Mwaka 2023 nitafia shambani, eeh Mungu nisaidie!

Mwaka 2023 nitafia shambani, eeh Mungu nisaidie!

Maneno huumba, Kwanini unataka kufa?

Hata kama ni emphasis of matter sio Kwa namna hiyo aisee!
 
Kilimo hakilipi, huo ndio ukweli. Tena wewe kwa akili fupi ulizonazo ndio kabisaa unaangukia pua.

Narudia tena,bongo kilimo hakilipi. Kinacholipa ni udalali wa kilimo. Huo mtaji ingia vijijini nenda kalanvue kwa wakulima aalafu wewe nenda kauze hapo ndio utapata pesa

Wanalima vijijini Yale ndio maisha yao, apate akose wala hawana shida. Mwaka huu atalima ekari 5, mwakani atalima ekari 2, mwaka unaofuata ekari 7. Ndio hivyo wanaishi siku zote

Makampuni makubwa ya mazao ya biashara iwe alizeti, korosho, pamba, tumbaku n.k huwa wananunua kutoka kwa wakulima, jiulize kwa nn wao hawalimi?
 
Shambani usiende kwa hisia, mwaka 2022 mimi nashukuru serikali haikupiga marufuku kuuza nje ya nchi ndio angalau nimerudisha gharama kwasababu mahindi yalikaukia shambani, nilitarajia kuvuna gunia 200 lakini nikaishia gunia 70. Nimewauzia wakenya.

Maharage nilitaka yavunwe gunia 80 lakini nimeishia kwenye 30 kwasababu kuna mvua kidogo ilileta wadudu halafu ikakata hivyo maharage karibu heka 15 yakaliwa. Mengi nilipata deal la watu wa mbegu nikawauzia. Alizeti angalau ilivumilia ukame na zipo gunia 120 nakaribia kuzikamua niuze.
Hapo Kazi Tu!

Heshima yako mkuu.
 
Kilimo hakilipi, huo ndio ukweli. Tena wewe kwa akili fupi ulizonazo ndio kabisaa unaangukia pua.

Narudia tena,bongo kilimo hakilipi. Kinacholipa ni udalali wa kilimo. Huo mtaji ingia vijijini nenda kalanvue kwa wakulima aalafu wewe nenda kauze hapo ndio utapata pesa

Wanalima vijijini Yale ndio maisha yao, apate akose wala hawana shida. Mwaka huu atalima ekari 5, mwakani atalima ekari 2, mwaka unaofuata ekari 7. Ndio hivyo wanaishi siku zote

Makampuni makubwa ya mazao ya biashara iwe alizeti, korosho, pamba, tumbaku n.k huwa wananunua kutoka kwa wakulima, jiulize kwa nn wao hawalimi?
Mkubwa sikupingi lakn umenpa maswal Sana, kwa mawazo yako wakulima waliofanikiwa huwatambui? Manyara Kuna karasinga analima maelfu y hekar za ngano hanunui hata debe moja, mbeya kweny schem y umwagliaji wanakotokea ihefu fc mashamba yabanilikiwa na kampun inakima mpunga sio mchezo kwhyo wote Hawa kwako unahtimisha kw kauli kilimo hakilipi?
 
Mkubwa sikupingi lakn umenpa maswal Sana, kwa mawazo yako wakulima waliofanikiwa huwatambui? Manyara Kuna karasinga analima maelfu y hekar za ngano hanunui hata debe moja, mbeya kweny schem y umwagliaji wanakotokea ihefu fc mashamba yabanilikiwa na kampun inakima mpunga sio mchezo kwhyo wote Hawa kwako unahtimisha kw kauli kilimo hakilipi?
Nakubali unasema makampun makubwa y kilimo mazao y biashara hawalimi, swal kwa mim nisie na kampun nispolima napata wapi mtaj wa kununulia? Pia unajikuta unafamilia je watoto pmj na Mama yao km wanainterest na kilimo niwazuie tusubr kununua?
 
Kilimo hakilipi, huo ndio ukweli. Tena wewe kwa akili fupi ulizonazo ndio kabisaa unaangukia pua.

Narudia tena,bongo kilimo hakilipi. Kinacholipa ni udalali wa kilimo. Huo mtaji ingia vijijini nenda kalanvue kwa wakulima aalafu wewe nenda kauze hapo ndio utapata pesa

Wanalima vijijini Yale ndio maisha yao, apate akose wala hawana shida. Mwaka huu atalima ekari 5, mwakani atalima ekari 2, mwaka unaofuata ekari 7. Ndio hivyo wanaishi siku zote

Makampuni makubwa ya mazao ya biashara iwe alizeti, korosho, pamba, tumbaku n.k huwa wananunua kutoka kwa wakulima, jiulize kwa nn wao hawalimi?
Mzee mpaka kilimo kikulipe kuna vitu vya kuzingatia.
Capital(lazima uwe na pesa)
Taarifa sahihi
Mbinu bora za kilimo
Mbegu bora
Viuatilifu na mbolea
Usimamizi mzuri
Na eneo kubwa la kutosha na zuri.

Ukiwa na hivyo vitu vyote hapo juu. Ingia shamba ukalime. Achana na habari ya kulima eka 1 sijui 2. Hizo ni za kula nyumbani. Commercial agriculture siku zote ni large scale
 
Nawasalimu kwa jina la aliye juu wakulima wenzangu.

Nasimama hapa kutangaza rasmi kwamba 2023 nitafia shambani. Nimejiridha pasipo na shaka kwamba mali utaipata shambani.

Kwa hiyo 2022 nimeitumia vizuri kujiandaa na kutafuta mtaji. Nasema nitafia shambani nikijiamini kwa sababu ya maandalizi niliyofanya. Nimekuwa na zana zote muhimu za kilimo. Trekta 2 ndogo 2WD zipo tayari mguu sawa,moja ikiwa ya kulima vibarua ili mapato yake yanisaidie kuhudumia mashamba kwa ufanisi wa hali ya juu. Ile ya pili sasa itakuwa kwa ajili ya mashamba yangu tu. Tayari harrow na planter vimepatikana. Hakuna kupanda kienyeji. Ni kitaalamu tu.

Upande wa mashamba naona ni gharama sana kuyamiliki. Zimepatikana ekari 120 Singida changamoto shamba ni pori linahitaji kusafisha. Nimeziweka kiporo mwakani. Kwa hiyo mwaka huu nitakodi tu.

Kwa kuanzia nimekodi ekari 150 katika mikoa miwili tofauti. Ekari 100 zao moja ekari 50 zao lingine. Gharama za kukodi bado chini sana 40,000- 50,000. Tayari amepatikana bwana shamba ampaye nitaingia naye partnership ya mwaka mmoja kwa asilimia fulani ya mapato yote. Yeye kazi yake ni kusimamia tu kulingana na utaalamu wake. Mimi nitamuhudimia kila kitu.

Kingine nimechagua sana kutumia teknolojia. Ukiwa na hela kidogo mambo mengi yanarahisishwa na teknolojia. Kupalilia mashine zipo, kufukuza ndege mashine zipo, kupanda na kuweka mbolea zipo. Kupiga dawa nk.

Kinachobaki hapo ni kumuomba Mungu tu ashushe mvua nzuri kustawisha mazao. Mimi ni mzuri wa Risk Management, nimeona kulima mazao yanayistahili ukamu kama dengu, mtama na alizeti.

Kwa hiyo kwa upande wangu nimejitahidi na nitajitahidi sana tu, sehemu iliyobaki ni ya Baba wa Mbinguni. Wakati mvua inanyesha wewe unafurahi kupata maji ya kunywa, mimi nafurahi kuvuna maekari.

Huu ni uzi ni kwa ajili ya watu wanaoamini kufanikiwa wakimtanguliza Mungu huku wakifanya kazi. Sio wale wanamlilia Mungu bila kufanya kazi wakiamini kwenye miujiza ya bila kazi. Sio wale wakatisha tamaa kwao kila kitu kigumu.

Hatutajadili stori za kukatishana tamaa. Haimaanishi kwamba hakuna changamoto, basi tulete changamoto na mbinu za kutatua.

Kifupi 2023 tupunguze maneno meengi na ngonjera tufanye kazi.
Kama utaruhusu naomba nitembelee shamba lako ili nijifunze kutokea hapo.
 
Kiberege, Ifakara, Malinyi huko kuna watu wanalima mpunga si mchezo. Dakawa hapo kwenye scheme ya mpunga watu wanalima hatari. Turiani kwenye miwa, Kilosa kwenye vitunguu, Bagamoyo kwenye mananasi, Segera kwenye mkonge. Moshi pale nadhani maeneo ya kifaru njoo hadi karibu na njia panda kilimo kinafanyika na wateja wao wengi wanatoka Kenya. Wahi asubuhi (saa 11 hadi 12 alfajiri) hayo maeneo uone Tata kibao zinazokuja beba mazao kupeleka Kenya. Maeneo yote hayo watu wamewekeza kwenye kilimo.

Ukisikia mtu anakuambia kitu flani hakilipi na bado anaendelea kukifanya, huyo tofauti na shetani ni ndogo sana([emoji16] just kidding, ila kuna ukweli ndani yake). Kama ingekua hailipi tungeacha kulima kibiashara. Hakuna binadamu alie tayari kutumia muda wake mwingi, nguvu zake nyingi, pesa zake nyingi katika kitu ambacho anajua hakina faida. Hakuna binadamu wa hivyo
 
Mkubwa sikupingi lakn umenpa maswal Sana, kwa mawazo yako wakulima waliofanikiwa huwatambui? Manyara Kuna karasinga analima maelfu y hekar za ngano hanunui hata debe moja, mbeya kweny schem y umwagliaji wanakotokea ihefu fc mashamba yabanilikiwa na kampun inakima mpunga sio mchezo kwhyo wote Hawa kwako unahtimisha kw kauli kilimo hakilipi?
Katika 100%, waliofanikiwa wakiwa ni 5% tu, hapo tafsiri yake nini?

Tanzania ni nchi maskini kwa sababu asilimia kubwa ni maskini, lakini haimaanishi Mo au GSM au bakhressa ni maskini

Mimi nimezungumzia majority. Kilimo hakilipi
 
Kilimo hakilipi, huo ndio ukweli. Tena wewe kwa akili fupi ulizonazo ndio kabisaa unaangukia pua.

Narudia tena,bongo kilimo hakilipi. Kinacholipa ni udalali wa kilimo. Huo mtaji ingia vijijini nenda kalanvue kwa wakulima aalafu wewe nenda kauze hapo ndio utapata pesa

Wanalima vijijini Yale ndio maisha yao, apate akose wala hawana shida. Mwaka huu atalima ekari 5, mwakani atalima ekari 2, mwaka unaofuata ekari 7. Ndio hivyo wanaishi siku zote

Makampuni makubwa ya mazao ya biashara iwe alizeti, korosho, pamba, tumbaku n.k huwa wananunua kutoka kwa wakulima, jiulize kwa nn wao hawalimi?
Sahihi
 
Shambani usiende kwa hisia, mwaka 2022 mimi nashukuru serikali haikupiga marufuku kuuza nje ya nchi ndio angalau nimerudisha gharama kwasababu mahindi yalikaukia shambani, nilitarajia kuvuna gunia 200 lakini nikaishia gunia 70. Nimewauzia wakenya.

Maharage nilitaka yavunwe gunia 80 lakini nimeishia kwenye 30 kwasababu kuna mvua kidogo ilileta wadudu halafu ikakata hivyo maharage karibu heka 15 yakaliwa. Mengi nilipata deal la watu wa mbegu nikawauzia. Alizeti angalau ilivumilia ukame na zipo gunia 120 nakaribia kuzikamua niuze.

Kwa hayo mazao kiongozi mfano Mahindi na maharage kwa hiyo idadi uliyotegemea kuvuna inatakiwa ulime heka ngapi kuweza kupata hiyo idadi uliyoitarajia kuvuna mkuu...?

Na utaratibu wa kuuza Kenya upoje wanakuja kuchukua huku au unawapelekea ndio unapatiwa pesa yako...?
 
Back
Top Bottom