Mwiba
JF-Expert Member
- Oct 23, 2007
- 7,607
- 1,750
Hakuna nchi ya Zanzibar.........
Someni katiba yetu (na ndiyo aliyoinukuu Mhe. Pinda).
"1. Tanzania ni nchi moja na ni Jamhuri ya Muungano."
Sasa wewe na huyo Pinda nyote inaonyesha mna matatizo huoni katika hiyo mistari kuna kiunganishi, halafu mwisho kuna neno Muungano ,Tanzania ni nchi moja lakini Tanganyika na Zanzibar ni nchi mbili kila moja inasheherekea siku ya UHURU wake japo wazenji wao tarehe yao wameipa mgongo kutokana na tabia za uhafidhina ,sasa hapo ipi iliyokuwa haipo naona hao ndio wanaotakiwa wawe na msimamo mkali kule Zanzibar wakati wowote zikiwasanifu wanaweza kutangaza mgogoro wa Muungano na hapo ulipofikia patawekwa frozen mpaka wananchi waulizwe kwani makelele yamekuwa mengi ,Je WaTanganyika si mtaanza kulana nyama.
Hebu nieleze kama sasa hivi itatokea Tanganyika kurudishiwa hadhi yake kama Nchi (Sasa hivi haipo ila Zanzibar ipo na kila kitu chake) WaTanganyika mtafanya nini ? Hakuna litakalofanyika kutakuwepo na mtafaruku mkubwa wa nguo kuchanika kwani haiwezekani kwa mafisadi Kuunda Serikali kwa kutumia Chama chao CCM ni lazima ufanywe Uchaguzi mkuu wa kwanza wa vyama vingi Tanganyika chama kitakachoshinda ndicho kitakachounda serikali ama sivyo , ndani ya CCM pande la Zanzibar CCM litakuwa halipo katika kutumika kuwaekea waTanganyika kiongozi asiepata kura nyingi (Inajulika wazi kura za CCM Zanzibar zinaelemea upande mmoja tu na hapo ndipo upande mwengine unapogalagazwa chini ) .Hivyo machafuko yataanza ndani ya CCM na kugawika mapande mapande hivyo ,na kuenea kwa mgawanyiko huo kwa mikoa mingine ambapo wananchi watakuwa huru zaidi bila ya kubanwa na mbinu za serikali ya Muungano
Hivyo kuibwaga CCM ni lazima idaiwe Tanganyika otherwise watakuwa wakijiuzulu na kuwekwa wengine.Na ndio hata kule Butiama Wahafidhina walikuwa na ubabe kuwambia wabara kama mnataka kutekeleza mwafaka basi chukueni Tanganyika yenu ,wanajua fika wakichukua Tanganyika ndio mwisho wa CCM bara.
Na ndio mpaka leo iwavyo na iwe lakini CCM ni lazima ishinde Zanzibar tumeona majeshi jinsi yanavyopelekwa Zanzibar ,tumeona jinsi polisi walivyomwagwa Pemba na mamluki kibao yote ni kuilinda CCM na utawala wa Tanganyika na sio Tanzania kama inavyofikiriwa na wengi.
Hivyo natoa mwito kwa vyama vya upinzani kuidai Tanganyika kwa nguvu zao zote ,kama alivyosimamia Rev.Mtikila basi vyama vya upinzani vilikuwa vimuunge mkono na kueneza propaganda ya hali ya juu ili Tanganyika irudishiwe mamlaka yake ya ndani kama ilivyo Zanzibar ,kwani kumbukumbu zinaonyesha Mh.Kikwete alikuwa mstari wa mbele katika kuidai Tanganyika na 100% alikwisha fanikiwa kilichomkwamisha ni yeye kuwemo ndani ya CCM ,just baada ya kufanikiwa walikuwa waruke na kutua kwenye Chama kingine ,lakini walibakia baada ya kuambiwa tukimeguka basi CCM tumekwisha.
Shime vyama vya upinzani kuing'oa CCM kupitia mlango wa Tanganyika Huru.