Muungano wa Tanganyika na Zanzibar na kero zake: Je, tuuvunje?
Mkubali msikubali katika huu muungano Zenj is the junior partner kwa mantiki ya sababu zote, Kwa population kwa maliasili hata kwa eneo tu.
For a long time Zenj wamekuwa wakitutake for a ride kwa udogo wao na sasa wanataka kingi.
Ni vyema muungano ukafilia mbali ili wenzetu warudi 1964.
Ila wajue kwamba
Ubaguzi wa rangi zanzibar upo
Ubaguzi wa kiitikadi usio na mfano Zbar upo
Matatizo ya kisiasa kati ya waliopindua na waliopinduliwa 1964 bado yapo
Umaskini uliokithiri ( kama huku bara ) Zbar uko

Kabla hamjatoka katika muungano yatatueni hayo la sivyo vibaraka wa sultani watakapokuja kwenu wabara itabidi tushirikiane nao tu.

Kuna jamaa kasema hapa angependa kuungana na Kenya na kuweka makao Nairobo-RUKSA and see how fast nyang'aus devour you.
Ina bidi wenzetu waelewe kuwa kwa temperature iliyopo tumeanza kuwachoka kwa manun'guniko yasiyo kwisha wakati umaskini wanajiletea wenyewe
 
Mkubali msikubali katika huu muungano Zenj is the junior partner kwa mantiki ya sababu zote, Kwa population kwa maliasili hata kwa eneo tu.
For a long time Zenj wamekuwa wakitutake for a ride kwa udogo wao na sasa wanataka kingi.
Ni vyema muungano ukafilia mbali ili wenzetu warudi 1964.
Ila wajue kwamba
Ubaguzi wa rangi zanzibar upo
Ubaguzi wa kiitikadi usio na mfano Zbar upo
Matatizo ya kisiasa kati ya waliopindua na waliopinduliwa 1964 bado yapo
Umaskini uliokithiri ( kama huku bara ) Zbar uko

Kabla hamjatoka katika muungano yatatueni hayo la sivyo vibaraka wa sultani watakapokuja kwenu wabara itabidi tushirikiane nao tu.

Kuna jamaa kasema hapa angependa kuungana na Kenya na kuweka makao Nairobo-RUKSA and see how fast nyang'aus devour you.
Ina bidi wenzetu waelewe kuwa kwa temperature iliyopo tumeanza kuwachoka kwa manun'guniko yasiyo kwisha wakati umaskini wanajiletea wenyewe
Ukiwa na dhana ya ufisadi lazima uchoke maana WaTanganyika watakuwa na nguzo ya kuona mafisadi wanashughulikiwa vilivyo,sio leo Hazina ya Tanganyika inaibiwa na viongozi waliomo ndani ya Serikali ya Muungano na hakuna wa kuwahoji maana serikali ya Tanganyika haipo.
 
Yakhe kwanini tuandikie mate wakati wino upo? Nenda pale forodhani na utaona magunia ya vyakula .mayai tungule(nyanya) na vyakula tele vinavyovushwa kwenda Zenj.
Si kama tunasikitika , hasha ila ndio kielelezo cha ukulima wa Zenj.
Mtu ukufikia hata nyanya unaagiza nje basi umekwisha!!
Mkipata mafuta yenu na mtakapokuwa mmezoea mtavilipia vitu hivi kwa dola!


Naam Zanzibar hakulimiki hivyo vitu unavyosema na kama si bara basi wangenunua kutoka sehemu nyengine. Unasema mbatata hebu jiulize sabuni(Zile miaka ya 1980 watu wa sehemu fulani walikuwa wakijipaka kama manukato) na vitu vyengine kama dawa za meno na kadhalika vinatoka Kenya jee nako kule kuna Muungano na Zanzibar. Suala la Biashara litafanyika tu maadam mna bidhaa ambazo Wazanzibar hawana.
Jee umeona mihogo ikitoka huko? Mwaka jana viazi vitamu vilikuwa vikitoka Zanzibar kuja Dar, mbali ya biashara za magendo zinazowanufaisha watu wa Pwani ya Bara.
 
Unajua Bara wanasita kuona Visiwani pakikosa amani kama Comoro! Na jirani sana toka Tanga au Dar?

Hakuna ushahidi kuwa Visiwani will do any better than Commoro maana hata
wale wa Visiwani wanaochuma raslimali bara huwa hawapendi kuwekeza kwao!
 
Lole Gwakisa, nakuunga mkono mia kwa mia, popo bawa wanajua wao! bara hakuna!
kila siku tunaona, anakataa nini? ndivyo walivyo, hawataki kupewa ukweli wao!Tuvunje Muungano, wapate mafuta, waingie kwa viza hapa Bara, waje wanunue vitu kwa dola. Vitu vyenyewe ni hivi vifuatavyo: nyama mbuzi, ng'ombe, kuku, bata, mchicha, vitunguu maji, vitunguu saumu, viazi mbatata, nyanya, njugu mawe, mahindi, mbaazi, maboga, ngano, etc.. Je, hivi vyakula vinatoka baharini? Muungano unawanufaisha wao!
wanapenda dhahabu kama nini! wanaipata wapi?! kama si bara?

:twisted:


Kumbe wananunua? tatizo lipo wapi Wakenya si nmnawauzia pia na wanataka Muungano mbona mnawaogopa? Wakenya wametaka Muungano mwanzo kuliko Commoro lakini mnashangilia aliekuja mwisha na kumuogopa wa mwanzo. Muungano ni mzuri tuungane na Kenya ili uwe Muungano Mkubwa au tunafikiri muungano ni ukoloni?
 
Wazanzibar wanawaombea watanganyika serikali, kwa ajenda gani? Nafikiri ingekuwa vyema kama wangedai wanavyovikosa. Tatizo la Zanzibar ni uroho wa viongozi wake na wala si wananchi. CUF wanajua chini ya muungano huenda wasiitawale Zanzibar Miaka 50 ijayo, na wale wa SMZ wanajiona kama ma DC chini ya muungano, na tetesi za kupatikana kwa mafuta kunazidi kuwatoa udenda. Wataangaisha sana, lakini hawataki kutaja manufaa ya muungano kuliko kulalamika kila siku. Wapemba pale Ilala na Tanganyika kote wanamiliki kiulaini rasilimali za kutisha pamoja na ardhi kuliko wa bara kule Zanzibar. Wa bara sasa hivi ni sifa tu ya kuwa na Zanzibar, kama ni mafuta hata huku bara yapo ya kuisha nusu milenia ijayo. Mtatoana macho muungano ukivunjika!


Unajuwa mpaka sasa sijaona mchangiaji kutoka bara aliechangia bila kuweka jazba na kupofuliwa na jazba.
_Kwani huu Muungano si wapande mbili? Iwapo mmoja anataka uhuru wa kumuamulia mwengine na huku yeye asiamuliwe hivyo inaingia akilini?
_ Kama upande mmoja kwa umoja wao unasema kuwa jambo fulani si la masilaha kwao kwanini upande wa pili usiwe tayari kulizungumza kwa lengo lakupata muafaka wa wote?
_Kama upande mmoja unafanya jambo kwa kutaka wao wenyewe kwanini inapofika upande mwengine kutaka kufanya kama vile iwe makosa?
Tukijijibu maswala hayo tutajuwa iwapo kilichokusudiwa ni muungano au kutawaliana.
 
Zanzibar inajitosheleza kwa kila kitu ,ila imeinamiwa na jinamizi la Muungano .
 
Na haya mambu ya kusheherekea kila mwaka ni ufisadi tu,kwa nini hizi sherehe zisiwepo kila baada ya miaka mitatu ,kila mwaka Uhuru,Muungano,wakulima sijui yaani wizi mtup.

Halafu haina haja ya Karume kuwepo wakati Raisi wa Tanganyika hajawahi kuhudhuria hata sherehe moja.
 
Hakuna hata mtu mmoja mwenye akili timamu na ambaye hajawa "brain washed" na kasumba ataeshindwa kufahamu umuhimu wa kuwepo serikali ya Tanganyika katika mfumo wa sasa wa Muungano. Wapo wenye hoja ya kuwa kutakuwa na gharama nyingi lakini hii si kweli kwani serikali ya Muungano na zile za Zanzibar na Tanganyika zitagawana majukumu na hiyo gharama haitokuwa kubwa hivyo kama tunavyodanganywa na kudanganyana kwani hazitokuwa zikifanya shughuli sawa, kwa mfano kama ni Wizara ya Elimu ya JMT itakuwa ina majukumu fulani ya kimuungano ambayo hayatakuwa yakishughulikiwa na serikali nyenginezo, kuna nchi kadhaa duniani ambazo zimo katika mfumo na wala hakuna kuchanganyana, mambo yapo wazi kuhusu serikali gani ina majukumu gani etc. Kuhusu vyeo na gharama za kiuendeshaji kwa serikali za Tanganyika na Zanzibar basi ni wao wenyewe wataamua wanataka mfumo gani wa kiuendeshaji wa serikali hizo, kama wanataka waziri wakuu 6 na mawaziri 50 basi ni juu yao na wao ndio watajua vipi watagharamia hayo. Serikali ya JMT inaweza kusimamia upatikanaji wa kodi na mapato lakini itakuwa inachukua asilimia fulani tu kuendeshea shughuli zake na yaliyobaki kupewa serikali ya sehemu ambako mapato yale yametokea, hili litaondoa kero la haya mambo ya mafuta na almasi, zaidi ya yote itapunguza hizi kero za muungano na kudumisha muungano wetu kuliko huku kuburuzana tu ambako zaidi ya kujisifu kuwa tumeungana hakuna zaidi tunalolipata mbali ya hizi kero tu.

Kuhusu kuwa na serikali moja nadhani hii ni "pipe dream", sitegemei waZanzibari katika miaka hamsini ijayo watalikubali hili, njia rahisi ni kuwapachika jamaa wa kiTanganyika Zanzibar ili waweze kupunguza hisia hizi na hata kupinga kuvunjika muungano pindi ikipigwa kura ya maoni huko mbeleli, hili hivi sasa tayari linafanyika lakini pia bado litahitaji miaka mingi tu. Ukweli usiofichika ambao waTanganyika wanashindwa au hawataki kuufahamu ni kuwa ingawaje Zanzibar imo kwenye muungano kwa miaka 45 sasa lakini bado wazanzibari walio wengi na hata viongozi wao wanahisia za kinchi, angalia kwa makini marais wao tokea Mzee Karume mpaka leo kila mmoja alikuwa hakubaliani na vitu ambavyo vinaiondolea Zanzibar haki ya kidola, mzee Karume alisema wazi kuwa "Muungano ni kama koti" pale alipoona anaingiliwa kwenye maamuzi na hata alidiriki kusema hadharani kuwa "Azimio la Arusha mwisho Chumbe", Mzee Aboud Jumbe mbali na kuunganisha vyama alimalizikia kudai serikali tatu, kwa wale watakaokumbuka hesabu ya 1+1=3 kutoka kwa Mwalimu Nyerere, hii ni mifano michache tu lakini ukweli ni kwamba wakati umewadia kuwa na serikali tatu na kudumisha muungano wetu na tuache hizi kasumba za kutotaka kwenda kinyume na maadili ya Mwalimu Nyerere, tukumbuke tu kuwa tayari tushauua ujamaa na kujitegemea kwa manufaa ya umma sasa inabidi tuanze kulishughulikia hili la muungano kabla halijaanza kutuletea matatizo zaidi, usipoziba ufa...........................utakuja jenga nyumba nzima.
 
Toka tumeungana Zanzibar haijatoa Raisi wa Muungano na kwa mfumo huu wa vyama vingi ndio tusahau,sasa ikiwa nchi moja hata nafasi ya uraisi wa mikasi itakosekana na uwaziri ndio kabisa hatuoni ndani halikadhalika siku za mwanzo watahamishwa wakuu wa mikoa kupelekwa mabara mara ya pili hakuna hata mmoja wote machogo.Mafisadi watahodhi hazina ya Zanzibar na kuteka fukwe zote ,i WaZanzibari watageuzwa watumwa ndani ya nchi yao.
 
Vipi Viswani ina watu mil. 1 na Bara 40!

Je hiyo serikali ya Muungano nani atagharamia? Mtasema Bara itoe 95% ya budgeti ya Muungano..maana uchumi wa Visiwani mdogo! Sii bora tu kuendelea na serikali mbili za sasa?

Kubwa mie nalililiona ni nani agharamie huu Muungano wa serikali ya 3!

Hii ndo rationale ya kuwa na selikali 2 kulingana na udogo wa Visiwani!

Mfano Visiwani wangekuwa na uchumi mkubwa na watu wengi..Nyerere na Karume wangeanzisha serikali 3 wakati ule!
 
Toka tumeungana Zanzibar haijatoa Raisi wa Muungano na kwa mfumo huu wa vyama vingi ndio tusahau,sasa ikiwa nchi moja hata nafasi ya uraisi wa mikasi itakosekana na uwaziri ndio kabisa hatuoni ndani halikadhalika siku za mwanzo watahamishwa wakuu wa mikoa kupelekwa mabara mara ya pili hakuna hata mmoja wote machogo.Mafisadi watahodhi hazina ya Zanzibar na kuteka fukwe zote ,i WaZanzibari watageuzwa watumwa ndani ya nchi yao.


Sidhani kama kutoa raisi ndio kutakuwa suluhisho la matatizo ya Muungano, Mwinyi (ingawa wengine wanadai si Mzanzibari) ni raisi tokea Zanzibar lakini wakati wake hakukuwa na tofauti yoyote ya maana kwenye huu muungano, mimi ninaona kuna juhudi za makusudi kuidhoofisha serikali ya Zanzibar ili tuwe na serikali moja huko mbele, hii nadhani ndio sera halisi ya CCM kwenye muungano hivyo musitegemee wao kukubali kuwa na serikali tatu, itakuwa kama wanarudi nyuma, having said that I still give them the benefit of the doubt.
 
Toka tumeungana Zanzibar haijatoa Raisi wa Muungano na kwa mfumo huu wa vyama vingi ndio tusahau,sasa ikiwa nchi moja hata nafasi ya uraisi wa mikasi itakosekana na uwaziri ndio kabisa hatuoni ndani halikadhalika siku za mwanzo watahamishwa wakuu wa mikoa kupelekwa mabara mara ya pili hakuna hata mmoja wote machogo.Mafisadi watahodhi hazina ya Zanzibar na kuteka fukwe zote ,i WaZanzibari watageuzwa watumwa ndani ya nchi yao.

unamaanisha nini zanzibar haijatoa hata raisi mmoja? Mwinyi alikuwa nani?
 
Vipi Viswani ina watu mil. 1 na Bara 40!

Je hiyo serikali ya Muungano nani atagharamia? Mtasema Bara itoe 95% ya budgeti ya Muungano..maana uchumi wa Visiwani mdogo! Sii bora tu kuendelea na serikali mbili za sasa?

Kubwa mie nalililiona ni nani agharamie huu Muungano wa serikali ya 3!

Hii ndo rationale ya kuwa na selikali 2 kulingana na udogo wa Visiwani!

Mfano Visiwani wangekuwa na uchumi mkubwa na watu wengi..Nyerere na Karume wangeanzisha serikali 3 wakati ule!

Angalia mfumo wa serikali ya nchi kama Canada, wana federal government ambayo ina majukumu yake na provincial government za kila sehemu ya muungano wao ambazo pia zina majukumu yake, kuna province ambazo kubwa na tajiri kama Ontario na Alberta na kuna province ni ndogo kama Prince Edward Island ambayo pia ni masikini, wanavyogharamia budget ya muungano wao ni kutokana na federal taxes ambazo ni sawa nchi nzima, vile vile kila province ina serikali yake na bunge lake, kila province ina haki ya kukusanya mapato ya ziada kwa matumizi katika province hiyo kama bunge la province hiyo litaona kuna haja ya kufanya hivyo. Vile vile wabunge wa bunge la Muungano wao wanatoka kwenye sehemu kulingana na idadi ya watu, kwa mfano kama province ina watu milioni moja basi haitotoa wabunge sawa na province yenye watu milioni mbili. Maana yake kama unachangia zaidi basi unakuwa na sauti zaidi 🙂
 
Katika katiba ya Jamhuri ya Muungano hakuna ndani yake kitu Tanzania Bara ,hivyo mapato yote ni ya Tanzania ,hapa kuna wizi ,au hamjui ?
 
Helikopta nayo imeshindwa kutua Zanzibar? Kama kweli hali mbaya ya hewa ndiyo sababu basi kuna uzembe mkubwa na watu watakiwa kuwajibika. Nijuavyo, na kwa ukaribu wa Dar na Zanzibar, weather ya znz lazima ifahamike hata kabla ndege haijaruka kwenda huko. Hivyo wangetumia helikopta instead. Aidha, hali ya hewa leo na jana haijawa na tofauti sana, so tahadhari ingechukuliwa mapema. I hope there are other reasons besides weather
 
Junius,
Mkuu unaposema hakuna Mzanzibar anayetaka Muungano ufe unakuwa tofauti na hoja nyingi nazozisoma humu..Mwiba, geme Theory na wengine wengi tu maelezo yao ni kutokuwepo kwa Muungano. Sasa nnachoelewa mimi sababu zote zinatokana na Muungano uliopo kutotambuliwa na wengi Wazannzibari..
Madai mengi yanahusu Bara na utawala wake wakati mimi nachofahamu ni kwamba Zanzibar iinataliwa na CCM Zanzibar hao kina Karume ambao sio tu wameiba Mapinduzi bali wamechukua hata mali zote na kuzifanya mali zao.. hata kidogo alichojenga marehemu baba yake kwa faida ya Wazanzibar leo hii ni mali yao (baraza la mapinduzi) na wajukuu wao..Tatizo sio Muungano uwe wa vyama ama nchi isipokuwa ni viongozi wabovu wanaoshindana kuchuma umaskini tuliokuwa nao.. Hizi ni sera za chama CCM ktk kujiandaa na Ubapari kwani wanataka kizazi chao kiwe ktk hali nzuri pindi Ubepari utakapo shamiri nchini.....It's simple as that. Hakuna chama hata kimoja nje ya CCM kinakubaliana na mfumo wa serikali yetu hivi sasa iwe bara au Visiwani hivyo tatizo haliwezi kuwa Muungano wenyewe hata kama ukivunjwa au kufanyiwa marekebisho ambayo bado yatakuwa for the interest of Party..

Nakubaliana sana na mtazamo wako ktk swala zima isipokuwa tu unachoshindwa kuelewa ni kwamba Muungano as Union hauna matatizo kabisa ila matumizi ya Muungano wenyewe..Wanachoomba wengi ni samli wakati hakuna maziwa, na kutokana na hasira za kukosa samli, suluhu rahisi kwao ni kuua ng'ombe kwa sababu maziwa hayawafikii wananchi..Hapa ndipo naposhindwa kuelewa mawazo mengi humu ndani kwani kama hutakuwa na ng'ombe kuna uwezekano gani wa kupata hata hayo maziwa acha mbali hiyo samli unayoitaka!..
Utasikia wakityoa mifano ya Jumuiya ya Afrika mashariki kama vile kuna uhusiano wowote kati ya Jumuiya ya nchi tawala na Muungano.

Mwiba,
Mkuu wangu sio kweli Zanzibar haitambuliwi duniani kwa sababu ya Muungano bali ukweli ni kwamba Tanganyika ndiyo isiyofahamika duniani..Na sidhani kama kuna mtu anataka kujua state za Missouri, Iowa, Mississippi au Ohio zinafahamika kiasi gani kulingana na New York, Florida, Michigan au California ili muungano wao uwe wa haki!
Pia, unapozungumzia Muungano wa nchi uliobomoka mkuu wangu ni muhimu ufuatilie pia kile kilichofuatia.. Yugoslavia ya jana sii ya leo, Urusi ya jana sii ya leo, Chec ya juzi sii ya jana na kadhalika, Uhasama uliopo kati ya nchi hizo huwezi hata kupima..kila moja yake ina historia mpya ya mauaji na ukabila kuliko wakati wowote, hivyo ni lazima nasi tuyaweke maswala haya bayana ili kila Mtanzania atakaye amua kuvunjika kwa Muungano apate kuelewa athari zake.. Ni rahisi sana kuzungumzia lakini inapotokea mkuu wangu ni sawa na swala la ndoa.. lazima mmoja wetu atapata mke/mme mwingine na mara zote wivu huingia kati na kuzua uhasama.
 
Naona umeishiwa Hoja kwani CUF pia walikwambieni mkatae SHIRIKISHO LA AFRIKA MASHARIKI? Kwani kwenu Muungano si sawa na Ibada kila ukiifanya sana ndio utapata pepo zaidi? Basi ipelekeni nchi shirikisho la Afrika Mashariki huko hilo Limuuungano litakuwa kubwa zaidi.


Ha haa mkuki kwa nguruwe tu 🙂 hiki ni kigezo kizuri kwa wenzetu waTanganyika kufahamu nini kimetutokea Wazanzibari, wanajua ndo maana hawataki shirikisho la Afrika Mashariki
 
Angalia mfumo wa serikali ya nchi kama Canada, wana federal government ambayo ina majukumu yake na provincial government za kila sehemu ya muungano wao ambazo pia zina majukumu yake, kuna province ambazo kubwa na tajiri kama Ontario na Alberta na kuna province ni ndogo kama Prince Edward Island ambayo pia ni masikini, wanavyogharamia budget ya muungano wao ni kutokana na federal taxes ambazo ni sawa nchi nzima, vile vile kila province ina serikali yake na bunge lake, kila province ina haki ya kukusanya mapato ya ziada kwa matumizi katika province hiyo kama bunge la province hiyo litaona kuna haja ya kufanya hivyo. Vile vile wabunge wa bunge la Muungano wao wanatoka kwenye sehemu kulingana na idadi ya watu, kwa mfano kama province ina watu milioni moja basi haitotoa wabunge sawa na province yenye watu milioni mbili. Maana yake kama unachangia zaidi basi unakuwa na sauti zaidi 🙂

Nkazahau,

Fed. gov. unayozungumzia kwa Visiwani na Bara..hizo 97% ya pesa kuendesha Fed. Gov. zitatoka bara!

Maana ukiangalia idadi ya watu: 97% ya Watanzania wanatoaka Bara na 03% ndo wanatoka visiwani!

Na kwa hiyo hata mawaziri atatoka tu mmoja au may be wawili, Wabunge yaani watakuwa 03% ya wabunge wa sasa yaani Visiwani watatoa tu Wabunge kama 10 wakati Bara watatoa zaido ya 300!

Bado tuko pale2: je hiyo serikali ya 3 nani ataiharamia? kama ni Bara: basi mfumo wa sasa bado una faida zaidi Visiwani!
 
Back
Top Bottom