Muuza duka wangu anatishia kunishtaki

Muuza duka wangu anatishia kunishtaki

RingaRinga

JF-Expert Member
Joined
Jul 10, 2015
Posts
1,047
Reaction score
521
Wanajamvi habarini za asubuhi,

Nilifunga mkataba na muuza duka wangu kwa ajili ya kazi ya duka langu.
Mkataba tuliufunga kwa mtendaji wa kijiji tarehe 7.1.2020.
Mkataba ulikuwa na mashahidi upande wake na mimi.
Pia alidhaminiwa na mtu mmoja mwenye mali zisizohamishika.

Tulikubaliana nitakuwa namlipa tsh 50,000/= kwa mwezi.
Kwa kuwa nina kamgahawa tulikubaliana atakula hotelini kwangu ugali samaki au nyama mara mbili kwa wiki, na siku zingine wali maharage na mbogamboga angepewa kama zitakuwepo.

Pia kwa kuwa alikuwa anatokea wilaya nyingine tulikubaliana nimpe makazi, kitanda na neti na kiwe na umeme ambapo nagharamika mimi.

Makubaliano tulivyoandikishana ilikuwa kwamba nisiporidhika na utendaji wake nina haki ya kumwachisha kazi na niwe nimemlipa malipo yake yote ya 50,000 kwa kila mwezi.

Kwa kuwa utendaji wa kijana umekuwa duni sana na imeshindikana kujirekebisha nimeamua kumwachisha kibarua.

Sasa kijana ananivimbia eti siwezi kumwachisha kazi ghafla bila kumpa mafao ya kuacha kazi na atanishtaki labda nimpe malipo ya miezi mitatu (150,000) ili ajipange kupata kazi sehemu nyingine.

Sheria ya ajira za namna hii inasemaje ndugu wana JamiiForums?
Lukonge
 
Nikweli unapaswa kumpa kiunua mgongo kwani amekutumia tangu mwaka 2020 mpa leo.Kitaalamu ulipaswa umpe mkataba wa miezi mitatu mitatu ili kuepuka kumpa kiinua mgongo cha kufanya mpe hiyo 150 muachane tu ila akienda kukushtaki kwenye swala la kazi utalazimika kumlipa zaidi ya hiyo.Me nimuajiriwa niko serikalini taratibu za kazi nazijua

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
Nikweli unapaswa kumpa kiunua mgongo kwani amekutumia tangu mwaka 2020 mpa leo.Kitaalamu ulipaswa umpe mkataba wa miezi mitatu mitatu ili kuepuka kumpa kiinua mgongo cha kufanya mpe hiyo 150 muachane tu ila akienda kukushtaki kwenye swala la kazi utalazimika kumlipa zaidi ya hiyo.Me nimuajiriwa niko serikalini taratibu za kazi nazijua

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
Fanyia kazi huu ushauri haraka sana na wakati mwingine toa mkataba wa muda mfupi
 
Wanajamvi habarini za asubuhi,

Nilifunga mkataba na muuza duka wangu kwa ajili ya kazi ya duka langu.
Mkataba tuliufunga kwa mtendaji wa kijiji tarehe 7.1.2020.
Mkataba ulikuwa na mashahidi upande wake na mimi.
Pia alidhaminiwa na mtu mmoja mwenye mali zisizohamishika.

Tulikubaliana nitakuwa namlipa tsh 50,000/= kwa mwezi.
Kwa kuwa nina kamgahawa tulikubaliana atakula hotelini kwangu ugali samaki au nyama mara mbili kwa wiki, na siku zingine wali maharage na mbogamboga angepewa kama zitakuwepo.

Pia kwa kuwa alikuwa anatokea wilaya nyingine tulikubaliana nimpe makazi, kitanda na neti na kiwe na umeme ambapo nagharamika mimi.

Makubaliano tulivyoandikishana ilikuwa kwamba nisiporidhika na utendaji wake nina haki ya kumwachisha kazi na niwe nimemlipa malipo yake yote ya 50,000 kwa kila mwezi.

Kwa kuwa utendaji wa kijana umekuwa duni sana na imeshindikana kujirekebisha nimeamua kumwachisha kibarua.

Sasa kijana ananivimbia eti siwezi kumwachisha kazi ghafla bila kumpa mafao ya kuacha kazi na atanishtaki labda nimpe malipo ya miezi mitatu (150,000) ili ajipange kupata kazi sehemu nyingine.

Sheria ya ajira za namna hii inasemaje ndugu wana JamiiForums?
Lukonge
Ni bora tuu umpatie hiyo pesa! La sivyo wewe mwenyewe tangulia mahakama ya kazi utalipa zaidi hata ya milioni 100
 
aise yaani hukupaswa kubishana nae , kimya kimya mpatie hiyo laki na nusu muachana, ukiendelea kuzungusha halafu wakaja wajanja wakamshtua imekula kwako. mahakani utaingiliwa zaidi Hadi hutaamini .

yaani unamfungisha mkataba wa ajira wa elfu 50 kwa mwezi , hapo ulijichanganya Sana .
 
Wanajamvi habarini za asubuhi,

Nilifunga mkataba na muuza duka wangu kwa ajili ya kazi ya duka langu.
Mkataba tuliufunga kwa mtendaji wa kijiji tarehe 7.1.2020.
Mkataba ulikuwa na mashahidi upande wake na mimi.
Pia alidhaminiwa na mtu mmoja mwenye mali zisizohamishika.

Tulikubaliana nitakuwa namlipa tsh 50,000/= kwa mwezi.
Kwa kuwa nina kamgahawa tulikubaliana atakula hotelini kwangu ugali samaki au nyama mara mbili kwa wiki, na siku zingine wali maharage na mbogamboga angepewa kama zitakuwepo.

Pia kwa kuwa alikuwa anatokea wilaya nyingine tulikubaliana nimpe makazi, kitanda na neti na kiwe na umeme ambapo nagharamika mimi.

Makubaliano tulivyoandikishana ilikuwa kwamba nisiporidhika na utendaji wake nina haki ya kumwachisha kazi na niwe nimemlipa malipo yake yote ya 50,000 kwa kila mwezi.

Kwa kuwa utendaji wa kijana umekuwa duni sana na imeshindikana kujirekebisha nimeamua kumwachisha kibarua.

Sasa kijana ananivimbia eti siwezi kumwachisha kazi ghafla bila kumpa mafao ya kuacha kazi na atanishtaki labda nimpe malipo ya miezi mitatu (150,000) ili ajipange kupata kazi sehemu nyingine.

Sheria ya ajira za namna hii inasemaje ndugu wana JamiiForums?
Lukonge
Mpe hiyo hela kwa maandish iachane nae Chief asije kukuletea jau
 
Back
Top Bottom