Zanzibar haijawahi kupewa haki sawa kivipi?
Naomba kueleweshwa maana si mjuzi sana wa mgao wa haki katika Muungano.
Sawa. Kama hili la "sovereignity. Rudia kabisa article za Muungano. Rudia Katiba ya Jamhuri ya Muungano. Rudia Hotuba zile za Nyerere. Zanzibar ime-surrender part of its sovereignity to the United Republic. Lakini (pia) makubaliano ni kuwa ita-retain some aspects of her sovereignity. Jee ime-retain kweli?
 

Mimi sasa nakuja na mtazamo wangu binafsi ni kwa nini nasema na kuamini kuwa zanzibar kisheria sio nchi hata kimataifa.

Navyoelewa mimi sovereignty kama alivyosema kuhani halina neno moja sahihi katika kiswahili,bali inaweza kuelezewa kuwa "ni uwezo wa kujiamulia mambo wenyewe pasipo kuingilia na mtu yeyote,uhuru huu ni absolute,kwa maana ya kuwa ni wa asilimia mia moja.Mambo yote mnayoyafanya hamuombi kibali kwa mtu wala kusema jambo fulani hatuwezi kulitungia sheri kwa kuwa faulani ndio mwenye mamlaka,mnao uwezo wa kwenda vitani wenyewe bila kuomba kibali toka kwa mtu mwingine. Hii ndio maana halisi ya sovereign.Na kulingana na international law,mataifa yote yanayotambulika kama nchi yana sovereignty.Sasa tuje katika suala la zanzibar na tanzania bara.

Ni wazi kuwa hapo kale kabla hatujawa na muungano wa mwaka 1964 tulikuwa na nchi mbili,yaani nchi ya zanzibar inayoundwa na visiwa vya pemba na unguja na nchi ya Tanganyika. Hili nadhani hakuna anayebisha.

Baada ya muungano wa mwaka 1964 nchi hizi mbili zilipoteza hadhi yake ya kuwa nchina kuunda nchi moja kubwa iitwayo Tanzania. Hii ndiyo inayojulikana na jumuiya ya kimataifa kuwa kuna nchi inaitwa Tanzania,iko afrika mashariki,upande wa mashariki inapakana na bahari ya hindi(note hawajasema upande wa mashariki inapakana na nchi ya zanzibar, la hasha) inapakana na bahari ya hindi. Hapo ina maana hii nchi inaunganisha zanzibar.

Baad ya nchi hizi mbili kupoteza hadhi yake ya kuitwa nchi automatically zilipoteza uwezo wake wa kujiamulia mambo yao kwa kuweka mambo yote chini ya muungano isipokuwa mambo machache ambayo hayakuwa kwenye mungano. Tanganika haikuishia hapo ikapoteza serrikali yake na kuifanya ile serikali ya muungano kuwa serikali yake itakayoiheshimu,wakati kwa sababu za kiutawala, zanzibar ikabakizwa na serikali yake, serikali ambayo ikapewa mamlaka yasiyo kamili na ndiyo maana ikapewa baraza la wawakilishi,rais,lakini ilipofika katika masuala ya ulinzi na usalama yote yakawa chini ya amiri jeshi mkuu ambaye ni Rais wa muungano.

Kutoka hapo zanzibar ikawa haiwezi kwenda vitani kwakuwa rais wa zanzibar si amiri jeshi mkuu,haiwezi kuingia mikataba ya kimataifa bila kuwa na kibali cha rais wa muungano,haiwezi kuyatungia sheria baadhi ya mambo kwa kuwa ni ya muungano, na pia ikajiweka chini ya katiba ya muungano ambayo inaifunga hata yenyewe.Kutokana na hali hii zanzibar ikawa haina sovereignty na kama ipo sio kamili.

Hiyo ni tafsiri ya kisheria,kwa maana ya kuwa in law zanzibar is note a sovereign state. Sasa tuje in fact. In fact zanzibar na Tanganyika bado ni chi kwa kuwa ardhi za nchi hizo na watu wake bado wapo na hata mipaka yake haikuvurugwa bado ipo,ndio ksema kuwa muungano ukivunjika tayari tutapata nchi mbili yaani Tanganyika na zanzibar.Tulichonacho sasa ni nchi moja yenye serikali mbili,ambapo serikali moja ni superiorkuliko ile nyingine.Yaani serikali ya muungano is superior to that of zanzibar.Kwa maana hiyo nchi hizi mbili in fact zingefutika tu,endapo labda zingeunganishwa kwa kutumia majembe na sululu kufukia ile bahari ya hindi ili ziungane kabisa,lakini geographically kwa kuwa bado zipo ndio maana nasema in fact au physically bado zipo.

Lakini kwa kuwa sheria hutumia legal fiction?in terms of legal fiction tuna nchi moja tu ya Tanzania. Fiction hii ni sawa na ile ya ndoa inayosema mke na mme wakioana watakuwa mwili mmoja. In law and in religiuos fiction that is true but in reality teye are still two individuals.Hakuna fusion they can stil be made back to individual personalities on divorce.

Hii ndio explanation yangu.
 
Makubaliano ya Zanzibar na Tanganyika ni kuwa- Tanganyika ina-surrender full sovereignity kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (nayo inabaki kama kivuli au ni Mfu). Zanzibar ina-surrender some aspects of its socereignity. na Ina-retrain some aspects za sovereignity kwa upeo ambao itabaki kuwa Autonomous, Na pia itaendesha na kuamua mambo yake yote ndani ya mipaka ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kelele za sasa ni hizi- Jee hii some aspects ya sovereignity ambayo Zanziba iko entitled kui-retain kwa mujibu wa makubalinao -inapatikana?
 

mimi ni mwanasheria kama wewe. lakini wanasheria kama wewe hatuwahitaji hapa bongo, kwasababu wanakuwa kama walisomea kichakani. nenda kapekue vitabu vyako tena, unachoongea ni kupotosha jamii na unaongea hivyo kwasababu you are biased unaelekeza kile mawazo yako yanavyosema, na sio sheria inavyosema. pole mkuu.
 

NAFIKIRI UNAKOSEA KUWATILIA MANENO MDOMONI WAZANZIBARI. WAO HAWAJATAKA WIZARA YA MAMBO YA NJE AMBAYO NDIO MSINGI WA KUWA SOVEREIGN STATE, WANACHOSEMA WAO NI NCHI AMBAYO SOVEREIGNTY YAKE IMECHUKULIWA NA SERIKALI YA MUUNGANO. KATIBA NI MAKUBALIANO NA WALA SI UNIVERSAL ENTITY KWA MATAIFA YOTE NA NDIO MAANA KILA TAIFA HUWA NA KATIBA YAKE.
SISI TULIKUBALIANA KUWA ZANZIBAR ITAKUWEPO KAMA NCHI LAKINI ITAKASIMU MADARAKA YAKE KWA SERIKALI YA MUUNGANO and that is it.
Comparisons and qoating of others will not help us here. we have to abide to what we had agreed even if ours is a peculiar union.
 
Mkataba wa montevideo wenyewe unataja sifa kuu nne zifuatazo za mamlaka kuitwa nchi:-
Population, Territory, Sovereignty, Government

Je,zanzibar inavyo vitu vyote hivyo vinne?
Kwa mujibu wa makubaliano yaliyounda Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Zanzibar inayo Serikali yake (SMZ- na Rais Amani Karume kwa hivi sasa). Zanzibar inayo Population inayotambulika (ndio hao Wazanzibari). Inayo mipaka yake (pamoja na huu iliopo Zanzibar channel unaotenganisha Zanzibar na Dar es salaam).Kwa mujibu wa makubaliano ya Muungano inawajibika ku-retain some aspects of her sovereignity. Jee amua wewe hiyo ni Nchi au si Nchi kwa mujibu wa -montevideo- yako.
 
Last edited:
Ukweli kisheria ni kwamba, zanzibar si nchi ila watu wanataka kulazimisha tu ili iwe nchi waseme wanataka kujitenga kwasababu zao binafsi. the issue here should not be whether Zanzibar is a state or not, it should be whether muungano uendelee au usitishwe, kwasababu kwa zanzibar kuwa nchi halina ubishi kabisa. lakini kwa mtazamo wangu, kwasababu muungano unahitaji watu wawili wakubaliane kama mmoja akikataa, unag'ang'ania wa nini? kule zenji CUF na CCM wote wanalalama kuwa zanzibar ni nchi na wote wamekuwa na mawazo ya kutaka kujitenga. sasa sisi wabara tunang'ang'ania nini wakati wenyewe hawatupendi na wala hawana hamu tena ya kuendelea kuwa ktk muungano na sisi? hata tukilazimisha, kama mioyoni mwao hawajaridhika itakuwa sio dawa, watakuja tu kuibua wakati wowote, cha maana ni kuvunja muungano huu kila mtu aanze kivyake, kwani sisi wabongo hatuwezi kuishi peke yatu bila zenji? wht do we gain from zanzibaris.....ni kuwapiga chini tu waende kivyao huko, na kuanzia siku hiyo, starting from Magomeni hadi kariakoo, wapemba na maduka yao yale wapewe masaa 24. period.
 
Hivyo Ndivyo Ilivyo Bw. Ngekewa. Na Hata Nyerere anajua hivyo. Msiwe wavivu- rejeeni kusoma hotuba zake- alitetea hilo. Zanzibar ku-retain some aspects of her sovereignity .Sasa hili lina i-qualify Zanzibar kuwa Nchi
 
Do u know the consequencies?
 

Kama Ni Mtu Wa Kutafakari Ungejiuliza Kwa Nini Wazanzibari Wote Wako Pamoja Kwa Hili Na Wale Wa Bara Wako Upande Mmoja Kwa Hili, Hapahitajiki Elimu Ya Darasa Kufahamu Kuwa Upo Mgogoro. Muungano Ni Bara Na Visiwani Wala Hakuna Mtu Wa Tatu Iwapo Hatukubaliani Lipo Tatizo Na Ushauri Wa Raza Ni Sahihi.
Kunhsu Shutuma Kwa Watu Ningekushauri Uache Kwani Karume Hajasema Chochote Kwa Hili Wakati Mpinzani Wake Mkubwa Seif Sharifu Ameshatowa Msimamo Wa Kumuunga Mkono Kwa Hili Na Kuhusu Raza Ana Haki Ya Kutowa Mawazo Yake Kama Ufanyavyo Wewe Na Mimi. Wazanzibari Tunamtambuwa Kuwa Mzanzibari Kama Mnavyowatambuwa Kina Rostam,mohammed Dewji, Manji Na Wengine.

Siasa Za Kudhibitiana Kwenye Haki Zisingekupa Uhuru Hata Wewew Kutamka Unayotamka Sasa,
 


Ukishasema some aspets hapo ndio utata unapoanzia kwani hata huo mkataba wa montevideo hausemi some aspects unasema sovereignty, hivyo sovereignty hii inatakiwa kuwa full,na ndio maana hata Tanganyika kabla yakuwa jamhuri(republic) mwaka 1961 bado haikuwa sovereign kwa kuwa ilikuwa bado inamtambua queen kama mkuu wa nchi australia hadi leo,visiwa vile vinavyotawaliwa na uingereza hali kadhalika,japo bado vina aspect of sovereignty.

Nadhani kama ulivyoisema hapo awali labda main issue iwe je,hizo some aspects of sovereignty walizoretain je wana full exercise? bado sio nchi kwa kuwa haina full sovereignty.Mamlaka ya RAIS wa zanzibar hayatofautiani na ya kandoro pale Dar kwani rais wa zanzibar anazo wizara wakati kwa kandoro zinaitwa idara,kandoro ana some aspects of sovereignty akiwa mkoani kwake dar ahali ambayo hata karume ndio ilivyo,mambo mengine hadi asubiri mkuu wa kaya.Kandoro mwenyewe anaweza kuamru jeshi la polisi mkoani kwake kufanya chochote linachoweza kufanya ila hawezi kuamuru JWTZ vivyo hivyo karume hawezi kuamuru JWTZ haya nadhani ndio yanayoleta huu utata.

Hata hivyo kama ilivyokwisha semwa kwenyhukumu ya akina machano hapo chini mahakama yenyewe ilishaona kuna utata kati ya vipengele vya katiba ya zanzibar naile ya muungano kuhusu sovereignty na kutoa ushauri kwa serikali mbili zikae na kuondoa hizo tofauti lakini cha kushangaza hadi leo hawajakaa ndio pinda anaibuka bungeni kusema two AGs wakae kuangalia namna ya kuondoa huo utata.

Believe me two AGs hawaiwezi hii kazi,inahitaji zaidi ya hao.Yatakuwa kama yale yle ya mwafaka kati ya CUF na CUF oooh sani zamakatibu wa kuu hazitoshi kuamua .....nk
 
Muungano hauna faida bara. Hao wanaofaidika nao, Zanzibar ndio wananyea kambi. Hakuna mjadala, turudishe Tanganyika. Zanzibar watabaki majirani, kama ilivyo kwa Kenya Rwanda DRC, Zambia n.k. Hata siku moja tusitake kuwahurumia, eti aah muungano ukifa Zanzibar itasambaratika... kwanza wao wanatucheka na ujinga wetu wa kuiua Tanganyika!

Hebu tuvunje. Tuwaache na Pemba na Unguja yao. Iwapo kutakuwa na mjadala wa kuendelea kuwa pamoja, Zenji iwe mkoa, kama Rukwa, Manyara etc
 
Waulize wasomi wenzio hao wanasheria. Ukivunja Muungano. Hilo suala linakuwa in-dispute. Mali zake zote zinapelekwa kwa msuluhishi. Kwa hivyo elewa hata ile Ofisi ya Katibu Kata kule Kijijini kwenu ni mali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Ukianza na Tanganyika yako Unaanza Alifu kwa Ujiti. Zanzibar wana system yao kule. Very Healthy- ina kila kitu Watakachofanya ni kujaliza tu Mambo ya Nje. Wana Vikosi vya SMZ. Huku wakati JWTZ na Polisi na Magereza tunavunja. Tanganyika itabidi uandikishe na uanzishe la kwako. Can u bear the consequencies?- Rejea Hotuba ya Nyerere wakati anawakanya G55 kudai Tanganyika yao.
 
sasa mzee, unafikiri hili bifu litaendelea hadi lini? unafikiri litakuja liishe? kama vipi ngoja tu tuanze upya ili tuachane na hawa kuku wanaokoroma kila siku. unatakiwa ujiamini, kama kuna tatizo lipo sehemu, you need to be ready for everything , hope you are a man huh!, usiogope changamoto alimradi tu in the future tutakuwa hatuna tena hayo matatizo. sijui unaelewa au?
 

Mzee Naondosha Imani Yangu Kwako Kuwa Umzee Wa Busara. Unamaanisha Nini Una Maana Wazanzibari Wachukuliwe Hatuwa Kwa Kudai Haki Yao? Nimeshituka Sana Na Ninajiuliza Mengi Kuhusu Huu Muungano .hivyo Wazanzibari Wana Makosa Au Ni (naogopa Kuwapa Jina Linalowastahiki )?
Sasa Tutaendesha Vipi Muungano Wa Watu Wa Calibre Mbili Tofauti?
Karume Ni Rais Wa Zanzibar Na Kwa Hili Wote Wanamsapoti Leo Unampaka Ujinga Na Uhaini Wa Kumfananisha Na Muhaini Wa Commoro
Ni Sawa Na Kusema Wazanzibari Wote Ni Wahaini(si Wanamsapoti)?
 

Unasahau ya kwamba vyote hivyo viko Bara, vinalipiwa kwa kiasi kikubwa na wabara, vinawaajiriwa wengi kutoka Bara, vingi vinaendeshwa na wabara etc.

Kimsingi ni kwamba nakubaliana na unavyosema ya kwamba kutahitajika kuwa na namna moja au nyingine ya kugawiana mali, hili ni suala ambalo halipingiki.
Umekuwa unajenga hoja ya kwamba Tanganyika itabidi waanze upya, waanze upya kivipi? Rejea ufunguzi wangu, karibia kila kitu kiko Tanganyika, mifumo yote ipo.
Cha kubadilisha ni kuondoa jina tu la "Muungano wa Tanzania" na kuweka "Tanganyika" au jina lolote lile watakalo kubaliana au kuchagua la kuwakilisha wabara!.
 
Mbona Slovakia na Check zilivunjika? Au USSR ije iwe Zanzibar? Kumbuka kuwa mfumo wa Muungano tulionao ni wa kishikaji zaidi kuliko wa kisheria. Utakuwaje na Serikali ya Mapinduzi halafu upande mwingine wa muungano unatumia serikali ya Muungano. Muungano ukivunjika mju kuwa wale Wabunge wote wanakuwa redundant na wanaondoka kwenye nafasi za serikalini. Can you accomodate all of them Pakacha?
 

Nafikiri sasa unafahamu. Pamoja na kuwa sikubaliani na mfano wako wa huyo Kandoro wako. Elewa kuwa makubaliano niku Zanzibar ihodhi mamalaka ya kujiendesha wenyewe. Jee kwa nini Jamhuri ya Muunganoi inaaiingilia Zanzibarkatika mamlaka hayo. Na ilhali makubaliano ya Muungano hayajaathiriwa. Ni hilo tu- linalohojiwa. Vitabuni (katika makaratasi) limeandikwa vizuri lakini katika utekelezaji ndio kuna walakin rekebisheni hali na acheni ubabe wa kuburuza.
 
Last edited:
Karume Ni Rais Wa Zanzibar Na Kwa Hili Wote Wanamsapoti Leo Unampaka Ujinga Na Uhaini Wa Kumfananisha Na Muhaini Wa Commoro
Ni Sawa Na Kusema Wazanzibari Wote Ni Wahaini(si Wanamsapoti)?

Lini CUF walikubali kumtambua Karume kama Rais wa Zanzibar?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…