Muungano wa Tanganyika na Zanzibar: Una faida gani na kwa manufaa ya nani?

Muungano wa Tanganyika na Zanzibar: Una faida gani na kwa manufaa ya nani?

wazanzbr wale watakuwa na nchi mbili,yaani kisiwa Cha unguja kitajitegemea na pemba pia itakuwa nchi, halafu wale wako mil.moja tu ,sisi tuko mil60+,dawa yao tukishavunja tu muungano tunapeleka vijana wetu zbr wakaoe mabnt wote wa zbar,baada ya miaka michache tutakuwa na watt wetu na wajukuu kule,hatimaye litakuwa koloni letu kwa mala nyingine
Na huku bara tugawane, wa mikoani mrudi mikoani mtuachie pwani yetu wapwani
 
Kuiachia Zanzibar ni jambo gumu sana. Ifahamike kuwa hatukuungana na Zanzibar kwa matakwa yetu. Lilikuwa ni ombi la US kwa Mwalimu Nyerere. Aliyesimamia hilo zoezi la kuhakikisha Zanzibar inakuwa chinibya Tanganyika ni Henry Kissinger, mtu anayeaminika kuwa na very high IQ, baada ya Mzee Jomo Kenyata kukataa. Yeye ndiye aliyetengeneza muundo huu wa Muungano usioeleweka ili Wazanzibar waone wapo kwenye Muungano, lakini Tanganyika ikiwa na uwezo wa kuingilia kitu chochote cha kiusalama, Zanzibar.

Zanzibar, Tanganyika inaishikilia kwa ombi la mataifa makubwa kwa sababu za kiusalama. Kwa hiyo, Zanzibar siyo rahisi kuiachia. Hii ndiyo sababu iliyo dhahiri lakini isiyotamkwa. Mambo ya sijui sisi ni damu moja, sijui nini, ni hadithi.
Hilo wazo kuwa USA ndio walishinikiza muungano mmeitoa wapi? Au ndio mambo ya kuruhusu wageni kutuandikia historia yetu. USA miaka ya sitini halikuwa taifa lenye shobo na mambo ya watu kama ilivyo siku hizi, kusema walishinikiza muungano ni kuwapa ujiko na u nafasi ambao hawana kwenye historia yetu ya kipindi hicho
 
Hilo wazo kuwa USA ndio walishinikiza muungano mmeitoa wapi? Au ndio mambo ya kuruhusu wageni kutuandikia historia yetu. USA miaka ya sitini halikuwa taifa lenye shobo na mambo ya watu kama ilivyo siku hizi, kusema walishinikiza muungano ni kuwapa ujiko na u nafasi ambao hawana kwenye historia yetu ya kipindi hicho
Kijana, siwezi kukulaumu. Nazungumza hili kwa uhakika mkubwa. Siyo kwa kuokoteza habari, bali kwa kuzungumza na watu waliohusika.

Yaelekea huijui vizuri historia ya nchi hii zaidi ya vile vitabu vya historia vya shule za msingi. Tulipopata uhuru, rafiki mkubwa wa Mwalimu alikuwa Rais Kenedy. Na nchi rafiki wakubwa wa Tanganyika ilikuwa US na Germany. Na Germany ilikuwa ndiye agharamie mpango wote wa maendeleo wa miaka 5.

Mashirikiano yetu mapya na Ujerumani Mashariki na kifo cha Kennedy, na sera za Rais mpya ya US, , na Germany kufuta mpango wa kugharamia mpango wa maendeleo wa miaka 5, ilimfanya Mwalimu kuchukia na kuwageukia Wajamaa, maadui wa US na Germany, kama njia ya kulipiza kisasi.

Tanganyika baada ya uhuru haikuwa na sera ya Ujamaa, ujamaa ulikuja baadaye, tuliposhindwa pa kushika.

Mwungano wa Tanganyika na Zanzibar, uliasisiwa na Marekani. Henry Kissinger ndiye aliyekutana na Mwalimu. Mwalimu wakati huo alikuwa hajawahi kukutana na Karume tangu awe Rais wa Zanzibar, na wala hakuwa na ukaribu naye. Wazanzibari walionekana kuwa karibu zaidi na Wakenya kuliko Watanganyika. Ndiyo maana karata ya kwanza ya Kissinger ilikuwa kwa Jomo Kenyatta. Alipokataa, Kissinger akamwona Mwalimu. Kisha Kissinger alenda Zanzibar kuonana na Karume akiongozana na Mzee Kaduma. Kissinger akarudi tena kwa Mwalimu kumwambia kazi amemaliza. Baada ya hapo ndipo Mwalimu akasafiri kwenda Zanzibar.

Mwalimu alikuwa rafiki mkubwa wa Rais J.F. Kennedy. Hata baada ya kifo cha Kennedy cha ghafla, kuuawa kwa risasi Nov 22, 1963, aliyemfuatia, Lyndon aliendeleza urafiki na Mwalimu, japo sera ya nje ya US ilikumbwa na misukosuko mingi. Baadaye ilipodhihirika kuwa sera ya nje ya Marekani kwa Afrika ilikuwa imebadilika kabisa, Mwalimu ikabidi aanze kuutazama Muungano kwa namna tofauti badala ya matakwa ya US. Na ndipo mambo mengine ya kuongezwa yakaanza kufikiriwa. Agenda kuu ya Muungano mwanzoni, ilikuwa ni kuipa haki Tanganyika kuwepo kijeshi Zanzibar, na kuzuia Zanzibar kuwa na sera ya nje, ambayo ilionekana kuelekea kwenye ujamaa.
 
Kweli Mkuu Zanzibar ni mzigo kwa Tanganyika kwa vile mumeweka majeshi kila mtaa na uslama wa taifa kwa kila mtu huku vifaru mkivi
Hizo ndizo akili Za Kiafrika. Czekoslovakia iligawanyika Na kuwa nchi mbili wala hatukusikia akili Kama zako
Na ndiyo maana mimi siyo M Czechoslovakia.

Sent from my Nokia 5.1 Plus using JamiiForums mobile app
 
We umeona wapi muungano ambao unabagua watu?

Wazanzbar kumiliki ardhi TANGANYIKA n ruksa ila mtanganyika kumiliki ardhi Zanzibar haiwezekani

Asee uvunjike hata leo hamna Zanzibar mlichoifaidisha TANGANYIKA Zaid mmetupa mzigo tu wa kuwakopea kulipa tulipe Watanganyika
muarobaini wa matatizo yote haya ni katiba tu.watangulizi waliitengeneza hiyo katiba kwa ajili ya kulinda maslahi yao na pia inawezekana mazingira ya wakati ule yaliwalazimu wafanye vile lkn kwa sasa hakuna njia nyingine zaidi ya kuwa na katiba mpya na sielewi kwa nn mamlaka zinaogopa kuwa na katiba mpya wakati majirani zetu wamezibadilisha katiba zao mara kibao.katiba tulionao inatubagua na pia inatoa mamlaka makubwa kwa watawala.
 
Zanzibar nje ya muungano neema tupu.
Nje Ya Muungano hakuna Zanzibar, kuna waunguja na wapemba, kinachofanya mjiite wanzanzibar ni sababu ya Muungano.

Halafu ni species tofauti, mkibaki wenyewe mtavurugana fasta tu, kwasababu inaonekana Waunguja wahodhi mambo mengi ndani ya Zanzibar so Muungano ukivunjika, wapemba watataka nchi yao pia.

Halafu inner circle ya Uongozi Zanzibar(deep state yenu) wana mali nyingi bara hawawezi kubali waanze utaratibu mpya wa umiliki wa mali zao huku bara.mnaopiga kelele ni watu wa kati na chini sio wakina Bakharesa.

Maneno ya Mwl JKN kuna siku yatatimia.
 
Ni bora huu Muungano wetu ukavunjika halafu tukawa nchi jirani zenye kupendana kuliko maelezo,ila hivi tulivyo inakuwa kama hatuelewani.
Tugawane mbao kisha kila mtu ajenge mtumbwi wake.
Tatizo wabara hawajiamini kujitawala,wanahisi watagawika ,Zanzibar imekuwa kama hirizi.
Unajua situation inaweza kuwa iko hivi (haimaanishi kuwa kweli iko hivyo): Ukivunja Muungano, wanatokea wajanja kutoka mahali fulani na kuchonganisha pande zote mbili, halafu baada ya hapo mnaanza kupigana, na baada ya hapo kila mmoja anakuwa dhaifu. Baada ya kuwa dhaifu, wanaweka sasa watu wao kila upande, kama watawala. Mtawala wa Zanzibar anakuwa ni ndugu na mtawala wa Tanganyika, halafu baada ya hapo wanaanza sasa kusomba kila kitu kilichoko Tanganyika na kilichoko Zanzibar kuanzia madini almasi na kila kitu. Vipi version hii ya utawala ndiyo unayoipendelea zaidi; yaani unaanza na vita kwanza halafu baadaye unakuja kuibiwa rasilimali zote ulizonazo?
Nilikiuwa natoa mfano tu!
 
Fanya kazi tunza familia yako , somesha watoto km unao, tafta njia mbadala za kujiongezea kipato tofauti na kaz unayofanya .
Ila ukiangaika na mambo ya muungano ni kupoteza mda wako na iyo akili ya kufikilia na kuwaza muungano iwekeze kwenye vtu vingne vyenye maana ktk maisha yako

Hii Tanzania au Tanganyika, Zanzibar umezaliwa na utakufa bila kuona ikivunjika zaidi inazidi imalika sku ad sku.
 
Hii ndio faida ya the freedom of expression, ingekuwa ni enzi za Mwalimu, wewe mtu huku mjini,; tungekusahau!, ambao wangekuona ni watu wa kijijini kwako tuu, tena ukitoka nje kuota jua!.

Enzi hizo hata kufikiri tuu kuuvunja muungano ni kosa kubwa la uhaini!.
P
Halafu tunamkweza na kumnukuu kila uchwao kwamba “Nyerere kasema hoja haipigwi rungu.” Kasema wapi na katenda nini kwenye utawala wake ?

Nyerere dhalimu, unamfungaje mtu kijijijini kwao kwa kosa la kutoa maoni kwamba muungano hau make sense??? Halafu unatudanganya eti hoja haipigwi rungu.

Amekufa anajua na anatubu kwamba katika mengi aliyo eff up, moja kubwa ni hili la kuhujumu haki za Watanzania wenzake.
 
Unajua ni nini?
WaZanzibar hawana mchango kwa maisha ya Bara. Hilo hata wewe unalijua. Kama nimepotoka,nakubali kurekebishwa kwa mifano halisi. Muungano unawapendelea wazanzibar na kuwadekeza hadi inakuwa kero. Ka nchi kama mkoa lakini wabunge utitiri. Hamuoni hata aibu kuwaita watu wabunge badala ya makatibu kata?

Nilichoota mimi miaka kadhaa nyuma, wakati nimekereka na huu muungano nyonya damu, ni kwamba. Cha muhimu kwa bara ni geographical position ya Zanzibar na tabia za Wazanzibar za uvivu na uarabu. Nikaota kwamba , ni lazime tuwashikilie ili muongozwe kwa sababu kinyume cha pale, tunayoyasikia kule yatakuwa dirishani. Nani atakuwa salama?
Namkumbuka yule mzee aliyekuwa mbunge kutoka Katavi aliyesema unaweza kuwakusanya wazenj kwa kupiga filimbi au ngoma na wote wakakutanika pamoja.Nyerere alisema angekuwa na uwezo angekisumia mbali kisiwa hiki.
 
Huu muungano unaniboa sana, yaani sisi Watanganyika tupo kwa ajili ya kuwanufaisha Wazanzibar tu, na kwa sasa Watanganyika tumerudi kuwa utumwani maana Rais ni Mzanzibar,kule kwao Rais Mzanzibar wanapanga wanachokitaka na kuamuru kifanyike na kinafanywa na sisi Watanganyika, ni upumbavu na uzuzu wa sisi Watanganyika
 
Lengo la muungano ni mwanzo wa kuunganisha Africa mzima, sasa dhahili haiwezekani, hivyo inapaswa kurudi nyuma. Ukikosea njia nawe mgeni urudi nyuma ukafuate njia nyingine, sasa muungano inabidi ufe kwa kuwa hauwezi songa mbele.
Kwanza kujipendelea, kujijali, wale mashehe walioshikiliwa wa Zenji wasingefutiwa mashitaka iwapo Rais angeendelea kuwa toka bara, kwani kila mmoja anamwonea huruma nduguye! Leo kero nyingi za muungano zitatatuliwa hata zile utatuzi wake una ukakasi, ila kwa kuwa mkubwa katoka huko.
Wanafiki wote wako kimya, hata pele mambo ya muungano yanatatuliwa kwa kulazimisha! Kama walivyokuwa kimya kipindi cha jiwe, wanamwacha akiaribu nchini, leo ndio wanajitokeza bandari ijengwe, haya bwana!
 
Wabara walioko Zenji hawana mali nyingi zisizo hamishika tofauti na hawa wakojani huku Bara.

Sent from my Nokia 5.1 Plus using JamiiForums mobile app

tofauti ilokuepo ni kuwa hao wakojani walioku bara hizo mali wanamiliki kisheria kwa hiyo kuwatimua kinguvu sio ishu nyepesi kabisa, lazima patakua na taratibu za kufuatwa. Lakini wabara walioko Zenj wanamiliku Ardhi kinyume na sheria.
 
Back
Top Bottom