Muungano wa Tanganyika na Zanzibar: Una faida gani na kwa manufaa ya nani?

Nasema hivyo coz huko uliko hawataki kusikia kitu kama hicho, ni kama unapingana na chama chako. Na siku zote uungwana kama upo kwanye kundi ambalo unadhani haliendani na unacho amini ni vizuri ni vizuri ukajiuzuru basi
Nijiuzuru nafasi ipi?
 
Siku hizi una akili. Sasa nimeamini Ulaya ndio kila kitu, kama paradiso vile yaani pamoja na yote ukikaa karibu na mzungu nawe unakuwa na akili (tukubaliane tu waafrika akili zetu za kuungaunga ndio maana mfalme wetu tuliyemchagua anaomba mpaka neti kwa wazungu pamoja na rasilimali zooooote!)
Mi nashangaa hiki Chama Cha Makalio kwa nini kinaing'ang'ania Z'bar nchi masikini, imejaa udini, ukabila, haiwataki Watanganyika, imeshajitenga
Tanganyika ni nchi tajiri saaana tatizo watawala wake wanafikiria kwa kutumia mdomo, tumbo na makalio
 
Zanzibar ni sehemu ya Tanganyika, piga ua garagaza! Liwalo na liwe...
 
Lukosi napingana na wewe katika mambo mengi ila kwa hili la Tanganyika yetu pamoja sana 100%.
 
Mkuu hata mimi nilikuwa na mawazo kama ya kwako. Ila sasa kama wanatufanyia ubaya mkubwa namna hii wakati tumeungana je tukiacha kuungana itakuwaje. Nyerere alikuwa na akili sana sababu alishaona jamaa pasuakichwa mbaya.
 
Zanzibar ni sehemu ya Tanganyika, piga ua garagaza! Liwalo na liwe...

Hicho kitu hakiwezekani kabisa,umewahi kusikia zanzibar kuna tembo,zanzibar si tanganyika milele.
 

hauna faida yoyote zaidi ya usumbufu hata ukivunjwa hakuna hasala!
 
Nashangaa hawa sisimizi-zanzibar chini ya kificho wa panju wataenda na zanzibar yao au la!
 
Wewe CCM kweli? au njaa ndo zilikuponza?

Makete Kwetuumeuliza swali ambalo hata mimi nimejiuliza kuhusu Chris Lukosi
Ila ana hoja ya ukweli,last year nilienda Zanzibar na kundi la watu fulani.Wazanzibari walitu identify kama Watanganyika.Na kwenye mazungumzo yao wanalitumia sana neno Tanganyika kutu identfy wa bara.Ni sisi wenyewe na serkali yetu ya CCM ambao tunajitoa ufahamu na kujiita Tanzania Bara,msamiati ambao wao hawana.
 
Last edited by a moderator:
labda nitumie lugha ya mifano,
hivi wewe huwezi kushirikiana na ndugu yako asie na kitu? asie na mali? nadhani kama waafrika na zanzibar kama ndugu zetu kihistoria tuna haki ya kushirikiana nao, sasa swala la serikali mbili au Tatu tujadili faida na hasara zake.

kwenye ndoa kuachana ni hasara zaidi kuliko kuvumiliana na kurekebisha pale penye mapungufu.

siipendi CCM asilani kwasababu ya upuuzi inaofanya; lakini kwenye hoja ya msingi ni budi tusimame pamoja kama Taifa.

UMOJA NI NGUVU UTENGANO UDHAIFU.
 
Ladies and Gentlemen, my view is Tanganyika, Zanzibar and Africa for the whole are interconnected each other.I'm frankly to say that, we are one blood before the scramble and partion of our continent conference held in German 1884.in addition,the border has crosses us and not us cross the border,and I think there is no honor to say either I'm from Tanganyika or Zanzibar.Furthermore,I think Africa is forgetting who is their enemy our real enemy is white people who made us in this mess.We don't need to fight among us for the border made by our real enemy.Wake up brothers and sisters.
 
Khaa!!! Mwagito Chris Mwa Lukosi!! muungano siyo suala la kisiasa pekee kama wengi wenye tamaa za madaraka wanavyofikiri. Muungano una sehemu nyingi za kujadili.. Wapo wabara wengi wanafaidika na muungano vilevile wazanzibari. Tujadili kwa mapana yake katika historia, uchumi, jamii, ulinzi nk. Siyo kurupuka tuu kama umegonga kisado cha mkangafu
 
Mkuu mbona Kenya inapakana na Somalia?
Leo umekula jicho la kuku nini? maana naona kichwa chako leo kinafanya kazi iliyokusudiwa na Mungu. Lakini hata sisi watanganyika tumepakana na Rwanda na Burundi, au kwa sababu watu wake hawana mrengo wa kimwigulu.
 
Khaa!! Kila siku huwa nasema na sisiti kusema kuwa Watz ni waji nga sana. Zamani ilikuwa nchi ya wakulima na wafanyakazi siku hizi ni nchi ya wanyonge na wanasiasa. Wanasiasa wanataka kila kitu tufikiri kisiasa (uwongo uwongo). Tujitibu kisiasa, tujenge barabara kisiasa hata tuoe kisiasa. Tuache ujinga, tuamue kwa maslahi ya wote na si kwa ajili ya hawa waganga njaa wachache au hawa majobless wenye uchu wa madaraka. Tuseme Noo kwa wapiga domo (wanasiasa) wanaobugia kodi zetu bila ya kufanya kazi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…