Infantry Soldier
JF-Expert Member
- Feb 18, 2012
- 15,892
- 16,476
- Thread starter
- #101
Hahahahaaaa aisee hii kali sasa mkuuMnaweza kumaliza miaka mitano shule haijafaulisha zamani ilikuwa ni jambo la kawaida.
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Hahahahaaaa aisee hii kali sasa mkuuMnaweza kumaliza miaka mitano shule haijafaulisha zamani ilikuwa ni jambo la kawaida.
Maharaba mwananguShkamoo Bamdogo
Kuna members ni wakongwe sana humuS
Safi Sana kaka, Hongera zako
Hiyo inaitwa gombania goli (Survival of the fittest)Safi Sana, naona ulikuwa njema sana Boss, hongera zako
Unakuta sanduku la posta hilo moja linatumiwa na watu kibao mpaka ndugu yake na rafiki yako wa kazini...Duuh
Ngoja na mie nitie langu;
Miaka ya 80's mwishoni...
Nilisoma shule kwa ndugu mkoa ulio mbali na nyumbani. Baada ya mitihani ya darasa la saba nikarudi nyumbani!
Ilipofika January mwanzoni Baba aliletewa simu ya maandishi(ama simu ya barua) sikumbuku vizuri. Simu yenyewe ililetwa na jirani aliekuwa anamiliki sanduku la Posta!
Mzee baba, humu kuna watu ni babu zetu ujue?Duh..hata sijafikiriwa kuzaliwa.
Walifaulu wanafunzi wangapi mwaka huo? Mmoja?Kweli kabisa. Sisi kijiji kizima kilikuwa kinafahamu
Sawa uncle1984
Vipaji Maalum. Unakuta katika marks 150 mtu kapiga 145Hizi shule zilizoongezekaga zimesaididia sana.enzi zetu ilikuwaga arusha sec tu.
Irliboru ilikuwaga ya wenye vipaji zaidi.
Bila ile vita bila shaka tungekuwa mbali sana zaidi ya hapaSana tu.
Daaah, zamani sana mkuu...Enzi zetu kwa Dar shule zilikuwa nne tu basi yaani Pugu,Minaki,Tambaza,Azania hakukuwapo na Benjamini Mkapa.
Mtoto wa kiume unatakiwa ukaze ili uende angalau hata Aza Boy.
97 - 4 = 93 hawa wote chaaaali, doooh Tanzania yetu imetoka mbali sana mkuuDuuh
Ngoja na mie nitie langu;
Miaka ya 80's mwishoni...
Nilisoma shule kwa ndugu mkoa ulio mbali na nyumbani. Baada ya mitihani ya darasa la saba nikarudi nyumbani!
Ilipofika January mwanzoni Baba aliletewa simu ya maandishi(ama simu ya barua) sikumbuku vizuri. Simu yenyewe ililetwa na jirani aliekuwa anamiliki sanduku la Posta!
Iliandikwa hivi;-
(........) AMEFAULU KWENDA SEKONDARI SHULE YA ....AJE MAPEMA KUWAHI MASOMO.
(.........)
Baada ya hapo nakumbuka sikulala kabisa hadi siku ya safari.
Darasani tulikuwa 97 tukawa tumefaulu wanne tu...!!
Duh, mwambie mama watoto wako anamsalimiaHahahahaaaa, eti ba'mdogo. Best siku hizi JF ninaiheshimu sana. Kuna uzi wangu wa asili ya muziki wa Zaire kuna member mule kaniambia alisoma secondary miaka ya 1970s wakati mimi nilikuwa ninamchukulia poa tu
Usiku mwema ba'mdogoMaharaba mwanangu
Mwaka gani uliingia hapo.Mimi niilingia hapo 1972 kila mkoa ulikuwa unatoa wanafunzi 10Aisee mimi ni mmojawapo... Na tulikuwa tunatoka sita tu mkoa mzima kwenda IFUNDA TECH kila mwaka... Nilijulikana ile mbaya yaani
Habari za wakati huu kaka na dada zangu wote wa hapa JamiiForums.
Ndugu zangu watanzania;
Mwaka 1999 kurudi nyuma ilikuwa ngumu sana kuchaguliwa shule ya secondary ya serikali. Wachache waliobahatika walijulikana kata/tarafa nzima. Je, wewe ni mmoja wao?
TABORA BOYS SECONDARY SCHOOL
View attachment 1661676
Juzi kuna mtoto wa jirani yangu alinifuata akaniambia brother ninaomba uniangalizie matokeo yangu ya darasa la saba. Mimi bila hiyana na smartphone yangu hii nikaingia katika website ya necta nikamuangalizia fresh tu. Dogo bwana alipata C flat masomo yoooote.
Nikajua ndio basi tena. Baada ya selection ya shule kutoka nikasikia huyu dogo amepangiwa shule moja ya kata mwendo kama wa dakika 20 kutoka hapa tunapokaa, ndio nikajisemea kimoyomoyo hakika dunia imebadilika kwa kasi sana.
Yaaani mtu anapata C flat bado anaenda secondary? Ninakumbuka dada yangu aliyeniachia ziwa, sasa hivi ni engineer, yeye ni moja kati ya wanafunzi 4 waliofaulu kwenda secondary shule ya serikali. Kumbuka enzi hizo kuchaguliwa tulikuwa tunaita kufaulu.
Yaaani wewe ukichaguliwa unaonekana umefaulu na wale ambao hawakuchaguliwa wanaonekana wamefeli ingawa kiuhalisia hawakuwa wamefeli ila shule zilikuwa ni chache mnoooo kiasi kwamba ni ngumu ku-accomodate wanafunzi wooote waliofaulu.
View attachment 1661678
Dada yangu alifaulu wakati huo baba anafanya kazi Wilaya ya ******* Mkoa wa Mbeya. Watu walifurahi familia nzima, lilipikwa pilau kana kwamba kuna sherehe ya kipaimara. Ndugu waliokuwa wanaishi karibu walikuja kumpa pongezi dada utadhani labda amejifungua mtoto.
Dada alikuwa maarufu sana kwa maana akiwa anaenda shuleni basi ni yeye tu ndiye aliyekua anaonekana asubuhi amevaa sare wakati huo wenzake aliomaliza nao darasa la saba bado wamelala au wameenda shambani.
Mgeni aliyekuwa hapafahamu nyumbani akiwa anaulizia kwa mama fulani wenyeji wanaanza kudadisi kwa kuambiana "au yule mama mjaluo ambaye mwanae anasoma secondary". Kwenda secodary ya serikali ilikuwa ni umaarufu kama dereva kwa maana enzi zile hakuna gari ya automatic transmission.
Gari zote ni manual na anayeweza kuendesha ni mzee mmoja au wawili tu mtaa mzima. Wanafunzi wa secondary walikuwa maarufu kama madereva kutokana na uchache wao.
View attachment 1661682
Matokeo yalikuwa yanasubiriwa kwa hamu na shauku kubwa sana kwa maana matokeo na selection zilikuwa zinakuja kwa pamoja tofauti na sasa hivi ambapo matokeo yanaanza kutoka na mwanafunzi au mzazi wake anaingia katika internet kisha baada ya mwezi mmoja mbele ndio selection inatangazwa.
Je, wewe ni mmoja ya wanafunzi wachache waliobahatika miaka ya 1990?
USISAHAU: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.
WAHENGA TU: Kuna mzee mmoja alisoma secondary miaka ya 1970s. Yeye binafsi aliwahi kuniambia kwamba enzi hizo waliokuwa wanasoma shule za secondary za serikali walikuwa wanaheshimika sana ukilinganisha na wale waliokuwa wanasoma shule za secondary za binafsi tofauti na hivi sasa ambapo wanafunzi wa private ndio wanaheshimika.
Je, kauli hii ina ukweli wowote ndani yake?