Kichuguu
Platinum Member
- Oct 11, 2006
- 17,048
- 22,790
Hapa kuna kichekesho sana; inaonyesha jinsi gani watu waliopewa madaraka ya kuongoza nchi hii walivyo na upeo mfupi wa kuelewa mambo. Dola na serikali ni vitu viwili tofauti kabisa. Kuwa na serikali hakumaanishi kuwa hiyo ni dola, hata wakati wa mkoloni tulikuwa na serikali yetu ikiongozwa na Gavana, lakini hatukuwa dola, bali tulikuwa sehemu ya dola ya mwingireza. Dola inaongozwa na amiri jeshi mkuu wa majeshi ya ulinzi na usalama tu ambaye anaweza kuipeleka nchi vitani.
Kwa mfano katika nchi ya Marekani ambayo nayo imeundwa kwa muungano wa states kadhaa; kila state ina serikali yake pamoja na mabunge yote mawili, bendera yake, mkuu wa state, na mawaziri wake. Zaidi ya hapo, kila state ina jeshi lake la polisi (State trooper) na mahakama yake mpaka mahakama kuu ya state. Mahakama kuu ya state iko chini ya mahakama kuu ya Federal, uamuzi wa mahakama kuu ya state unaweza kutenguliwa na mahakama kuu ya Federal; nadhani sote tunakumbuka kuhusu maamuzi ya mahakama za State of Florida na Federal kuhusu vote recount katika uchaguzi wa mwaka 2000 na jinsi Federal walivyo-overide maamuzi ya mahakama ya State of Florida. Mkuu wa state pia ndiye amiri jeshi mkuu wa National Guard katika state yake, lakini madaraka yake hayo yako chini ya yale ya amiri jeshi mkuu wa majeshi yote ya ulinzi ya Marekani. Kwa hali hiyo, state hizo hazijiiti dola kwa sababu zote ziko chini ya amiri jeshi mmoja tu ambaye ni rais wa marekani.
Inawezekana kweli zanzibar ina serikali na kiongozi wa serikali pamoja na mahakama, na jeshi la KMKM lakini haina mamlaka ya kuingia vitani kwa vile mwamuzi wa mwisho kuipeleka nchi vitani ni amiri jeshi mkuu wa majeshi ya ulinzi na usalama anayeishi pale magogoni; huyo ndiye mwenye dola; Karume hana dola kabisa. Zanzibar siyo dola. wafuasi wake wanota dola hawa; amelewa madaraka sasa anataka zaidi.
Je hii purukushani ya kudai dola ni kutaka kukana mamlaka ya Kikwete ili asiwalazimishe kukamilisha mwafaka kati ya CCM na CUF?
Kwa mfano katika nchi ya Marekani ambayo nayo imeundwa kwa muungano wa states kadhaa; kila state ina serikali yake pamoja na mabunge yote mawili, bendera yake, mkuu wa state, na mawaziri wake. Zaidi ya hapo, kila state ina jeshi lake la polisi (State trooper) na mahakama yake mpaka mahakama kuu ya state. Mahakama kuu ya state iko chini ya mahakama kuu ya Federal, uamuzi wa mahakama kuu ya state unaweza kutenguliwa na mahakama kuu ya Federal; nadhani sote tunakumbuka kuhusu maamuzi ya mahakama za State of Florida na Federal kuhusu vote recount katika uchaguzi wa mwaka 2000 na jinsi Federal walivyo-overide maamuzi ya mahakama ya State of Florida. Mkuu wa state pia ndiye amiri jeshi mkuu wa National Guard katika state yake, lakini madaraka yake hayo yako chini ya yale ya amiri jeshi mkuu wa majeshi yote ya ulinzi ya Marekani. Kwa hali hiyo, state hizo hazijiiti dola kwa sababu zote ziko chini ya amiri jeshi mmoja tu ambaye ni rais wa marekani.
Inawezekana kweli zanzibar ina serikali na kiongozi wa serikali pamoja na mahakama, na jeshi la KMKM lakini haina mamlaka ya kuingia vitani kwa vile mwamuzi wa mwisho kuipeleka nchi vitani ni amiri jeshi mkuu wa majeshi ya ulinzi na usalama anayeishi pale magogoni; huyo ndiye mwenye dola; Karume hana dola kabisa. Zanzibar siyo dola. wafuasi wake wanota dola hawa; amelewa madaraka sasa anataka zaidi.
Je hii purukushani ya kudai dola ni kutaka kukana mamlaka ya Kikwete ili asiwalazimishe kukamilisha mwafaka kati ya CCM na CUF?