MUZIKI: SILAHA KUNTU KUELEKEA MEI MOSI HII

MUZIKI: SILAHA KUNTU KUELEKEA MEI MOSI HII

ALT

Member
Joined
Oct 6, 2021
Posts
78
Reaction score
90
Wanabodi

Habari zenu.
Kuna watu wengi wanao uwezo wa kutunga nyimbo. Nawaalika watu wote wenye uwezo huo katika uzi huu.

Tungeni mashairi yenye heshima na staha kuelekea mei mosi hii(2022). Zimebaki siku chache sana kufahamu mbichi na mbivu juu ya stahiki za wafanyakazi wote hapa Tanzania.

Kumbukeni, muziki una nguvu kubwa kwasababu unaathiri hisia moja kwa moja, nani ajuaye? Usishangae mashairi haya yakaleta mema mei mosi hii. Njooni hapa wanamuziki. Wanasiasa kwanza watulie, hebu muziki uongee.

Naanza na huyu,

Mtunzi: Clion odhiambo

Verse 1
Mola mbariki mwajiri, mjaze afya njema, hekima, akili
Ajue tupo wafanyakazi wazalendo kweli, tusopenda udokozi
Mei mosi hii basi, (tuongezee kasalari, hakakutoshi wafanyakai, bila ya mangi kutoka hatuli)×2

Verse 2

Matumizi yangu yote ni ukopaji, hakajatoka ila kameisha kasalari
Kodi ya nyumba, watoto ada, makato kata, jamii(kata), songesha(kata), benki( kata), kuyuma, kupokea(kata)

(Hakatutoshi, kasalari, bila ya mangi nyumbani mimi sili, mwajiri, boresha salari, mwajiri, ongeza salari)×2

Kiambatanisho: Audio , jina ka-salari

Kwa wale wa kuangalia video, katafteni huko yutyubu chaneli yake uyo jamaa "official clion odhiambo"

karibuni watunzi kwa vitu kuntu, mziki kuntu...zingatia heshima na staha
" nani ajuaye, yumkini, sauti hii ya hisia inaweza kusikika kwa wafalme na wafalme wakatabasamu mei hii ya mosi"😊😉
 
Mbona wanamuziki hawadondoshi mashairi?
 
Back
Top Bottom