Mwaka 1999 kurudi nyuma ilikuwa ngumu sana kuchaguliwa shule ya Sekondari ya Serikali. Waliobahatika walijulikana kata nzima. Je, wewe ni mmoja wao?

Mwaka 1999 kurudi nyuma ilikuwa ngumu sana kuchaguliwa shule ya Sekondari ya Serikali. Waliobahatika walijulikana kata nzima. Je, wewe ni mmoja wao?

Duh! Hicho kilikuwa kipindi kigumu sana (1990 kwenda nyuma). Nadhani hapo ilikuwa baada ya miaka 18 ya kufunga mkanda. Shuleni kwetu tulifaulu watoto 3 tu kati ya wanafunzi takribani 300 wa darasa la 7. Wawili kati yao, walikuwa watoto wa walimu.
 
Sisi tulifaulu watatu tu,mimi nikiwa nimewaongoza wenzangu kwa wingi wa alama nilizopata.Na pia nilikuwa mwanafunzi bora na jina langu mpaka leo lipo kwenye ubao maalumu wa majina ya wanafunzi bora kwenye ofisi ya Mwalimu mkuu.Hakika kufaulu ilikuwa ni fahari sana enzi zetu
 
Duuh
Ngoja na mie nitie langu;

Miaka ya 80's mwishoni...
Nilisoma shule kwa ndugu mkoa ulio mbali na nyumbani. Baada ya mitihani ya darasa la saba nikarudi nyumbani!

Ilipofika January mwanzoni Baba aliletewa simu ya maandishi(ama simu ya barua) sikumbuku vizuri. Simu yenyewe ililetwa na jirani aliekuwa anamiliki sanduku la Posta!
Unakuta sanduku la posta hilo moja linatumiwa na watu kibao mpaka ndugu yake na rafiki yako wa kazini...
 
Duuh
Ngoja na mie nitie langu;

Miaka ya 80's mwishoni...
Nilisoma shule kwa ndugu mkoa ulio mbali na nyumbani. Baada ya mitihani ya darasa la saba nikarudi nyumbani!

Ilipofika January mwanzoni Baba aliletewa simu ya maandishi(ama simu ya barua) sikumbuku vizuri. Simu yenyewe ililetwa na jirani aliekuwa anamiliki sanduku la Posta!

Iliandikwa hivi;-
(........) AMEFAULU KWENDA SEKONDARI SHULE YA ....AJE MAPEMA KUWAHI MASOMO.
(.........)

Baada ya hapo nakumbuka sikulala kabisa hadi siku ya safari.
Darasani tulikuwa 97 tukawa tumefaulu wanne tu...!!
97 - 4 = 93 hawa wote chaaaali, doooh Tanzania yetu imetoka mbali sana mkuu
 
Kinachonifanya nipandwe na hasira ni kwamba

1.waliopata division 1 , 2 na 3 woote kwa sasa wanakuwa treated kama watu sawawaliofaulu na woote wanapangiwa shule .

2.wanaosoma vipaji maalum na wale wasiosoma vipaji maalum woote wanakuwa treated sawa means watapata mikopo woote na watakutana chuo kimoja.

3.kwa vyuoni hakuna tofauti kati ya aliyepata first class na upper second maana woote hao wanakuwa treated sawa mfano kuapply scholarship wanachukua kuanzia upper second kwenda juu.

Tanzania elimu imekufa .
 
Hahahahaaaa, eti ba'mdogo. Best siku hizi JF ninaiheshimu sana. Kuna uzi wangu wa asili ya muziki wa Zaire kuna member mule kaniambia alisoma secondary miaka ya 1970s wakati mimi nilikuwa ninamchukulia poa tu
Duh, mwambie mama watoto wako anamsalimia
 
Nilimaliza 2008 darasa la saba nakumbuka matokeo ilikua unaenda kuangalia kwa mtendaji/manispaa sina kumbukumbu vizuri pale kuna matokeo ya jumla ya wilaya yakiwa yametenganishwa kwa kila tarafa...kulikua na nyomi la watu balaaa nilipopewa matokeo kua nimefaulu Azania mtaa mzima walijua sifa kila kona dah zamani raha japo 2008 haikua mbali sana ni miaka 12 nyuma tu hapo.
Habari za wakati huu kaka na dada zangu wote wa hapa JamiiForums.

Ndugu zangu watanzania;

Mwaka 1999 kurudi nyuma ilikuwa ngumu sana kuchaguliwa shule ya secondary ya serikali. Wachache waliobahatika walijulikana kata/tarafa nzima. Je, wewe ni mmoja wao?

TABORA BOYS SECONDARY SCHOOL
View attachment 1661676

Juzi kuna mtoto wa jirani yangu alinifuata akaniambia brother ninaomba uniangalizie matokeo yangu ya darasa la saba. Mimi bila hiyana na smartphone yangu hii nikaingia katika website ya necta nikamuangalizia fresh tu. Dogo bwana alipata C flat masomo yoooote.

Nikajua ndio basi tena. Baada ya selection ya shule kutoka nikasikia huyu dogo amepangiwa shule moja ya kata mwendo kama wa dakika 20 kutoka hapa tunapokaa, ndio nikajisemea kimoyomoyo hakika dunia imebadilika kwa kasi sana.

Yaaani mtu anapata C flat bado anaenda secondary? Ninakumbuka dada yangu aliyeniachia ziwa, sasa hivi ni engineer, yeye ni moja kati ya wanafunzi 4 waliofaulu kwenda secondary shule ya serikali. Kumbuka enzi hizo kuchaguliwa tulikuwa tunaita kufaulu.

Yaaani wewe ukichaguliwa unaonekana umefaulu na wale ambao hawakuchaguliwa wanaonekana wamefeli ingawa kiuhalisia hawakuwa wamefeli ila shule zilikuwa ni chache mnoooo kiasi kwamba ni ngumu ku-accomodate wanafunzi wooote waliofaulu.

View attachment 1661678

Dada yangu alifaulu wakati huo baba anafanya kazi Wilaya ya ******* Mkoa wa Mbeya. Watu walifurahi familia nzima, lilipikwa pilau kana kwamba kuna sherehe ya kipaimara. Ndugu waliokuwa wanaishi karibu walikuja kumpa pongezi dada utadhani labda amejifungua mtoto.

Dada alikuwa maarufu sana kwa maana akiwa anaenda shuleni basi ni yeye tu ndiye aliyekua anaonekana asubuhi amevaa sare wakati huo wenzake aliomaliza nao darasa la saba bado wamelala au wameenda shambani.

Mgeni aliyekuwa hapafahamu nyumbani akiwa anaulizia kwa mama fulani wenyeji wanaanza kudadisi kwa kuambiana "au yule mama mjaluo ambaye mwanae anasoma secondary". Kwenda secodary ya serikali ilikuwa ni umaarufu kama dereva kwa maana enzi zile hakuna gari ya automatic transmission.

Gari zote ni manual na anayeweza kuendesha ni mzee mmoja au wawili tu mtaa mzima. Wanafunzi wa secondary walikuwa maarufu kama madereva kutokana na uchache wao.

View attachment 1661682

Matokeo yalikuwa yanasubiriwa kwa hamu na shauku kubwa sana kwa maana matokeo na selection zilikuwa zinakuja kwa pamoja tofauti na sasa hivi ambapo matokeo yanaanza kutoka na mwanafunzi au mzazi wake anaingia katika internet kisha baada ya mwezi mmoja mbele ndio selection inatangazwa.

Je, wewe ni mmoja ya wanafunzi wachache waliobahatika miaka ya 1990?

USISAHAU: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.
 
Ni kweli zamani waliokua wanaenda private ni waliofeli au kukosa nafasi shule za serikali tofauti na sasa..na pia hata kwenye ajira wa zamani walipewanafasi waliokua wamemaliza serikalini kabla ya private
WAHENGA TU: Kuna mzee mmoja alisoma secondary miaka ya 1970s. Yeye binafsi aliwahi kuniambia kwamba enzi hizo waliokuwa wanasoma shule za secondary za serikali walikuwa wanaheshimika sana ukilinganisha na wale waliokuwa wanasoma shule za secondary za binafsi tofauti na hivi sasa ambapo wanafunzi wa private ndio wanaheshimika.

Je, kauli hii ina ukweli wowote ndani yake?
 
Back
Top Bottom