani unaisikia tu hujapatapo kufika.
 

Mkuu kwenye hili hoja zote zimeshasemwa wazi kuwa Zanzibar ni mkoa ndani ya muungano, sasa unapoteza muda wako tu maana mimi sio rais wa jamhuri, wala kiongozi wa serikali na sioni hoja yoyote toka kwako ya muhimu sana kuijadili,

Labda nirudie tu kuwa Zanzibar ni mkoa wa jamhuri ya muungano na rais wenu ni sawa na RC, sasa usichoelewa ni kipi hapa unataka nirudie rudie? Mimi huko ?Zanzibar nikatafute nini? Wala sijawahi kufika huko na sina mpango hata hivi karibuni wa kufika huko nikafanye nini hjasa cha maaana huko?
 
Nimefikiria sana, sioni mantiki ya malalamiko yenu, mmepea nafasi za upendeleo kibao kama wale wengine bado hamjaona hilo. Unajua kwa nini tunawapa nafasi za upendeleo?

Think mzee think positively.

Kutubembeleza tubaki kwenye makucha yenu lakini kama upendeleo hata Wanawake wanapendelewa zaidi kwani lengo liwe asilimia 100.
 

Una haki kuwa na mtizamo huo lakini sio kweli kuwa kuvunjika kwa Muungano kutaleta mgawanyiko Zanzibar. Unguja na Pemba hazikuungana bali ni sehemu za nchi na taifa moja. Kutunyanyasa na kutudharau kwenu kusithibitishe au kuhalalishwa kwa kisingizio cha mgawanyiko wa visiwa vyetu. Tupeni uhuru wa kujiendeleza tuwaonyesheni.
 
Date::8/20/2008
Wabunge washauri serikali ya Mapinduzi Z'bar ifutwe

Tausi Mbowe, Dodoma
Mwananchi

MJADALA wa Muungano umeingia katika sura mpya baada ya wabunge kuibua madai ya kutaka iundwe serikali moja ya Muungano badala ya mfumo wa sasa wa serikali mbili.

Kauli hiyo ya wabunge imetolewa wakati tayari Muungano umekuwa ukitikiswa kwa nguvu kutokana na hoja ya Zanzibar si nchi au la.

Wakichangia makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano), kwa nyakati tofauti wabunge hao, wengi wao wakiwa wanatoka Bara walisema, dawa pekee ya Muungano huo ni kuundwa kwa serikali moja ya Jamhuri ya Muungano, ingawa dawa hiyo ni chungu.

“Dawa pekee ya Muungano ni kuelekea katika serikali moja ya Jamhuri ya Muungano, ingawa dawa hiyo ni chungu lakini hii ndio italeta Utanzania wa kweli, badala ya kuwa na serikali mbili au tatu,” alisema Mbunge wa Mchinga (CCM), Mudhihir Mudhihir.

Mudhihir alisema, mtafaruku unaoendelea sasa kutokea bungeni, ni mazoea na tamaa za utawala kwa baadhi ya viongozi na kulazimisha kulumbana kwa kugombea majina au serikali kila upande, jambo ambalo halina mantiki kwa sababu majina hayo (Tanganyika na Zanzibar) hakuna anayejua maana yake.

Mjadala huo ulionekana wazi kuwagawa wabunge kwa misingi ya utaifa, ambapo Wazanzibari walionyesha wazi kutaka kuundwa kwa serikali tatu, huku Watanganyika wakitaka serikali moja.

Wabunge wa CCM na CUF, wanaotoka katika visiwa vya Zanzibar waliungana katika hoja ya kuwa na serikali tatu.

Awali, Mbunge wa Kongwa, Job Nugai (CCM), alisema ni matarajio yake kuwa na serikali moja ambayo Rais wa Zanzibar atakuwa Makamu wa Rais, itakuwa ndiyo jibu la matatizo ya Muungano na si kuwa na serikali tatu.

Hoja hiyo iliungwa mkono na Mbunge Nkasi, Ponsian Nyami (CCM) na kutahadharisha kuwa iwapo Muungano utavunjika, sababu itakuwa chokochoko za Wazanzibari ambao wameshindwa kuwa wawazi kuhusu mustakabali wa Muungano.

Mbunge wa Kilwa Kaskazini, Samson Mpanda (CCM), alitahadharisha kwamba, Wazanzibari wana kitu wanachokitaka kupitia hoja hiyo na kuwataka wawe wazi badala ya kufanya mambo chini kwa chini kwa kisingizio cha kutaka kuundwa kwa serikali tatu ya Tanganyika.

Mbunge wa Nzega, Lucas Selelii (CCM), aliwaonya watu wanaotaka kuvunja Muungano akisema kuwa, ni hatari kwa kuwa utarudisha nyuma maendeleo ya taifa hili.

Selelii alisema, hasara ya kuvunja Muungano ni kubwa zaidi inavyofikiriwa na kuwataka Watanzania kusonga mbele kwa kuwa na serikali moja badala ya tatu.

Wakati Wabunge kutoka Tanzania Bara, wakitaka kuundwa kwa serikali moja, wabunge kutoka visiwani ambao wote waliosimama kuchangia hoja hiyo walitaka kuundwa kwa serikali ya Tanganyika ili kuwe na serikali tatu.

Mbunge wa viti maalumu, Maulida Komu (Chadema), alisema haungi mkono hoja kwa sababu inamtesa moyoni kutokana na usiri mkubwa uliopo katika hoja hiyo.

Komu ambaye alionyesha kushangazwa na kitendo cha Rais wa Jamhuri ya Muungano kuingia wa kwanza wakati wa sherehe za Mapinduzi ya Zanzibar na Rais wa Zanzibar kuwa wa mwisho.

Alisema hizo ni kasoro za Muungano na kutaka zirekebishwe haraka
kwa kuwa Rais wa Jamhuri ndiye Rais wa Tanzania Bara na Visiwani.

Awali, Mbunge wa Magomeni, Mohamed Amour Chomboh (CCM), alionya watu wanaovaa ngozi ya kondoo wakati ni chui, akimaanisha baadhi ya wabunge waliokuwa wakitoa kauli za kukebehi kama Zanzibar si nchi wakati ina bendera na wimbo wake wa taifa.

Naye Mbunge wa Konde, Dk Ally Taarabu Ally (CUF), alisema umefikia wakati kwa serikali kuwashirikisha wananchi ili kupata suluhisho sahihi la Muungano.

Kauli hiyo pia iliungwa mkono na Kamati ya Bunge ya Katiba, Sheria na Utawala ambayo iliishauri serikali kuchukua changamoto zote zilizojitokeza kuhusu Muungano na kuzipatia ufumbuzi wa kudumu kwa kuwashirikisha wananchi.

Akizungumza kwa niaba ya Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mbunge wa viti maalumu, Pindi Chana, alisema wakati umefika kwa serikali kuanzisha mjadala wa kitaifa kwa lengo la kuwashirikisha wananchi kujadili suala hilo.

Naye msemaji mkuu wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Riziki Omar Juma, alisema muundo na mfumo wa Muungano ndio unaosababisha matatizo hayo, kwa kuwa Katiba ya Jamhuri ya Muungano na sheria

nyingine zimeshindwa kuzingatia na kutambua maana, dhamira na matakwa halisi ya Muungano huo kupitia hati za awali za Muungano.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…