Among the Many books that have been written about the Zanzibar Revolution ;I suggest for those who haven't already read," The Revolution in Zanzibar" by Don Petterson is a worthwhile read.
 
Uhuni uliofanyika Janury 12, 1964( unfortunately leo "tunaadhimisha") ndio donda sugu linaloleta political instability visiwani mpaka leo.

Ndio maana kila nikisikia "mazungumzo ya muafaka" I fall off my chair laughing.....
 
Uhuni uliofanyika Janury 12, 1964( unfortunately leo "tunaadhimisha") ndio donda sugu linaloleta political instability visiwani mpaka leo.
Kamanda yale ni Mapinduzi....
Nakutakia kila la Heri katika kusherehekea siku hii adhimu
 
Na Salma Said, Zanzibar (Mwananchi)
WAKATI leo Wazanzibari wanasherehekea leo miaka 44 ya Mapinduzi, kuna baadhi ya

washiriki wa mapinduzi hayo wanajutia vitendo vilivyofanywa wakati huo.


Akizungumza kwa masikitiko jana, mshiriki mmoja ambaye hatajwi sana katika wana mapinduzi, Ali Omar Juma (Lumumba) alisema anajutia vitendo alivyofanya kila

zinapomjia fikra za mauaji ambapo nyumba zilivamiwa na kuporwa.


Mzee Lumumba ambaye hivi sasa anaishi katika maisha duni Mtoni Nje kidogo na Mji wa Zanzibar, hakutarajia kuishi maisha hayo kutokana na mchango wake mkubwa katika mapinduzi hayo.


Alisema kwamba wakati wakifanya hivyo, walikuwa na lengo na kujikomboa lakini kuna baadhi ya watu walikuwa na malengo mengine ambayo yalikwenda kinyume na utu wa ubinadamu.


Sherehe za Mapinduzi huadhimishwa kila ifikapo Januari 12 ambapo siku kama hiyo ndio Zanzibar ilipinduliwa na wazalendo na kuuangusha utawala wa kisultani uliokuwa ukiongozwa na Jamshid Bin Abdaalah.


Katika kusherehekea Mapinduzi miradi kadhaa hufunguliwa visiwani hapa ikiwemo

mashule, vituo vya afya na na barabara ambapo viongozi wa kitaifa hushiriki katika

maadhimisho hayo.


Utawala wa kisultani ulijikita kwa miaka kadhaa Zanzibar huku wazalendo wakikosa

fursa na haki za nchi yao kutokana na ubaguzi uliokuwepo ambapo baada ya kufanyika

Mapinduzi haki zote zilirudi kwa raia wa Zanzibar.


Mapinduzi hayo yaliongozwa na Jemedari Hayati Mzee Abeid Amani Karume akiongozana na wenzake ambao waliunda timu ya watu 14 iliyokuwa ikiratibu na kushughulikia mchakato wa kufanyika Mapinduzi pamoja na kundi la Umma Party ambao kwa kiasi kikubwa walifanikisha mapinduzi hayo.
 
Fainali uzeeni, mara baada ya mapindunzi wengi, walianza kuishi maisha ya anasa kubwa na kujisahau kabisa katika kuwekeza nguvu zao mara baada ya kustaafu. Sasa nguvu zimewaishia wanaanza kulia lia...!
 
Fainali uzeeni, mara baada ya mapindunzi wengi, walianza kuishi maisha ya anasa kubwa na kujisahau kabisa katika kuwekeza nguvu zao mara baada ya kustaafu. Sasa nguvu zimewaishia wanaanza kulia lia...!

wengine walisahau kuwa kuna uzee wakawa wanapigania vimwana vya kimanga.

walisahau hata dhamira za chama chao kuwa ni kuwakomboa wanyonge hasa wa kiafrika.
 

Mkuu utakuwaje ukweli wakati hata haujui CCM ilizaliwa lini?

Kama ni kweli simulizi zilizotolew humu, inatakiwa watu wa Zanzibar mumpe heshima za pekee Mwalimu Nyerere (RIP). Huyu ndiye aliyewahifadhia Sultan baada ya kukataliwa na Kenya, huyu ndiye aliyetuma askari kumbana Field Marshall na ndiye aliyewaongolea jina mizi Okello miongini mwao. Ni Mwalimu tena baada ya kuuawa kwa Karume (RIP) ndiye aliyewahifadhi wakina Babu na kuwaepusha yale yaliyowapata wakina Hanga, Mdungi na wengine. Badala ya kushinda kulaumu inabidi waangalie vyema historia yao na wawape credit wale wanaostahili! Kumbe hiyo Tanganyika ambayo hamishi kuisemea ovyo ndiyo kila wakati imekuwa kimbilio lenu wakati wa matatizo.
 
Mkuu utakuwaje ukweli wakati hata haujui CCM ilizaliwa lini?

inatakiwa watu wa Zanzibar mumpe heshima za pekee Mwalimu Nyerere (RIP).

Heshima ya Mwl. Nyerere ipo pale pale... kwa kuweza kuyatambua mapinduzi ya Zenj. Ili jina lake lisipotee barabara moja mjini Zenj imepewa jina lake...
 

Usimnange mwenzio, kapitiwa tu kama ilivyokutokea wewe hapo juu!
 
Historia ya mwafrika huenda sambamba na Umaskini, kutawaliwa na fitna. Hadi hapo tutakapo jua nini thamani ya UHURU na malengo ya mapinduzi kuondoa vitu hivyo na sio kuvidumisha ndipo mwafrika ataweza ona pepo ya hapa duniani.
Besides that sisi sote manyani tu! uhuru na salama yetu ni kuishi juu ya miti.
 
Usimnange mwenzio, kapitiwa tu kama ilivyokutokea wewe hapo juu!

Asante Mkuu! Mwenyezi anajinsi ya kutuumbua sisi wenye mazoea ya kujifanya wajuaji kupita kiasi. Samahani Mtu wa Pwani kwa kukunanga(?) kama alivyosema Kithuku.
 
Mtindo:Wa MAPINDUZI !!
Umma party kwa kushirikiana na ASP

Na ASP kushirikiana na TANU

Na TANU kushirikiana na Muingereza na Mmarekani yamefanikishwa Mapinduzi!!

Umma party wamepinduliwa kwa kutumiwa ASP

Na ASP wamepinduliwa na TANU

Na TANU wamepinduliwa na Mmarekani na Muingereza na kuitwa CCM !!
Sasa kuna ishara ya Muingereza na Mmarekani kuipinduwa CCM baada ya kumaliza kazi waliopewa!!

Na ndio maana Mapinduzi yakawa DAIMA.
 
Nimesoma kwa uangalifu, makala zote hapo juu kuhusu mjadala huu. Ni lazima nikiri mimi ni mgeni katika ukumbi huu wa JF na siku shiriki, hata kwa kusoma tu, wakati suala hili lilipojadiliwa siku hizo za awali, hata hivyo, ningeomba nami nitowe mawazo yangu kama ifuatavyo.

Sultani alikuwa na haki ya kutawala Oman. Kimsingi alikuwa hana haki ya kuitawala Zanzibar. Alipohamishia Makao Makuu ya utawala wake kutoka Oman na kuyaleta Zanzibar, alikuwa hawatendei haki Wazanzibar. Alikuwa akitawala Zanzibar kwa nguvu na hakuwa na tofauti yoyote na Wakoloni wengine. Hata Waingereza walikabidhiwa Zanzibar na pwani yote ya Kenya na Sultan kwa ulinzi wa himaya ya Sultani na Sultani mwenyewe kwa jumla.

Kwa ajili hiyo, hoja ya kusema kuwa Sultani hakuwa na serikali wakati Mohammed Shamte akiwa Waziri Mkuu haina msingi imara. Serikali ilikuwa ya Sultani. Na wakati wote serikali ikiwa ya Sultan ni lazima tukubali kuwa Wazanzibar walikuwa bado hawajajikomboa kisiasa, kiuchumi na kijamii.

Baada ya kusema yote hayo hapo juu, inanibidi hapa niweke bayana kuwa siungi mkono vita au vurugu ya aina yoyote, katika kuleta mapinduzi ya kisiasa katika nchi yoyote na kwa wakati wowote ule. Na ninayalaani mauji holela ya binadamu wasio na hatia, iwe yamefanywa na ASP huko Zanzibar au CCM nchini Tanzania.

Hakuna shaka yoyote ushindi wa muungano wa ZNP na ZPPP ulishabikiwa kwa mizengwe iliyopangwa ili kudumisha utawala wa Sultani katika visiwa vya Zanzibar. Siwezi hata kidogo kushawishika vinginevyo. Mimi si mtu wa Zanzibar, lakini wakati mambo haya yakitokea kule Zanzibar, nilikuwa mtu mzima aliyesoma na akili zangu timamu. Najua, si wakati ule wala si wakati huu, unapoendelea kuwatawala watu, iwe kwa mabavu au kwa mizengwe, unakalia kuti kavu na wewe kuanguka si ajabu. ASP walikuwa na uwezo wa kusubiri au kulamikia maonevu waliofanyiwa, lakini unapoona hakuna njia nyingine ya kupata mtu haki yake, ndio mambo mabaya kama haya ya mapinduzi ya Zanzibar yanapotokea. Kwa
sababu hii, naona lawama za mauaji yale inasimama sawasawa katika mabega ya ASP na ZNP/ZPPP; pia na kwa Sultani na Waingereza.

Na kwa wote walioguswa na maafa haya, kwa namna moja au nyingine nawapa pole. Ni bahati mbaya ya matokeo ya kihistoria. Ingekuwa bora pia tusisikie kauli za kuwa eti watu wanadai kuwa "yale mapanga bado tunayo" au "kwani sisi tulipata bendera kwenye kisahani." Kauli kama hizi zinaashiria utawala wa kimabavu na kimizengwe. Matokeo yake, mwisho unakuwa ni yale yale, "anayeishi kwa upanga, hufa kwa upanga huo huo. Historia haiachi kujirudia. Tujifunze. Ukimpeleka paka ukutani, akawa hana njia ya kutokea, atakurudia akukwaruze na hata pengine akutoe macho.

Tuache siasa za visasi, "yaliyopita si ndwele, tugange yajayo."
 
Muafaka wa Zanzibar umefika hatua gani?



TULIPATWA na faraja kubwa wakati yalipoanza mazungumzo ya makatibu wakuu wa vyama vya CCM na CUF huko Zanzibar, yenye lengo la kutafuta ufumbuzi wa mpasuko wa kisiasa visiwani humo.
Tulipata kuandika huko nyuma kwamba, tukiwa sehemu ya Watanzania wapenda demokrasia tulisema bayana kuhusu msimamo wetu wa kuyaunga mkono mazungumzo hayo ya heri.

Hata hivyo wakati tukisema hayo, tulieza wazi wazi kuwapo kwa wasiwasi kuhusu dhamira ya kundi dogo la wahafidhina lenye lengo la makusudi kabisa la kuyavuruga mazungumzo hayo kwa sababu wanazozijua wao.

Tulisema hivyo tukitambua kuwa kwa zaidi ya miaka 15 sasa, tangu Tanzania itangaze rasmi kuukubali mfumo wa ushindani wa vyama vingi, kumekuwa na mambo ambayo kimsingi yamekuwa yakizua maswali magumu kuhusu utayari wetu wa kuukubali mfumo huo na kuheshimu matokeo yake.

Ushahidi wa wazi kuhusu hilo ulikuwa ukijionyesha huko Zanzibar ambako chaguzi zote tatu za vyama vingi zimekuwa zikizingirwa na mambo ya ajabu ajabu ambayo kimsingi ndiyo yamezaa mazungumo haya ya sasa na mengine kabla yake.

Pamoja na ukweli huo basi, wasomi, wanasiasa na taasisi zinazoheshimika kwa pamoja wamekuwa wakitoa mapendekezo mbalimbali kuhusu namna ya kuendesha mambo visiwani humo, ambayo kwa bahati mbaya yamekuwa yakikwamishwa na viongozi walio madarakani na hususan wale wa upande wa Zanzibar.

Kwa mfano, huko nyuma, kwa zaidi ya mara moja chama hicho tawala kilionekana kikifanya mchezo wa kuigiza wa kufanya kile ambacho machoni kilikuwa kikionyesha nia njema kabisa ya kutafuta ufumbuzi wa kudumu wa tatizo la Zanzibar.

Mwaka 2001 kwa mfano, baada ya hali ya kisiasa visiwani huko kuchafuka, CCM ililazimika kukutana na viongozi wa CUF na kukaa meza moja katika vikao ambavyo vilizaa muafaka wa Oktoba mwaka huo huo.

Hata hivyo, muafaka huo ambao pamoja na mambo mengine ulipendekeza kuangaliwa kwa uwezekano wa kuundwa kwa serikali ya umoja wa kitaifa, umeendelea kupuuzwa kwa matendo na kwa maneno na viongozi wa CCM hususan wale wa upande wa Zanzibar.

Jambo la ajabu ni kwamba, hata baada ya vikao halali vya chama hicho tawala na viongozi wake wakuu kutangaza kwamba, walikuwa wameamua kutafuta ufumbuzi wa kudumu wa tatizo la Zanzibar, bado kumekuwa na maneno ya ajabu kutoka kwa viongozi wa pande zote yanayoiweka hali katika mazingira magumu.

Wakati maneno ya kichochezi ya baadhi ya viongozi wa CCM Zanzibar yakionekana kutokomea, ni ajabu kwamba hivi sasa si viongozi wa CCM wala wale wa CUF wanaoonekana kutoa matumaini yoyote.

Hata hivyo tukiwa sehemu ya Watanzania tunaofuatilia kwa karibu mchakato mzima wa suala hilo, tunaamini kwamba pande zote mbili zimejifunza vya kutosha kutoka Kenya, ambako mazungumzo yao ya kusaka muafaka yanatoa mwelekeo mwema katika kipindi kifupi.

Hali hiyo imesababisha baadhi ya Watanzania wenzetu kwa siku kadhaa sasa kutuuliza hatua ambayo vikao vya kamati ya makatibu wakuu imefikia katika kusaka muafaka, ambao sasa unaweza kuonekana kama ni jambo ambalo halipo.

Tunachoweza kuvieleza vyama vya CCM na CUF ni kwamba, ukimya wao umeshaanza kuwatia wasiwasi wananchi wanaotaka kujua kwa hamu ni wapi yalipofikia mazungumzo ya muafaka. Ni lini basi yatahitimishwa?

tanzania daima
 
Msekwa aendeleza ngonjera za muafaka Visiwani Zanzibar
Na Muhibu Said

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimesema mazungumzo ya kutafuta muafaka wa kisiasa kati yake na Chama cha Wananchi (CUF), yaliyoanza Januari 17, mwaka jana, bado yanaendelea.


Kauli hiyo ilitolewa na Makamu Mwenyekiti wa CCM, Pius Msekwa, alipoulizwa na Mwananchi kuhusu hatma ya mazungumzo hayo, muda mfupi baada ya kuhudhuria kikao cha Taasisi ya Demokrasia Tanzania (TCD), katika Ukumbi wa Mayfair, jijini Dar es Salaam jana.


"Mazungumzo bado hayajafika mwisho," alisema Msekwa na kuongeza kuwa sababu ya kuendelea kwa mazungumzo hayo ni kuwapo kwa vipengele vya ambavyo bado vinajadiliwa na wajumbe wa kamati za vyama hivyo.


Hata hivyo, alisema baadhi ya vipengele tayari vimeshajadiliwa na kufikiwa makubaliano kati ya pande hizo.


Alisema haoni kuwa ni busara mazungumzo yakaisha kama wanavyotaka baadhi ya watu bila kujadili vipengele vyote vya mazungumzo na kufikia muafaka.


Aliwashangaa wanaong'ang'aniza mazungumzo hayo yaishe haraka bila kuzingatia suala hilo na kuwataka wawape muda wajumbe wa kamati ya vyama hivyo wakamilishe mazungumzo juu ya vipengele vilivyobaki.


Awali, Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Shariff Hamad ambaye ni Kiongozi wa Kamati ya Mazungumzo hayo kutoka chama hicho, alikataa kuzungumzia suala hilo.


"No comment (sina la kusema)," alisema Maalim Seif alipotakiwa na Mwenyekiti wa TCD, John Cheyo kuzungumzia suala hilo ukumbini hapo jana.


Mazungumzo ya muafaka yalianza Januari 17, 2007 kwa kikao cha kwanza kilicho wakutanisha makatibu wakuu wa vyama hivyo na mchakato wa mazungumzo ukaanza.


Mausla yaliyojadiliwa ni pamoja na uchaguzi Mkuu wa Zanzibar wa Oktoba 30, 2005 na taathira zake, usawa na haki katika kuendesha siasa, masuala ya utawala ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, njia za kuimarisha mazingira ya maelewano ya kisiasa na uendeshaji wa uchaguzi huru na wa haki Zanzibar, na utaratibu wa kutekeleza programu ya utekelezaji wa makubaliano yatakayofikiwa katika mazungumzo haya.

?

Kwa mujibu wa Rais Jakaya Kikwete ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM, mambo ambayo yameshajadiliwa na kufikiwa hatua nzuri.


Mapema, Mwenyekiti wa TCD Cheyo alisema TCD inawapongeza wabunge kwa kazi nzuri waliyoifanya kwenye mkutano wa kumi wa Bunge uliopita katika kupambana na ufisadi wa fedha za umma.


Cheyo ambaye ni Mwenyekiti wa chama cha UDP na Mbunge wa Bariadi Mashariki, alisema sekretarieti vya TCD imeagiza kuwa vikao hicho vifanyike katika ngazi mbalimbali nchini.


Alisema uongozi wa TCD umeamua nafasi ya Mwenyekiti wake, iendelee kushikiliwa naye na ile ya Makamu Mwenyekiti wa taasisi hiyo utashikiliwa na Msekwa katika kipindi cha mwaka mmoja.


Kikao hicho kilihudhuriwa na viongozi wakuu wa vyama vyenye wabunge, akiwamo Msekwa, Maalim Seif (CUF), Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa TLP, Augustine Mrema, Cheyo na wajumbe wao.

mwananchi
 
"Mazungumzo bado hayajafika mwisho," alisema Msekwa na kuongeza kuwa sababu ya kuendelea kwa mazungumzo hayo ni kuwapo kwa vipengele vya ambavyo bado vinajadiliwa na wajumbe wa kamati za vyama hivyo.
 

Hiyo kauli (bold) ya Mrema imeniacha sina mbavu...lakini ni kweli,kuna umuhimu wa kutumia panya kunasa panya wengi zaidi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…