Mwaka mzima ndani ya safina ya Nuhu, usafi ulifanyikaje?

Mwaka mzima ndani ya safina ya Nuhu, usafi ulifanyikaje?

lazima ukumbuke hawakupanda kwenye safina kwaajili ya safari kutoka point A-B lengo lilikua kujinusuru na gharika kwaiyo popote maji yalipowapeleka ilikua sawa kikubwa usalama wao adi maji yalipokauka, ayo maswali unayouliza ata mtoto wangu wa miaka mitatu hawezi kuuliza maswali ya kipuuzi kama yako.
Kama umeshindwa kuelezea, uchafu ulitolewaje kwenye safina, basi usileta vioja, kumbe una mtoto wa darasa la tatu, hongera, usiache kumuandikisha tuisheni.
 
Mkuu uliza na ukubwa wa mlango uliowapitisha watu wote wale na wanyama.. Utapata jibu la usafi ulivyofanyika
 
Kulikuwa na milango kwa juu.
Kumbuka jinsi njiwa alivyotumwa na kuleta jani baada ya gharika kutulia.
Pia kulikuwa na milango ya kuingiza hewa ambayo walikuwa wanaivuta ili kuishi.
Kapteni alikuwa Nuhu mwenyewe.


Sent using Jamii Forums mobile app
Wapi imeandikwa kuwa Nuhu, alikuwa kapteni? Utani huu, kinyesi cha tembo, dainoso, na kadhalika kinatolewa, kupitia katundu kadogo ka juu, pamoja na mikojo?
 
Wapi imeandikwa kuwa Nuhu, alikuwa kapteni? Utani huu, kinyesi cha tembo, dainoso, na kadhalika kinatolewa, kupitia katundu kadogo ka juu, pamoja na mikojo?
Wapi imeandikwa Safina ilikuwa haifanyiwi Usafi.
 
Umeleta jambo la kiimani halafu unataka sayansi ndio ijibu; kazi kweli kweli! Hivi kisayansi inawezekana mtu kutembea juu ya maji? Je kisayansi yawezekana mtu kufufuliwa!? Kisayansi pia inawezekana kuweka mikono juu ya mgonjwa na kusema sema baadhi ya maneno halafu mgonjwa akapona!? Kwa kua suala ulilolileta ni la kiimani, basi acha majibu ya kiimani yafanye kazi badala ya sayansi! Kwanza kitabu gani cha sayansi kimewahi kueleza habari za gharika la Nuhu!? Kama hakuna then acha kitabu hicho hicho ulicho tumia kujua habari za hilo gharika kijibu chenyewe badala ya Abort, Nelkon and Parker au UP na bwana Lambert
Right on point mkuu! Mleta mada anajichanganya, au basi kisayansi atwambie kama mtu anaweza kupata ujauzito bila mbegu ya kiume kukutana na mbegu ya kike!?

Akishindwa kutupa haya majibu akubali majibu kutoka kitabu alichokitumia kuleta uzi huu.
 
Kama umeshindwa kuelezea, uchafu ulitolewaje kwenye safina, basi usileta vioja, kumbe una mtoto wa darasa la tatu, hongera, usiache kumuandikisha tuisheni.
Mtoto wa miaka mitatu sio DARASA LA TATU!. Mgum sana kuelewa wewe
 
nguruwe hali kila kitu, itakuwa hujui. ni mchaguzi sana wa chakula na ana uwezo mkubwa wa kutambua sumu. ukimpa chakula kipya hali mpaka akinuse. nguruwe ni msafi. anachagua wapi pa kunya na pa kulala, (labda eneo liwe dogo). maji, chakula kilicho haribika au kuchacha hali. mfumo wake wa umeng'enyaji wa chakula ni sawa na binadamu.
 
Yawezekana waliishi na uchafu wao ndani ya safina mpaka walipokuja kutoka nje!. Fikiria hili.
Umuhimu wa Usafi (hygiene) ulianza tiriwa mkazo kuanzia karne ya 19 (hapo tunaongelea miaka ya 1801s - 1900s) kabla ya hapo hakukuwa na usafi kabisa. Miji ya Paris, England, Florence, Athens unayoiona leo haikuwa misafi kabisa. Hii ilipelekea magonjwa yalioua sana watu kipindi hicho.
Watu walianza kufikiria hasa kiundani mwishoni mwa karne ya 19 kuelekea ya 20 kipindi cha Age of Enlightenment au Age of Reason. Hapo ndipo uelewa kuhusu masuala mbalimbali duniani, vumbuzi, na demokrasia zilipoanza kucharge bongo za watu. Soma hizi:-
1.Mwaka 430AD (kabla ya kuzaliwa Yesu) kulitokea ugonjwa uliouwa sana watu huko Athens -Ugiriki ulijulikana kama The Plague of Athens.
2. Mwaka 165-180AD (baada ya kristo) ugonjwa mwingine ulijitokeza ukaua sana watu huko Ugiriki ulijulikana kama The Antonine Plague nao sababu haijulikani lakini yasemekana ni uchafu. Inakadiriwa watu Millioni 5 walifariki.
3. Kufikia karne ya 14 bado watu walikuwa ni wachafu hawakuwa wamejielewa kiasi cha kufata kanuni bora za usafi. Inakadiriwa watu Millioni 50 walikufa duniani sababu ya ugonjwa fulani uliojulikana kama "Black Death", uliambukizwa kupitia Panya, hii ni sawa na 25% - 60% ya watu wote Ulaya.
So nachotaka kukielezea hapa ni kwamba yawezekana Nuhu na wanyama waliishi na uchafu wao ndani ya safina na kwakuwa uchafu ulikuwa kitu cha kawaida kipindi chao basi hakukuwa na haja ya kuutoa nje ya safina!.
Nadharia ya Mungu kuwafunga njia za kuutoa nje ya mwili kiimani inaweza leta mantiki pia, kama aliweza leta Simba na Swala ndani ya zizi moja ashindwe vipi kufunga kutoa uchafu.
Cc: Malcom Lumumba
 
Moja kwa moja, unaona kwamba uhai wa viumbe vyote ndani ya Safina na Nuhu akiwemo, ulikuwa hatarini, kipindupindu, isinge waacha salama, na hata pumu.
 
Umeleta jambo la kiimani halafu unataka sayansi ndio ijibu; kazi kweli kweli! Hivi kisayansi inawezekana mtu kutembea juu ya maji? Je kisayansi yawezekana mtu kufufuliwa!? Kisayansi pia inawezekana kuweka mikono juu ya mgonjwa na kusema sema baadhi ya maneno halafu mgonjwa akapona!? Kwa kua suala ulilolileta ni la kiimani, basi acha majibu ya kiimani yafanye kazi badala ya sayansi! Kwanza kitabu gani cha sayansi kimewahi kueleza habari za gharika la Nuhu!? Kama hakuna then acha kitabu hicho hicho ulicho tumia kujua habari za hilo gharika kijibu chenyewe badala ya Abort, Nelkon and Parker au UP na bwana Lambert
Ashindwaye kukuelewa atakuwa kiburi
Nalog off
 
Back
Top Bottom