THERE IS NO REVOLUTION WITHOUT SACRIFICE.

IN OTHER WAY

IN ANY REVOLUTION SOME HAVE TO PERISH.==HAWA HUITWA MASHUJAA
 
HUYU JAKAYA KIKWETE NDIO HUYUHUYU MKUU wa AU?au ni mwenginene na yule alikwenda kule kenya?ndio huyuhuyu aliye pelka majeshi kule COMORO?
Amma kweli mpende jirani yako kuliko nafsiyako lakini haya sio mageni kani tuna hata pale air port yetu mgeni anapwa kipaumbele na heshima nyingi lakini mimi mTZ mwaenyewe nitasumbuliwa na kunyanyaswa kama sio kwetu, mungu ibariki tanzania mungu ibarikizanzibar hakuna tena wa kututetea ispokuwa wewe tu.
 

Wale wanaotazama mambo kwa kuangalia upande mmoja tu kwa kweli wanachukiza sana. Kwa nini kila mtu anataka aone upande wa CUF tu wanaopenda kuwa na huo mseto. Kwa nini upande wa pili nao usieleze yake, kwa nini sauti ya wanachama na wafuasi wa upande wa pili(CCM -Zanzibar) ambao naamini ndiyo wengi populationwise nayo isisikilizwe. Kama hawauwafiki mseto wache na wao waseme na wana haki ya kusikilizwa. watoe sababu zao. na kitafutwe kitu cha mbadala kwani huo mseto ndio solution pekee. Ni ujinga kabisa kuwalaumu wajumbe wa CCM- Zanzibar kwani na wao wanawakilisha watu, au hamwaoni kwa sababu hawajaandamana au kulala mabarabarani , au kugombana na nguvu ya dola?
 

mwafrika wa kike, bado una point. don't give up easily. iki kichwa cha habari hakisomwi na wanacuf tu, ambao wanaweza kuhamasika na kuingia mitaani, la hasha, pia kinasomwa na JK ambaye anaweza kuangalia uzito wa jambo hili na kubadilika.

Mwanakiji hawa watu ni ndugu zetu, namna tunavyowakemea mafisadi wa uchumi wetu, ndivyo tunavyopaswa kuwakemea mafisadi wa uhuru wa zanzibar. sijaridhika kuwa sasa ni muda wa kutumia lugha nyepesi, wakati lugha hiyohiyo tuliitumia kwa ndugu zetu wa chadema kule Kiteto.

mimi sitaipigia campaign CCM kwa ajili ya kuwakandamiza CUF eti kwa sababu mimi ni mbara. sijui kama nimeenda stepi mbili zaidi ya title
 

Mushobozi,

Hata mimi nilifikiria hivyo. Unajua kati ya mambo ambayo wakenya leo hii wametambua ni kuwa walikuwa wakifunika chini ya kapeti lugha zote za malalamiko ya ukandamizaji wa kikabila kwa kuyaita ya kichochezi hadi juzi chupa ilipopasuka kwa presha.

Kuna wakati kufunika maneno tu bila kutoa suluhisho si swala zuri na hii ndiyo ilikuwa argument yangu. Hata hivyo nilikubali kuwa katika jamii yetu kuna section ya watu ambao wanachukulia mambo kwa maana tofauti na hivyo hii ingeweza kupelekea mwisho mbaya katika jamii.

katika hilo sikuwa na argument zaidi ya kugive up ingawa bado naamini kuwa kama ccm wakiendelea kucheza mchezo huu wa kunta kintiko basi kuna mambo watakuja kujutia siku moja (GOD Forbid).

Asante!
 

Vipi yakhe sasa wewe ulitaka awe dikteta. Awazuwie wajumbe kutoka Zanzibar wasiseme, pale, maoni ya wanaowawakilisha. If peoples power fahamu tu iko pande zote. Usiione hiyo iliyoko CUF tu bali CCM-Zanzibar nako pia iko na ndiyo kubwa (the latent people's power). Ni vyema kuwasikiliza kama hawataki mseto wanataka nini na siyo kuwashurutisha (kuwalazimisha) katika jambo ambalo linagusa maslahi na maisha yao ya kila siku. Kwani solution huko ni mseto tu. Jee, hakuna njia mbadala?
 

HISTORIS YA ZENJ NI NGUMU SANA....JAMBO NALOLIJUA NI KUWA HAKUNA ZENJ BILA MUUNGANO.MPEMBA KAMWE HATOTAWALA ZANZIBAR,NASAEMA KAMWE HALITOTOKEA....ZENJ SIYO YA WAPEMBA AU WANA CUF
 

jamani tuache itikadi; kama ni uvumilivu, hawa watu ni wavumilivu sana. ikumbukwe kuwa hata wanachama wa cuf walishaijia uongozi Cuf na kuwafungia ofisi zao kuwa wanawasaliti.

kama ni maongezi yanatosha, hata mimi ningekuwa panapohusika niko tayari kutoa damu yangu kuwa rutuba nikijua kuwa wakati fulani italilia ardhini kama damu za watu wengine.

any way that is the way i am ila SERIKALI YA KENYA MWANZONI ILIKATAA NAFASI YA UWAZIRI MKUU ILA BAADA YA DAMU KUMWAGIKA BILA KUISHA KILA MTU ALIKUJAEWA NA KUKUBALI NAFASI HIYO.

I REPEAT VERBALLY AND ARTICULATELY KUWA SWALA HILI LA HAKI YA RAIA AU WATU FULANI LIHESHIMIKE, TUACHE UZANZIBAR NA UZANZIBARA. TUWALAZIMISHE WANACCM KUELEWA NYAKATI.
 
historis Ya Zenj Ni Ngumu Sana....jambo Nalolijua Ni Kuwa Hakuna Zenj Bila Muungano.mpemba Kamwe Hatotawala Zanzibar,nasaema Kamwe Halitotokea....zenj Siyo Ya Wapemba Au Wana Cuf

Na Hakuna Tanzania Bila Ya Ccm
Chama Cha Maisha
 

Mzee mwanakijiji. Wewe unaonekana kuwa ni mtu wa busara labda kidogo tu nikupe tip. Mara nyingi Wazanzibari ni (washairi) wana mtindo wa kusema between the lines. Naamini hoja ya-basi na tufanye kura ya maoni yakhe- ina maana ya kutabanahisha kuwa kauli ya kuwa watu wote wanataka mseto siyo ya kweli, hasa katika mazingira ya viongozi tulionao hivi sasa (pande zote CUF na CCM Zanzibar ambao tunatarajia kuwaweka katika mseto- ukweli nikuwa hawatapikika) Sasa na wasikilizwe wanachama, wapenzi, wafuasi, wapiga debe wa pande zote mbili nini wanataka na iwepo satuwa ya kuleta ufumbuzi wa kweli na wa kudumu utakaokubaliwa na wote. Kama ni people's power basi sehemu kubwa iko kwa wale walio katika upande wa CCM-Zanzibar kwe sababu ndio wengi. Jee na wao waingie barabarani kama hamtawasikiliza? Wajumbe wa CCM Zanzibar wasilaumiwe bure. Walichokifanya ni kueleza kile wanachoamini (au wasichoamini) wanaowawakilisha.
 
Chama Cha Majambazi (CCM) sio chama cha kuaminika hata kidogo, siku zote watatumia kila aina ya njia za ulaghai na udanganyifu ili waendelee kutawala. Nadhani Wazanzibar wameshavumilia vya kutosha na kuendelea kukubali huu upumbavu unaoletwa na CCM itakuwa ujinga mwingine. Sitoshangaa CCM wakiitisha hizo kura za maoni halafu wakaiba tena hizo kura na kuweka matokeo wanayotaka wao. Yaani ni usanii mtupu unaoendelea ambao uunaongozwa na Msanii Mkuu Jakaya Kikwete.
 
Moja kwa moja nasema kama Kikwete ni Mkuu wa Majeshi,kama Kikwete ni Mwenyekiti wa CCM,kama Kikwete ni Mwenyekiti wa AU na kama Kikwete ndie aliewaahidi Wazanzibar walio wengi kuwa muwafaka utatimizwa na upo karibu kumalizika basi yeye ndie mhusika mkuu kwa lolote lile litakalotokea Zanzibar ,ifahamike wazi kuwa kwa CCM hawa akina karume na genge lake hawana uwezo wa kuizuia CUF hata dakika moja na hawana ubavu wa kuzuia maamuzi ya CCM Butiama kwa kupinga kitu chochote kile zaidi ya kutomezwa au kuamriwa na kufuata ,baraka hizi za maamuzi moja kwa moja anahusika Mkuu wa Kaya na mtandao wake katika kuendeleza ukandamizaji wa haki za binadamu waishio Zanzibar.
Inaposemwa Kikwete ,ikiwa leo wazanzibari wataingia barabarani amri ya piga uwa itatoka kwa Mkuu wa majeshi kama ilivyotoka kwa Mkapa alipokwenda kuwaua waPemba 2001,na kutoa wakimbizi ambao hadi hii leo wengine wapo kenya na Somalia.
Hivyo alietoa amri ni Kikwete ,kuna maraisi wengi tu wanashitakiwa baada ya kutokea mauaji ,anytime Mkapa anaweza kushitakiwa na hili limo katika agenda za waPemba wanaoomba ni huyu jamaa asije akajifia na mapema lakini wakipata nafasi tu basi Mkapa atapandishwa kizimbani ,hilo alijue popote alipo ,akumbuke tu waliouwa wakati waHitler basi tunasikia wakipandishwa kwenye kitalu na kujibu mashitaka.
Huyu Kikwete ndie alieandika waraka rasmi kuwaomba CUF wasijitoe katika mazungumzo ,je aliogopa kitu gani au ni lipi lilomfanya aandike barua ile kwa haraka ,sasa ikiwa ni muislamu moja kwa moja ataingia katika kundi la wanafiki maana ametoa ahadi na hakuitimiza na wala hajasikika kutoa kauli ,tusubiri hotuba yake ya kila mwisho wa mwezi.
Wazanzibari wanasema weka jeshi na polisi kando uwawachie wao na CCM aonekane nani mwanamme.
Kwa vile Chama cha CCM kimeukataa muafaka inambidi Makamba ajiuzulu na kwa kuongezea jamaa wanasubiri kauli rasmi ya CCM ili waanze vituko ,halafu chama chenyewe ni CUF fujo wanaliweza bila ya shaka yeyote ,maana sasa wameshaamini kama ustarabu hauna mshiko ,tena sio Zanzibar tu safari hii ni Tanzania nzima ukichanganya na uhuni wa ufisadi basi ndio lazima watu watajua kama embe ni tunda.Na sikilizeni Zanzibar sasa wanasema nini wamishageuza kura ya maoni ya vyama wanasema kura ya maoni Muungano na sio hapa watauvunja Muungano kupitia umoja wa Mataifa hayo ni mazungumzo yalioanza mitaani ,jamani hili kundi la Karume linajulikana kama la wahifidhina halina wafuasi kabisa wasiwadanganye huko na kusema wana watu ,hamna kitu wandugu kama mnavyowaandama mafisadi kuwa ni kundi fulani basi na huko Zenji nako hili ni kundi lenye mfano wa hao mafisadi.Ikiwa huwezi kuagiza simenti mpaka upitie kwa mke wa Karume ,nani wa kuwahoji ,viwanja na ardhi wanagaiana wana familia tu mapande kwa mapande nani wa kuwahoji zanzibar ni visiwa vidogo tu,watu wote wameshawachoka ,wala Kikwete asijidanganye kwa kuona kuwaweka watu hawa kutampa suport ya kupita uchaguzi wa 2010 ,kama alivyofanya mbinu za yeye kupita na wengine watapita huko huko ,na mtaona CCM Zanzibar ni wale wale tokea miaka hiyo ila huku Tanganyika kila mmoja anakuja na timu yake ,hivyo hakuna lisilo kuwa na mwisho unaweza mwisho ukawa mtamu au mchungu.Kama kutatokea fujo Zanzibar basi wa kulaumiwa ni Mh.Kikwete hilo halina rangi ni jeupe pepe.
 
Posted Date::3/31/2008
CUF wadai Rais Kikwete anachezea amani ya Zanzibar
Muhibu Said, Dar na Salma Said, Zanzibar
Mwananchi

BAADHI ya wajumbe wa baraza la wawakilishi wa Chama cha Wananchi Zanzibar, wamedai kuwa Rais Jakaya Kikwete anachezea amani ya visiwani hapa.

Kauli hiyo, waliitoa jana kwa nyakati tofauti wakati wakitoa maoni yao kuhusiana na tamko la mwafaka wa kiasiasa lilitolewa katika Kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya Chama Cha Mapinduzi (NEC) kilichomalizika juzi katika Kijiji cha Butiama mkoani Mara.

Mwakilishi wa Viti Maalum (CUF), Zakia Omar alisema hakuna dhamira ya kweli katika kuutatua mgogoro wa kisiasa visiwani Zanzibar kutokana na tamko hilo la CCM.

Alisema kuna maamuzi mengi tu ambayo serikali ya CCM imekuwa ikiyachukua bila hata ya kuwashirikisha wananchi, na inakuwaje hili la mwafaka, washirikishwe wananchi.

Maamuzi mengi yameamuliwa bila ya kutushirikisha sisi wananchi leo wanatwambia kupigwe kura ya maoni... mimi naona kama wana-'bytime' tu," alisema mwakilishi huyo.

Alitaja baadhi ya maamuzi yaliyowafikiwa bila ya kuwashirikisha wananchi kuwa ni kujiuzulu kwa aliyekuwa Rais wa Zanzibar, Aboud Jumbe Mwinyi bila ya kuchukuliwa maoni ya mtu yeyote.

Mwakilishi huyo, alisema kwa mujibu wa hati ya muungano, Rais wa Zanzibar, anakuwa Makamu Mwenyekiti wa CCM, lakini kufuatia mabadiliko ya 11 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano, wamepitisha vifungu na kumuondolea madaraka bila ya kuwapo kura ya maoni pamoja na maamuzi mengi yakiwemo yale ya kupeleka majeshi ya Tanzania katika vita vya Somalia na Comoro.

Kwa upande wake, Mansour Ali Yusuf, alisema inaonekana kana kwamba mbinu hiyo ya kutaka kupata kura ya maoni, ni mchakato wa kuhakikisha kwamba, watu wachache wateule wanaendelea kuiongoza Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) , wakisaidiwa na Serikali ya Muungano, iliyotumika ni mbinu ya kuwadanganya wananchi kuwa suala hilo ni gumu na haliwezi kupatiwa uamuzi wa haraka bila ya kuwepo kura ya maoni.

Naye Yussuf, alisema sio kweli kama Kikwete hawezi kutafuta suluhu isipokuwa anachofanya ni kuwalinda wahafidhina ambao kama watapata nafasi wangependa watawale milele.

Baadhi ya wananchi jana walikuwa katika mijadala mikali katika kila sehemu ambapo baadhi yao walisema sasa Rais Kikwete anataka kucheza na amani kwa kuwaachia viongozi wa Zanzibar kufanya maaamuzi ya kihuni.

Kilichoamuliwa Butiama, ni uhuni na sasa wanataka kutuchagulia nchi. Maana hatutakubali... wanataka yale yaliyotokea Kenya sasa yaje Zanzibar,? alisema mzee mmoja wa makamu katika Soko la Darajani.

Mapema wajumbe wote wa Baraza la Wawakilishi wa CUF, jana asubuhi, walitoka nje ya kikao cha Baraza hilo wakati kikiendelea, kuitikia wito wa chama hicho wa kuhudhuria kikao cha dharura.

Kabla ya kuchukua uamuzi huo, wajumbe hao awali waliingia ndani ya kikao cha Baraza la Wawakilishi kama kawaida na kusikiliza maswali na majibu, lakini kabla mchakato huo kumalizika, walianza kutoka nje mmoja baada ya mwingine.

Wajumbe hao walitoka nje wakati Waziri wa Maji, Ujenzi, Nishati ya Ardhi Mansour Yussuf Himid akiwasilisha muswada wa Sheria ya Kusajili Wahandisi, Wasanifu na Wakadiriaji Majengo.

Mnadhimu wa Baraza la Wawakilishi wa Kambi ya Upinzani, Soud Yussuf Mgeni aliwaongoza wajumbe wenzake kutoka nje ya kikao hicho, huku akisema wamelazimika kufanya hivyo, kutokana na unyeti wa jambo lenyewe ambalo linahusisha amani katika nchi.

Mgeni alithibitisha wajumbe hao kuondoka barazani na kwamba, walikwenda Makao Makuu ya chama hicho Mtendeni kwa kikao cha dharura ambacho pamoja na mambo mengine kitajadili kilichojitokeza Butiama.

Tumetoka kwenye Baraza tunakwenda kwenye kikao muhimu tulichoitwa na chama chetu, sisi tunawawakilisha wananchi, kwa hiyo, lazima la leo lifanywe leo hakuna kusubiri, alisema.

Mnadhimu huyo, alisema wamechukua uamuzi wa kutoka nje ya kikao cha baraza bila ya kumuarifu Spika , lakini taarifa zaidi atazipata atakapoangalia upande wanaokaa wawakilishi wa Kambi ya Upinzani.

Spika hatujamuarifu rasmi, lakini bila ya shaka atafahamu tu baadaye kwa sababu akitupa jicho ataona hakuna mtu upande wetu kwa hivyo?atajua...atajua tu,? alisema Mgeni haraka haraka huku akiingia ndani ya gari dogo na kwenda Mtendeni.

Spika wa Baraza hilo, Pandu Ameir Kificho alisema hajapokea taarifa zozote kuhusiana na wajumbe wa kambi ya upinzani kuondoka ghafla katika kikao hicho.

Sina taarifa ya kuondoka kwao, ingawa niliwaona wakiingia na baadaye kutoka wote, sina tafsiri juu ya kitendo hicho..., alisema Spika.

Hata hivyo, baada ya kuwasilishwa muswada wa Waziri Himid, Mwenyekiti wa Kamati, aliwataka CUF kuwasilisha maoni ya kambi yao kana kwamba hajaona upande wake wa kushoto kama kulikuwa hakuna mtu, jambo lililozua vicheko kwa wajumbe walioketi upande wa kulia ambao ni wa CCM.

Mheshimiwa njoo uwasilishe maoni ya kambi ya upinzani, aliwachekesha wajumbe wa CCM.

Wakati huo huo; Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Chama cha Wananchi (CUF), imewaita wabunge na wawakilishi wake, katika kikao cha dharura kitakachofanyika leo jijini Dar es Salaam kujadili tamko hilo la CCM.

Mbali na kikao hicho, CUF pia inatarajia kutoa tamko lake rasmi leo asubuhi kueleza msimamo wake kuhusu tamko hilo la NEC ya CCM.

NEC katika tamko lake lililosomwa na Makamu Mwenyekiti wa CCM Taifa, Pius Msekwa kwa wajumbe wa halmashauri hiyo na waandishi wa habari baada ya kumalizika kwa kikao chake cha siku mbili kijijini Butiama mkoani Mara juzi usiku, ilisema imeyakubali mapendekezo yaliyomo katika taarifa ya mazungumzo ya mwafaka.

Hata hivyo, ikasema imeazimia kuwa ikiwa makubaliano hayo yatakubaliwa, yataleta mabadiliko makubwa katika mfumo wa utawala wa Zanzibar na kwamba, kwa kuliangalia jambo hilo, ni lazima wananchi wote wa Zanzibar watapaswa kuliamua kwa njia ya kura ya maoni.

Kutokana na hali hiyo, NEC ilisema imeiagiza Kamati ya Mwafaka ya CCM kurejea tena katika mazungumzo na wenzao wa CUF ili kuliamua jambo hilo.

Kutokana na hali hiyo, Katibu wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya CUF Taifa, Said Miraji aliliambia gazeti hili jijini Dar es Salaam jana kuwa, wamelazimika kuitisha kikao cha dharura kati ya kamati yake na wabunge na wawakilishi wote wa chama hicho.

Miraji ambaye pia ni Mkurugenzi wa Blue Gurad Taifa, alisema kikao hicho, kitafanyika leo Makao Makuu ya chama hicho, Buguruni, jijini saa 11:00 jioni na ajenda kuu itahusu kujadili tamko hilo la kikao cha NEC na hatua ambazo wabunge na wawakilishi wataona kuwa zinafaa kuchukua kuhusiana nalo.

"Hapo hakuna jambo la kuficha, kila kitu sasa ni wazi," alisema Miraji.

Kabla ya kikao hicho, Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Shariff Hamad, atakutana na waandishi wa habari Makao Makuu ya chama hicho, leo asubuhi.

Mkurugenzi wa Haki za Binadamu na Mahusiano na Umma wa CUF Zanzibar, Salim Bimani, aliliambia gazeti hili jana kuwa, katika mkutano huo, Maalim Seif ambaye atakuwa na Makamu Mwenyekiti wake, Machano Khamis Machano, anatarajiwa kutoa kutoa tamko kuhusu msimamo wa chama hicho kuhusiana na la NEC CCM kuhusu mwafaka.

"Kubwa litakalozungumzwa na Katibu Mkuu, ni kutoa tamko kuhusu msimamo wa chama kama alivyoahidi katika mkutano hadhara katika Uwanja wa Garagara, Mtoni Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja juzi kuhusu tamko la NEC Butiama," alisisitiza Bimani.
 
HISTORIS YA ZENJ NI NGUMU SANA....JAMBO NALOLIJUA NI KUWA HAKUNA ZENJ BILA MUUNGANO.MPEMBA KAMWE HATOTAWALA ZANZIBAR,NASAEMA KAMWE HALITOTOKEA....ZENJ SIYO YA WAPEMBA AU WANA CUF

Usiwe mtumwa wa Historia yakhe. Kuwa mwanamaendeleo. Time Factor. Mpemba iko siku atatawala. Seif angelikwishatawala, lakini ni mtu wa pupa. jazba na hawezi kukaa na watu, ni mtu wa kulazimisha nataka liwe na liwe sasa hivi.Kama unaijua historia Seif ni mtu aliyependwa na Wazanzibari, wote, Viongozi wote (na hata Mwalimu Nyerere) na angetawala pale aliporudishwa Zenj na Mzee Mwinyi baada ya mkasa wa Alhaj Jumbe, kama angetulia akamaliza ngwe ya kwanza na Mzee Idrissa (ile ilikuwa transsition) lakini alitekeleza ile nataka liwe na liwe. Hiyo asituletee katika hali ya sasa. I bet Hamad Rashid, Bw. Abubakar wa Mgogoni na wengi wengine, pale, waliotulia siku moja watatinga katika Ikulu ya Zenj. Inshaalla.
 

NAONA UNA ALLEGATION NAO!
 

Mchezo hapa ni kuitisha uchaguzi mwezi wa kumi mwaka 2009. Matokeo yatakuwa kura za hapana kwa serikali ya mseto 52% na za kukubali serikali ya mseto 47%, zilizoharibika 1%. Baada ya hapo CUF wataanza kuandamana kupinga matokeo, kesi itafunguliwa mahamakani, na mahakama itaahidi kutoa uamuzi mwezi wa tano mwaka 2010, wakati huo ccm watakuwa wameanza kupitisha mtu wa kugombea uraisi wa Zanzibar 2010 na kampeni zitaanza na mambo yote yatakuwa kama ilivyokuwa 1995, 2001, na 2005 na process yote itaanza all over again!
 
Tukupe kikonbe cha kahawa Mh. Mwiba unazungumza kama uko kijiweni. Tawire. Lete hoja Bwana zinazosimama katika misingi ya utawala bora, na demokrasia. Hivyo kun fa ya kun?. Wenzio wasiseme wanachoamini au kuamua. Kwa sababu eti unaweza kulalabarabarani na kusubiri polisi akukrupushe kwa bakora halafu uliye, wanionea, Hizo seram zimepitwa na wakati yakhe.
 

Ndio Mchezo wa kuigiza kama wa kina Mzee Jangala au Kingwendu unaotaka kufanywa na CCM.
 

Kuna haja ya kupata nakala ya hukumu ya kesi ya kutaka kuipindua serikali ya Zanzibar, ambapo majaji katika mahakama ya rufaa waliamua kwamba Zanzibar si dola (Sovereign state). Ukisoma hukumu ile utagundua mambo mengi sana kuhusu, nini maana ya dola, nchi n.k.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…