Nafikiri kuna haja ya kuweka vugu nvugu jipya sasa kukikomboa kizazi hiki kipya. Hapo zamani waliokuwa wanaweza kusema wakibanwa. Lakini sasa alhamdullillah. sasa mnaoweza kutoa maoni mshirikiane mkizindue kizazi kipya. kielewe ubabaishaji huu ambao umefanyika katika zama za ukoloni na vyama vyote hivyo- vikatumia nguvu za wazalendo (washirazi wa Kipemba, Kihadimu na kitumbatu) kujiimarisha. Baadaye mapinduzi nasikitika kuwa mapinduzi hayo hayakuwanufaisha ipasavyo hao Washirazi wazalendo
bali wameburuzwa tu huku Waafrika wakishika himaya, na sasa katika mfumo wa vyama vingi naona Washirazi hao wanaburuzwa tu(ama wawe CCM ama wawe CUF). Ukweli wao ndio wenye nguvu kutokana na wingi wao,lakini wapi bado ni victims tu. sasa hawa ni hao walioko Chokocho. Paje, Kidoti, Fumba na kadhalika siyo wenye jamaa zao Dubai, Songea, Anjuwani, Mombasa au hadharamut au London au Scandinavia.