Buchanan,......Sijazungumzia wale ambao wameoana na Wabara na hakuna unyanyapaa wowote! Sasa hizi kauli za akina Seif anapodai kuwa "kajitu toka Bara" (akimaanisha Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba) kuhoji mambo ya Zanzibar hazionyeshi nia njema na zinawafanya watu kuanza kuhoji kulikoni! Kwani hakuna lugha ya kistaarabu ya kutamka, hata kama kweli Wazanzibari wameingiliwa? ........!
Kwani nani kasema kajitu toka bara ina maana ya Makamba? Kwani haiwezi kuwa JK? Hapa tatizo ni lugha? Nadhani hii lugha haijamtukana wala kumdhalilisha yeyote, inajaribu kutoa muonekano wa mtu ambaye hana maamuzi yoyote ya maana... na ndiyo maana maamuzi yote katika mazungumzo yaliyofikiwa katika mchakato wa CUF na CCM iliyohusisha wabara hazijafanikiwa including JK mwenyewe ambaye ktk hotuba yake alisema mpasuko ni kipaumbele lakini alishindwa kupiga hatua kama rais na kama mwenyekiti wa CCM. Sasa kama wazanzibari wamekutana na kupiga hatua si lazima wao ndiyo waonekane watu kwa sababu wamefikia maamuzi? Watu ambao hawana maamuzi kama akina Makamba lazima wasemwe vijitu.....