Mwaka mzima ndani ya safina ya Nuhu, usafi ulifanyikaje?

Mwaka mzima ndani ya safina ya Nuhu, usafi ulifanyikaje?

Manton

JF-Expert Member
Joined
Mar 27, 2012
Posts
1,163
Reaction score
1,523
Habari za wakati huu, wachambuzi makini wa masuala mbalimbali ya kunoanoa bongo; ni yangu matarajio kwamba mko salama! Naliweka swali hili mezani kutokana na kwamba nategemea kupata majibu ya kisayansi kuliko majibu yatokayo na mahaba ya kiimani na ndiyo sababu ya kuliweka jambo hili hapa na siyo kwenye jukwaa la dini.

Katika, kitabu cha Mwanzo 7:11, inaonyesha Nuhu, akiwa na miaka 600, tarehe 17 ya mwezi wa pili wa huo mwaka mvua kubwa ilianza kunyesha kwa wingi na kukoma baada ya siku 40, wakati ambapo aliendelea kukaa kwenye hiyo safina hadi maji yalipokukauka kwenye uso wa dunia, akatoka nje ya safina: Mwanzo 8:13-15, wakati Nuhu akiwa na miaka 601, tarehe 27 ya mwezi wa pili wa mwaka mwingine baada ya gharika; sawa na mwaka mmoja na siku 10 alizokaa kwenye safina tangu mvua iliponyesha na kukoma.
Sasa kwa kuwa kulikuwamo na wanyama najisi na wasafi, je, usafi ulifanyikaje, ili kuruhusu kuwepo kwa hali ya hewa nzuri, yakufanya maisha yaendelee bila bughudha wala kutia shaka kwa msomaji?
 
Kama Noah alikuwa smart enough kutengeneza Safina , basi alikuwa smart pia kutengeneza njia ya kudondosha uchafu wa wanyama kutoka kwenye kila chumba kwenda chini.

Watu wa zamani walikuwa wako smart kuliko watu wa sasa ... embu niambie professor gani anaweza kutengeneza pyramid!!! Watu wanadhania kuwa na technology ndio kunafanya watu wa sasa wawe smart kuliko wa zamani. Watu wa zamani walifanya mambo makubwa bila umeme.

Pili,kama Mungu aliwafanya wanyama wawili wawili wa march kwenda kwenye safina , anauwezo pia wa kuwafanya wanyama wakibanwa na haja waende pembeni ya Safina na wageukie baharini kutoa haja.
 
Mi
Kwa hiyo toa ushuhuda kwa mtoa mada namna uchafu wa wanyama uliopanda nao ktk Noah ulivyosafishwa au kutoka ikiwa mvua ilinyesha siku 40 bila kukatika.
Ninachokumbuka nilipanda ya kuku na bata na wote waliwekwa kwenye box kwaiyo uchafu wote ulikuwa kwenye box lao kwa habari ya kwamba ulisafishwaje ni kwa aliyewabeba
 
Umeleta jambo la kiimani halafu unataka sayansi ndio ijibu; kazi kweli kweli! Hivi kisayansi inawezekana mtu kutembea juu ya maji? Je kisayansi yawezekana mtu kufufuliwa!? Kisayansi pia inawezekana kuweka mikono juu ya mgonjwa na kusema sema baadhi ya maneno halafu mgonjwa akapona!? Kwa kua suala ulilolileta ni la kiimani, basi acha majibu ya kiimani yafanye kazi badala ya sayansi! Kwanza kitabu gani cha sayansi kimewahi kueleza habari za gharika la Nuhu!? Kama hakuna then acha kitabu hicho hicho ulicho tumia kujua habari za hilo gharika kijibu chenyewe badala ya Abort, Nelkon and Parker au UP na bwana Lambert
 
humo ndani ya box hao ya kuku na bata kama ulivyoandika kwa hiyo Noal alibeba had mabox?
mkuu noah yenyewe hiii hapa mabox yakuwepo na kuku na bata ndani yake
 

Attachments

  • IMG_20180522_233714.png
    IMG_20180522_233714.png
    141.4 KB · Views: 56
Kama Noah alikuwa smart enough kutengeneza Safina , basi alikuwa smart pia kutengeneza njia ya kudondosha uchafu wa wanyama kutoka kwenye kila chumba kwenda chini.

Watu wa zamani walikuwa wako smart kuliko watu wa sasa ... embu niambie professor gani anaweza kutengeneza pyramid!!! Watu wanadhania kuwa na technology ndio kunafanya watu wa sasa wawe smart kuliko wa zamani. Watu wa zamani walifanya mambo makubwa bila umeme.

Pili,kama Mungu aliwafanya wanyama wawili wawili wa march kwenda kwenye safina , anauwezo pia wa kuwafanya wanyama wakibanwa na haja waende pembeni ya Safina na wageukie baharini kutoa haja.
Umejibu vyema
 
Back
Top Bottom