Mwaka mzima ndani ya safina ya Nuhu, usafi ulifanyikaje?

Mwaka mzima ndani ya safina ya Nuhu, usafi ulifanyikaje?

Habari za wakati huu, wachambuzi makini wa masuala mbalimbali ya kunoanoa bongo; ni yangu matarajio kwamba mko salama! Naliweka swali hili mezani kutokana na kwamba nategemea kupata majibu ya kisayansi kuliko majibu yatokayo na mahaba ya kiimani na ndiyo sababu ya kuliweka jambo hili hapa na siyo kwenye jukwaa la dini.

Katika, kitabu cha Mwanzo 7:11, inaonyesha Nuhu, akiwa na miaka 600, tarehe 17 ya mwezi wa pili wa huo mwaka mvua kubwa ilianza kunyesha kwa wingi na kukoma baada ya siku 40, wakati ambapo aliendelea kukaa kwenye hiyo safina hadi maji yalipokukauka kwenye uso wa dunia, akatoka nje ya safina: Mwanzo 8:13-15, wakati Nuhu akiwa na miaka 601, tarehe 27 ya mwezi wa pili wa mwaka mwingine baada ya gharika; sawa na mwaka mmoja na siku 10 alizokaa kwenye safina tangu mvua iliponyesha na kukoma.
Sasa kwa kuwa kulikuwamo na wanyama najisi na wasafi, je, usafi ulifanyikaje, ili kuruhusu kuwepo kwa hali ya hewa nzuri, yakufanya maisha yaendelee bila bughudha wala kutia shaka kwa msomaji?
Umeweka swali la kiimani unataka majibu kisayansi we vepe
 
Sawa ila kuna kila sababu ya kumuuliza mungu ambae ndie alietoa maagizo na ramani ya safina na kama si hivyo basi hatutapata majibu kabsa ndugu.
Kwa kuwa wapo wanadamu wanao jinasibu kuwasiliana na Mungu moja kwa moja siku hizi kama wakati Mwanzo, basi lazima wanayo majibu ya kisayansi yasiyo acha maswali zaidi, ngoja waje nayo!
 
Nimejiuliza sana kuhusu story ya Noah na Safina uwa sipati majibu. Swali langu kuu ni je lile gharika lilifika mpk huku kwetu Afrika au lilikuwa sehemu tu ndogo ya taifa flani. Mungu nipe Imani kwenye hili
 
sasa wewe huoni kuwa ni uongo
kwa akili yako,;
mtu anaweza kutembea juu ya maji?
inawezekana mtu kufufuliwa?
mtu aliyekatika mkono au mguu anaweza kuombewa vikaota?(achana na usanii wa magonjwa unayodanganywa eti wamepona kwa magonjwa yasiyoonekana)
Uliyemnukuu umemuelewa?
Anasema acha sayansi ijitetee yenyewe na duni pia ijitetee yenyewe!.

Mtoa mada analeta suala la dini lakin anataka majibu ya kisayansi hapo ndo tatizo lilipoanzia. Amenukuu vifungu vya biblia lakn anataka unapojibu unukuu abort na vinginevyo
 
Ashakum si matusi natanguliza msamaha kwanza
*Walikuwa wanaogaje humo ndani ya safina?

* Faragha walikuwa wanakutanaje?

*Haja ndogo na kubwa ilikuwaje humo ndani maana wanyama wote walio kuwemo humo?

Mimi sina utashi wala ufahamu kuliko mungu hapa najiuliza tu kinamna ya binadamu ndio maana nimetanguliza kuomba msamahaa kwa disclaimers wote.
 
Ni sawa na Usafi unavyofanyikwa kwenye Meli.
Kwenye Meli kuna vyoo na ma jaba ya takataka,
Mabafu ya kuoga yapo pia,
Hifadhi ya chakula ipo,
Vyumba vya kulala vipo.
Meli ni mfano wa safina, takataka zinakusanywa na kumwagwa Baharini.
Kwenye Safina nako pia takataka zilikusanywa na kumwagwa kwenye maji.
Kuna shida gani hapo ?
Swali lako ni jepesi tu kuwa chombo kinachoelea usafi unafanyi kama kawaifa na uchafu humwagwa majini katika mahali maalum mbali huko kilindini.
 
Kama maji yalikuwepo kuizunguka hiyo safina swala la usafi siyo hoja. Safina ni kama meli kubwa tu.
 
yani kwenye safina simba umuweke na mbuzi halafu asiliwe?
polar bear walimchukuaje kuta kule north!!!
sloth(the slowest animal on planet earth) kutoka australia kwenda israel angetumia miaka 200 kufika
tutoleeni fairytales zenu hapa
ha haha hahaaa
 
yani kwenye safina simba umuweke na mbuzi halafu asiliwe?
polar bear walimchukuaje kuta kule north!!!
sloth(the slowest animal on planet earth) kutoka australia kwenda israel angetumia miaka 200 kufika
tutoleeni fairytales zenu hapa
wanasema kuwa wakati huo dunia ilikuwa ni ndogo " haikuwa imekuwa kwa ukubwa huu uliopo sasa "" atii baada ya gharika kupita ulikuja kutokea mtikisiko mkubwa ulioweza kugawa mabara ...
 
Na hao nguruwe walikua wangap wakawezakula uchaf wa viumbe vyote. Na uchafu wa nguruwe nao ulitupwa wapi. Kwa hiyo hata walikuwa wakioga, wakinyoa, wakifua, vazi likichakaa alikuwa anakula nguruwe. WATU MNA MAJIBU YA KIJINGA SANA, MEPESI
hahaaa ..nguruwe alikuwa anakula mavi ya wenzie halafu anakunya nakula mavi Yke "" achili mbali" mabaki mengine ya uchafu yaliyokuwa yanapatikana humo .....hahaaa Hawa Jamaa story zao bwana ""
 
Ni sawa na Usafi unavyofanyikwa kwenye Meli.
Kwenye Meli kuna vyoo na ma jaba ya takataka,
Mabafu ya kuoga yapo pia,
Hifadhi ya chakula ipo,
Vyumba vya kulala vipo.
Meli ni mfano wa safina, takataka zinakusanywa na kumwagwa Baharini.
Kwenye Safina nako pia takataka zilikusanywa na kumwagwa kwenye maji.
Kuna shida gani hapo ?
Swali lako ni jepesi tu kuwa chombo kinachoelea usafi unafanyi kama kawaifa na uchafu humwagwa majini katika mahali maalum mbali huko kilindini.
Kufunikwa lami ndani na nje unakueleweje? Kama safina ili kuwa kama meli, captain alikuwa nani, na ilikuwa ikisafiri kuelekea wapi?
 
wanasema kuwa wakati huo dunia ilikuwa ni ndogo " haikuwa imekuwa kwa ukubwa huu uliopo sasa "" atii baada ya gharika kupita ulikuja kutokea mtikisiko mkubwa ulioweza kugawa mabara ...
ahahaaaaaaaa
watunzi wa biblia walikuwa ni majinias na vilaza at the same time
 
Back
Top Bottom