Mwaka 2025 ni mwaka wa kutangaza matokeo ya kazi iliyofanywa na CCM na Rais Samia

Mwaka 2025 ni mwaka wa kutangaza matokeo ya kazi iliyofanywa na CCM na Rais Samia

KARLO MWILAPWA

JF-Expert Member
Joined
Apr 10, 2019
Posts
2,789
Reaction score
4,951
KAZI KUBWA KWA MAENDELEO MAKUBWA.

Mwaka 2025 ni mwaka wa kutangaza matokeo ya kazi iliyofanywa na CCM na Rais Samia ambayo ni kubwa sana na itachukua muda mrefu kuielezea lakini hata kipofu anaona kilichofanyika. Kuanzia kwenye ujenzi, ulinzi, usalama, demokrasia hakika kazi kubwa imefanyika.

Kama mtanzania ninayefurahishwa na KAZI iliyofanywa na awamu ya mama chini ya kaulimbiu yake ya KAZI IENDELEE basi nimetafakari kumpatia mama kauli mbiu itakayoendeleza kauli mbiu ya KAZI IENDELEE

Hapo ndio wazo la kauli mbiu KAZI KUBWA KWA MAENDELEO MAKUBWA liliponijia akilini. Kwa nini KAZI KUBWA KWA MAENDELEO MAKUBWA?

Kwa kuwa mama alianza na KAZI IENDELEE ambayo ni mwendelezo wa HAPA KAZI TU basi mwendelezo wa KAZI IENDELEE NI KAZI KUBWA KWA MAENDELEO MAKUBWA.

Kaulimbiu ya KAZI KUBWA KWA MAENDELEO itachochea na kuhamasisha watu kujibiidisha kwa bidii ili kupata maendeleo MAKUBWA. Hivyo kila mtu ataona msingi wa MAENDELEO makubwa ni kazi KUBWA.

Pia, kauli mbiu hii itasaidia kutangaza kazi za serikali zenye kuleta maendeleo makubwa na itamkumbusha kila mtumishi wa serikali kuwa kazi KUBWA itapelekea maendeleo makubwa sana.

Pia, itasaidia kuwatia moyo wa uvumilivu wananchi kwamba kazi KUBWA inayofanyika nia na dhumuni ni maendeleo makubwa hata kama maendeleo hayoonekana Leo lakini mbeleni yapo.

Pia, itachochea vijana kuwaza kwa upana na kubuni kazi KUBWA ili wapate maendeleo makubwa.
 
Rais Samia anapitia na kusoma yanayojadiliwa, Chama kimechagua kaulimbiu yenye muelekeo na maoni yangu kwenye huu uzi
 
Back
Top Bottom