Mwabukusi: Waziri hana Mamlaka ya kufuta Kijiji na asili ya Watu wa Ngorongoro

Mwabukusi: Waziri hana Mamlaka ya kufuta Kijiji na asili ya Watu wa Ngorongoro

Rais wa Tanganyika Law Society (TLS) Boniface Mwabukusi, amesema Waziri hana Mamlaka ya Kufuta Vijiji vya Ngorongoro

Ameyasema hayo leo 20/08/2024 Mkoani Dar Es Salaam alipokuwa anaongea na Waandishi wa habari. Amesema kama TLS wanaaangalia cha kufanya. "Wale wananchi wa Ngorongoro hawapaswi kupuuzwa, Warudishiwe huduma Muhimu pia Warudishiwe vituo cha kupigia Kura. Ni lazima tujue chanzo cha Tatizo Ngorongoro ni nini?". Amesema Mwabukusi

Mwabukusi amelipongeza Jeshi la Polisi kwa kuwakamta wabakaji na kuwafikisha Mahakamani. Amesema kuwafikisha mahaksmani ni hatua ya kwanza, ametaka Polisi imfikishe Mahakamani aliyewatuma pia. Pia amewata Polisi kumuachia na kumuweka wazi mwanamke alipata madhira ili haki yake ipatikane ikiwrmo kupewa msaada wa kisheria..

Stsy tuned

=====

20 Agosti, 2024

TAARIFA KWA UMMA

KUHUSU WITO WA WANANCHI WA NGORONGORO NA MAENEO MENGINE KUTAKA KUHESHIMIWA KWA HAKI ZAO

Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) kimepata taarifa kupitia mitandao ya kijamii kwa njia ya video iliyosambaa kwenye mitandao hiyo ikionyesha maandamano yaliyofanywa mnamo tarehe 18 mwezi Agosti, 2024 na mamia ya Wananchi wa Ngorongoro wakidai kuheshimiwa kwa haki zao. Katika maandamano yao miongoni mwa mambo mengine, Wananchi hao wamesikika wakilalamikia kuondolewa kwenye maeneo yao kinyume na utaratibu bila wao kuridhia pamoja na kuondolewa kwa huduma zote za kijamii kama vile shule, huduma za afya pamoja na maji. Kutokuwepo kwa huduma hizi muhimu kumepelekea Wananchi hao kuendelea kuishi katika mazingira magumu.

Tamko la Umoja wa Mataifa Juu ya Haki za Watu wa Asili la Mwaka 2007 limeeleza wazi katika ibara ya 10 kwamba watu wa asili hawataondolewa kwa nguvu kutoka kwenye ardhi au maeneo yao, uhamisho wowote wa watu wa asili hauwezi kufanyika bila idhini yao huru

Kwa mujibu wa ibara ya 24 (1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka 1977, kila mtu anayo haki ya kumiliki mali na haki ya hifadhi ya mali yake aliyonayo. Haki ya kumiliki mali ni moja ya haki ya msingi ya binadamu. Ibara 24 (2) imeeleza wazi kwamba mtu yoyote hatonyang’anywa mali yake isipokuwa kwa kuzingatia taratibu za kisheria ikiwepo ulipwaji wa fidia stahiki.

TLS inatoa rai kwa Serikali kuonyesha nia yake ya dhati kwa kurudisha huduma zote za kijamii kwa Wanachi wa Ngorongoro kwa kuwa ni haki yao. Pia, vituo vya kujiandikisha kwa ajili ya kupigia kura ambavyo Wanachi wa Ngorongoro wanalalamika kwamba havipo katika maeneo yao virudishwe ili wapate kuitumia haki yao ya kikatiba ya kujiandikisha na kuboresha taarifa zao kwa ajili ya uchaguzi wa Serikali za mitaa uliopangwa kufanyika mwezi Novemba mwaka 2024 pamoja na Uchaguzi mkuu utakaofanyika mwaka 2025.

Baraza la Uongozi la TLS limeona jambo hili la Ngorongoro na maeneo mengine linahitaji ufuatiliaji wa kina zaidi na kwa sababu hiyo, Baraza limeamua kuunda kamati maalum itakayofuatilia jambo hili kwa ukaribu ikiwa ni pamoja na kuwasiliana na Idara, Wizara na vyombo vyote vinavohusika na suala la Ngorongoro ili kujua ukweli zaidi na kuhakikisha misingi ya sheria za nchi yetu inafuatwa.

Kamati iliyoundwa inajumuisha wajumbe wafuatao:

*Dr. Rugemeleza Nshala
*Tike Mwambipile
*Bumi Mwaisaka
*Laetitia Petro Ntagazwa na
*Paul Kisabo.

Miongoni mwa mambo mengine kamati itafanya mambo yafuatayo:

*Kufanya mashauriano na taasisi mbalimbali pamoja na kutembelea baadhi ya maeneo yenye migogoro ili kujua uhalisia wa migogoro husika.

*Kufanya Mapitio ya Sera ,Sheria na Mazoea pamoja na kuzichambua kuhusiana na umiliki wa Ardhi kwa Wazawa pamoja na shughuli za uwekezaji na Uhifadhi na kubaini uzingativu wa Haki za Msingi za Raia katika maeneo husika kwa kuzingatia Katiba, Sera na Sheria za Nchi.

*Kuandaa kongamano (Symposium) la Kitaifa kuhusiana na namna bora ya kufanya maendeleo kwa kuzingatia na kulinda haki za Wazawa katika Ardhi zao za Asili pamoja na haki zao za Kijamii, Kiuchumi na Kiutamaduni katika maeneo yanayofikiwa na shughuli za uwekezaji.

*Kubaini mashauri au hatua zote ambazo zimechukuliwa na walalamikaji pamoja na walalamikiwa kisheria na kiutaratibu katika kuhakikisha uzingativu wa sheria na kubaini majina ya watu ambao kweli wameridhia kuondoka kwa hiyari kwenye maeneo yao na ambao hawakuridhia kuondoka kwa hiyari kwa sababu ya wao kuamua kubaki katika eneo lao la asili Ngorongoro.

*Kubaini na kulishauri Baraza la Uongozi la Chama Cha Mawakili wa Tanganyika juu ya hatua zakuchua ili kupata ufumbuzi wa kudumu kuhusu swala la migogoro ya Ardhi inayosababishwa na mipango ya uwekezaji au uhifadhi.

Kamati inatarajiwa kumaliza kazi tajwa ndani ya muda wa kipindi cha siku 30.

TLS inawaomba Wanachama, Wananchi pamoja na wadau mbalimbali wa Sheria kutoa ushirikiano kwa Kamati maalum iliyoundwa ili TLS kwa mamlaka iliyopewa chini ya kifungu cha 4 cha Sheria iliyounda TLS (Tanganyika Law Society Act Cap. 307) iweze kutimiza wajibu wake wa kuishauri Serikali na Kulinda haki za Wananchi kwa lengo la kupata suluhisho la kudumu.

Imetolewa na Baraza la Uongozi la Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS)

Boniface A.K Mwabukusi

Rais
# RUBBISH
 
Kafanye utafiti uache bla bla Mr Stuxnet.

Wamasai hawajawahi kuwa chanzo cha Mazingira kuharibika over centuries ambazo wamekaa hapo.
Utafiti upo na huo ndiyo umwetumika kuwapunguza. Nakupa official report ya Kamishna wa Uhifadhi hapa:

"Wakati Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro inaanzishwa mwaka 1959 ilikuwa na idadi ya watu wasiozidi 8,000 na mifugo isiyozidi 261,000, idadi hii ya watu kwa wakati huo ilionekana kuwa ndogo lakini iliendelea kuongezeka hadi kufikia kaya 23,889 zenye watu zaidi 100,000 na mifugo zaidi ya 850,000 (taarifa hizi ni kwa mujibu wa sensa ya mwaka 2022).

Ongezeko hili la watu na mifugo limekuwa changamoto kwa zaidi ya
miaka sitini toka kuanzishwa kwa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro kutokana na muingiliano wa shughuli za uhifadhi, utalii na maendeleo ya jamii ya watu wanaoishi ndani ya hifadhi, ili kuinusuru mamlaka ya hifadhi ya Ngorongoro.

Serikali baada ya kupitia tafiti mbalimbali zilizofanywa na watafiti mbalimbali zote zikihusu matumizi mseto ya ardhi ya eneo la hifadhi ya ngorongoro na athari zake kwa ustawi wa mamlaka pamoja na jamii ya wananchi wanaoishi ndani ya
hifadhi serikali ya awamu ya sita ilichukua uamuzi wa busara wa kuwaelimisha wananchi wanaoishi ndani ya hifadhi ya Ngorongoro kuhama wao wenyewe kwa hiari kwenda maeneo mengine yaliyotengwa na serikali pamoja na sehemu nyingine wanazochagua wao wenyewe kwa ajili ya kupisha uhifadhi pamoja na kuboresha maisha yao, maeneo mahususi yaliyotengwa na serikali kwa ajili ya wananchi kuhamia ni pamoja na kijiji cha Msomera kilichopo katika wilaya ya Handeni, Saunyi wilaya ya Kilindi na Kitwai B wilaya ya Simanjiro."

(Richard Kiiza, Kamishina wa Uhifadhi wa Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro)
 

🔴LIVE: TLS WAFUNGUKA SAKATA LA UTEKAJI NA MASAI NGORONGORO​


View: https://m.youtube.com/watch?v=0D_CSblrS5c


Mimi nina mtazamo tofauti na hawa wanasheria wetu kuhusiana na huu mgogoro....
1. Ikumbwe kuwa maeneo karibia yote yenye wanyama (National Parks, kuna kipindi huko nyuma kuna baadhi ya watu hata vijiji walilazimika kuhamishwa na kupewa maeneo mbadala ili kuyapisha yabaki kama hifadhi ya wanyama kwa faida ya watanzania wote.

2. Ninavyokumbuka kwenye historia, Wamasai waliachwa Ngorongoro kwa sababu tu walionekana hawakuwa na madhara kwa wanyama na mazingira (kipindi hicho wakiwa wachache) hivyo ilionekana kuwa, wangeendelea kuishi hapo huku wakibakia na utamaduni wao (mavazi, nyumba nk) ili kusiwe na mgogoro kati yao na wanyama/mazingira.

3. Tafasiri potofu inayo tolewa ni kuwa, Serikali inawafurusha/inawafukuza wamasai eneo lao la ngorongoro; wakati tafsiri sahihi ni kuwa, Serikali imeonesha nia ya kubadilisha matumizi ya eneo la ardhi ya Ngorongoro libakie kama mbuga ya wanyama kwa faida ya watanzania wote. Na hii imekuja kwa nia njema kwani wamasaai wameongezeka sana hivyo kuleta ukinzani kwa mazingira lakini pia maendeleo yanayo pelekea wamasai wabadilishe utamaduni wao kwa kujenga nyumba za kisasa, nk nk nk
Ikumbukwe kuwa; Serikali ingeweza kupitisha na kuanza utekelezaji wa zoezi la kuwahamisha mara moja ila badala yake, ikaona iendeshe zoezi hilo taratibu kwa maridhiano kitu ambacho, watu wenye nia ovu wamekuwa wakipotosha nia njema ya serikali.

Sijui kwanini ikifika kwa Wamasai ionekane kuwa ni tatizo na sio kwa Watanzania wengine wengi walio pisha/hamishwa maeneo yao nyakati tofauti tofauti kupisha miradi mbalimbali kwa faida ya watanzania wote?

Naona kama huu mgogoro unabebwa kwa mbeleko ila sijui ni kwa maslahi ya nani?

Mwisho japo sio kwa umuhimu; mimi sio mwanasheria ila huo ndio mtazamo wangu
 
Rais wa Tanganyika Law Society (TLS) Boniface Mwabukusi, amesema Waziri hana Mamlaka ya Kufuta Vijiji vya Ngorongoro

Ameyasema hayo leo 20/08/2024 Mkoani Dar Es Salaam alipokuwa anaongea na Waandishi wa habari. Amesema kama TLS wanaaangalia cha kufanya. "Wale wananchi wa Ngorongoro hawapaswi kupuuzwa, Warudishiwe huduma Muhimu pia Warudishiwe vituo cha kupigia Kura. Ni lazima tujue chanzo cha Tatizo Ngorongoro ni nini?". Amesema Mwabukusi

Mwabukusi amelipongeza Jeshi la Polisi kwa kuwakamta wabakaji na kuwafikisha Mahakamani. Amesema kuwafikisha mahaksmani ni hatua ya kwanza, ametaka Polisi imfikishe Mahakamani aliyewatuma pia. Pia amewata Polisi kumuachia na kumuweka wazi mwanamke alipata madhira ili haki yake ipatikane ikiwrmo kupewa msaada wa kisheria..

Stsy tuned

=====

20 Agosti, 2024

TAARIFA KWA UMMA

KUHUSU WITO WA WANANCHI WA NGORONGORO NA MAENEO MENGINE KUTAKA KUHESHIMIWA KWA HAKI ZAO

Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) kimepata taarifa kupitia mitandao ya kijamii kwa njia ya video iliyosambaa kwenye mitandao hiyo ikionyesha maandamano yaliyofanywa mnamo tarehe 18 mwezi Agosti, 2024 na mamia ya Wananchi wa Ngorongoro wakidai kuheshimiwa kwa haki zao. Katika maandamano yao miongoni mwa mambo mengine, Wananchi hao wamesikika wakilalamikia kuondolewa kwenye maeneo yao kinyume na utaratibu bila wao kuridhia pamoja na kuondolewa kwa huduma zote za kijamii kama vile shule, huduma za afya pamoja na maji. Kutokuwepo kwa huduma hizi muhimu kumepelekea Wananchi hao kuendelea kuishi katika mazingira magumu.

Tamko la Umoja wa Mataifa Juu ya Haki za Watu wa Asili la Mwaka 2007 limeeleza wazi katika ibara ya 10 kwamba watu wa asili hawataondolewa kwa nguvu kutoka kwenye ardhi au maeneo yao, uhamisho wowote wa watu wa asili hauwezi kufanyika bila idhini yao huru

Kwa mujibu wa ibara ya 24 (1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka 1977, kila mtu anayo haki ya kumiliki mali na haki ya hifadhi ya mali yake aliyonayo. Haki ya kumiliki mali ni moja ya haki ya msingi ya binadamu. Ibara 24 (2) imeeleza wazi kwamba mtu yoyote hatonyang’anywa mali yake isipokuwa kwa kuzingatia taratibu za kisheria ikiwepo ulipwaji wa fidia stahiki.

TLS inatoa rai kwa Serikali kuonyesha nia yake ya dhati kwa kurudisha huduma zote za kijamii kwa Wanachi wa Ngorongoro kwa kuwa ni haki yao. Pia, vituo vya kujiandikisha kwa ajili ya kupigia kura ambavyo Wanachi wa Ngorongoro wanalalamika kwamba havipo katika maeneo yao virudishwe ili wapate kuitumia haki yao ya kikatiba ya kujiandikisha na kuboresha taarifa zao kwa ajili ya uchaguzi wa Serikali za mitaa uliopangwa kufanyika mwezi Novemba mwaka 2024 pamoja na Uchaguzi mkuu utakaofanyika mwaka 2025.

Baraza la Uongozi la TLS limeona jambo hili la Ngorongoro na maeneo mengine linahitaji ufuatiliaji wa kina zaidi na kwa sababu hiyo, Baraza limeamua kuunda kamati maalum itakayofuatilia jambo hili kwa ukaribu ikiwa ni pamoja na kuwasiliana na Idara, Wizara na vyombo vyote vinavohusika na suala la Ngorongoro ili kujua ukweli zaidi na kuhakikisha misingi ya sheria za nchi yetu inafuatwa.

Kamati iliyoundwa inajumuisha wajumbe wafuatao:

*Dr. Rugemeleza Nshala
*Tike Mwambipile
*Bumi Mwaisaka
*Laetitia Petro Ntagazwa na
*Paul Kisabo.

Miongoni mwa mambo mengine kamati itafanya mambo yafuatayo:

*Kufanya mashauriano na taasisi mbalimbali pamoja na kutembelea baadhi ya maeneo yenye migogoro ili kujua uhalisia wa migogoro husika.

*Kufanya Mapitio ya Sera ,Sheria na Mazoea pamoja na kuzichambua kuhusiana na umiliki wa Ardhi kwa Wazawa pamoja na shughuli za uwekezaji na Uhifadhi na kubaini uzingativu wa Haki za Msingi za Raia katika maeneo husika kwa kuzingatia Katiba, Sera na Sheria za Nchi.

*Kuandaa kongamano (Symposium) la Kitaifa kuhusiana na namna bora ya kufanya maendeleo kwa kuzingatia na kulinda haki za Wazawa katika Ardhi zao za Asili pamoja na haki zao za Kijamii, Kiuchumi na Kiutamaduni katika maeneo yanayofikiwa na shughuli za uwekezaji.

*Kubaini mashauri au hatua zote ambazo zimechukuliwa na walalamikaji pamoja na walalamikiwa kisheria na kiutaratibu katika kuhakikisha uzingativu wa sheria na kubaini majina ya watu ambao kweli wameridhia kuondoka kwa hiyari kwenye maeneo yao na ambao hawakuridhia kuondoka kwa hiyari kwa sababu ya wao kuamua kubaki katika eneo lao la asili Ngorongoro.

*Kubaini na kulishauri Baraza la Uongozi la Chama Cha Mawakili wa Tanganyika juu ya hatua zakuchua ili kupata ufumbuzi wa kudumu kuhusu swala la migogoro ya Ardhi inayosababishwa na mipango ya uwekezaji au uhifadhi.

Kamati inatarajiwa kumaliza kazi tajwa ndani ya muda wa kipindi cha siku 30.

TLS inawaomba Wanachama, Wananchi pamoja na wadau mbalimbali wa Sheria kutoa ushirikiano kwa Kamati maalum iliyoundwa ili TLS kwa mamlaka iliyopewa chini ya kifungu cha 4 cha Sheria iliyounda TLS (Tanganyika Law Society Act Cap. 307) iweze kutimiza wajibu wake wa kuishauri Serikali na Kulinda haki za Wananchi kwa lengo la kupata suluhisho la kudumu.

Imetolewa na Baraza la Uongozi la Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS)

Boniface A.K Mwabukusi

Rais
Hizi ndio spana tulitaka

Sio blah blah za Sungusia limwana CCM
 
KUENDELEA KUKAA NA KUHARIBU UHAI WA HIFADHI HAIKUBALIKI,WAMASAI WALIO WENGI WAMEONDOKA KWA HIYARI YAO NA KWENDA MSOMERA,SASA HAO MNAOWAPIGIA KIFUA WAENDELEE KUBAKIA HAPO NI WA KUWAINGIZA KWENYE SHIDA TUH.
Tumia herufi ndogo ndogo tu mkuu utaeleweka!

Ila ujue kwamba Maalimu! Kuna mambo yatupasa tuungane ili kuwashinikiza viongozi wetu kuyaangalua upya kwa msatakabali wetu sote, yaani wao na wananchi kwa ujumla

Nadhani hakuna kosa kwenye hili Ostaz Juma au siyo?
 
Utafiti upo na huo ndiyo umwetumika kuwapunguza. Nakupa official report ya Kamishna wa Uhifadhi hapa:

"Wakati Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro inaanzishwa mwaka 1959 ilikuwa na idadi ya watu wasiozidi 8,000 na mifugo isiyozidi 261,000, idadi hii ya watu kwa wakati huo ilionekana kuwa ndogo lakini iliendelea kuongezeka hadi kufikia kaya 23,889 zenye watu zaidi 100,000 na mifugo zaidi ya 850,000 (taarifa hizi ni kwa mujibu wa sensa ya mwaka 2022).

Ongezeko hili la watu na mifugo limekuwa changamoto kwa zaidi ya
miaka sitini toka kuanzishwa kwa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro kutokana na muingiliano wa shughuli za uhifadhi, utalii na maendeleo ya jamii ya watu wanaoishi ndani ya hifadhi, ili kuinusuru mamlaka ya hifadhi ya Ngorongoro.

Serikali baada ya kupitia tafiti mbalimbali zilizofanywa na watafiti mbalimbali zote zikihusu matumizi mseto ya ardhi ya eneo la hifadhi ya ngorongoro na athari zake kwa ustawi wa mamlaka pamoja na jamii ya wananchi wanaoishi ndani ya
hifadhi serikali ya awamu ya sita ilichukua uamuzi wa busara wa kuwaelimisha wananchi wanaoishi ndani ya hifadhi ya Ngorongoro kuhama wao wenyewe kwa hiari kwenda maeneo mengine yaliyotengwa na serikali pamoja na sehemu nyingine wanazochagua wao wenyewe kwa ajili ya kupisha uhifadhi pamoja na kuboresha maisha yao, maeneo mahususi yaliyotengwa na serikali kwa ajili ya wananchi kuhamia ni pamoja na kijiji cha Msomera kilichopo katika wilaya ya Handeni, Saunyi wilaya ya Kilindi na Kitwai B wilaya ya Simanjiro."

(Richard Kiiza, Kamishina wa Uhifadhi wa Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro)
✅✅✅ HAKUNA HOJA YOYOTE ITAKAYOISHINDA HOJA YA UHIFADHI WA ENEO LA UHIFADHI WA URITHI WA KIDUNIA, NI LAZIMA WATU WAPUNGUZWE KWA LAZIMA KUNUSURU UHIFADHI, ARE THEY TREATED BAD #NO, JE KATIKA UHAMISHWAJI WAO UTU UNAZINGATIWA? #YES!
 
TLS-Ni tawi la chadema au ni kitu Gani?, tulitaraji TLS kingekuwa ni chombo cha kisheria chenye mfumo wa kitaifa tofauti kabisa imepoteza weledi wake na ni vyema IKAFUTWA KABISA, aidha ikaundwa upya chini ya kanuni maalumu, zisizotoka nje ya misingi yake ya kisheria,ingependeza kikawa ni chombo ambacho kinahoji kabla ya kudandia hoja ambazo zingine zina nia njema, kwa taifa hili.
 
Utafiti upo na huo ndiyo umwetumika kuwapunguza. Nakupa official report ya Kamishna wa Uhifadhi hapa:

"Wakati Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro inaanzishwa mwaka 1959 ilikuwa na idadi ya watu wasiozidi 8,000 na mifugo isiyozidi 261,000, idadi hii ya watu kwa wakati huo ilionekana kuwa ndogo lakini iliendelea kuongezeka hadi kufikia kaya 23,889 zenye watu zaidi 100,000 na mifugo zaidi ya 850,000 (taarifa hizi ni kwa mujibu wa sensa ya mwaka 2022).

Ongezeko hili la watu na mifugo limekuwa changamoto kwa zaidi ya
miaka sitini toka kuanzishwa kwa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro kutokana na muingiliano wa shughuli za uhifadhi, utalii na maendeleo ya jamii ya watu wanaoishi ndani ya hifadhi, ili kuinusuru mamlaka ya hifadhi ya Ngorongoro.

Serikali baada ya kupitia tafiti mbalimbali zilizofanywa na watafiti mbalimbali zote zikihusu matumizi mseto ya ardhi ya eneo la hifadhi ya ngorongoro na athari zake kwa ustawi wa mamlaka pamoja na jamii ya wananchi wanaoishi ndani ya
hifadhi serikali ya awamu ya sita ilichukua uamuzi wa busara wa kuwaelimisha wananchi wanaoishi ndani ya hifadhi ya Ngorongoro kuhama wao wenyewe kwa hiari kwenda maeneo mengine yaliyotengwa na serikali pamoja na sehemu nyingine wanazochagua wao wenyewe kwa ajili ya kupisha uhifadhi pamoja na kuboresha maisha yao, maeneo mahususi yaliyotengwa na serikali kwa ajili ya wananchi kuhamia ni pamoja na kijiji cha Msomera kilichopo katika wilaya ya Handeni, Saunyi wilaya ya Kilindi na Kitwai B wilaya ya Simanjiro."

(Richard Kiiza, Kamishina wa Uhifadhi wa Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro)
Sasa si unaon report kama hii imekaa kimchongo sana.

Hapa inaongelea ongezeko la watu ambalo ni very slow and trivial for span of 60yrs.

Bado report hii haioneshi athari za kimazingira zimekuwaje
 
TLS-Ni tawi la chadema au ni kitu Gani ni, tulitaraji TLS kingekuwa ni chombo cha kisheria chenye mfumo wa kitaifa tofauti kabisa imepoteza weledi wake na ni vyema IKAFUTWA KABISA, aidha ikaundwa upya chini ya kanuni maalumu, zisizotoka nje ya misingi yake ya kisheria,ingependeza kikawa ni chombo ambacho kinahoji kabla ya kudandia hoja ambazo zingine zina nia njema, kwa taifa hili.
Haters ambao hamjui hata majukum ya kisheria ya TLS. Mnajali mkono kinywani tu......Hand To Mouth😆😆😆
 
✅✅✅ HAKUNA HOJA YOYOTE ITAKAYOISHINDA HOJA YA UHIFADHI WA ENEO LA UHIFADHI WA URITHI WA KIDUNIA, NI LAZIMA WATU WAPUNGUZWE KWA LAZIMA KUNUSURU UHIFADHI, ARE THEY TREATED BAD #NO, JE KATIKA UHAMISHWAJI WAO UTU UNAZINGATIWA? #YES!
Hao NEMC washawapiga stop msifukuze vinadamu.
 
Mimi nina mtazamo tofauti na hawa wanasheria wetu kuhusiana na huu mgogoro....
1. Ikumbwe kuwa maeneo karibia yote yenye wanyama (National Parks, kuna kipindi huko nyuma kuna baadhi ya watu hata vijiji walilazimika kuhamishwa na kupewa maeneo mbadala ili kuyapisha yabaki kama hifadhi ya wanyama kwa faida ya watanzania wote.

2. Ninavyokumbuka kwenye historia, Wamasai waliachwa Ngorongoro kwa sababu tu walionekana hawakuwa na madhara kwa wanyama na mazingira (kipindi hicho wakiwa wachache) hivyo ilionekana kuwa, wangeendelea kuishi hapo huku wakibakia na utamaduni wao (mavazi, nyumba nk) ili kusiwe na mgogoro kati yao na wanyama/mazingira.

3. Tafasiri potofu inayo tolewa ni kuwa, Serikali inawafurusha/inawafukuza wamasai eneo lao la ngorongoro; wakati tafsiri sahihi ni kuwa, Serikali imeonesha nia ya kubadilisha matumizi ya eneo la ardhi ya Ngorongoro libakie kama mbuga ya wanyama kwa faida ya watanzania wote. Na hii imekuja kwa nia njema kwani wamasaai wameongezeka sana hivyo kuleta ukinzani kwa mazingira lakini pia maendeleo yanayo pelekea wamasai wabadilishe utamaduni wao kwa kujenga nyumba za kisasa, nk nk nk
Ikumbukwe kuwa; Serikali ingeweza kupitisha na kuanza utekelezaji wa zoezi la kuwahamisha mara moja ila badala yake, ikaona iendeshe zoezi hilo taratibu kwa maridhiano kitu ambacho, watu wenye nia ovu wamekuwa wakipotosha nia njema ya serikali.
Sijui kwanini ikifika kwa Wamasai ionekane kuwa ni tatizo na sio kwa Watanzania wengine wengi walio pisha/hamishwa maeneo yao nyakati tofauti tofauti kupisha miradi mbalimbali kwa faida ya watanzania wote?

Naona kama huu mgogoro unabebwa kwa mbeleko ila sijui ni kwa maslahi ya nani?

Mwisho japo sio kwa umuhimu; mimi sio mwanasheria ila huo ndio mtazamo wangu
Shida unatoa Chadema unaweka ccm

😆😆😆
 
KUENDELEA KUKAA NA KUHARIBU UHAI WA HIFADHI HAIKUBALIKI,WAMASAI WALIO WENGI WAMEONDOKA KWA HIYARI YAO NA KWENDA MSOMERA,SASA HAO MNAOWAPIGIA KIFUA WAENDELEE KUBAKIA HAPO NI WA KUWAINGIZA KWENYE SHIDA TUH.
Usiwe mwepesi wa kuonesha ujinga wako, tena kwa watu wenye uelewa.

Wamasai waliohamishiwa Tanga ni 8,000. Wamasai ndani ya Ngorongoro ni 120,000. Haya kwa hesabu inayohitaji akili ndogo kabisa, watu 120,000 ukitoa watu 8,000, wanabakia wangapi?
Kwa uwezo wako mdogo, unaona hao 8,000 ni wengi kuliko 120,000 - 8,000?
Kwa nini siku hizi idadi ya wajinga JF inazidi kuongezeka kwa kasi?
 
TLS-Ni tawi la chadema au ni kitu Gani ni, tulitaraji TLS kingekuwa ni chombo cha kisheria chenye mfumo wa kitaifa tofauti kabisa imepoteza weledi wake na ni vyema IKAFUTWA KABISA, aidha ikaundwa upya chini ya kanuni maalumu, zisizotoka nje ya misingi yake ya kisheria,ingependeza kikawa ni chombo ambacho kinahoji kabla ya kudandia hoja ambazo zingine zina nia njema, kwa taifa hili.
TLS haiwezi kufutika, utafutika wewe kwa kukosa uwezo wa akili. Viumbe wasio na akili huwa wanajifuta wenyewe.
 
MAHOTELI YANAHARIBU VIPI MAZINGIRA??HAO WAFUGAJI WAMEKUWA WENGI NA MIFUGO YAO KILA SIKU INAZIDI KUKUA,MALISHO YA MIFUGO YAO NI HAPO HAPO MBUGANI,SHUGHULI ZAO ZA KIBINADAMU KAMA KUKATA KUNI,MITI NA KUCHOMA MOTO MISITU NI HAPO HAPO MBUGANI,SASA UNATAKA WAACHWE HAPO HADI LINI??NA SISI TUNATEGEMEA SERENGETI NA NGORO NGORO KUTUINGIZIA FEDHA ZA KIGENI KWA UTALII??

KWANINI LAKINI CHADEMA HAMTUMII AKILI MAFALA NYINYI??
Imebidi nicheke tu' 😂 😂 😂 kwahiyo brother hao twiga na swala hawazaliani? Na kama wanazaliana wanakula wapi? Vipi mnawapelekeaga chakula kwenye parcel?

Hopeless
 
Kwa kweli tumshukuru Mungu. Kila wakati yanapokuwepo maharamia, huwainua watetezi.

Shetani ameleta majuha ya kuwapora wananchi rasilimali zao, lakini Mungu amewainua watetezi.

Tunamwomba Mungu uzidi kumlinda, kumjalia hekima, na kumpa ushindi Mwambukusi na timu yake dhidi ya maharamia wasiojali maisha ya binadamu wengine.
 
Imebidi nicheke tu' 😂 😂 😂 kwahiyo brother hao twiga na swala hawazaliani? Na kama wanazaliana wanakula wapi? Vipi mnawapelekeaga chakula kwenye parcel?

Hopeless
THATS WHY NASEMA CHADEMA WANAWATUMIA MBUMBUMBU KAMA WAFUASI WAO UCHWARA KUTUPIGIA KELELE MITANDAONI HUMU.

TWIGA.SWALA WAKIZALIANA WANAATHIRI VIPI SHUGHULI ZA UFIHADHI??INFACT SISI TUNATAKA HAO WAMASAI WATOKE HUKO MBUGANI ILI HAO TWIGA NA SWALA WAZALIANE KWA WINGI HATA VIZAZI VIJAVYO WAJE KUNUFAIKA KAMA TUNAVYONUFAIKA SISI.

BINADAMU KWAKE SIYO MBUGANI,HAO WATAKE WASITAKE WATATOKA HUKO.
 
KUENDELEA KUKAA NA KUHARIBU UHAI WA HIFADHI HAIKUBALIKI,WAMASAI WALIO WENGI WAMEONDOKA KWA HIYARI YAO NA KWENDA MSOMERA,SASA HAO MNAOWAPIGIA KIFUA WAENDELEE KUBAKIA HAPO NI WA KUWAINGIZA KWENYE SHIDA TUH.
Kacheze mieleka mkuu
 
Mimi nina mtazamo tofauti na hawa wanasheria wetu kuhusiana na huu mgogoro....
1. Ikumbwe kuwa maeneo karibia yote yenye wanyama (National Parks, kuna kipindi huko nyuma kuna baadhi ya watu hata vijiji walilazimika kuhamishwa na kupewa maeneo mbadala ili kuyapisha yabaki kama hifadhi ya wanyama kwa faida ya watanzania wote.

2. Ninavyokumbuka kwenye historia, Wamasai waliachwa Ngorongoro kwa sababu tu walionekana hawakuwa na madhara kwa wanyama na mazingira (kipindi hicho wakiwa wachache) hivyo ilionekana kuwa, wangeendelea kuishi hapo huku wakibakia na utamaduni wao (mavazi, nyumba nk) ili kusiwe na mgogoro kati yao na wanyama/mazingira.

3. Tafasiri potofu inayo tolewa ni kuwa, Serikali inawafurusha/inawafukuza wamasai eneo lao la ngorongoro; wakati tafsiri sahihi ni kuwa, Serikali imeonesha nia ya kubadilisha matumizi ya eneo la ardhi ya Ngorongoro libakie kama mbuga ya wanyama kwa faida ya watanzania wote. Na hii imekuja kwa nia njema kwani wamasaai wameongezeka sana hivyo kuleta ukinzani kwa mazingira lakini pia maendeleo yanayo pelekea wamasai wabadilishe utamaduni wao kwa kujenga nyumba za kisasa, nk nk nk
Ikumbukwe kuwa; Serikali ingeweza kupitisha na kuanza utekelezaji wa zoezi la kuwahamisha mara moja ila badala yake, ikaona iendeshe zoezi hilo taratibu kwa maridhiano kitu ambacho, watu wenye nia ovu wamekuwa wakipotosha nia njema ya serikali.

Sijui kwanini ikifika kwa Wamasai ionekane kuwa ni tatizo na sio kwa Watanzania wengine wengi walio pisha/hamishwa maeneo yao nyakati tofauti tofauti kupisha miradi mbalimbali kwa faida ya watanzania wote?

Naona kama huu mgogoro unabebwa kwa mbeleko ila sijui ni kwa maslahi ya nani?

Mwisho japo sio kwa umuhimu; mimi sio mwanasheria ila huo ndio mtazamo wangu
Kwanza inaonekana huna uelewa wa mambo haya. Ni uwongo mkubwa kudai kuwa hata mbuga nyingine za wanyama, kuna wakazi asilia waliohamishwa. Huo ni uwongo mkubwa.

Unatakiwa kwanza ufahamu jinsi hizi mbuga za wanyama na hifadhi za misitu zilivyokuwa zinapatikana. Maeneo mengi ambayo kulikuwa na wanyama wengi, wakiwemo wanyama wakali, watu walikuwa wakiyakimbia maeneo hayo. Hawakuwa wanaweka makazi. Hivyo kwa nyakati mbalimbali, Serikali ilikuwa inaweka mipaka ya hifadhi, siyo kuwahamisha wananchi ili maeneo yao yabadilike kuwa hifadhi. Kuna wakati wanadamu walikuwa wakiongezeka na kuonekana maeneo yao ya makazi na shughuli zao za kiuchumi, hayatoshi, serikali ilikuwa inabadilisha mipaka ya hifadhi kwa kupunguza eneo la hifadhi. Mara chache sana mipaka ya hifadhi ilikuwa inaongezwa kwa kumega maeneo ya vijiji na kuyaingiza kwenye hifadhi, na sababu kubwa ilikuwa kutengeneza buffer zone ili wanyama wasiuawe kiurahisi na wanadamu. Na maeneo mengi ya vijiji yaliyomegwa na kuunganishwa na hifadhi, wakati wa utawala wa Magufuri, yalirudishwa kwa wanavijiji.

Jielemishe uelewe utofauti wa kufuta makazi ya wananchi na kubadilisha mipaka. Na huko nyuma, hakujawahi kutokea eneo lolote la hifadhi eti wananchi walihamishwa toka eneo la asili na kwenda kutupwa wilaya nyingine. Leo uongozi huu wa kiharamia unawaondoa kwa nguvu wananchi kwenye maeneo yao ya asili, kuwavusha mkoa mmoja na kwenda kuwatupa mbali kabisa mkoa mwingine kwa manufaa ya mwarabu ambaye hataki wamasai wawepo eneo hilo.

Lazima wananchi wenye upendo wa kweli kwa Taifa letuna watu wake, tusimame na wamasai kuhakikisha watawala hawafanyi uharamia dhidi ya Taifa, tena kwakuwafurahisha wageni.
 
Back
Top Bottom