CHIBURABANU
JF-Expert Member
- Sep 19, 2013
- 2,921
- 3,474
Sana tu.Kenya wanajitahidi kwa kiasi fulani
Hizi shule zilizoongezekaga zimesaididia sana.enzi zetu ilikuwaga arusha sec tu.Mwaka gani hiyo mkuu?me 2003 ndiyo nimeanza form 1 hapo arusha secondary school nikitokea Naura primary school.Enzi hizo Arusha kuna shule tano tu za secondary ambazo ni Arusha sec,Arusha day,Kaloleni,Sinoni na Ilboru(hii ilikuwa ya vipaji maalumu)
Mwaka gani hiyo mkuu?Hizi shule zilizoongezekaga zimesaididia sana.enzi zetu ilikuwaga arusha sec tu.
Irliboru ilikuwaga ya wenye vipaji zaidi.
1984Mwaka gani hiyo mkuu?
Kweli kabisa. Sisi kijiji kizima kilikuwa kinafahamuHabari za wakati huu kaka na dada zangu wote wa hapa jamiiforums.
Ndugu zangu watanzania;
Mwaka 1999 kurudi nyuma ilikuwa ngumu sana kuchaguliwa shule ya secondary ya serikali. Wachache waliobahatika walijulikana kata/tarafa nzima. Je, wewe ni mmoja wao?
TABORA BOYS SECONDARY SCHOOL
View attachment 1661676
Juzi kuna mtoto wa jirani yangu alinifuata akaniambia brother ninaomba uniangalizie matokeo yangu ya darasa la saba. Mimi bila hiyana na smartphone yangu hii nikaingia katika website ya necta nikamuangalizia fresh tu. Dogo bwana alipata C flat masomo yoooote.
Nikajua ndio basi tena. Baada ya selection ya shule kutoka nikasikia huyu dogo amepangiwa shule moja ya kata mwendo kama wa dakika 20 kutoka hapa tunapokaa, ndio nikajisemea kimoyomoyo hakika dunia imebadilika kwa kasi sana.
Yaaani mtu anapata C flat bado anaenda secondary? Ninakumbuka dada yangu aliyeniachia ziwa, sasa hivi ni engineer, yeye ni moja kati ya wanafunzi 4 waliofaulu kwenda secondary shule ya serikali. Kumbuka enzi hizo kuchaguliwa tulikuwa tunaita kufaulu.
Yaaani wewe ukichaguliwa unaonekana umefaulu na wale ambao hawakuchaguliwa wanaonekana wamefeli ingawa kiuhalisia hawakuwa wamefeli ila shule zilikuwa ni chache mnoooo kiasi kwamba ni ngumu ku-accomodate wanafunzi wooote waliofaulu.
View attachment 1661678
Dada yangu alifaulu wakati huo baba anafanya kazi Wilaya ya ******* Mkoa wa Mbeya. Watu walifurahi familia nzima, lilipikwa pilau kana kwamba kuna sherehe ya kipaimara. Ndugu waliokuwa wanaishi karibu walikuja kumpa pongezi dada utadhani labda amejifungua mtoto.
Dada alikuwa maarufu sana kwa maana akiwa anaenda shuleni basi ni yeye tu ndiye aliyekua anaonekana asubuhi amevaa sare wakati huo wenzake aliomaliza nao darasa la saba bado wamelala au wameenda shambani.
Mgeni aliyekuwa hapafahamu nyumbani akiwa anaulizia kwa mama fulani wenyeji wanaanza kudadisi kwa kuambiana "au yule mama mjaluo ambaye mwanae anasoma secondary". Kwenda secodary ya serikali ilikuwa ni umaarufu kama dereva kwa maana enzi zile hakuna gari ya automatic transmission.
Gari zote ni manual na anayeweza kuendesha ni mzee mmoja au wawili tu mtaa mzima. Wanafunzi wa secondary walikuwa maarufu kama madereva kutokana na uchache wao.
View attachment 1661682
Matokeo yalikuwa yanasubiriwa kwa hamu na shauku kubwa sana kwa maana matokeo na selection zilikuwa zinakuja kwa pamoja tofauti na sasa hivi ambapo matokeo yanaanza kutoka na mwanafunzi au mzazi wake anaingia katika internet kisha baada ya mwezi mmoja mbele ndio selection inatangazwa.
Je, wewe ni mmoja ya wanafunzi wachache waliobahatika miaka ya 1990?
USISAHAU: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.
Duh..hata sijafikiriwa kuzaliwa.1984
Sasa hivi C mbili na D moja unaingia advance
Tena unaweza kuta C za civics na nutrition, D ya Bible/Islamic knowledge
Chuo E mbili
Akitoka hapo hataki kazi za bodaboda, eti anataka kazi za hadhi yake, hivi wana hadhi gani hawa mbwa!!!!
Jamaa anapaswa kuomba radhikupata vi A na B flats ushaita binadamu wenzako mbwa, ungepata hata nusu ya utajiri wa bakhresa ambaye hata principle za business pengine hata hazijui. Si ndo ungejiona hustahili kutumia oxygen ya bure kama maskini wa tandale
Shule gani?Nimeiona moja kati ya shule nlizosoma kati ya hizo picha!!
Safi Sana, naona ulikuwa njema sana Boss, hongera zakoEnzi zetu kwa Dar shule zilikuwa nne tu basi yaani Pugu,Minaki,Tambaza,Azania hakukuwapo na Benjamini Mkapa.
Mtoto wa kiume unatakiwa ukaze ili uende angalau hata Aza Boy.
Ila binafsi nilichaguliwa Ilboru kata nzima nilikuwa mwenyewe ila DsM nzima tulikuwa watatu tu.
Advance tukatupwa mzumbe pale kwa DsM tulikuwa wa tano mkoa mzima.
Safi Sana kaka, Hongera zakoDuuh
Ngoja na mie nitie langu;
Miaka ya 80's mwishoni...
Nilisoma shule kwa ndugu mkoa ulio mbali na nyumbani. Baada ya mitihani ya darasa la saba nikarudi nyumbani!
Ilipofika January mwanzoni Baba aliletewa simu ya maandishi(ama simu ya barua) sikumbuku vizuri. Simu yenyewe ililetwa na jirani aliekuwa anamiliki sanduku la Posta!
Iliandikwa hivi;-
(........) AMEFAULU KWENDA SEKONDARI SHULE YA ....AJE MAPEMA KUWAHI MASOMO.
(.........)
Baada ya hapo nakumbuka sikulala kabisa hadi siku ya safari.
Darasani tulikuwa 97 tukawa tumefaulu wanne tu...!!
Shkamoo Bamdogo1984
Juzi kuna. Denti nimeonana nae ni mtoto wa jirani yangu nikamuuliza kuhusu matokeo akanijibu wamefauli darasa zima kasoro mmoja nikasema kazi ipoMnaweza kumaliza miaka mitano shule haijafaulisha zamani ilikuwa ni jambo la kawaida.
Hahahahaaaa, eti ba'mdogo. Best siku hizi JF ninaiheshimu sana. Kuna uzi wangu wa asili ya muziki wa Zaire kuna member mule kaniambia alisoma secondary miaka ya 1970s wakati mimi nilikuwa ninamchukulia poa tuShkamoo Bamdogo
Pole sana. Akili ulikuwa nazo sema shule sasa ndio chache. Inaonekana dada alikuwa maarufu sana hapo mtaani?acha kabisa.nakumbuka tokeo limetoka sister kafaulu kachaguliwa jangawan mim nimefeli.na ukicheki hapo kirecords nilikua nakimbiza darasa zima sema ndio hivo.yan unastresika.home wote wanakuona huna akili.
Hii nchi imetoka mbali sana bestJuzi kuna. Denti nimeonana nae ni mtoto wa jirani yangu nikamuuliza kuhusu matokeo akanijibu wamefauli darasa zima kasoro mmoja nikasema kazi ipo