Muungano wa Tanganyika na Zanzibar na kero zake: Je, tuuvunje?
Solution ya hii kitu ni serikali tatu na kuwaacha wachapane bakola wenyewe kwanza.
Tunawabembeleza sana kuliko faida tunayopata, sioni kuna haja gani ya kuwa nao, nchi zote zenye mafuta Africa ni matatizo matupu wao wanafikiri watakuwa exceptional.

Ushauri kwa zanzibar

Daini uhuru wenu ulitekwa na tanganyika ili muwe huru kutumia mafuta yenu peke yenu.
 
sio vyote tuwe tuna Share basi hayo mafuta tuwaachie na sisi tutafute yakwetu

sio kila rasili mali tuwe pomoja
 
Poa tu,

Komoro juzi tu wameomba kujiunga na Bara!

Visiwani hawajui jinsi wengine wanavyolilia kuungana na Bara!

Jawabu malalamishi haya ni Komoro kuwakubalia ombi lao!
 
Fact: zanzibar mwaka jana wamekusanya kodi $20m kwa mwaka na wamesamehe $19m. (ilikua ni mzozo sana mwaka jana kwenye baraza la wawakilishi). bara wanakusanya kodi $300m kwa mwezi na sio $20m kwa mawaka. Kwa hiyo ukae ukijua bajeti ya zanzibar inafadhiliwa na bara.


Wacha upotoshaji. Tangu lini bajeti ya Zanzibar ikabebwa na Serikali ya Muungano? Hebu tupe data.
Kwani hayo makusanyo ya $ 300 millioni kwa bara hata yanatosha kwa Bara kiasi cha kupata ziada ya kuendesha Bajeti ya Zanzibar?
 
Dr. Rashid Mkurugenzi Mkuu TANESCO alikiri mwenyewe kuwa Visiwani wanalipia umeme wao wanavyopenda! Yaani wanalipia kiasi kidogo sana.. na wana deni kubwa sana!

Ni aibu ila ni kweli!
 
Dr. Rashid Mkurugenzi Mkuu TANESCO alikiri mwenyewe kuwa Visiwani wanalipia umeme wao wanavyopenda! Yaani wanalipia kiasi kidogo sana.. na wana deni kubwa sana!

Ni aibu ila ni kweli!

Leo hii unamuamini Dr Rashid
 
zanzibar hawana hela za kujiendesha wenyewe wanaishi kutokana na (kodi na mapato mengine) yatokayo bara.

miaka yote wa bara walikua wanalipia umeme ghali, ili zanzibar watumie bure mbona hawakuwa wanalalamika

kwani hata bara siwanataka hiyo rasilimani mbona ujasema na wao wanaangalia, kutaka iwe yako ni swala jingine na kuangalia ni swala jingingine usichanganye habari.
swala la zanzibar kuangalia rasimali yake sidhani kama ni liatatokea kama wameweza kutoa msamaha wa kodi $19m na wao mapato yao ni $20m.

Zanzibar hawana hella lakini hii haina maana kuwa Tanganyika inabeba umasikini wa Zanzibar. Wazanzibari wako duni kimaisha kwa sababu ya vikwazo vya kiuchumi vinavyowekwa na Tanganyika na wala si kweli kuwa Tanganyika inatowamsaada kwa Zanzibar. Ziko shemu ambazo fedha ya Tanganyika inakwenda Zanzibar. Sehemu hizo ni zile sehemu zinazohakikisha hatamu za kuikalia Zanzibar Kiuchumi zinadumishwa . Sehemu hizo ni majeshi, usalama na vyama vya siasa.
Kuna nyakati Tanganyika hujitangazia hali ya hatari kwa njaa kwa jina la Tanzania na misaada ya Chakula ikija hubaki Tanganyika peke yake. Huu ungekuwa mfano mzuri wa kuonekana kuwa Tanganyika inajali na inasaidia ndugu zao wakati wa shida, lakini wapi hii ni ile Changu changu chako chetu.
 
Visiwani siku zote hata wapewe nini ..yaani hawatachoka kulalamika!

Haya--umeme bei karibu na bure

ulinzi na usamala- Muungano

Mambo ya Muungano--bara!

Bunge la Muungano--Bara

Halafu leo hii kodi husamehe 50% na kukusanya tu 50%!

Sasa hapo kwenye kodi ni nani wa kumlaumu?

Chimbeni basi hata hayo mafuta basi..ni yenu Bara hatutawaingilia!

Ni bora kwanza kuwekeza ktk elimu kwanza..kuwa na Wazanzibari wengi waliosoma..ili kuweza basi kusimamia raslimali hizo zinazodaiwa za mafuta!
 
Last edited:
Jamani, huu Muungano wetu na Zanzibar tuufanye kama Ndoa ya Kiserikali ya kizungu, inajengwa kwa msingi wa upendo, maridhiano na haki sawa. Mke akitaka madaraka zaidi katika kutumia anachozalisha, anapewa uhuru huo. Hata ikifika wakati akajiona mume huyu hana maslahi naye tena, pendo limenyauka, wanavunja mkataba, wanashikana mikono, wanabaki marafiki.

Kama kuna gesi na mafuta ni mali halali ya Zanzibar, kitu ambacho Bara tunapaswa kufanya, ni kuwapa Wanzanzibari kila wanachokitaka bila kuwaburuza.

Hizo pesa za gesi na mafuta kama ni za kutosha, tusiwape pesa za kuendesha serikali yao, yaani wajitegemee. Ufike wakati walipe mpaka umeme na kupunguza kuibeba Zanzibar. Hata uanachama wa OIC tuwape.

tanzania Bara isiwe kama Mume mwenye wivu, akiona mke anafanikiwa, anamdidimiza ili aendelee kuwa tegemezi.

Wapenda haki, waliyoyasoma yale mambo 11 kwenye hati za Muungano za 1964, na namna jinsi yalivyoongezwa mpaka sasa ni 28, atasymphasize na haki za Wazanzibari, hata Hayati Karume akifufuka, akasikia rais wa Zanzibar sio Makamo, ataacha laana kwa bara.

Pamoja na muungano wetu, Tanganyika kufuta utaifa wake na kuitwa Tanzania, Zanzibar ilibaki na utaifa wake kama nchi isiyo na nguvu za dola.

Kuwaachia mafuta yao ni hatua muhimu kuelekea kwenye muungano wa haki sawa wa serikali tatu ambao utaondoa kero
Zote, ama tuiachie Zanzibar ifanye uchaguzi huru, wapinzani wachukue nchi na kuuweka rehani muungano.


PASCO,

Umenizimisha kwa kigezo chako cha Muungano wetu eti mke na mume na kwa mfananisho wako, Zanzibar ni mke.
Wanafaa kupewa talaka tatu wasirudi tena hata wakitaka.Nasikia kuna kisura mwengine (Comorro) anataka mume na ameshamzimia Tanganyika.
 
Dr. Rashid Mkurugenzi Mkuu TANESCO alikiri mwenyewe kuwa Visiwani wanalipia umeme wao wanavyopenda! Yaani wanalipia kiasi kidogo sana.. na wana deni kubwa sana!

Ni aibu ila ni kweli!


Tutalipa hilo deni kwa mafuta isiwe nongwa kudaiwa Zanzibar wakati hata hao TANESCO wenyewe mbona wahoi kwa madeni. Deni si wizi wala unyanganyi.
 
Bara tunaona ni heri mali zilizo ardhini, madini na gas, ziwafaidishe kina barrick na wenzao kwa kuwawacha wachimbe kiholela kuliko kuzitumbukiza katika Muungano ili ndugu zetu wa Zanzibar na wao wafaidike, japo kidogo! lakini kwa kuwa wao wanyonge basi hata mafuta au gas ikiwepo huko, na sisi ni yetu.

Jamani, kwa hili inabidi aidha tuwakubalie, chao ni chao na chetu ni chetu, au, chao ni chetu na chetu ni chao, lakini hii ya, chao ni chetu na chetu ni chetu, haikubaliki kabisa ni dhulma ya wazi wazi.

Nawaunga mkono wa Zanzibar kwa kudai haki yao na nadhani katika hili wameungana na hawana huyu ni chama gani.
 
Visiwani siku zote hata wapewe nini ..yaani hawatachoka kulalamika!

Haya--umeme bei karibu na bure

ulinzi na usamala- Muungano

Mambo ya Muungano--bara!

Bunge la Muungano--Bara

Halafu leo hii kodi husamehe 50% ya kiasi kinachokusanywa!

Sasa hapo kwenye kodi ni nani wa kumlaumu?

Umeme unauzwa kwa bei ya juu Zanzibar, kumbuka mgogoro wa suala hilo.

Ulinzi na usalama wa kitu gani? Tumezungukwa na bahari na nchi iliyokaribu labda itakuwa na interest na visiwa vyetu ni Tanganyika hao wanaotulinda.
Kuhusu Usalama Fedha tunazowalipa JKU, KMKM, Valantia zingetosha kuwalipia polisi wetu kwanza hatuhitaji polisi wengi ikiwa tutathibiti uuingiaji wa majambazi kutoka nje.
Hakuna mambo ya Muungano bali mambo ya Tanganyika na hata Bunge ni la Tanganyika. Mambo mangapi yanayozungumzwa ndani ya Bunge yanayohusu Zanzibar?
Kodi mnayotoza hatuna uwezo wa kuilipa. Tutalipia nini ikiwa njia zote za uchumi mmezifunga?
Tungeruhusiwa Bandari huru tungepata fedha za kulipia kodi, tungeachiwa tupate misaada kwa kujiunga na mashirika ya misaada tungeiendeleza nchi na kupata uwezo wa kulipia kodi kubwa.
SAsa tunachotaka tuchimbe mafuta yetu ili tupate kulipa kodi kubwa MZALENDOHALISI anazuia.Vyereje?
 
Kodi mnayotoza hatuna uwezo wa kuilipa. Tutalipia nini ikiwa njia zote za uchumi mmezifunga?
Tungeruhusiwa Bandari huru tungepata fedha za kulipia kodi, tungeachiwa tupate misaada kwa kujiunga na mashirika ya misaada tungeiendeleza nchi na kupata uwezo wa kulipia kodi kubwa.
SAsa tunachotaka tuchimbe mafuta yetu ili tupate kulipa kodi kubwa MZALENDOHALISI anazuia.Vyereje?

bandari ikiwa huru inamaanisha z'bar itakosa robo tatu ya mapato ya kodi. si utaua nchi.

credit crunch bado unaongelea mambo ya misaada...

angalia mkoa wa kinondoni una watu sawasawa na z'bar lakini angalia z'bar ilivyokuwa na viongozi wengi...

mwanza ni kubwa na idadi ya watu ni mara mbili na uchumi wake ni mkubwa kuliko wa z'bar. ni uongozi wenu ndio unaharibu z'bar na sio bara. z'bzr needs efficient management, na sio "hapa pangu".
 
bandari ikiwa huru inamaanisha z'bar itakosa robo tatu ya mapato ya kodi. si utaua nchi.

credit crunch bado unaongelea mambo ya misaada...

angalia mkoa wa kinondoni una watu sawasawa na z'bar lakini angalia z'bar ilivyokuwa na viongozi wengi...

mwanza ni kubwa na idadi ya watu ni mara mbili na uchumi wake ni mkubwa kuliko wa z'bar. ni uongozi wenu ndio unaharibu z'bar na sio bara. z'bzr needs efficient management, na sio "hapa pangu".


Mafuta yaongeza mgogoro wa Muungano

Na Salma Said, Zanzibar

KUNA dalili kwamba mzimu wa Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere kuhusu Zanzibar, unaanza kuumomonyoa Muundo wa Serikali ya Muungano, baada ya wawakilishi wa CCM na CUF kuungana na kudai kuna upungufu mwingi katika mambo yaliyokubaliwa katika hati ya Muungano mwaka 1964.


Madai hayo yalitolewa jana wakati wajumbe wa Baraza la wawakilishi walipokuwa wakichangia mjadala baada ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ), kuwasilisha taarifa yake juu ya mapendekezo ya uendeshaji wa kazi ya utafutaji na uchimbaji mafuta na gesi asilia katika visiwa hivyo.


Kikao hicho kilichoongozwa na Ali Mzee Ali kilielezea mengi kutoka kwa wajumbe kuhusiana na kutoridhishwa na ushauri wa Mshauri Mwelekezi juu ya utafutaji wa mafuta na gesi asilia.

Mwakilishi wa Jimbo la Mkanyageni (CUF) Haji Faki Shaali alisema, hakuna haja ya SMZ kukubali kulifanya suala la mafuta na gesi asilia, kuwa chini ya Muungano.


Akitolea mfano Muungano wa nchi za Kifalme za Emirates (UAE), Shaali alisema, kila nchi katika muungano huo inatumia rasilimali zake bila kuingiliwa na nyingine.


Naye mwakilishi wa jimbo la Amani (CCM), Ali Denge Makame alisema kutokana na Tanzania Bara kuwa na rasilimali nyingi, ni busara mafuta na gesi asilia iliyoko Zanzibar, vikaachiwa SMZ kama ilivyo tanzanite, dhahabu na madini kwa Tanzania bara.


Aliwashauri wawakilishi wenzake waafiki mpango wa kukataa pendekezo la kutumiwa kwa maeneo ya bahari kuu na Serikali ya Muungano kutokana na eneo hilo kuwa la Zanzibar na lina vyanzo vingi vya nishati.


Kiongozi wa upinzani katika Baraza la wawakilishi Abubakar Khamis Bakari, alisema suala la mafuta liliingizwa kinyemelela kwa hila za Rais Nyerere katika mambo ya Muungano.

Bakari alisema, chini ya mfumo wa chama kushika hatamu, Serikali ya Muungano chini ya uongozi wa Hayati Nyerere, ilitumbukizwa suala la mafuta na gesi bila ridhaa ya SMZ licha ya kuwa hatua kadhaa zilichukuliwa kutaka suala hilo litolewe.


“Mwaka 1984 mimi nilikuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali. Nilipoona dalili chafu, niliwaendea wakubwa wangu Rais marehemu Idris Abdul Wakil na Waziri Kiongozi wake Maalim Seif Sharif Hamad kuwaeleza kuna tatizo na wao wakaniambia niende Tanganyika kwa majadiliano zaidi,” alisema.


Alisema alipofika Tanganyika, alikutana na Waziri Mkuu Dk Salim Ahmed Salim na Mwanasheria Mkuu wa serikali wakati huo akiwa Jaji Joseph Warioba na kwenda nao hadi Msasani nyumbani kwa Mwalimu Nyerere kujadili suala hilo kwa undani.


Khamis alizidi kuliambia Baraza la Wawakilishi kuwa, Nyerere alikubali kuwa jambo hilo limeingizwa kinyemela na litashughulikiwa kisheria lakini jambo la kushangaza hadi leo hii limebaki bila kutolewa uamuzi.


Mwakilishi huyo alimtahadharisha Waziri wa Maji, Ujenzi, Nishati na Ardhi, Mansoor Yusuf Himid kwamba, asikubali kuahidiwa urais na kuanza kuwageuka wawakilishi wenzake na ikiwa atafanya hivyo, atahukumiwa na umma wa Wazanzibari.


Akichangia mjadala huo Mwakilishi wa Jimbo la Magomeni (CCM) Salmin Awadh Salmin, aliitaka SMZ kufanya haraka kuunda chombo cha Udhibiti na Usimamizi wa nishati ya Mafuta na Gesi Asilia bila kuzubaa na kusubiri kwani wakati wake umeshafika kufanya hivyo.


“SMZ iunde ZPDC yake haraka haraka kama ilivyofanya wakati wa kuunda Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa serikali na Elimu ya Juu na hilo halina haja ya kusubiri ushauri wa mtaalam mwelekezi” Alisema mwakilishi huyo huku akipongezwa na pande mbili za vyama hivyo.


Salmin alisema, hata suala la uvuvi katika bahari kuu ni la muungano lakini Serikali ya Muungano inaendesha kazi hizo bila kuishirikisha SMZ.


Mwakilishi wa Chambani (CUF) Abass Juma Muhunzi alisema, utata wa mafuta na gesi asilia ni matokeo ya kuchezewa na kufinyangwafinyangwa kwa mkataba wenye masuala 11 ya muungano mwaka 1964 na kuongezwa mambo mengine bila idhini ya Wazanzibari.


Muhunzi alisema Zanzibar imepoteza sauti katika medani za Kimataifa na sasa inadidimia kiuchumi na hata taasisi za kimataifa na kampuni kubwa ziko Bara.


Kwa upande wake mwakilishi wa Jimbo la Gando (CUF) Said Ali Mbarouk, alisema huenda sheria ya mafuta kutajwa kuwa itafanya kazi Tanzania Bara na Tanzania Visiwani, imekusudiwa katika visiwa vya SongoSongo, Mafia na Ukerewe na si Zanzibar.


Awali akiahirisha kikao hicho jana mchana, Spika wa Baraza la Wawakilishi Pandu Ameir Kificho, aliwataka wawakilishi kujadili hoja hiyo bila jazba kwa lengo la kujenga na kutazama maslahi ya umma.


Spika huyo na Waziri Kiongozi wa SMZ Shamsi Vuia Nahodha, hawakuhudhuria kikao cha majadilano hayo kilichoanza saa 11 jioni hadi saa 1.45 usiku.


Kesho wawakilishi hao wanatarajia kuendelea na mjadala huo wakijadili ripoti ya Mshauri Mwelekezi na maoni ya serikali yaliowasilishwa katika kikao hicho.
 
Serikali ya Mungano (Bara) wanafanya kila hila kuimaliza Zanzibar kiuchumi, ili tu ifikie mahali Wazanzibari waseme tumeshindwa kujiendesha. Na ndio maana kila kitu chenye nia ya kuinua Zanzibar, inasemwa kipelekwe kwenye mamlaka ya Muungano.
Haya yote ni janja ya Serikali mbili kuelekea moja, kwamba mamlaka ya Zanzibar ifutwe kabisa.
Viongozi wa Bara waelewe suala la Serikali moja lilishachelewa na haliwezekani tena kutokea! Wazanzibari macho mawili wanatazama.
Just wacheni ujanja na boresheni mbili zilizopo, ili kila moja ijue mipaka yake na bila ya kuathiri utendaji wa Serikali nyengine.
MKIZIDI KUTUSUKUMA KWENYE SERIKALI MOJA! NA HIZI MBILI PIA MTAZIKOSA SOON.
 
Fact: zanzibar mwaka jana wamekusanya kodi $20m kwa mwaka na wamesamehe $19m. (ilikua ni mzozo sana mwaka jana kwenye baraza la wawakilishi). bara wanakusanya kodi $300m kwa mwezi na sio $20m kwa mawaka. Kwa hiyo ukae ukijua bajeti ya zanzibar inafadhiliwa na bara.

Habari kutoka gazeti la udaku nini?

KUNA HII HABARI HAPA ISOME!

Zanzibar yavuka lengo la ukusanyaji kodi kwa mwezi

2008-06-12 16:33:46
Na Moris Lyimo, Jijini

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imekusanya jumla ya shilingi bilioni 8.2 na kuruka lengo la kukusanya bilioni 7. 2 kutoka kwenye vyanzo mbalimbali vya mapato katika kipindi cha mwezi Machi Mwaka huu.

Taarifa ya hali ya uchumi ya kila mwezi inayotolewa na Benki Kuu ya Tanzania, imesema ongezeko hilo ambalo ni sawa na asilimia 13.9, imetokana zaidi na ongezeko la bidhaa zinazoingizwa nchini na kodi za bidhaa.

Pia ongozeko hilo ni kutokana na ongezeko la marejesho ya mapato ya kodi, uhusiano kati ya wakala wa ukusanyaji kodi ambao ni Mamlaka ya Mapato nchini, TRA na Bodi ya Mapato Zanzibar, ZRB.

Inasema taarifa hiyo kuwa viwango vya kodi katika kipindi hicho ilikuwa ni Shilingi Bilioni 1.6 iliyotokana na makusanyo ya kodi za bidhaa zinazoingia na kuzidi lengo la bilioni 1.4 zilizotakiwa kukusanywa kwa kipindi hicho.

Kodi ya ushuru wa forodha imechangia Sh. Bilioni 2.4 na kupita lengo la Sh. Bilioni 2.2, hivyo kufanya makusanyo ya kodi katika eneo hilo kufikia asilimia 33.3.

Pia hali nzuri ya makusanyo y visiwani humo katika kipindi hicho yametajwa kuwa ni kutokana na hali nzuri ya kodi ya sekta ya utalii na marejesho kutoka bara.

Taarifa inaendelea kueleza kuwa kodi ya mapato iliyokusanywa ni kiasi cha Shilinghi Bilioni Moja juu ya lengo la kukusanya mapato ya aina hiyo ambayo yalikuwa ni Sh. Milioni 900 yatokanayo na marejesho ya kodi ya mapato wakati makusanyo mengine yalifikia Sh.Bilioni 2.1 na kuzidi lengo la kukusanya Sh. Bilioni Mbili.

Mapato yaliyotokana na taasisi zisizolipa kodi yalikuwa Sh. Milioni 900 ambayo ni juu ya lengo la Sh. Milioni 500 zilizotokana na ongezeko la makusanyo ya wizara na kufikia asilimia11.0 ya mapato yote.

Benki Kuu imeongeza katika taarifa yake hiyo kuwa kwa kipindi cha Julai mwaka jana hadi Machi mwaka huu, makusanyo yalifikia Sh. Bilioni 67.6, hivyo kupita lengo la makusanyo ya sh. Sh. Bilioni 65.5 kwa asilimia 2.1.

* SOURCE: Alasiri
 
Last edited:
Jengine Semilong

Kama unajua ukubwa wa Zanzibar na watu wake, umeshapata jibu kwamba hayo mapato yao yangewatosheleza wenyewe.

Ukubwa wa pua sio wingi wa makamasi.

Hata Singapore ni nchi ndogo sana barani Asia lakini inajitosheleza yenyewe nakushinda ufukara wa nchi kubwa kama INDIA
 
Nyingine hii hapa




Bajeti ya Serikali ya Zanzibar kusomwa leo Na Salma Said, Zanzibar

BAJETI ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) ya mwaka wa fedha wa 2008/09 itasoma leo jioni kwenye Ukumbi wa Baraza la Wawakilishi na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais anayeshughulikia Fedha na Uchumi, Dk Mwinyihaji Makame Mwadini.


Katibu wa Baraza la Wawakilishi, Ibrahim Mzee alisema maandalizi yote yamekamilika na kikao hicho kitaanza asubuhi kwa maswali na majibu na jioni Bajeti ya Serikali itasomwa na waziri anayehusika.


Akitoa muhtasari wa bajeti hiyo, Waziri Makame alisema kasi ya ukuaji wa uchumi imekuwa na kufikia 6.8 kutoka asilimia 6.5 katika kipindi cha mwaka jana.


Mwelekeo wa bajeti ya mwaka wa fedha wa 2008/09 umepewa jina la Bajeti ya Maendeleo kutokana na sehemu kubwa ya bajeti hiyo ikiielekezwa kwenye shughuli za maendeleo kuliko matumizi ya kawaida ambapo asilimia 28.7 imeelekezwa kwenye matumizi ya kawaida.


Alisema kasi ya ukuaji wa uchumi wa pato la taifa inatarajiwa kuongezeka kutoka ukuaji wa wa asilimia 6.5 mwaka 2007 hadi asilimia 6.8 mwaka 2008 huku serikali ikihitaji kutekeleza kwa ukamilifu Mkakati wa Kukuza Uchumi na Kupunguza Umasikini.


Waziri huyo amesema serikali itaendelea kutoa msisitizo kwenye maendeleo ya kilimo na miundombinu kama sekta saidizi.


Dk Mwinyihaji alisema hali ya matatizo yanayoendelea duniani matarajio ya awali yalionesha kuwa uchumi wa Zanzibar kwa mwaka wa fedha 2008/09 utaendelea kuimarika licha ya athari za umeme zuilizojitokeza kwa mwezi mzima sasa.


Alisema kwa mwaka wa fedha 2008/09, serikali inakusudia kutekeleza programu 20 zikiwemo programu mpya tano na miradi ya maendeleo 64, kati yake imo miradi mipya 13.


Alisema malengo ya mpango wa bajeti ya mwaka 2008/09 serikali imelenga kukusanya mapato ya ndani yenye jumla ya Sh134.550 billioni sawa na asilimia 21.4 ya pato la taifa kati ya mapato hayo Sh 124.709 billioni yanayokana na mapato ya kodi na Sh 9.841 billioni yanayokana na mapato yasiokuwa ya kodi.


Dk. Mwinyihaji alisema serikali katika kipindi cha mwaka wa fedha inategemea kupokea misaada na mikopo kutoka nje yenye thamani ya Sh 205.16 billioni inayojumuisha Sh 23.407 billioni ambazo ni mgao wa asilimia 4.5 ya misaada ya kibajeti (GBS) kupitia serikali ya muungano.


Kati ya fedha hizo zimo pia Sh.8 billioni kutoka Mpango wa Misahama ya Madeni (MDRI).


Serikali alisema pia itaendelea kukopa kwa nia ya kuziba pengo la bajeti kutoka fedha za ndani kwa kupitia mfumo wa Hati Fungate za Serikali ambapo mikopo hiyo imepangwa kupunguzwa mwaka hadi mwaka kwa lengo la kuepukana na athari za kiuchumi ambapo jumla ya Sh 2.0 billioni zitapatikana kupitia kiazio hicho.


Mapato ya viazio vyote hivyo Dk Mwinyihaji amesema yanajumuisha uwezo wa serikali katika bajeti ya mwaka wa fedha 2008-09 huku jumla ya mapato yote ni Sh 341.709 billioni.


Waziri huyo alisema serikali ilikadiria kukusanya jumla ya Sh 114.5 billioni mapato ya ndani ikiwa ni asilimia 37.7 zaidi ya makadirio ya mwaka 2006/07 ya Sh 83.1 billioni kiwango hicho cha makadirio ya mapato ya ndani ni sawa na asilimia 17.2 ya pato la taifa kwa mwaka 2007.


Alisema utekelezaji halisi hadi mwezi Machi 2008 ulifikia asilimia 73.6 ya lengo la mwaka sawa na Sh. 84.3 billioni na matarajio ya makusanyo hadi mwisho wa Juni 2008 ni kufikia Sh111.4 billioni sawa na asilimia 97.3 ya lengo kwa mwaka.


Misaada na mikopo kutoka nje hadi mwezi Machi 2008 serikali ilipata Sh 49.1 billioni sawa na asilimia 41.2 ya makadirio ya Sh 119.1 billioni huku upande wa misaada ya kibajeti (GBS) serikali ilipokea Sh 26.1 sawa na asilimia 96.5 katika jumla ya Sh 27.1 billioni zilizopangwa kutolewa mwaka mzima.


Kwa mwaka wa fedha wa 2008/09 matumizi ya kazi za kawaida itakuwa Sh149.4 billioni sawa na asuilimia 43.7 ya matumizi yote huku matumizi ya kazi za maendeleo jumla ya Sh 192.2 billioni sawa na asilimia 56.3 ya matumizi yote yaliopangwa.


Kati ya fedha hizo, Sh 18.5 billioni ni mchango wa serikali na Sh 173.7 billioni zitatokana kwa wahisani wa maendeleo.
 
Na Ali Suleiman, Zanzibar

BAJETI ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) itasomwa leo jioni huku ikionesha kuwapo kiwango cha ukuaji wa uchumi na kuimarika kwa sekta ya utalii na uwekezaji.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Fedha na Uchumi, Dkt. Mwinyihaji Makame, anatarajiwa kuwasilisha makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2008/9 hapo katika kikao cha Baraza la Wawakilishi.

Maandalizi ya kikao hicho yamekamilika na wajumbe wa Baraza la Wawakilishi kutoka kambi ya CCM kwa muda wa siku moja walikuwa wamejichimbia Kiwengwa.

Wajumbe hao walikuwa wakipigwa msasa na Makamu Mwenyekiti wa CCM, Zanzibar, Rais Amani Abeid Karume, akiwataka kuelekeza juhudi na nguvu zao katika majimbo ya uchaguzi kwa ajili ya kuleta maendeleo.

Rais Karume alisema mwakilishi bora ni anayeshughulikia matatizo ya wananchi katika jimbo alimochaguliwa na ambaye pia yuko mstari wa mbele kusaidia maendeleo katika jimbo lingine bila ya kujali itikadi za kisiasa.

Taarifa za Ofisi ya Rais, Fedha na Uchumi ilisema uchumi umekua kwa asilimia 6.8 na kusema tatizo la kukosekana kwa nishati ya umeme kwa mwezi mmoja sasa, halijaathiri mwelekeo wa uchumi.


Baadhi ya mambo ambayo yanatajwa kuchangia ukuaji wa uchumi ni uwekezaji kwa asilimia 37.5 kutoka sh. bilioni 101.3 mwaka juzi hadi sh. bilioni 139.3 mwaka jana.

Pia kuimarika kwa sekta ya utalii na uwekezaji vimechangia kwa kiasi kikubwa ukuaji uchumi ambapo jumla ya watalii 137,111 waliingia nchini mwaka juzi na kiwango kuongezeka hadi 143,265 mwaka jana sawa na ongezeko la asilimia 4.5. (Majira)
 
Kitu kimoja najiuliza kila siku kuwa hawa Serikali ya Muungano na Zanzibar huwa hawakai pamoja na kuelezana ukweli au vipi . Nzanzibar inapata 4.5% kutoka kwenye kodi ya mapato ya Muungano ambayo yanakusanywa Tanzania bar, wakati yale yanayokusanywa Tanzania Visiwani yanabaki huko Visiwani kwa 100%.

Mapato yanayotokana na Gas yote hukusanywa na TPDC na kupelekwa hazina, Mapato yanayotokana na kodi za madini hukusanywa na Wizara ya Nishati na Madini na kupelekwa Hazina.

TPDC pekee yake inakusanya mapato yasiyopungua 17 Billion Ths kwa mwaka , je 4.5% ya 17 Billion Tshs ni ngapi???? na Je , Wanzanzibar wanaopewa huo mgao ni % ngapi ya Wa Tanzania wote. Kwa hiyo hadi hapo inaonesha kuwa mapato ya Gas wanapata na Mapato ya madini wanapata by 4.5% hilo halina mjadala.

Labda kama kuna agenta ingine inayofanya Gas na mafuta viwe vyao lakini isiwe kwenye mapato ya Gas na Madini.
 
Back
Top Bottom