Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Hongera sana mkongwe...1995 Ilboru secondary form 1. Yes. Ilikuwa sifa kubwa sana. Ilboru ilikuwa na wanafunzi toka tanzania nzima. Top 200 students kitaifa, 100 mzumbe, 100 ilboru.
Mkuu, inaonekana hicho choo ni noma sana. Vp vijana hawakukipa jina la masihara?Mkuu umenionesha bweni langu la Kimweri hapa Tabora boys kwa chini huku uwanjani kuna choo kinanuka ukitaka kuingia lazima uvue nguo zote nje ndio uingie vinginevyo ukitoka wenzako wanakukimbia
Miaka hiyo ya 1970s mimi nilikuwa bado sijazaliwa ndio maana nimeweka humu ili wakongwe wanipe majibuSasa mkuu enzi kulikuwa na private schools kweli au chogi
Adv ipi hiyo? Na ya nchi ganiVipi wee mbna umeandila kwa jazba sana? [emoji23][emoji23][emoji23]
Nimeshtushwa na hiyo number 1980 kaka!Unashangaa nini kijana wangu
Sikumbuki jina, ndo zinazoingia huko ndo zinazotumika kwanda kuchota maji ya kupikia jikoni no one cares ☹️☹️☹️Mkuu, inaonekana hicho choo ni noma sana. Vp vijana hawakukipa jina la masihara?
Hakika mkuuNi fahari kwa mzazi!
Kanda ya ziwa hususan Mwanza na Musoma...Kweli kabisa 2005 mambo yalibadilika kabisa kwasababu ya uwepo wa shule nyingi za kata (Zikiitwa Voda fasta/yebo yebo baadhi ya maeneo kanda ya ziwa).
Niliwahi kuomba tempo katika kampuni moja ya ulinzi kule Dar...Masomo yalikua matatu tu... Lugha, Maarifa na hisabati hapo lazima utafute marks 100+ kati ya 150 ndio uanze kufikiria kupangiwa shule...
Wanafunzi walio maliza form six walipata kupiga Tempo kwenye mashule kadhaa.
Tuache utani watoto wa siku hizi wanafaulu sana! kuliko sisi tuliosoma zamani....Juzi kuna. Denti nimeonana nae ni mtoto wa jirani yangu nikamuuliza kuhusu matokeo akanijibu wamefauli darasa zima kasoro mmoja nikasema kazi ipo
Hahahahaaa pole sana mkuu kwa maana sio kwa maneno machafu ya watanzania kama ninavyowajua...Nakumbuka nilikuwa nasumbua kata nzima na kwa tarafa nakuwa wa pili au wa tatu kwenye ile mitihan tulikuwa tunafanya pamoja(nishasahau inaitwaje)
Kimbembe necta 1st selection sikuchaguliwa
Watani zangu WAHA wapo vizuri sana katika sekta hiyo ya kamati ya ufundiKipindi hicho matokeo wanabandika ofisi ya DC. Nakumbuka baada ya kuchaguliwa kwenda secondary nilikimbilia Mwanza kwenda kufichwa kuogopa macho ya wabaya wetu maana ningerogwa. Chezea Kigoma wewe
Imesaidia sana watoto wa mama zangu wadogo kule vijijiniHizi shule za kata wanazoita Asante Lowassa zimesaidia kuaccomodate idadi kubwa sana ya wanafunzi kila Kata ingawa wengine hawana sifa za ufaulu.
Wengi wao katika mada hii wapo realAisee, kwenye huu uzi kila mtu anasema alifaulu.
Jf raha sana, ukianzisha mada ya magari basi kila mtu atasema analo.
Yes mkuu. Umri unasogea kwa kasi kubwaHongera sana mkongwe...
Mkuu wewe hujasema ulifaulu kwenda shule gani naona unamuongelea dada tuHabari za wakati huu kaka na dada zangu wote wa hapa JamiiForums.
Ndugu zangu watanzania;
Mwaka 1999 kurudi nyuma ilikuwa ngumu sana kuchaguliwa shule ya secondary ya serikali. Wachache waliobahatika walijulikana kata/tarafa nzima. Je, wewe ni mmoja wao?
TABORA BOYS SECONDARY SCHOOL
View attachment 1661676
Juzi kuna mtoto wa jirani yangu alinifuata akaniambia brother ninaomba uniangalizie matokeo yangu ya darasa la saba. Mimi bila hiyana na smartphone yangu hii nikaingia katika website ya necta nikamuangalizia fresh tu. Dogo bwana alipata C flat masomo yoooote.
Nikajua ndio basi tena. Baada ya selection ya shule kutoka nikasikia huyu dogo amepangiwa shule moja ya kata mwendo kama wa dakika 20 kutoka hapa tunapokaa, ndio nikajisemea kimoyomoyo hakika dunia imebadilika kwa kasi sana.
Yaaani mtu anapata C flat bado anaenda secondary? Ninakumbuka dada yangu aliyeniachia ziwa, sasa hivi ni engineer, yeye ni moja kati ya wanafunzi 4 waliofaulu kwenda secondary shule ya serikali. Kumbuka enzi hizo kuchaguliwa tulikuwa tunaita kufaulu.
Yaaani wewe ukichaguliwa unaonekana umefaulu na wale ambao hawakuchaguliwa wanaonekana wamefeli ingawa kiuhalisia hawakuwa wamefeli ila shule zilikuwa ni chache mnoooo kiasi kwamba ni ngumu ku-accomodate wanafunzi wooote waliofaulu.
View attachment 1661678
Dada yangu alifaulu wakati huo baba anafanya kazi Wilaya ya ******* Mkoa wa Mbeya. Watu walifurahi familia nzima, lilipikwa pilau kana kwamba kuna sherehe ya kipaimara. Ndugu waliokuwa wanaishi karibu walikuja kumpa pongezi dada utadhani labda amejifungua mtoto.
Dada alikuwa maarufu sana kwa maana akiwa anaenda shuleni basi ni yeye tu ndiye aliyekua anaonekana asubuhi amevaa sare wakati huo wenzake aliomaliza nao darasa la saba bado wamelala au wameenda shambani.
Mgeni aliyekuwa hapafahamu nyumbani akiwa anaulizia kwa mama fulani wenyeji wanaanza kudadisi kwa kuambiana "au yule mama mjaluo ambaye mwanae anasoma secondary". Kwenda secodary ya serikali ilikuwa ni umaarufu kama dereva kwa maana enzi zile hakuna gari ya automatic transmission.
Gari zote ni manual na anayeweza kuendesha ni mzee mmoja au wawili tu mtaa mzima. Wanafunzi wa secondary walikuwa maarufu kama madereva kutokana na uchache wao.
View attachment 1661682
Matokeo yalikuwa yanasubiriwa kwa hamu na shauku kubwa sana kwa maana matokeo na selection zilikuwa zinakuja kwa pamoja tofauti na sasa hivi ambapo matokeo yanaanza kutoka na mwanafunzi au mzazi wake anaingia katika internet kisha baada ya mwezi mmoja mbele ndio selection inatangazwa.
Je, wewe ni mmoja ya wanafunzi wachache waliobahatika miaka ya 1990?
USISAHAU: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.
Muacheni ndio jamii ilivyo huwezi kosa wakorofikabisa mkuu sio ustaarabu
Unaweza kukuta darasa la saba walikuwa hata 70 alafu wawili tu ndio walichaguliwaNi kweli
Nakumbuka baba mkubwa aliwahi nihadithia enzi hizo walichaguliwa wawili tu kwenda sekondari
Andika tena mkuu mimi bado sijakuelewaHivi watu wa zamani walikuwa wakiajiriwa kazini walikuwa wanajua kazi sawa na walikuwa kazini?